Tuesday, January 14, 2020

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI, KWENYE UAPISHO WA RAIS WA MSUMBIJI, FILIPE NYUSI.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Benjamin Mkapa, wakati akiondoka nchini, katika uwanja wa Julius Nyerere, kuelekea Msumbiji kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli, kwenye uapisho wa Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi. Januari 14, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, leo Januari 14, 2020 ameondoka nchini kwenda Msumbiji, ambako atamwakilisha Rais John Pombe Magufuli, kwenye uapisho wa Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi. Kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Benjamin Mkapa, ambaye pia yupo katika msafara huo.


Read More

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA, AZINDUA JENGO LA MAHAKAMA YA WILAYA YA RUANGWA, MKOANI LINDI.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiweka jiwe la msingi la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, mkoani Lindi, kushoto Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa, Ibrahim Juma. Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akipeana mkono na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa, Ibrahim Juma, baada ya kuweka jiwe la msingi la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, iliyopo mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikata utepe, wakati alipozindua jengo la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikagua Jengo la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, baada ya kuzindua rasmi jengo hilo, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikagua Jengo la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, baada ya kuzindua rasmi jengo hilo, Januari 13, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya ruangwa, baada ya kuzindua Jengo la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya ruangwa, baada ya kuzindua Jengo la Mahakama ya Wilaya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akimwagilia mti, mara baada ya kuupanda, kwenye uzinduzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.

Read More

MAHAKAMA KAMILISHENI UJENZI WA MIUNDOMBINU-MAJALIWA



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa uongozi wa Mahakama nchini uhakikishe unakamilisha ujenzi wa miundombinu ya Mahakama ili kuwapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu na kutumia gharama kubwa katika kutafuta haki zao.

Amesema kuna wilaya 139 Tanzania Bara, kati ya wilaya hizo wilaya 111 zilizo na huduma ya Mahakama za Wilaya na wilaya nyingine 28 bado zinahudumiwa na Mahakama za Wilaya za jirani ambazo zimepewa mamlaka ya kisheria kuhudumia Mahakama zisizo na majengo ya Wilaya.

Ametoa wito huo leo (Jumatatu, Januari 13, 2020) wakati akizindua jengo la Mahakama ya wilaya ya Ruangwa. Amesema ni vema uongozi wa Mahakama uhakikishe kuwa yale yote waliyojipangia kwenye mpango wao wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Miundombinu ya Mahakama 2016/17 – 2020/21 unatekelezwa kwa wakati.

Waziri Mkuu amesema kabla ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Wilaya Ruangwa mwaka 2009, wananchi wa wilaya hiyo walilazimika kusafiri umbali wa kilomita 180 kufuata huduma za mahakama wilayani Lindi. Mahakama hiyo itarahisisha upatikanaji wa haki wilayani Ruangwa.

“Umbali huo mrefu ulisababisha wananchi wengi kupoteza muda mwingi ambao wangeutumia kwa shughuli za uzalishaji mali.  Wakati mwingine wananchi hao walikosa haki zao kwa kushindwa kumudu gharama za usafiri kuhudhuria mashauri yao wilayani Lindi.”

Waziri Mkuu amesema Mahakama ni muhimu katika kudumisha amani na kuleta maelewano ndani ya nchi au jamii ambayo huwa ni kichocheo cha shughuli za kiuchumi, hivyo ameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kuamua kujenga Mahakama hiyo Wilayani Ruangwa pamoja na sehemu nyingine nchini.

Amesema kupitia Mahakama, migogoro mingi hupata usuluhishi na hivyo kuimarisha hali ya amani na utulivu.  “Kwa lugha nyingine,Mahakama inapokuwa imara Taifa letu huvutia uwekezaji kwa kuwa wawekezaji wanakuwa na uhakika na usalama wao pamoja na mali zao. 

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Serikali kwa upande wake itaendelea kushirikiana na Mahakama kuhakikisha kuwa mipango yake iliyojiwekea inatekelezwa kama ilivyokusudiwa, kwani bado kuna kazi kubwa mbele yao.

Wakati hu huo, Waziri Mkuu ameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kukusanya mapato kupitia mfumo wa Kielekitroniki wa Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali (Government electronic Payment Gateway, GePG) kwani Serikali ilielekeza kila taasisi itumie mfumo huo ili kupunguza mianya ya rushwa na upotevu wa fedha.

