Tuesday, March 20, 2018

SERIKALI YATEKELEZA MAOMBI 5 YA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO WILAYANI LONGIDO

Baadhi ya mifugo wakiwa katika eneo la kunywa maji kablaya kuuzwa katika Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido amablo limejengwa kwa  ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF)

Sehemu ya kunyweshea mifugo iliyojengwa katika ​​Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido kwa ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).

Muonekano wa Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido baada ya kupata nishati ya mwanga kwa ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
Serikali kupitia, Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), imetekeleza maombi 5 ambayo yanawasaidia wafugaji hao  kuongeza thamani ya mifugo yao  kupitia Soko la Kimkakati la mifugo Longido lililojengwa na Program hiyo.
Mwishoni mwa mwaka 2017, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  (Sera, Bunge, Ajira ,Kazi,  Vijana na Watu wenye Ulemavu ) Mhe.Jenista Mhagama, alikuwa na ziara ya kukagua  ujenzi wa soko hilo wilayani humo, ambapo  baada ya ukaguzi alikutana na wafanyabiashara ya mifugo, ambao  waliwasilisha maombi  5,  ambayo yangeweza kuongeza Thamani Biashara za Mifugo na kutatua  kero zote  za wafanyabiashara wa mifugo wilayani humo.
“Serikali ya awamu ya tano imeamua kuwasikiliza watu wanyonge na ambao wanajituma kuchapa kazi, lakini pia lengo la Program ya MIVARF ni kuongeza kipato kwa  wananchi hasa waishio vijijini, kwa mantiki hiyo nilimuelekeza Mratibu wa Program Kutekeleza maombi yao haraka sana ili wafugaji hawa wapate tija ya ufugaji kupitia soko hili”alisema Mhagama
Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Mifugo wilayani Longido, Saruni Laizer amesema maombi waliyowasilisha serikalini ili waweze kupata tija ya mifugo kupitia soko la Kimkakati la Mifugo Longido yamefanyiwa kazi na Program ya MIVARF ndani ya miezi mitatu tangu wayasilishe, ikiwa ni; Mizani ya kupima mifugo, Maji ya kunyweshea mifugo, machinjio, Josho, pamoja na  umeme.
“Tulihitaji maji hapa ili mifugo isije ikafa wakati inasubiri kuuzwa kwa kukosa maji, lakini umeme hapa ni muhimu kwani biashara zetu zinafanyika usiku, tayari hadi jenereta imeletwa kwa ajili ya kuhakikisha biashara haikwami kwa dharura yoyote ile, lakini mizani itasaidia kutowauza mifugo kwa kuangalia kwa macho bali kwa uzito wao” alisema Laizer
Mhagama alitoa maagizo hayo baada ya kukagua  Soko la kimkakati lililojengwa na Serikali kupitia Ofisi Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
Soko hilo litawanufaisha wananchi wapatao 14,2000  wa wilayani Longido ambapo asilimia 95 ni wafugaji na wanaojishughulisha na biashara za mifugo.
Soko  hilo la kimkakati ambalo halijafunguliwa rasmi , tayari halmashauri ya wilaya hiyo imeweza kukusanya mapato ya kiasi cha shilingi milioni 106 kwa mwaka  2016/2017 ambapo kwa makusanyo hayo yamewezesha halmashauri hiyo kuvunja rekodi ya miaka kumi iliyopita kwa kukusanya shilingi bilioni 1.3 kwa mara ya kwanza  kwani awali mapato yake yalikuwa chini ya bilioni moja.
MIVARF;  ni Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko na Huduma za Kifedha Vijijini  iliyobuniwa  na serikali ya Tanzania  kwa  kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo yaani (IFAD) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB).   Programu hii inatekelezwa  katika mikoa 29 ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani  tangu mwaka 2011.

