Monday, August 24, 2020

MAAFISA OFISI YA WAZIRI MKUU WAPIGWA MSASA UTEKELEZAJI MAJUKUMU


Baadhi ya maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao(TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akisisitiza umuhimu wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Mtaalamu wa masuala ya Sera kutoka Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) Apronius Mbilinyi akiendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mafunzo hayo ya siku tano yanajikita katika namna ya kufanya Uchambuzi wa sera, Tathmini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa Sera hizo, utaalamu katika Uandishi wa Ripoti pamoja na namna bora ya  kutekeleza shughuli za Uratibu.  Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Baadhi ya maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo likiwa ni kutekeleza kwa ufanisi na weledi majukumu waliyokasimiwa. Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao, jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), Dickson Mwanyika akisisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kupata mafunzo ya kujenga uwezo kwa watumishi wa umma  lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo, jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Mchumi mwandamizi Ofisi ya Waziri Mkuu, Happiness Mugyabuso akipitia makabrasha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi hiyo, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa shughuli za serikali Paul Sangawe akisisitiza umuhimu wa ufanisi na weledi katika kutekeleza uratibu wa shughuli za serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi hiyo, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Afisa Tawala Mwandamizi  ofisi ya Waziri Mkuu Stephen Magoha akichangia juu ya masuala ya Uratibu wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko wakati akisisitiza umuhimu wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Read More

Friday, August 21, 2020

MAJALIWA ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE WA RUANGWA


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Ruangwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)  kutoka kwa Frank Chonya ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ruangwa, Agosti 21, 2020.

Read More

Tuesday, August 18, 2020

WAZIRI MKUU: WATANZANIA TUBADILIKE, TUJIVUNIE VYETU

         *Akagua mradi wa kiwanda cha sukari na shamba la miwa Bagamoyo


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wabadilike na wajifunze kujivunia kilicho chao. "Lazima tubadilike Watanzania, tuwe wazalendo, tukisemee kitu chetu, tujivunie kitu chetu na tujivunie ujuzi tulionao," amesema.

 

Ametoa wito huo leo (Jumanne Agosti 18, 2020) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa na wafanyakazi wa kiwanda cha sukari cha Bagamoyo (BSL), katika kata ya Makurunge, wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

 

Waziri Mkuu ambaye alifika kiwandani hapo na kukagua ujenzi wa kiwanda unaoendelea, pia alikagua miundombinu ya mradi wa shamba la miwa ikiwemo vitalu vya mbegu, miche, maabara ya kupima maji na udongo na miundombinu ya umwagiliaji.

 

"Ninasema tubadilike sababu nimeenda kwenye maabara yao na kukuta wataalamu wetu wako vizuri, wanafanya utafiti wa udongo, maji na mbegu. Wameelezea vizuri utafiti wao na matokeo tumeyaona ni mazuri.”

 

“Rais wetu alisema Watanzania tunaweza, na leo nimethibitisha kwamba Watanzania tunao uwezo wa kazi lakini tatizo letu hatuwezi kujisemea wenyewe. Lazima tujisifu, tujisemee kuhusu umahiri tulionao. Ni kwa nini tujidharau?", alihoji.

 

"Nataka tubadilike sababu Watanzania tunaweza. Baadhi yao wanatoka hapa hapa Bagamoyo. Nimemuuliza ulisoma wapi, akajibu Chuo cha Kilimo Kaole, na hiki kiko Bagamoyo. Wengine wanatoka SUA (Chuo cha Kilimo cha Sokoine). Lazima turingie nchi yetu, lazima tuitangaze nchi yetu na ni lazima tuisemee nchi yetu," amesisitiza.

 

Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa eneo hilo lenye hekta 10,000 ili lilimwe miwa na kujenga kiwanda cha sukari, ulilenga kuongeza uzalishaji wa sukari nchini. "Tunahitaji kupata mashamba mengi ya miwa ili tuongeze uzalishaji wa sukari nchini".