Amesema amefurahi kusikia kuwa kwa kutumia mfumo wa GePG, Mahakama iliweza kuongeza kiwango cha makusanyo kutoka sh. bilioni 1.6 mwaka 2017 hadi sh. bilioni 2.5 mwezi Desemba 2019 baada ya kuanza kutumia GePG. “Fedha hizi zitatumika kuchangia ujenzi wa mahakama na miundombinu mingine ya kiuchumi unaoendelea katika kila kona nchini.”

“Ni ukweli usiofichika kwamba hata wananchi nao wanafarijika kuona kuwa kile mnachowatoza kinaenda moja kwa moja kwenye mfuko mkuu wa Serikali, na baadaye kiasi fulani kinarudi kwenu kujenga miundombinu ya kisasa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.”

Waziri Mkuu amesema kuwa hayo ndiyo malengo na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli. “Aidha, kwa kufanya hivyo, mnachangia utekelezaji wa malengo yaliyoainishwa vema kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025.”

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma amesema kwa muda mrefu, Mahakama ya Tanzania imekuwa ikikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba, na uchakavu wa majengo katika ngazi zote za Mahakama, yaani Mahakama za Mwanzo, Mahakama za Wilaya, Mahakama za Hakimu Mkazi (Mahakamaza Mikoa), Mahakama Kuu na hata Mahakama ya Rufani.

Amesema ili kukabiliana na ukubwa wa changamoto ya upungufu na uchakavu wa majengo yake, Mahakama ya Tanzania ilitayarisha Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Miundombinu (2016-2021). “Mpango huu umetathmini hali ya majengo ya Mahakama katika Mikoa na Wilaya zote za Tanzania Bara.”
Jaji Mku amesema mpango huo umelenga kupunguza au kuondoa kabisa uhaba na uchakavu. Jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa ni kielelezo cha utekelezaji wa Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Miundombinu ya Mahakama ya Tanzania. 
 
Pia, Jaji Mkuu ametumia ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa watumishi wa Mahakama, majengo kwamba hayo ya kisasa na miundombinu bora, iambatane na upatikanaji wa huduma bora kwa mwananchi. 
“Kila mtumishi wa Mahakama (kama walivyo watumishi wote wa umma) anao Mkataba na watumiaji wa huduma za Mahakama. Kipimo chetu cha kutimiza masharti ya Mkataba huu, ni nguzo ya pili ya Mpango Mkakati wa Mahakama ambayo ni ‘Upatikanaji na Utoaji wa Haki kwa Wakati’, hivyo siku zote watumishi wa Mahakama tukumbuke kuwa Mahakama hii ni mali ya wananchi na wananchi wana haki ya msingi ya kupata huduma iliyo bora kwa wakati.” 

Amewasihi watumishi wa Mahakama ya Wilaya Ruangwa na Mahakama nyingine hapa nchini kuacha kabisa mienendo na tabia ambazo zinakiuka miiko na maadili ya kazi kwa watumishi wa umma. “Jengo hili lisiwe na mianya au viashiria vya ukosefu wa maadili.”
Read More

Monday, January 13, 2020

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA, AZINDUA JENGO LA TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA (TAKUKURU) WILAYANI RUANGWA.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya ruangwa, wakati wa uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), lililopo katika Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya ruangwa, wakati wa uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), lililopo katika Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, wakati alipozindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiweka jiwe la msingi, wakati alipozindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikata utepe, wakati alipozindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, wakati alipozindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, akizungumza na wananchi wa Wilaya ya ruangwa, wakati wa uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), lililopo katika Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brig. Jenerali John Mbungo, wakati alipozindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akipanda mti, baada ya kuzindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 13, 2020.


Read More

TAKUKURU KAMILISHENI UCHUNGUZI MAPEMA-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Taasisi ya Kuzua na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ukamilishe mapema uchunguzi dhidi ya madudu yaliyoibuliwa katika mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 na wizi uliofanywa na viongozi wa AMCOS kwa wakulima wa ufuta na korosho ikiwemo wilaya ya Ruangwa.

Ameyasema hayo leo wakati akizindua jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Ruangwa lililogharimu zaidi ya sh. milioni 142. Ametoa wito kwa TAKUKURU kuwa imara na kuweza kutembea kifua mbele katika mapambano hayo. 

Waziri Mkuu amesema  pamoja na TAKUKURU kuendelea na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku pia ameuagiza uongozi wa taasisi hiyo ukamilishe mapema utekelezaji wa maagizo mbalimbali ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoyatoa kwao kwa nyakati tofauti.

