Monday, August 24, 2020
MAAFISA OFISI YA WAZIRI MKUU WAPIGWA MSASA UTEKELEZAJI MAJUKUMU
Friday, August 21, 2020
MAJALIWA ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE WA RUANGWA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Ruangwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka kwa Frank Chonya ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ruangwa, Agosti 21, 2020.
Tuesday, August 18, 2020
WAZIRI MKUU: WATANZANIA TUBADILIKE, TUJIVUNIE VYETU
*Akagua mradi wa kiwanda cha sukari na shamba la miwa Bagamoyo
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wabadilike na wajifunze kujivunia kilicho chao. "Lazima tubadilike Watanzania, tuwe wazalendo, tukisemee kitu chetu, tujivunie kitu chetu na tujivunie ujuzi tulionao," amesema.
Ametoa wito huo leo (Jumanne Agosti 18, 2020) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa na wafanyakazi wa kiwanda cha sukari cha Bagamoyo (BSL), katika kata ya Makurunge, wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.
Waziri Mkuu ambaye alifika kiwandani hapo na kukagua ujenzi wa kiwanda unaoendelea, pia alikagua miundombinu ya mradi wa shamba la miwa ikiwemo vitalu vya mbegu, miche, maabara ya kupima maji na udongo na miundombinu ya umwagiliaji.
"Ninasema tubadilike sababu nimeenda kwenye maabara yao na kukuta wataalamu wetu wako vizuri, wanafanya utafiti wa udongo, maji na mbegu. Wameelezea vizuri utafiti wao na matokeo tumeyaona ni mazuri.”
“Rais wetu alisema Watanzania tunaweza, na leo nimethibitisha kwamba Watanzania tunao uwezo wa kazi lakini tatizo letu hatuwezi kujisemea wenyewe. Lazima tujisifu, tujisemee kuhusu umahiri tulionao. Ni kwa nini tujidharau?", alihoji.
"Nataka tubadilike sababu Watanzania tunaweza. Baadhi yao wanatoka hapa hapa Bagamoyo. Nimemuuliza ulisoma wapi, akajibu Chuo cha Kilimo Kaole, na hiki kiko Bagamoyo. Wengine wanatoka SUA (Chuo cha Kilimo cha Sokoine). Lazima turingie nchi yetu, lazima tuitangaze nchi yetu na ni lazima tuisemee nchi yetu," amesisitiza.
Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa eneo hilo lenye hekta 10,000 ili lilimwe miwa na kujenga kiwanda cha sukari, ulilenga kuongeza uzalishaji wa sukari nchini. "Tunahitaji kupata mashamba mengi ya miwa ili tuongeze uzalishaji wa sukari nchini".
“Hivi sasa mahitaji ya suakri nchini yamefikia tani 450,000 kwa sukari ya mezani. Ile sukari ya viwandani ambayo inatumika kutengeneza soda, biskuti na pipi mahitaji yake ni tani 165,000 ambayo hapa nchini hatuizalishi, kwa hiyo inabidi tuiagize kutoka nje ya nchi.”
Amesema uzalishaji wa sukari ya mezani kwa sasa unafikia tani 380,000 kwa viwanda vyote vilivyopo na kwamba bado kuna bakaa ya tani 70,000. Amesema mbali ya viwanda vilivyopo vya TPC, Kagera, Mtibwa, Kilombero, Manyara na Bagamoyo bado kuna maeneo ya kulima miwa huko Tarime na Kigoma. “Tunawaalika wawekezaji walime miwa na kuzalisha sukari zaidi.”
Akielezea kuhusu ujenzi wa kiwanda hicho, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na kazi inayofanyika na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutahakikisha sukari inapatikana kulekule na pia itatoa fursa ya kilimo cha miwa kwa wakazi wa maeneo jirani.
