Tuesday, November 27, 2018

MAJALIWA AWASILI CHATO KUANZA ZIARA YA MKOA WA GEITA

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Geita,  Mhandisi Robert Gabriel wakati alipowasili kwenye Kiwanja  cha Ndege cha Chato kuanza ziara ya kazi mkoani Geita, Novemba 27, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Waziri wa Nishati na Mbunge wa Chato, Dkt. Medard Kalemani wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Chato kuanza ziara ya mkoa wa Geita Novemba 27, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi waliojitokeza kumlaki wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Chato kuanza ziara ya Kazi mkoani Geita, Novemba 27, 2018.  Wapili kushoto ni Waziri wa Nishati na Mbunge wa Chato, Dkt. Medard Kalemani, kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI,  George Mwita Waitara na Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na mtoto, Naomi Nkingwa ambaye alishirkiana na wanakwaya wa Kikundi cha Mwagazege cha Chato kumwimbia wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha ndege cha Chato kuanza ziara ya kazi Mkoani Geita, Novemba 27, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj  Said Kalidushi wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Chato kuanza ziara ya kazi mkoani Geita, Novemba 27, 2018.  Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt. Medard Kalemani wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Chato kuanza ziara ya Kazi Mkoani Geita, Novemba 27, 2018. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj Said Kalidushi.
Read More

MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI WA GEITA.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Geita  kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Novemba 27, 2018. Kulia ni Mbunge wa Chato na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita,  Mhandisi Robert Gabriel.

Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Geita wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Novemba 27, 2018.


Read More

WAKUU WA MIKOA, WILAYA NA WAKURUGENZI SIMAMIENI UWAJIBIKAJI-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wahakikishe wanasimamia vizuri uwajibikaji na utowaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo yao bila ya woga. 

Kadhalika, Waziri Mkuu amemtaka kila mtumishi wa umma nchini awajibike katika kufanya kazi kwa bidii na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano haitowavumilia watumishi ambao ni wezi, wabadhilifu, wavivu  na haitosita kuwachukulia hatua.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na watumishi, viongozi wa mkoa, wilaya ya Geita na taasisi za umma katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Mamlaka ya Mji Geita.

“Watumishi fanyeni kazi kwa bidii na msitarajie kuundiwa tume pale mnapofanya vibaya, ukiharibu kazi tunakushughulikia hapo hapo na huu ndio msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.”

Waziri Mkuu aliwaeleza watumishi hao kuwa wanatakiwa wafanye kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni za kazi na pia watambue dhamana kubwa waliyonayo, ambayo ni kuwahudumia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza watumishi wa umma hususani Wakuu wa Idara wahakikishe wanakuwa na kitabu cha Ilani ya Uchanguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili wapate muelekeo wa utekelezaji washughuli zao.

Waziri Mkuu amesema kitabu cha Ilani ya uchanguzi cha CCM 2015/2020 kina maelekezo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo kila idara inatakiwa kuangalia maelekezo yaliyotolewa kuhusu idara husika na kuyafanyia kazi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alimuhakikishia Waziri Mkuu kwamba yeye kwa kushirikiana na viongozi wenzake watayafanyia kazi maelekezo yote ambayo ameyatoa.

 (mwisho)
Read More

SERIKALI IMEJIPANGA KUMALIZA TATIZO LA MAJI NCHINI-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepanga kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa kuchimba visima virefu na vifupi pamoja na kutumia maji ya maziwa na mito na kuyapeleka katika maeneo mbalimbali ya wananchi nchini. 

Pia, Waziri Mkuu amewaagiza wakuu wa wilaya kusimamia uhifadhi wa maeneo ambayo yana vyanzo vya maji ili kuyafanya yaendelee kuwa chepechepe, hivyo kuhakikisha vijiji vyote vinapata maji ya uhakika. “Lazima maeneo hayo yatambuliwe na yahifadhiwe.”

Ameyasema hayo leo (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa shule Sekondari Bugando kata ya Nzera wilayani Geita, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi za siku nne mkoani Geita.

Waziri Mkuu amesemaSerikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yao ya makazi.