Read More

WAZIRI MKUU AMKABIDHI MSAADA BIBI TACLA HAMIDU (MLEMAVU)

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemkabidhi Bibi Tecla Hamidu ambaye ni mlemavu wa miguu sh. milioni tano ili aweze kuongezea katika mtaji wake. Ametoa fedha hizo leo (Jumanne, Machi 20, 2018) ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake aliyoitoa Februari 22, 2018 kwenye Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemkabidhi Bibi Tecla Hamidu ambaye ni mlemavu wa miguu sh. milioni tano ili aweze kuongezea katika mtaji wake.Ametoa fedha hizo leo (Jumanne, Machi 20, 2018) ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake aliyoitoa Februari 22, 2018 kwenye Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes).


Read More

Monday, March 19, 2018

WAZIRI MKUU AFUNGUA MKUTANO WA 65 WA BARAZA LA MAWAZIRI WA AFYA AFRIKA (ESCA )

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Afya wa Uganda .Sarah Opendi ,wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 65 wa Baraza la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Nchi  za Mashariki Kati na Kusini mwa Africa (ESCA Health Community) kushoto ni Wazri wa Afya wa Malawi Atupele Muluzi,Waziri Mkuu amefungua mkutano huo jana March 19/2018 Jijini Dar es salaam



Read More

Sunday, March 18, 2018

WAZIRI MKUU ASHUHUDIA MCHEZO WA KIRAFIKI VIJANA WA NGORONGORO HEROES NA MOROCCO KATIKA UWANJA WA UHURU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Morocco nchini, Abdelilah Benryane . walipokutana  kushuhudia mchezo wa kirafiki wa kimataifa, Timu ya Taifa Vijana  walio chini ya Umri wa miaka 20 (Ngorongoro Heroes )na Timu ya Morocco. Ambao umefanyika jana kwanye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam March 18, 2018.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya mashabiki wa Tanzania na Morocco walio kuja kushudia mchezo wa kirafiki wa Kimataifa  wa Timu ya Taifa Vijana  walio chini ya Umri wa miaka 20 (Ngorongoro Heroes )na Timu ya Morocco.Kushoto kwa Waziri Mkuu ni Balaozi wa Morocco Nchini Tanzania ,Abdelilah Benryane . mchezo huo umefanyika jana kwanye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam March 18, 2018.

Read More

Saturday, March 17, 2018

WIZARA SABA KUKUTANA KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI MPAKANI MWA TANZANIA NA ZAMBIA

Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji Nchini, imeamua kuzikutanisha wizara saba zinazohusika moja kwa moja na changamoto zinazopunguza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara na Wawekezaji mpakani mwa Tanzania na Zambia.
Akiongea wakati wa ziara ya kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mpango wa maboresho ya Mazingira ya biashara na uwekezaji katika mkoa wa Songwe na maeneo yaliyopo mpakani mwa Tanzania na Zambia, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora amesema mara baada ya kuhitimisha  ziara yake  tarehe 17 Machi, 2018, atakutana na makatibu wakuu wa wizara zinazopaswa kutoa suluhisho la changamoto hizo.
Nitakutana na makatibu wakuu wenzangu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Mambo ya nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za mikoa  na Serikali za mitaa (TAMISEMI) na naamini maazimio tutakayotoa katika kikao hicho yatakuwa suluhisho la kuondoa changamoto zinazojitokeza hapa mpakani mwa Tanzania na Zambia” , amesema Kamuzora.
Akibainisha changamoto za mazingira ya Biashara na uwekezaji mpakani mwa Tanzania na Zambia, Mkuu wa mkoa wa Songwe, Luteni Mstaafu, Chiku Galawa amesema, changamoto kubwa mpakani hapo ni usalama kwa wafanyabiashara na biashara zao, ambapo kwa mazingira ya mpaka huo imekuwa vigumu kuuimarisha.
“Mpaka wetu umejengwa kila mahali , hivyo uhalifu unakuwa mgumu kuuzuia Kuna watu wanakunywa pombe Zambia ambazo tumezizuia hapa nchini kuuzwa, na kurudi wamelewa Tunduma, suala la biashara haramu ya ubadilishaji wa fedha inayofanywa mtaani  kinyume na sheria na taratibu za nchi ni changamoto , lakini wafanyabiashara wanakwepa kodi kutokana na kuwa kunabaadhi ya watanzania sehemu ya nyumba zao zipo Zambia nyingine ipo Tanzania hivyo ushuru wa forodha haukusanywi kwa madai wanapeleka bidhaa hizo kwa watanzania kwani hawapitishi bidhaa hizokwenye lango husika” alisema Galawa
Galawa amebainisha mipango ambayo Mkoa umejipanga katika kuhakikisha wanakabili changamoto hizo, kuwa ni kuliweka Daftari la wakaazi katika mfumo wa kielektroniki ambalo litajumuisha wakaazi wote wa Tunduma kuanzia umri wa mwezi mmoja na litakuwa linahuishwa kila wakati, Upimaji wa mji waTunduma nao unaendelea na kila mmiliki  wa ardhi atapewa hati, pia litajengwa soko kubwa mpakani hapo ili kufanya menejimenti ya biashara mpakani.
Aidha, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu alikutana na wadau wa sekta binafsi, pamoja na wateja katika Kituo cha Forodha cha Pamoja Tunduma, ambao walishauri sekta zinazohusika na Mazingira ya Biashara na Uwekezaji mpakani hapo kwa upande wa Tanzania  na Zambia zikutane ili  kuharakisha kutatua changamoto zinazopunguza ufanisi wa biashara mpakani hapo.