 

“Hivi sasa mahitaji ya suakri nchini yamefikia tani 450,000 kwa sukari ya mezani. Ile sukari ya viwandani ambayo inatumika kutengeneza soda, biskuti na pipi mahitaji yake ni tani 165,000 ambayo hapa nchini hatuizalishi, kwa hiyo inabidi tuiagize kutoka nje ya nchi.”

 

Amesema uzalishaji wa sukari ya mezani kwa sasa unafikia tani 380,000 kwa viwanda vyote vilivyopo na kwamba bado kuna bakaa ya tani 70,000. Amesema mbali ya viwanda vilivyopo vya TPC, Kagera, Mtibwa, Kilombero, Manyara na Bagamoyo bado kuna maeneo ya kulima miwa huko Tarime na Kigoma. “Tunawaalika wawekezaji walime miwa na kuzalisha sukari zaidi.”

 

Akielezea kuhusu ujenzi wa kiwanda hicho, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na kazi inayofanyika na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutahakikisha sukari inapatikana kulekule na pia itatoa fursa ya kilimo cha miwa kwa wakazi wa maeneo jirani.

 

Amewataka maafisa kilimo waende wakatoe elimu kwa wananchi kuhusu kilimo cha miwa. “Wapeni uhakika wa soko ili wasisite kushiriki kwenye hiki kilimo. Wananchi watavutiwa wakijua kuna faida kwenye kilimo hicho lakini pia kiwanda kitapata tani za ziada na kuongeza uzalishaji wake,” amesisitiza.

 

Mapema, Mkurugenzi wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Abubakar Bakhresa alimshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia shamba hilo na kuahidi kuendana na dhamira ya Serikali ya kupunguza tatizo la upatikanaji wa sukari nchini.

 

Akielezea hatua zilizofikiwa kwenye mradi huo, Mkurugenzi wa Mahusiano wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Hussein Sufian alisema gharama ya mradi huo ni dola za Marekani milioni 100 na kwamba hadi sasa wameshapata asilimia 70 ya mtaji.

 

“Benki ya Kilimo (TADB) imetukopesha dola za Marekani milioni 6.5, Benki ya CRDB wametukopesha dola za Marekani milioni 25, makampuni ya Bakhresa tumetoa dola za Marekani milioni 30 na benki ya Standard Chartered imetukopesha dola za Marekani milioni 10. Tunayashukuru mabenki za ndani kwa kukubali kutuunga mkono,” alisema.

 

Alisema kampuni yao mpaka sasa imetoa ajira kwa watu 600 ambapo 500 kati yao wanatoka kwenye vijiji jirani vinavyozunguka eneo la mradi na kwamba mara baada ya awamu ya kwanza kukamilika, uzalishaji utakapoanza wataweza kuajiri watu 1,500. “Awamu ya pili inatarajiwa kuwahusisha wakulima wa nje (outgrowers scheme) kwani mradi utawapa fursa ya kushiriki kilimo cha miwa na kupata soko la uhakika kutoka kiwandani,” alisema.

 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Japhet Justin alisema mbali ya kiwanda hicho cha sukari, wamelenga pia kuwanufaisha wakulima wadogo wa miwa. “Kwa kawaida wenye mabenki wanaamini ili aweze kumkopesha mkulima ni lazima aone eneo lake analomiliki.”

 

“Sisi tumeona fursa, na tumeamua wakulima watakaopata mikataba baina yao na kiwanda cha sukari Bagamoyo, tutachukua mikataba hiyo iwe dhamana ya kupata mikopo ya kuendeleza mashamba yao. Hii ni kwa sababu kuna vijiji vitano tayari vimefanyiwa upimaji na kuna uwezekano wa hekta 3,600 zitakazotumika kulima miwa.”

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo, alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kutoa eneo hilo ili BSL ianzishe kilimo cha miwa. “Tunamshukuru kwa sababu ametuongezea zao jingine la biashara.”

 

“Kabla ya hapo, tulikuwa na zao la korosho ambalo mwaka jana limewaingizia wakulima shilingi bilioni 60. Pia zao la ufuta liliwaingizia shilingi bilioni 19. Mwaka huu umetuita Tanga na kutuelekeza tuanzishe zao la mkonge, kwa hiyo kilimo cha miwa kimekuwa zao la nne mkoani kwetu na hivi sasa kuna kata tano ambazo ziko tayari kulima miwa.”