Amesema ameshuhudia kazi nzuri waliyoifanya na wanayoendelea kuifanya kupitia uchunguzi na ufuatiliaji wa madai ya malipo ya wakulima wa zao la ufuta na korosho.“Kamilisheni chunguzi hizi zote kwa wakati ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya wale wote waliopatikana na hatia.”

Amesema rushwa huathiri utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. “Kutokana na ukweli huo, Serikali imetoa msukumo wa pekee katika kushughulikia vitendo vya rushwa na ufisadi. Msukumo huo, umechangia kwa kiasi kikubwa hususan katika kipindi hiki, utekelezaji wa miradi mikubwa na ya kimkakati kwa ufanisi na kwa wakati.” 

Amesema wananchi wanatakiwa wafahamu kwamba kwamba nchi yoyote ambayo rushwa imetamalaki siyo rahisi kuwa na uwezo wa kiuchumi utakaoiwezesha nchi hiyo kumudu kulipa madeni ya ndani na ya nje. “Hata hivyo, kwa upande wa Tanzania tunashuhudia jinsi Serikali ya awamu ya tano inavyolipa madeni.” 

Kwa mfano, kati ya Julai na Septemba, 2019, sh. bilioni 85.72 zimetolewa ikiwemo bilioni 50 za madai ya pensheni; bilioni 22 za madai ya watumishi wa umma ikiwemo kiinua mgongo kwa wastaafu 3,019 na malimbikizo ya mishahara kwa watumishi 1,435; bilioni 10.24 zimelipa watoa huduma na zaidi ya bilioni 2 kwa ajili ya wakandarasi na wahandisi washauri. Hayo ni matokeo ya jitihada za kupambana na rushwa zinazofanywa na Serikali.

Amesema tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, imekuwa ikijipambanua na vita dhidi ya rushwa na ufisadi. Hivyo, kitendo hicho cha kuendelea kulipa madeni ni ishara ya mafanikio ya Serikali katika jitihada zake za kuzuia na kupambana na rushwa nchini. Serikali itaendelea kudhibiti mianya yote ya rushwa katika utendaji mzima wa Serikali.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema tafiti za hivi karibuni zilizofanywa na wadau wa mapambano dhidi ya rushwa na Utawala Bora kama vile Transparency International (TI), MO Ibrahim na Afrobarometer zinaonesha kuwa kwa miaka mitatu mfululizo, yaani 2016 hadi 2018 Tanzania imeendelea kufanya vyema katika mapambano dhidi ya rushwa na utawala bora. 

Amesema mafanikio hayo ya kujivunia ni jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kusimamia kwa dhati mapambano dhidi ya rushwa kwa usimamizi wa Taasisi ya Kuzua na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambayo ndicho chombo kilichopewa dhamana kisheria. 


“Tambueni kwamba uongozi mzima wa juu kabisa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Makamu wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu) uko pamoja nanyi katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi. 

Pia ameagiza kuanzishwa kwa vilabu vya kupambana na rushwa katika shule ili wanafunzi waweze kuwa na uelewa na kuweza kutoa taarifa za rushwa. 

Akizungumzia kuhusu jengo alilolizindia amesema muhimu sana kwa taasisi nyeti kama ya TAKUKURU kumiliki majengo yake yenyewe. Kuhusu hali ya majengo ya ofisi za TAKUKURU katika ngazi ya mikoa na hata wilaya, amemwagiza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa alishughulikie suala hilo.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo amesema jengo hilolimejengwa kwa muda wa miezi saba kuanzia tarehe 11/06/2018 na kukamilika tarehe 25/01/2019.Hadi kufikia hatua hii ya uzinduzi, jengo hili limegharimu jumla ya Sh. 142,857,142.86.”
Akizungumzia kuhusu uchunguzi kiongozi huyo amesema kwa kipindi cha mwaka 2019 TAKUKURU imefanya uchunguzi kwenye tuhuma kubwa ikiwemo ya utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Magufuli aliyoyatoa Jumanne Oktoba 15, 2019 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Ruangwa.