Lengo la Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji Nchini ni Kupunguza gharama za Kufanya biashara nchini kwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara na Wawekezaji, mpango huo unaotekelezwa na Idara, Wizara na Wakala wa Serikali  kwa uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Read More

WIZARA SABA KUKUTANA KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI MPAKANI MWA TANZANIA NA ZAMBIA

Mkuu wa mkoa wa Songwe, Luteni Mstaafu, Chiku Galawa akiteta jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora wakati wa ziara ya kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mpango wa  maboresho ya Mazingira ya biashara na uwekezaji mkoani Songwe, tarehe 17 Machi, 2018.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora akiendesha kikao  kilicho jumuisha watendaji wa serikali na sekta binafsi  wakati wa ziara ya kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mpango wa maboresho ya Mazingira ya biashara na uwekezaji mkoani Songwe, tarehe 17 Machi, 2018.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora akiongozwa na  Meneja wa Kituo cha Forodha cha Pamoja Tunduma, Jomimosa Nsindo wakati wa ziara ya kutembelea maeneo ya utekelezaji wa maboresho ya Mazingira ya biashara na uwekezaji , mpakani mwa Tanzania na Zambia, tarehe 17 Machi, 2018.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Profesa, Faustin Kamuzora akifuatilia maelezo ya wateja wa Kituo cha Forodha cha Pamoja Tunduma (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kutembelea maeneo ya utekelezaji wa maboresho ya Mazingira ya biashara na uwekezaji , mpakani mwa Tanzania na Zambia, tarehe 17 Machi, 2018.  

Read More

Friday, March 16, 2018

MAJALIWA AKUTANA NA MAKAMU MKUU WA UDSM

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa William Anangisye, ofisini kwa Waziri Mkuu mini Dodoma, Machi 16, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa William Anangisye ofisini kwa Waziri Mkuu mini Dodoma, Machi 16, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa William Anangisye ofisini kwa Waziri Mkuu mini Dodoma, Machi 16, 2018.


Read More

Sunday, March 11, 2018

WAKULIMA 2000 WAONGEZA KIPATO KWA UJENZI WA DARAJA LA MIVARF

Muonekano wa Daraja la Masware lililopo katika kijiji cha Masware Kata ya Kiru Wilayani Babati, daraja hilo limejengwa na Mradi wa Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za kifedha Vijijini (MIVARF).
Baadhi ya waendesha pikipiki ambao ni wakazi wa kijiji cha Masware Kata ya Kiru Wilayani Babati wakipita  katika Daraja la Masware lililojengwa na Mradi wa Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za kifedha Vijijini (MIVARF).