 

Read More

Monday, August 17, 2020

MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA VIONGOZI WA DINI

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full  Gospal Bibble Fellowship, Zakary Kakobe akizungumza katika  Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

Mufti  na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir  Ally  akizungumza katika  Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Abubakar Kunenge wakati alipowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam kufungua Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.  Wa pili kushoto ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum.

Read More

MAJALIWA AZUNGUMZA KATIKA MAHAFALI YA VYUO NA VYUO VIKUU JIJINI DAR ES SALAAM

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Mic Mdegela ambaye ni Mwanachuo wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anayesoma kozi ya Menejimenti ya  Rasilimaliwatu baada ya kuzungumza  na kutoa vyeti katika Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Kheri James.
MAJALIWA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Mic Mdegela ambaye ni Mwanachuo wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anayesoma kozi ya Menejimenti ya  Rasilimaliwatu baada ya kuzungumza  na kutoa vyeti katika Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Kheri James.

Wanavyuo wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza katika  Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya  jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika  Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu jijini vya Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. 

Read More

Thursday, August 13, 2020

MAJALIWA ASALIMIANA NA WANANCHI WA MTAMA AKIWA NJIANI KWENDA RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na wananchi wa Mtama waliojitokeza kumlaki barabarani wakiongozwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Nape Nnauye, Agosti 13,2020.  Mheshimiwa Majaliwa alikuwa akitoka Dar es salaam kwenda Ruangwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na wananchi wa Mtama waliojitokeza kumlaki barabarani wakiongozwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Nape Nnauye, Agosti 13,2020.  Mheshimiwa Majaliwa alikuwa akitoka Dar es salaam kwenda Ruangwa.

 

Read More

MAJALIWA AKAGUA UKARABATI WA BARABARA YA SOMANGA - MBWEMKURU KATIKA KIJIJI CHA MTANDI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ukarabati wa barabara ya Somanga – Mbwemkuru katika kijiji cha  Mtandi Kata ya Kiranjeranje wilayani Kilwa , Agosti 13, 2020. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Arch.Elius Mwakalinga.
 

Read More

Sunday, August 9, 2020

MAJALIWA AKAGUA UJENZI WA MELI MPYA MWANZA

 

*Aitaka mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa wiki ijayo meli inaanza kazi

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekagua ukarabati  mkubwa wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi tu na kuagiza mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa kuanzia wiki ijayo meli hiyo inaanza kazi ya kusafirisha abiria na mizigo kwa kuwa ukarabati umekamilika na sasa inaendelea kukaa tu  hali ambayo ni hasara kwa Serikali.

 

Pia, Waziri Mkuu ametoa siku mbili kwa mamlaka inayohusika na utoaji wa kibali cha kuanza kazi kwa meli hiyo ihakikishe inatoa kibali hicho haraka na  ratiba ya safari itangazwe kwa sababu  Watanzania wanahamu  ya kuanza kuhuduiwa na meli hiyo.

 

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) baada ya kukagua meli hiyo ambayo tayari imeshafanya safari ya majaribio  kwa  kusafirisha  abiria kutoka Mwanza hadi Bukoba mkoani Kagera ambako ilirudi na abiria na mizigo.

 

Maeneo aliyokagua kwenye meli hiyo ni pamoja na vyumba vya abiria vikiwemo vyumba maalumu kwa ajili ya huduma za mama na mtoto, chumba cha kuongozea meli, vyumba vya migahawa na chumba cha injini.

 

“Nimeona ukarabati mkubwa uliofanywa, nimeona injini mpya, meli imekamilika na ilishafanyiwa majaribio ya aina zote kubeba abiria na kubeba mizigo na wataalamu wamejiridhisha kuwa inauwezo wa kubeba abiria na mizigo.”

 

Waziri Mkuu ameongeza kuwa “Haya yote ni mawazo na mipango ya Rais Dkt. John Magufuli pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020. Tumetekeleza na tunaendelea kutekeleza.”