Amewataka maafisa kilimo waende wakatoe elimu kwa wananchi kuhusu kilimo cha miwa. “Wapeni uhakika wa soko ili wasisite kushiriki kwenye hiki kilimo. Wananchi watavutiwa wakijua kuna faida kwenye kilimo hicho lakini pia kiwanda kitapata tani za ziada na kuongeza uzalishaji wake,” amesisitiza.
Mapema, Mkurugenzi wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Abubakar Bakhresa alimshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia shamba hilo na kuahidi kuendana na dhamira ya Serikali ya kupunguza tatizo la upatikanaji wa sukari nchini.
Akielezea hatua zilizofikiwa kwenye mradi huo, Mkurugenzi wa Mahusiano wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Hussein Sufian alisema gharama ya mradi huo ni dola za Marekani milioni 100 na kwamba hadi sasa wameshapata asilimia 70 ya mtaji.
“Benki ya Kilimo (TADB) imetukopesha dola za Marekani milioni 6.5, Benki ya CRDB wametukopesha dola za Marekani milioni 25, makampuni ya Bakhresa tumetoa dola za Marekani milioni 30 na benki ya Standard Chartered imetukopesha dola za Marekani milioni 10. Tunayashukuru mabenki za ndani kwa kukubali kutuunga mkono,” alisema.
Alisema kampuni yao mpaka sasa imetoa ajira kwa watu 600 ambapo 500 kati yao wanatoka kwenye vijiji jirani vinavyozunguka eneo la mradi na kwamba mara baada ya awamu ya kwanza kukamilika, uzalishaji utakapoanza wataweza kuajiri watu 1,500. “Awamu ya pili inatarajiwa kuwahusisha wakulima wa nje (outgrowers scheme) kwani mradi utawapa fursa ya kushiriki kilimo cha miwa na kupata soko la uhakika kutoka kiwandani,” alisema.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Japhet Justin alisema mbali ya kiwanda hicho cha sukari, wamelenga pia kuwanufaisha wakulima wadogo wa miwa. “Kwa kawaida wenye mabenki wanaamini ili aweze kumkopesha mkulima ni lazima aone eneo lake analomiliki.”
“Sisi tumeona fursa, na tumeamua wakulima watakaopata mikataba baina yao na kiwanda cha sukari Bagamoyo, tutachukua mikataba hiyo iwe dhamana ya kupata mikopo ya kuendeleza mashamba yao. Hii ni kwa sababu kuna vijiji vitano tayari vimefanyiwa upimaji na kuna uwezekano wa hekta 3,600 zitakazotumika kulima miwa.”
Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo, alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kutoa eneo hilo ili BSL ianzishe kilimo cha miwa. “Tunamshukuru kwa sababu ametuongezea zao jingine la biashara.”
“Kabla ya hapo, tulikuwa na zao la korosho ambalo mwaka jana limewaingizia wakulima shilingi bilioni 60. Pia zao la ufuta liliwaingizia shilingi bilioni 19. Mwaka huu umetuita Tanga na kutuelekeza tuanzishe zao la mkonge, kwa hiyo kilimo cha miwa kimekuwa zao la nne mkoani kwetu na hivi sasa kuna kata tano ambazo ziko tayari kulima miwa.”
Monday, August 17, 2020
MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA VIONGOZI WA DINI
MAJALIWA AZUNGUMZA KATIKA MAHAFALI YA VYUO NA VYUO VIKUU JIJINI DAR ES SALAAM
Thursday, August 13, 2020
MAJALIWA ASALIMIANA NA WANANCHI WA MTAMA AKIWA NJIANI KWENDA RUANGWA
MAJALIWA AKAGUA UKARABATI WA BARABARA YA SOMANGA - MBWEMKURU KATIKA KIJIJI CHA MTANDI
Sunday, August 9, 2020
MAJALIWA AKAGUA UJENZI WA MELI MPYA MWANZA
*Aitaka mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa wiki ijayo meli inaanza kazi
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekagua ukarabati mkubwa wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi tu na kuagiza mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa kuanzia wiki ijayo meli hiyo inaanza kazi ya kusafirisha abiria na mizigo kwa kuwa ukarabati umekamilika na sasa inaendelea kukaa tu hali ambayo ni hasara kwa Serikali.