Amesema Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kila kijiji kinapata huduma ya maji safi na salama, hivyo amewaagizawatendaji wote wa vijiji kuainisha maeneo yote yenye misitu na vyanzo vya maji na kuhakikisha yanalindwa.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema mbali na huduma ya maji, pia Serikali imedhamiria kusambaza umeme katika vijiji vyote ambavyo bado havijaunganishiwa nishati hiyo nchini vitaunganishiwa katika awamu ya tatu ya Mradi wa Nishati Vijijini (REA).

“Rais wetu Dkt. John Magufuli anataka kuona nyumba ya kila Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu na ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema  wananchi hawatowajibika tena katika kulipia gharama za nguzo wala fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na Serikali.

Naye, Mbunge wa jimbo la Geita Vijijini, Joseph Musukuma ameishukuru Serikali kwa utekelezaji wa miradi na ahadi zikiwemo na zile zilizotolewa za Rais Dkt. John Magufuli. “Nashukuru Serikali pia kwa kutuzindulia hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Geita.”

Kuhusu suala la umeme, Mbunge huyo ameishukuru Serikali kwa kuwa vijiji vyake vyote vimeshaunganishiwa umeme isipokuwa vitongoji vichache, ambapo ameomba navyo viunganishiwe nishati hiyo muhimu kwa maendeleo ya wananchi.

Awali,Waziri Mkuu alikagua na kuzindua hospitali ya wilaya ya Geita inayojengwa katika kata ya Nzera na aliupongeza uogozi wa halmashauri ya wilaya ya Geita kwa hatua waliyofikia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
(mwisho)
Read More

MAJALIWA AZINDUA MRADI WA MAJI WA IMALABUPINA - ICHWANKIMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Viongozi wa Dini wakati alipowasili kwenye  eneo la Mradi wa Maji wa Imalabupina - Ichwankima kuweka jiwe la msingi la Mradi huo wilayani Chato, Novemba 27, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa Mradi wa Maji wa Imalabupina - Ichwankima wilayani Chato Novemba 27, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mwita Waitara na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandishi Robert Gabriel.

Read More

MAJALIWA AZINDUA KITUO CHA AFYA CHA BWANGA WILAYANI CHATO



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole  Bibi Jenifer Erasto  aliyelazwa katika wodi ya wazazi  kwenye  Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato wakati alipotembelea Kituo hicho na Kuweka Jiwe la Msingi la  Maradi wa Ukarabati wa Kituo, Novemba 27, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi baada ya kukagua  na Kuzindua Ukarabati wa Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato, Novemba 27, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la Msingi la Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato, Novemba 27, 2018. Watatu kulia ni Waziri wa Nishati na Mbunge wa Chato, Dkt. Medard Kalemani  na wapili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mwikwabe Mwita Waitara. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi  Robert Gabriel na wapili kushoto ni  Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj  Said Kalidushi.

Read More

Monday, November 26, 2018

SERIKALI YAZINDUA VIZA NA VIBALI VYA UKAAZI VYA KIELEKTRONIKI

  
*Yawataka watakaopewa kufanya shughuli zilizoelekezwa kwenye vibali vyao

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezindua huduma za viza na vibali vya ukaazi vya kielektroniki na amewataka watu wote watakaopewa vibali hivyo kutii sheria kwa kufanya shughuli ambazo wameelekezwa kwa mujibu wa vibali vyao na si vinginevyo.

Amesema utoaji wa huduma hizo ni miongoni mwa jitihada za Serikali katika kuvutia uwekezaji, hususan katika sekta ya viwanda kwani hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa vibali hivyo kwa raia wa kigeni na kuchochea kasi ya maendeleo ya kiuchumi.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Novemba 26, 2028) wakati akizindua huduma za viza na vibali vya ukaazi vya kielektroniki katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam na kwamba hatua hiyo itasaidia kuondoa urasimu na ucheleweshwaji wa huduma pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi.

Amesema Idara ya Uhamiaji inatarajia kuanza kutoa huduma tajwa kwa raia wa kigeni muda wowote kuanzia sasa na kwa kupitia huduma hiyo, raia wa kigeni wataweza kuomba vibali hivyo kwa njia ya kielektroniki wakati wowote na mahali popote walipo.