 

Baada ya kukagua meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa chelezo pamoja na meli mpya na alieleza kuwa ameridhishwa na kazi inayoendelea kufanyika na amewataka Watanzania waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

 

Awali, Meneja Miradi ya Kimkakati inayotekelezwa na Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Luteni Kanali Vitus Mapunda alisema miradi hiyo minne ya ukarabati mkubwa wa meli ya Mv Victoria Hapa Kazi Tu, MV Butiama Hapa Kazi Tu, ujenzi wa chelezo na ujenzi wa meli mpya inayojulikana kama MV Mwanza Hapa Kazi Tu itagharimu sh. 152,916,249,842.

 

Alisema ukarabati wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mizigo tano 400 umegharimu sh. 22,712,098,200. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini, Kemendo na Bukoba.

 

“MV Butiama itakayobeba abiria 200 na mizigo tani 100 ukarabati wake umegharimu sh. 4,897,640,000. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini na Nansio Ukerewe. Ukarabati wa chelezo umegharimu sh. 36,152,511,642 na ujenzi wa meli mpya utagharimu sh. 89,154,000,000.”

 

Alisema kukamilika kwa miradi hiyo ya kimkakati kutafungua fursa nyingi za ajira binafsi na kupunguza gharama za usafirishaji sambamba na kuongeza tija katika shughuli za biashara hivyo kuwafanya wananchi wanyonge wengi kunufaika. Ujenzi wa Meli mpya unatarajiwa kukamilika Agosti 2021.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa nahodha wa meli ya  MV New Victoria – Hapa Kazi Tu, Bembele Samson Ng’wita (wa pili kulia)  wakati alipoikagua meli hiyo ambayo ukarabati wake umekamilika, kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa nahodha wa meli ya  MV New Victoria – Hapa Kazi Tu, Bembele Samson Ng’wita (wa pili kulia)  wakati alipoikagua meli hiyo ambayo ukarabati wake umekamilika, kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozwa na nahodha wa meli ya  MV  New Victoria – Hapa Kazi Tu,  Bembele Samson Ng’wita kukagua meli hilo ambayo ukarabati wake umekamilika , kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.


 

Read More

Saturday, August 8, 2020

WAZIRI MKUU ATOA WIKI MOJA KWA WIZARA YA ELIMU

 

*Ni kuhusu ucheleweshwaji wa michango ya wanafunzi NHIF

 

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa muda wa wiki moja kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kukutana na Wakuu wa Vyuo Vikuu nchini ili kubaini vyuo ambavyo vimeshindwa kuwasilisha michango ya wanafunzi katika Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) licha ya wanafunzi kulipa fedha hizo.

 

“Katibu Mkuu Wizara ya Elimu kashughulikie jambo hili tujue mifumo wanayotumia, pia nataka kujua ni wanafunzi wangapi ambao wamelipa na hawajapewa vitambulisho na kwa nini na nani amesababisha haya na hatua alizochukuliwa. Taarifa hiyo nataka niipate tarehe 16 mwezi huu, wiki moja inakutosha.”

 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kwanza kwa mwaka 2019/2020 wa Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi ya Elimu ya Juu Tanzania(TAHLISO) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

 

Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanafunzi hao yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Peter Niboye ambaye alisema kwamba kumekuwepo na ucheleweshaji wa vitambulisho vya bima ya afya unaotokana na baadhi ya vyuo kuchelewa kufikisha fedha NHIF.

 

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuziagiza Menejimenti zote za vyuo vikuu nchini ziendelee kushirikiana kwa karibu na Serikali za Wanafunzi kwenye vyuo vyao ili waweze kushughulikia changamoto za wanafunzi kwa wakati.

 

Akizungumzia kuhusu wabunifu pamoja na wanafunzi bora, Waziri Mkuu amesema “Naiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia isimamie utambuzi wa masuala mbalimbali ya kitaaluma iwe ni kwenye teknolojia, afya na hawa wabunifu watambuliwe na waendelezwe. Tuwe na benki ya wabunifu waliobuni kazi ambazo zinaweza kusaidia jamii.”