Pia, Waziri Mkuu ametoa siku mbili kwa mamlaka inayohusika na utoaji wa kibali cha kuanza kazi kwa meli hiyo ihakikishe inatoa kibali hicho haraka na ratiba ya safari itangazwe kwa sababu Watanzania wanahamu ya kuanza kuhuduiwa na meli hiyo.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) baada ya kukagua meli hiyo ambayo tayari imeshafanya safari ya majaribio kwa kusafirisha abiria kutoka Mwanza hadi Bukoba mkoani Kagera ambako ilirudi na abiria na mizigo.
Maeneo aliyokagua kwenye meli hiyo ni pamoja na vyumba vya abiria vikiwemo vyumba maalumu kwa ajili ya huduma za mama na mtoto, chumba cha kuongozea meli, vyumba vya migahawa na chumba cha injini.
“Nimeona ukarabati mkubwa uliofanywa, nimeona injini mpya, meli imekamilika na ilishafanyiwa majaribio ya aina zote kubeba abiria na kubeba mizigo na wataalamu wamejiridhisha kuwa inauwezo wa kubeba abiria na mizigo.”
Waziri Mkuu ameongeza kuwa “Haya yote ni mawazo na mipango ya Rais Dkt. John Magufuli pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020. Tumetekeleza na tunaendelea kutekeleza.”
Baada ya kukagua meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa chelezo pamoja na meli mpya na alieleza kuwa ameridhishwa na kazi inayoendelea kufanyika na amewataka Watanzania waendelee kuwa na imani na Serikali yao.
Awali, Meneja Miradi ya Kimkakati inayotekelezwa na Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Luteni Kanali Vitus Mapunda alisema miradi hiyo minne ya ukarabati mkubwa wa meli ya Mv Victoria Hapa Kazi Tu, MV Butiama Hapa Kazi Tu, ujenzi wa chelezo na ujenzi wa meli mpya inayojulikana kama MV Mwanza Hapa Kazi Tu itagharimu sh. 152,916,249,842.
Alisema ukarabati wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mizigo tano 400 umegharimu sh. 22,712,098,200. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini, Kemendo na Bukoba.
“MV Butiama itakayobeba abiria 200 na mizigo tani 100 ukarabati wake umegharimu sh. 4,897,640,000. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini na Nansio Ukerewe. Ukarabati wa chelezo umegharimu sh. 36,152,511,642 na ujenzi wa meli mpya utagharimu sh. 89,154,000,000.”
Alisema kukamilika kwa miradi hiyo ya kimkakati kutafungua fursa nyingi za ajira binafsi na kupunguza gharama za usafirishaji sambamba na kuongeza tija katika shughuli za biashara hivyo kuwafanya wananchi wanyonge wengi kunufaika. Ujenzi wa Meli mpya unatarajiwa kukamilika Agosti 2021.
Saturday, August 8, 2020
WAZIRI MKUU ATOA WIKI MOJA KWA WIZARA YA ELIMU
*Ni kuhusu ucheleweshwaji wa michango ya wanafunzi NHIF
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa muda wa wiki moja kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kukutana na Wakuu wa Vyuo Vikuu nchini ili kubaini vyuo ambavyo vimeshindwa kuwasilisha michango ya wanafunzi katika Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) licha ya wanafunzi kulipa fedha hizo.
“Katibu Mkuu Wizara ya Elimu kashughulikie jambo hili tujue mifumo wanayotumia, pia nataka kujua ni wanafunzi wangapi ambao wamelipa na hawajapewa vitambulisho na kwa nini na nani amesababisha haya na hatua alizochukuliwa. Taarifa hiyo nataka niipate tarehe 16 mwezi huu, wiki moja inakutosha.”