Waziri Mkuu amesema watakaopewa vibali wanatakiwa kufanya shughuli zao kwa mujibu wa vibali vyao kwa sababu kufanya shughuli tofauti na ilivyoainishwa kwenye kibali ni kosa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Uhamiaji.

Amesema matumizi ya mtandao katika utoaji wa huduma za viza na vibali vya ukaazi ni hatua ya mfano, kwani inakwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na teknolojia na sera ya Serikali ya matumizi ya TEHAMA katika shughuli za Serikali (e-government).

Amesema Serikali inatarajia kuwa, matumizi ya mifumo hiyo itaongeza ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa kuwa mteja ataweza kulipia huduma hizo mwenyewe moja kwa moja pasipo kupitia kwa mawakala au mtu yeyote.

“Natoa wito kwa Maafisa, Askari pamoja na Watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji kuhakikisha kuwa mifumo hiyo inatunzwa pamoja na kuendeleza miundombinu yote ya kiutendaji.” 

Waziri Mkuu amesema kwa kuzingatia ahadi ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ya kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi na raia wa kigeni, Maafisa Uhamiaji wanatakiwa kutoa huduma hiyo kwa wakati, weledi na kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Uhamiaji.

Amesema mfumo wa huduma hizo utaunganishwa na mifumo mingine ya Serikali, ambayo inatoa huduma kwa wananchi na wageni kama vile Mifumo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Idara ya Kazi – Ofisi ya Waziri Mkuu, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mfumo wa Malipo ya Serikali Kimtandao (GePG). 

 (mwisho)
Read More

MAJALIWA AZINDUA VIZA NA VIBALI VYA UKAAZI VYA KIELEKTRONIKI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Nchini, Dkt. Anna Makalala wakati alipowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam  Kuzindua  Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki , Novemba 26, 2018.  Katikati ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Viongozi wa Idara ya Uhamiaji wakati alipowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam kuzindua Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektrtoniki,  Novemba 26, 2018.

Baadhi  ya Washiriki wa Uzinduzi wa  Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza kabla ya uzinduzi huo kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam , Novemba 26, 2018.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza katika uzinduzi wa Viza na Vibali  vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha Mikutano cha  Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam,  Novemba 26, 2018.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa Viza na Vibali  vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa  cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam,  Novemba 26, 2018. 

Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji, Dkt. Anna Makalala akizungumza katika uzinduzi wa Viza na Vibali  vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa  cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam,  Novemba 26, 2018.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi, Hamamad Masauni akizungumza katika uzinduzi wa Viza na Vibali  vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa  cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam,  Novemba 26, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua  Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua  Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizindua Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga,  kulia ni  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamad  Masauni na wapili kulia ni Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji, Dkt. Anna Makalala.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde baada ya Kuzindua Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki  kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  Nchini (TAKUKURU)  Kamishaina wa Polisi, Diwani Athumani baada ya Kuzindua Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mstaafu, Augustino Ramadhani baada ya Kuzindua Viza na Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius  Nyerere jijini Dar es salaam, Novemba 26, 2018. 

Read More

WAZIRI MHAGAMA ATEMBELEA KIWANDA CHA MATAIRI CHA GENERAL TYRE ARUSHA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akieleza jambo kwa watendaji wa NSSF wakati wa ziara yake katika kukagua sehemu ya miradi yenye hisa za shirika hilo ikiwemo kiwanda cha General tyre.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiuliza jambo kwa Mkurugenzi wa Uwekezaji NSSF Bw.Gabriel Silayo (wa kwanza kushoto) wakati wa ziara yake katika moja ya mradi wenye hisa za shirika hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama (katikati) akiwa katika ziara yake katika kiwanda cha matairi cha General Tyre Arusha.wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Uwekezaji NSSF Bw.Gabriel Silayo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama pamoja na Watendaji kutoka NSSF na baadhi ya viongozi wa kiwanda cha Matairi cha General Tyre wakiangalia hali ya miundombimu katika kiwanda hicho.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiangalia malighafi zinazotumika kutengeneza matairi na zilizohifadhiwa katika chumba maalumu katika kiwanda hicho.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiweka saini katika kitabu cha wageni katika ofisi za kiwanda cha General Tyre alipotembelea kukagua miradi yenye hiza NSSF pamoja na kuona hali halisi ya kiwanda hicho.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiangalia moja ya tairi lilipo katika kiwanda cha Matairi cha General Tyre Arusha wakati wa ukaguzi wa Miradi yenye hisa NSSF tarehe 26 Novemba, 2018.