 

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa taarifa ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia inaeleza kuwa tangu kufunguliwa kwa vyuo nchini tarehe 01 Juni, 2020 wanafunzi wote walioripoti wapo salama na wanaendelea vema na masomo yao.

 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Niboye  amesema wanajivunia kufanya kazi kwa karibu na Bodi ya Mikopo na Mfuko wa Bima ya Afya na imechangia kutokuwepo kwa migomo ya wanafunzi.

Akitoa tamko la jumuia hiyo katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu, amesema TAHLISO inamuunga mkono mlezi wao na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika uchaguzi huo na watahakikisha  anashinda kwa kishindo.

Mwenyekiti huyo amesema TAHLISO imefanya uamuzi huo baada ya kuridhishwa na utendajikazi wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. Magufuli ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama ya elimu, umeme, maji, miundombinu na afya.

 

OWM

Read More

Monday, July 13, 2020

WAZEE NACHINGWEA WAMCHANGIA RAIS DKT. MAGUFULI, WAZIRI MKUU AWASHUKURU AAHIDI KUFIKISHA SALAM

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akimsikiliza Mzee Hamis Kambona (wapili kutoka kushoto) wakati akipokea  mchango wa Shilingi laki moja kutoka kwa wazee wa wilaya na Nachingwea kwa ajili ya kumchangia, Rais Dkt.  John Magufuli katika kampeni za uchaguzi wa  mwaka huu, kwa kutambua mchango mkubwa katika kuiletea Tanzania maendeleo. Tukio hilo lilifanyika kwenye uwanja wa Ndege wa Nachingwea wakati Waziri Mkuu alipowasili akiwa jiani kwenda Ruangwa, Julai 13, 2020.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akipokea risiti ya malipo ya shilingi Laki moja kutoka kwa Mzee Abdalah Saidi Kaliondima, kwa ajili ya kumchangia, Rais Dkt. John Magufuli katika kampeni za uchaguzi wa mwaka huu, kwa kutambua mchango mkubwa katika kuiletea Tanzania maendeleo, Tukio hilo lilifanyika kwenye uwanja wa Ndege wa Nachingwea wakati Waziri Mkuu alipowasili akiwa jiani kwenda Ruangwa, Julai 13, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akipokea risiti ya malipo ya shilingi Laki moja kutoka kwa Mzee Abdalah Saidi Kaliondima, kwa ajili ya kumchangia, Rais Dkt. John Magufuli katika kampeni za uchaguzi wa mwaka huu, kwa kutambua mchango mkubwa katika kuiletea Tanzania maendeleo, Tukio hilo lilifanyika kwenye uwanja wa Ndege wa Nachingwea wakati Waziri Mkuu alipowasili akiwa jiani kwenda Ruangwa, Julai 13, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwashukuru wazee wa wilaya na Nachingwea baada ya kupokea risiti ya malipo ya shilingi Laki moja walizozitoa kwa ajili ya kumchangia, Rais Dkt.  John Magufuli katika kampeni za uchaguzi wa  mwaka huu, kwa kutambua mchango mkubwa katika kuiletea Tanzania maendeleo. Tukio hilo lilifanyika kwenye uwanja wa Ndege wa Nachingwea wakati Waziri Mkuu alipowasili akiwa jiani kwenda Ruangwa, Julai 13, 2020.

Read More

Wednesday, July 8, 2020

MAJALIWA ATEMBELEA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO NALIENDELE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama maziwa yanayotokana na korosho wakati alipotembelea  Taasisi ya Utafiti wa Kilimo, Naliendele, Mtwara, Julai 7, 2020. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa. 

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi  ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dr. Fortunus Kapinga (kushoto) kuhusu utafiti wa mbegu bora za mhogo unaofanyika katika Taasisi hiyo, Julai 7, 2020. Wa pili kushoto ni Mtafiti Mkuu katikaTaasisi hiyo, Bernadetha Kimata. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Berbadetha Kimata ambaye ni  Mtafiti Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo, Naliendele ya Mtwara  kuhusu utafiti wa mbegu za mhogo wakati alipoitembelea, Julai 7, 2020. Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni Mstaafu, George Mkuchika. 