Baadhi ya watembea kwa miguu ambao ni wakazi wa kijiji cha Masware Kata ya Kiru Wilayani Babati wakipita  katika Daraja la Masware lililojengwa na Mradi wa Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za kifedha Vijijini (MIVARF).

Na Mwandishi wetu
Wakulima 2000 kutoka  vijiji sita vya, Kata ya Kiru Wilayani Babati wameongeza kipato kutokana na ujenzi wa daraja lililojengwa na Mradi wa Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za kifedha Vijijini (MIVARF),  ikiwa ni sehemu ya malengo ya mradi huo katika kuongeza kipato nchini hususan  maeneo ya vijijini.
Wakulima hao wa Kata ya Kiru, inayojumuisha kaya 306, walishindwa kuongeza kipato kwa takribani  miaka 38,  tangu mwaka 1978, baada ya Daraja walilokuwa wanatumia kusombwa na Mafuriko hadi mwaka 2016, Serikali kupitia Mradi wa MIVARF ilipojenga  Daraja hilo ambalo limeanza kutumika sasa na  kuchochea shughuli zao za  kiuchumi .
Akiongea  na timu ya  wataalamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na  Mradi  wa MIVARF mara baada ya kutembelea Kijiji cha Masware lilipojengwa Daraja hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Babati Hamis Malinga amesema, Serikali kupitia Mradi wa MIVARF imeweza kuchochea uwekezaji katika kata hiyo
Kiwanda cha Sukari cha Manyara kimeweza kuongeza uzalishaji kutoka tani 15 hadi 30 kwa siku kutokana na ujenzi wa daraja la kijiji cha Masware ambalo limesaidia kuboresha biashara baina ya vijiji na kuongeza kipato kwa wananchi. Aidha, Usafirishaji wa mazao na bidhaa ulikuwa wa gharama kubwa sana lakini kwa jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kupitia mradi huu tumeweza kuona maendeleo makubwa katika Vijiji hivi”, alisema Mkurugenzi Malinga.
Kwa upande wa wakulima wa kijiji  cha Masware wamesema ujenzi wa Daraja hilo umeongeza kipato chao kwani wanaweza kusafirisha mazao yao kwa urahisi pamoja na vijana wamepata ajira kupitia usafiri wa pikipiki maarufu kama “bodaboda”  unaotumiwa kusafirisha abiria
“Tangu ujenzi wa daraja hili tumeweza kupeleka mazaoyetu katika soko tunalotaka ambapo awali haikuwa rahisi, wakulima walikuwa wanalanguliwa gunia moja la mahindi lilikuwa likiuzwa kuanzia shilingi elfu 20,000 hadi 30,000 lakini kwa ujenzi wa daraja hili wananchi wanaweza kuuza mahindi kuanzia elfu 50,000 hadi 60,000 kwa gunia moja” amesema Aboubakar  Mohamed.
Naye Mkulima wa Kijiji hicho Zena Mpinga ameeleza  kuwa, “kabla ya ujenzi wa daraja hilo wanawake na wamama wajawazito walikuwa wakisafiri kwa shida na kwa gharama kubwa sana ambapo ukisafiri kwa kutumia pikipiki maarufu kama “bodaboda” ilikuwa ni shilingi elfu 10,000 kutokana na ukosefu wa kivuko imara na bora na kulazimu kuzunguka na pikipiki kijiji jirani ila kwa sasa usafiri wa bodaboda ni shilingi elfu 2000 hadi 3000 tu inakufikisha na kuweza kukamilisha mahitaji yako kwa wakati.
Programu ya Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), inaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kutekelezwa katika Halmashauri 76 za Tanzania Bara na Zanzibar, ikiwa  imegharamiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (IFAD) na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (ADB) kwa kushirikiana na  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Read More

Monday, March 5, 2018

WAZIRI MKUU AKUTANA NA BALOZI WA UFARANSA NCHINI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Frederic Clavier, kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Machi 5, 2018.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Frederic Clavier, kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Machi 5, 2018

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Frederic Clavier (katikati), kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam, Machi 5, 2018, kushoto ni mwakilishi mkazi wa Nchi ya Ufaransa, Emanuel Baudran.