“Kupitia uchunguzi ule, tumebaini kwamba zaidi ya vyama 30 vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) vya Mkoani Lindiviliwadhulumu wakulima wa zao la ufuta kiasi cha zaidi ya sh.Bilioni sh. 1.23.  Kupitia uchunguzi huo tuliwakamata na kuwahoji zaidi ya viongozi 300 wa AMCOS zilizokuwa zinahusika katika dhuluma hii. Tulifanikiwa kuokoa zaidi ya sh. bilioni 1.042. Fedha hizi zilikuwa ni mali ya wakulima wa ufuta ambao walidhulumiwa fedha hiyo na Viongozi wa Vyama vya AMCOS.”

Kadhalika Brigedia Jenerali Mbungoamesema pamoja na kufanikiwa kujenga majengo ya ofisi za TAKUKURU katika wilaya saba bado inakabiliwa na uhaba wa majengo ya kudumu ya ofisi. Amesema TAKUKURU ina jumla ya ofisi 28 za mikoa na ofisi 117 za wilaya huku mahitaji halisi ni majengo 28 kwa ofisi za Mikoa na majengo 117 kwa ofisi za wilaya. 
Naye, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuendeleza mapambazo dhidi ya rushwa, hivyo uzinduzi wa jengo hilo ni miongozi mwa harakati hizo.

Read More

Thursday, January 9, 2020

WAZIRI MKUU AFUTA MNADA WA NAFAKA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefuta mnada wa nafaka ulioendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Januari 7, 2020 na kuuagiza uongozi wa mamlaka hiyo kutangaza upya zabuni baada ya kutoridhishwa na taratibu zilifanyika awali.

Mnada huo ambao unahusisha mahindi tani 5,000 na ngano tani 460.12 unafanyika baada ya wahusika kushindwa kutimiza masharti ya kiforodha, hivyo Serikali imeamua kuuza ili kufidia gharama zake. Nafaka hizo ziliingia nchini Machi 2017.

Waziri Mkuu amesitisha mnada huo leo (Alhamisi, Januari  9, 2020) wakati akizungumza na Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa wa TRA, Bw. Ben Asubisye, ofisi ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni Jijini Dar es Salaam. 

Waziri Mkuu ameagiza kutangazwa upya kwa mnada mwingine wa kuuza mahindi hayo sambamba na ngano na wahakikishe masuala yote kuhusu mnada huo yanakamilika ndani ya siku tatu kuanzia leo tarehe 09 Januari 2020.

“Mahindi yameuzwa kwa bei ya sh. 340 kwa kilo moja ambayo ni chini na bei ya soko kwa sababu bei ya mahindi sokoni kwa sasa ni sh. 800. Zabuni imetangazwa kwa muda mfupi watu wameshindwa kushiriki. Ilifunguliwa saa 8 mchana na imefungwa saa 5 usiku.”
Kadhalika, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa TRA uhakikishe mnada unaofuata unakuwa wa wazi, huru pamoja na kutoa muda wa kutosha kwa wananchi wote kushiriki ili kuondoa malalamiko. 

“Kwa kuwa mnada unafanyika kwa njia ya mtandao, hakikisheni matumizi ya mtandao yanakuwa rafiki kwa wananchi wote watakaovutiwa kuwasilisha zabuni zao.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa TRA ishirikiane na mamlaka nyingine za Serikali kuhakikisha wanunuzi wa nafaka hizo hawaziingizi sokoni kwa ajili ya matumizi ya binadamu. Nafaka hizo zimepimwa na kuthibitika kuwa zinafaa kwa matumizi ya wanyama.
Read More