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kwanza kwa mwaka 2019/2020 wa Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi ya Elimu ya Juu Tanzania(TAHLISO) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanafunzi hao yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Peter Niboye ambaye alisema kwamba kumekuwepo na ucheleweshaji wa vitambulisho vya bima ya afya unaotokana na baadhi ya vyuo kuchelewa kufikisha fedha NHIF.
Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuziagiza Menejimenti zote za vyuo vikuu nchini ziendelee kushirikiana kwa karibu na Serikali za Wanafunzi kwenye vyuo vyao ili waweze kushughulikia changamoto za wanafunzi kwa wakati.
Akizungumzia kuhusu wabunifu pamoja na wanafunzi bora, Waziri Mkuu amesema “Naiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia isimamie utambuzi wa masuala mbalimbali ya kitaaluma iwe ni kwenye teknolojia, afya na hawa wabunifu watambuliwe na waendelezwe. Tuwe na benki ya wabunifu waliobuni kazi ambazo zinaweza kusaidia jamii.”
Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa taarifa ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia inaeleza kuwa tangu kufunguliwa kwa vyuo nchini tarehe 01 Juni, 2020 wanafunzi wote walioripoti wapo salama na wanaendelea vema na masomo yao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Niboye amesema wanajivunia kufanya kazi kwa karibu na Bodi ya Mikopo na Mfuko wa Bima ya Afya na imechangia kutokuwepo kwa migomo ya wanafunzi.
Akitoa tamko la jumuia hiyo katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu, amesema TAHLISO inamuunga mkono mlezi wao na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika uchaguzi huo na watahakikisha anashinda kwa kishindo.
Mwenyekiti huyo amesema TAHLISO imefanya uamuzi huo baada ya kuridhishwa na utendajikazi wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. Magufuli ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama ya elimu, umeme, maji, miundombinu na afya.
Monday, July 13, 2020
WAZEE NACHINGWEA WAMCHANGIA RAIS DKT. MAGUFULI, WAZIRI MKUU AWASHUKURU AAHIDI KUFIKISHA SALAM
Wednesday, July 8, 2020
MAJALIWA ATEMBELEA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO NALIENDELE
Tuesday, July 7, 2020
TUTAFUFUA VYUO NA VITUO VYA UTAFITI WA KILIMO-MAJALIWA
Friday, July 3, 2020
WAZIRI MKUU AFUNGUA MAONESHO YA 44 YA BIASHARA
MAJALIWA AFUNGUA MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DAR ES SALAAM
| Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020. |
| Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020. |
| Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020. |
MITANDAO YA KIJAMII
Popular Posts
-
Na. OWM, Dodoma. Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, imefanya ukaguzi wa utekelezaji wa sheria Na.5 y...
-
Wataalamu wa Afya moja wakiwa katikapicha ya pamoja wakati wa mkutano wa wataalamu wa Afya moja uliojikita katika ulinzi na usalama...
-
Na. OWM, ARUSHA Wataalam wa sheria kutoka katika sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wameshauri...
-
Washiriki wa Mkutano wa mwaka wa Wataalamu wa Maabara wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano wa mwaka kwa wataalam wa maabara w...
-
TAMOBA wafanya wasilisho la mfumo maalum wa kielektroniki wa ulinzi na usalama wa Bodaboda na BajajiKampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaj Association (TAMOBA) imefanya wasilisho maaluum kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mfumo maalum wa ...
-
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, ajira na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, ambaye ndiye anayesimamia Kamati ina...
-
*Aagiza fedha zilizotengwa zikatumike katika kujengea hospitali Dodoma Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameahirisha maadhimisho ya sik...
-
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki akipokea maelezo ya namna mashine zinavyochakata mifuko chakavu na ...
-
Katika kuhakikisha malengo ya kutatua masuala ya ajira na kazi, yanafikiwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Mhe. Samia Suluhu H...
-
Katibu wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiuliza jambo kwa Kaimu Meneja wa Uwa...