Read More

Sunday, November 25, 2018

MAJALIWA AZINDUA KAMPENI YA SIKU 16 YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA JIJINI DODOMA.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wapili kulia), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto)  na   Mratibu wa Kitaifa wa Shirika la  Wanawake Katika Sheria  na Maendeleo Barani Afrika ( WILDAF), Anna Kulaya  wakati alipowasili kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kuzindua Kampeni ya Siku  16 ya Kupinga Ukatili  wa Kijinsia, Novemba 25, 2018.

Baadhi ya wananchi wakimsikiliza  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozindua kampeni ya Siku 16 ya Kupinga Ukatili wa Kijinsia kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Novemba 25, 2018. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wapili kulia), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto)  na   Mratibu wa Kitaifa wa Shirika la  Wanawake Katika Sheria  na Maendeleo Barani Afrika ( WILDAF), Anna Kulaya  wakati alipowasili kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kuzindua Kampeni ya Siku  16 ya Kupinga Ukatili  wa Kijinsia, Novemba 25, 2018.

Read More

MAJALIWA AKUTANA NA MWENYEKITI WA BARAZA LA TAIFA LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI, DKT. FESTUS LIMBU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokutana na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Dkt. Festus Limbu (watatu kulia)  na baadhi ya Watendaji wa Baraza hilo, Ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Novemba 24, 2018.  Wapili kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,  Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama na kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi,  wapili kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Baraza, Suleiman Malela na kulia ni Mchumi wa Baraza, Erad Mushi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokutana na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Dkt. Festus Limbu (watatu kulia)  na baadhi ya Watendaji wa Baraza hilo, Ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Novemba 24, 2018.  Wapili kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,  Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama na kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi,  wapili kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Baraza, Suleiman Malela na kulia ni Mchumi wa Baraza, Erad Mushi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimina na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Dkt. Festus Limbu kabla ya mazungumzo  yao yaliyowashirikisha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mainuna Tarishi na Watendaji wa Baraza. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Novemba 24, 2018.

Read More

Friday, November 23, 2018

TUTAENDELEA KUSHIRIKIANA NA VYUO VIKUU VYOTE NCHINI-MAJALIWA



*Asisitiza lengo ni kuona vikitoa elimu yenye kukidhi ubora na viwango 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikiano na miongozo kwa vyuo vikuu vyote nchini, vya binafsi na vya umma ili viendelee kutoa elimu ya juu yenye ubora na viwango vinavyotakiwa kwa lengo la kukidhi matakwa na ushindani kwenye soko la kitaifa na kimataifa. 

Amesema suala hilo ni muhimu likapewa uzito unaostahili kwani wahitimu hao wakitoka vyuoni wanakwenda kutoa huduma katika jamii ya Watanzania na pia ya kimataifa, hivyo ni muhimu elimu inayotolewa ikazingatia ubora na viwango vinavyostahiki.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Novemba 23,2018) kwenye mahafali ya tisa ya chuo kikuu cha Mtakatifu Yohana cha Tanzania Kampasi ya Chifu Mazengo, Dodoma yaliyofanyika kwenye ukumbi wa CCM.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, inatambua na kuthamini mchango wa Sekta Binafsi hususan wa vyuo vikuu binafsi kama Chuo Kikuu cha Mtakatifu Yohana cha Tanzania, katika maendeleo ya elimu ya juu. 

“Serikali inatambua mchango wa vyuo hivyo katika kupanua fursa kwa Watanzania wengi kupata elimu ya juu, ambapo hadi sasa udahili wa wanafunzi wa elimu ya juu kwenye vyuo vikuu binafsi nchini ni takriban asilimia 25 ya wanafunzi wote.”

Amesema Serikali inatambua mchango wa chuo kikuu cha Mtakatifu Yohana cha Tanzania katika kutayarisha watalaamu wa fani mbalimbali. Aidha, tangu kuanzishwa kwake mwaka 2007, chuo hicho kimetoa wahitimu zaidi ya 10,000.