Wednesday, January 8, 2020

WAZIRI MHAGAMA ARIDHISHWA NA HATUA ZA UJENZI WA JENGO LA NEC DODOMA

 NA.MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ametembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa jengo la Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi zilizopo eneo la Njedenwa Jijini Dodoma na kusema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa.
Alikagua mradi huo, Januari 07, 2020 ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mhe. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyoyatoa Novemba 18, 2019 alipotembelea na kukagua mradi huo na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi na kutoa maagizo hayo baada ya TBA kusimamisha zoezi la ujenzi kwa ongezeko la gharama za  kutoka bilioni 13 hadi bilioni  32 na hivyo kumtaka Waziri Mhagama kufuatilia.
Ziara ya Waziri Mhagama imebaini maendeleo mazuri ya ujenzi na kufikia hatua ya asilimia 75 baada ya Tume hiyo kuingia mkataba SUMA JKT kuwapongeza wakandarasi kwa hatua hiyo wanayoendelea nayo.
“Kwa kipindi chote ambacho SUMA JKT imeendeela na kazi ya ujenzi wa jengo hili hali inaridhisha na ni vyema kuhakikisha mnaendana na kasi inayotakiwa kwa kuzingatia gharama zilizokubalika za bilioni 16,”Alisistiza Waziri Mhagama
Alieleza kuwa ujenzi wa majengo ya Serikali ni moja ya hatua za kuhakikisha zoezi la kuhamisha watumishi Dodoma linafanikiwa kwa kuendelea kuweka miundombinu rafiki ya ofisi zao.
Mpaka sasa tayari watumishi wapatao 14868 wameshahamia hapa Dodoma hivyo tutaendelea kuandaa mazingira ikiwemo ujenzi wa ofisi hizo kwa kuzingatia kazi ya Uratibu huo ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu,”alisema Mhagama
Alifafanua kuwa, kukamilika kwa jengo hilo kutasaidia kuhakikisha watumishi wa ofisi hiyo wanatoa huduma vizuri kwa kuzingatia mwaka 2020 ni mwaka wa uchaguzi mkuu ambapo itasadia utendaji wa kazi.
Waziri Mhagama ameendelea kueleza kuwa   , miongoni mwa majukumu ya Ofisi yake ni kuhakikisha inaratibu shughuli zote za kuhamisha watumishi wa Serikali na kuweka mazingira mazuri ya ofisi zao ili kuendelea kuitumikia nchi kwa weledi na kujiletea maendeleo yao kwa kutoa wa huduma bora zinazostahili.
Kwa upande wake mmoja wa wasimamizi wa ujenzi wa majengo hayo Mhandisi Michael Mussa alieleza kuwa, wataendelea kufanya kazi kwa viwango vinavyotakiwa ili kuwa na majengo yenye ubora kwa kuzingatia gharama zilizofikiwa kwenye mkataba wa ujenzi huo.
“Tumefarijika kwa ujio wa Mhe. Waziri na tunaahidi tutajenga kwa kipindi kilichopangwa kwa kuzingatia gharama zilizopo kwenye mkataba wa ujenzi huu,”alieleza Mhandisi Michael.
Muonekano wa sehemu ya jengo la Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyopo eneo la Njedengwa Jijini Dodoma.
Mhandisi Michael Mussa akimuonesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama namna ujenzi unavyoendeelea katika miradi inayosimamiwa na Ofisi yake ikiwemo majengo ya Serikali Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha watumishi wanakuwa na mazingira mazuri ya utendaji kazi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipokea maelezo kuhusu ujenzi wa majengo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoka kwa Kanali Mabele ambaye ni Msimamizi mkuu wa mradi huo kutoka SUMA JKT.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama pamoja na Kanali Mabele ambaye ni Msimamizi mkuu wa mradi huo kutoka SUMA JKT wakiangalia sehemu ya majengo ya Ofisi  za Tume ya Uchaguzi yanayoendelea kujengwa  Jijini Dodoma wakati wa ziara yake katika mradi huo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiweka saini katika kitabu cha wageni alipotembelea majengo hayo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akikagua ujenzi wa Majengo ya Ofisi ya Tume ya Uchaguzi yaliyopo Jijini Dodoma alipotembelea kujinea namna hatua hizo zinavyoendelea.

Read More

Saturday, January 4, 2020

MRADI WA HOTELI NI MUHIMU KWA UTALII-MAJALIWA


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mradi wa ujenzi wa hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar ni muhimu katika kuimarisha sekta ya utalii na huduma   za malazi kwa wageni wanaotumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Amesema mradi huo unakwenda sambamba na juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar za kuimarisha uwanja wake wa ndege ili kuongeza uwezo wake katika kutoa huduma bora kwa abiria na wafanyakazi wa mashirika ya ndege ya ndani na nje ya nchi. 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Januari 4, 2020), wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa hoteli hiyo. Miongoni mwa watakaonufaika na mradi huo ni pamoja na wasafiri wanaopita Zanzibar kwa ajili ya kuunganisha ndege na baadaye kuendelea na safari.

Waziri Mkuu ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar inayojengwa katika eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yam waka 1964.

Ujenzi wa hoteli hiyo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni 8.5. sawa na sh. bilioni 19.55. “Ama kwa hakika uwekezaji huu ni mkubwa na naamini wawekezaji hawa wengeliamua kuwekeza katika nchi nyingine yoyote, nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wangelipokelewa kwa mikono miwili.”  