Read More

Sunday, March 4, 2018

WAZIRI MKUU ASHIRIKI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI MATAMBALALE

 Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akichanganya udongo wa tofali, wakati akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari Matambalale, katika kata ya Matambalale,Wilayani Ruangwa. Machi 4, 2018,

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akiweka udongo wakati akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari Matambalale, katika kata ya Matambalale,Wilayani Ruangwa. Machi 4, 2018,

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akiweka udongo wakati akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari Matambalale, katika kata ya Matambalale,Wilayani Ruangwa. Machi 4, 2018,

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akiweka udongo wakati akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari Matambalale, katika kata ya Matambalale,Wilayani Ruangwa. Machi 4, 2018,

Read More

WAZIRI MKUU AKIWA SIZARANI JIMBONI RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akiwa kwenye picha ya pamoja na wazee Omar Issa kulia na mzee Mussa Lambamba katikati, katika Kata ya Narungombe, Wilayani Ruangwa, Suleiman Likuche Waziri Mkuu yupo Wilayani ruangwa kwenye Ziara yake ya kikazi jimboni, katikati ni mzee Mussa Lambamba. Machi,3 2018,
Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akisalimiana na Diwani wa kijiji cha Chikwale kata ya Mbwemkulu, Wilayani Ruangwa, Suleiman Likuche, Waziri Mkuu yupo Wilayani ruangwa kwenye Ziara yake ya kikazi jimboni. Machi,3 2018.

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chikwale kata ya Mbwemkulu, Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu yupo Wilayani ruangwa kwenye Ziara yake ya kikazi jimboni. Machi,3 2018.

Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akizungumza na mzee Omar Issa, katika Kata ya Narungombe, Wilayani Ruangwa, Suleiman Likuche Waziri Mkuu yupo Wilayani ruangwa kwenye Ziara yake ya kikazi jimboni, katikati ni mzee Mussa Lambamba. Machi,3 2018.
Read More

WAZIRI MKUU AKABIDHI PIKIPIKI MBILI KWA JESHI LA POLISI

 Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akikabidhi pikipiki mbili kwa Kamanda Mkoa wa Lindi, ACP. Pudensiana Protas, zilizotolewa na kampuni ya WU ZHOU Investment Company kwa Jeshi la Polisi, wakati alipo tembelea kituo hicho jana, Machi 4, 2018 , Wilayani Ruangwa. 
 Waziri Mkuu, Kassim.Majaliwa akikabidhi pikipiki mbili kwa Kamanda Mkoa wa Lindi, ACP. Pudensiana Protas, zilizotolewa na kampuni ya WU ZHOU Investment Company kwa Jeshi la Polisi, wakati alipo tembelea kituo hicho jana, Machi 4, 2018 , Wilayani Ruangwa. 



Read More

Thursday, March 1, 2018

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI MBECHA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la Zahanati, iliyopo  katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, iliyojengwa kwa ufadhili wa Taasisi ya African Relief Organization, wa kwanza kushoto ni Sheikh Abdallah Ndauga (wapili kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya African Relief Organization Sheikh Ibrahim Yusuf, na kulia ni mke wa Waziri Mkuu Mary Majaliwa, Machi 1, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Gasper Byakanwa, katika kijiji cha Mchenganyumba Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwara Februari 28, 2018,

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na Mkewe Mary Majaliwa, wakiwasalimia watoto wa shule ya msingi Mbecha, katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu yupo Wilayani humo kwa ziara ya kikazi jimboni, Machi 1, 2018.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya African Relief Organization Sheikh Ibrahim Yusuf, iliyojenga Zahanatiiliyopo  katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, Machi 1, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsalimia mtoto Shafii Khamis, katika kijiji cha Mtakuja, Kata ya Nanganga Wilayani Ruangwa, Machi 1, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akuzungumza na wananchi wa kijiji cha Mtakuja, Kata ya Nanganga Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu yupo Wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi jimboni, Machi 1, 2018.

Read More