Amesema kati ya wahitimu hao wapo Wafamasia, Wauguzi, Walimu wa Sayansi, Walimu wa Sanaa, Wataalamu wa Maabara, na Wasimamizi na Waendeshaji wa fani mbalimbali kama Utawala, Masoko na Wahasibu, mchango ambao unahitajika kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa uchumi wa Taifa katika nyanja tajwa.

Waziri Mkuu amesema baadhi ya wahitimu watapata ajira lakini si kila mhitimu atapata fursa ya kuajiriwa, hivyo Serikali itaendelea kuunga mkono azma yao kama chuo kikuu ya kutoa wahitimu wenye tabia, utashi na uwezo wa kutengeneza kazi na siyo watafuta kazi tu.


Akizungumzia kuhusuchangamoto zinazokabili sekta ya elimu ya juu, amesema baadhi ya changamoto zinafanana katika vyuo vikuu vyote nchini na pia zipo changamoto zinazokabili vyuo vikuu binafsi na wakati mwingine zipo changamoto zinazohusu chuo kikuu kimoja kimoja. 

Amesema moja ya changamoto kubwa katika elimu ya Juu ni uhaba wa Wahadhiri wenye sifa stahiki ili kuendana na ongezeko la wanafunzi wanaojiunga na vyuo vyao. “Nafahamu jitihada ambazo vyuo vikuu binafsi vinafanya katika kuendeleza Rasilimali Watu wao na hasa katika eneo la taaluma ili viwe na Wahadhiri na Maprofesa wa kutosha.” 

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito vyuo vingine binafsi nchini viwekeze katika eneo la kuendeleza Rasilimali Watu kwa bidii zaidi na kwa upande wa Serikali, ipo mikakati mbali mbali ya kuajiri lakini pia kusomesha wale waliopo kazini ili kufikia viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa. 

Waziri Mkuu amesema changamoto nyingine inayovikabili vyuo vikuu ni miundombinu ya kufundishia na kujifunzia kama vile mabweni na nyumba za watumishi, hivyo kusababisha baadhi ya vyuo  kushindwa kukidhi matakwa ya ithibati zao na kuzuiwa kufanya udahili au kufungiwa kabisa.

“Ni kweli tunahitaji Watanzania wengi wapate elimu ya juu kwenye vyuo vyetu vikuu. Hata ninyi wanafunzi, mngependa kupata elimu iliyo bora itakayoweza kuwasaidia maishani na itakayowakomboa kifikra, itakayowapa ujuzi na maarifa ya kupambana na changamoto za maendeleo. Kila mmoja anataka elimu bora na si bora elimu.” 

Waziri Mkuu amesema kuwa dhamira hiyo ndiyo inayoifanya Serikali kupitia Tume ya Vyuo Vikuu kuhakikisha kuwa vyuo vyote visivyokidhi matakwa ya ithibati yao haviendelei kutoa mafunzo ya aina yoyote. “Nitoe rai kwa vyuo vikuu vyote vizingatie matakwa ya ithibati zao ili viweze kutoa elimu iliyo bora itakayokidhi matamanio ya Watanzania na ushindani wa soko la ndani na nje.”

Kuhusu Chuo Kikuu cha Mtakatifu Yohana cha Tanzania ambacho kimeomba kuruhusiwa kufanya udahili baada ya kufungiwa, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako kujiridhisha iwapo chuo hicho kimekidhi vigezo kabla ya kukipa kibali cha kudahili wanafunzi wapya.

(mwisho)
Read More

WAZIRI MKUU AHUDHURIA MAHAFALI YA SAINT JOHN

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu, Wizara wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa. James Mdoe, katika Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwasili kwenye Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) yaliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018.

Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  katika Mahafali ya Tisa ya Chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018.

Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  katika Mahafali ya Tisa ya Chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia Wahitimu, kwenye Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018. 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia Wahitimu, kwenye Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018. 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia Wahitimu, kwenye Mahafali ya Tisa ya Chuo Kikuu cha Saint  John (SJUT) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 23, 2018. 

Read More