“Hata hivyo, mazingira mazuri ya uwekezaji hapa Zanzibar na uzalendo alionao Mhe. Mohamed Raza, Mwenyekiti wa ‘Royal suites group of companies’ vilipelekea ushawishi mkubwa wa hoteli ya aina hii kujengwa hapa Zanzibar.” 

Waziri Mkuu amesema kuwa “Nyote mtakubaliana nami kuwa viwanja vingi vya ndege vilivyopo kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki, havina hoteli kubwa na za kisasa zilizopo karibu na viwanja hivyo. Uamuzi wa kujenga mradi huu ni sahihi, kwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla ni mahali salama na wezeshi kwa biashara na uwekezaji.” 

Amesema kwa upande mwingine, Serikali zinaendelea kuimarisha amani na utulivu, miundombinu wezeshi ya kiuchumi, huduma za fedha na mifumo ya kodi ili kuvutia uwekezaji. “Mambo haya ni muhimu sana katika kuvutia wawekezaji katika sekta mbalimbali kwa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.” 

Hivyo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa pongezi za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein kwa juhudi wanazoendelea kuzifanya za kushajiisha uwekezaji. “Tunawashukuru sana.”

Amesema kwa upande wa Zanzibar, katika kipindi hiki cha miaka tisa ya Awamu ya Saba, ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, jumla ya miradi ya uwekezaji 304 yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 3.74 imeidhinishwa na mingine iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji. 

Utekelezwaji wa miradi hiyo, umetoa mchango mkubwa katika kukuza ajira, teknolojia, kuongeza mapato ya Serikali na kuimarisha ustawi wa Wananchi wetu. “Hivyo, nawapongeza wawekezaji wetu wote waliowekeza na wanaoendelea kuwekeza hapa nchini. Wawekezaji hawa wameonesha imani na upendo mkubwa kwetu, nasi tunaahidi kufanya nao kazi kwa ushirikiano makubwa.”

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Mohammed Ramia amesema mradi huo ni muhimu kwa kuwa utakapokamilika utaenda kuongeza mapato ya Serikali. 

Amesema hoteli hiyo ni ya kwanza kwa Zanzibar kwa sababu mbali ya kuwa na ukumbi wa watu mashuhuri (VIP Business Lounge) ambao wageni wake watakuwa na uwezo wa kukamilisha taratibu za abiria wa ndege (check in) na taratibu za uhamiaji moja kwa moja kutoka katika ukumbi huo.

Awali, Afisa Mtendaji Mkuu  wa Royal Group of Companies,  Bw. Hassan Mohammed Raza alisema ujenzi wa hoteli hiyo yenye vyumba 61, kumbi tatu za mikutano zenye uwezo uwezo wa kuchukua watu 600 ina hadhi ya nyota nne, ulianza februari 2019 na unatarajiwa kukamilika Septemba mwaka huu.

Alisema nembo ya Golden Tulip ni sehemu moja ya kampuni ya pili kwa ukubwa duniani kwa upande wa hoteli ukiwa chini ya mwavuli wa Louvre Hoteli ambayo inamilikiwa na Shanghai Municipal Council. Mtandao huo una hoteli zaidi ya 8,000 duniani, hivyo hoteli yao italazimika kufuata na kutimiza vigezo bora vya hoteli katika sekta ya hoteli duniani.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikagua Jengo la Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar, baada ya kuweka jiwe la msingi la hoteli hiyo, Januari 4, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikagua Jengo la Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar, baada ya kuweka jiwe la msingi la hoteli hiyo, Januari 4, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Mohammed Ramia , baada ya kuweka jiwe la msingi wa Jengo la Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar, Januari 4, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi wa Jengo la Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar, Januari 4, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi wa Jengo la Hoteli ya Golden Tulip Airport Zanzibar, Januari 4, 2020.


Read More

Thursday, January 2, 2020

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA, AWAJULIA HALI WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA, MKOANI LINDI.

Mke wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa, akimjulia hali Mzazi, Zena Issa, wakati altpotembelea Wodi ya Wazazi, katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 2, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na wananchi, baada ya wakiwajulia hali wagonjwa, katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 2, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwa na Mkewe Mary, wakimsalimia Mzazi, Zulfa Juma, wakati wakiwajulia hali wagonjwa, katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 2, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwa na Mkewe Mary, wakimsalimia Mzazi, Zulfa Juma, wakati wakiwajulia hali wagonjwa, katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi, Januari 2, 2020.

Read More