Read More

Tuesday, July 7, 2020

TUTAFUFUA VYUO NA VITUO VYA UTAFITI WA KILIMO-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli itahakikisha kwamba vyuo na vituo vyote vya utafiti wa kilimo nchini vinafufuliwa, hivyo Wizara ya Kilimo inatakiwa kutenga fedha za kutosha katika bajeti yake kila mwaka. 

“Nataka niwahakikishie Serikali yenu imedhamiria kuimarisha kilimo pamoja na utafiti wake. Mwezi mmoja uliopita nilikuwa Mlingano mkoani Tanga kuona shughuli za utafiti wa zao la mkonge lakini miezi miwili iliyopita nilikuwa kwenye chuo kipya tulichokianzisha kule Kigoma cha utafiti cha Kihinga na nimeona kazi yake na tutapata mafanikio makubwa.”

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo jana (Jumanne, Julai 07, 2020) alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele iliyoko mkoani Mtwara kwa lengo la kujionea shughuli za utafiti wa mazao mbalimbali ya kilimo zinazoendelea kituoni hapo. 

Alisema Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefurahishwa na kazi nzuri za utafiti wa mazao mbalimbali zinazofanywa na vituo vya utafiti na matokeo mazuri ya utafiti huo kwa wakulima wa Watanzania.

Waziri Mkuu alisema “Azma ya kusimamia na kuona vyuo vya utafiti vinafanya kazi yake vizuri ni pamoja na maboresho haya kwanza wizara husika lazima itambue  kuwa vyuo vya utafiti vinamchango mkubwa, wizara kwenye bajeti zake ipeleke fedha nyingi kwenye utafiti na tuone utafiti unagundua mambo na yale yanayogunduliwa yaende yakafanyiwe kazi.”

Vilevile, Waziri Mkuu alisema idadi ya udahili wa wanafunzi katika vyuo vya kilimo itaongezwa ili wapatikane wataalamu na watafiti wengi ambao wanahitajika sana katika kufanikisha mapinduzi ya kilimo nchini.

Tasisi ya hiyo ya Kilimo ya Naliendele ni miongoni mwa vituo vya utafiti wa kilimo nchini ambavyo vimewawezesha wakulima wengi kujiongezea tija na kujikwamua kiuchumi baada ya kutumia mbegu bora zinazozalishwa kituoni hapo kama za korosho, ufuta na muhogo.
  
(mwisho)
Read More

Friday, July 3, 2020

WAZIRI MKUU AFUNGUA MAONESHO YA 44 YA BIASHARA

*Asema Serikali itaendelea kuviwezesha viwanda vidogo, vya kati
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ili kuviwezesha viwanda vidogo sana, vidogo na vya kati kukua na kufanya kazi kwa tija zaidi.

Ametoa kauli hiyo leo jioni (Ijumaa, Julai 3, 2020) wakati akifungua rasmi Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (44TH DITF) yaliyoanza Julai mosi, 2020 kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu ambaye amefungua maonesho hayo kwa niaba ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli amesema ili nchi iweze kuwa na mafanikio makubwa, taasisi za kifedha hazina budi kuweka mikakati ya kutoa huduma ya mikopo rafiki ili kuwezesha ukuaji wa viwanda kwa kuzingatia viwanda vidogo na vya kati ikiwemo vinavyoratibiwa na SIDO katika kila mkoa.

“Taswira hii ya maendeleo ya sekta ya viwanda inafanana na taswira ya maendeleo ya viwanda katika nchi karibu zote duniani. Kwa mfano, Japan, viwanda vidogo sana, vidogo na vya kati vinachukua takribani asilimia 99 ya sekta ya viwanda; Kenya asilimia 98; Malaysia asilimia 97.3; Indonesia asilimia 99.9; Canada asilimia 98 na Ujerumani asilimia 99.”

Amesema Serikali inaendelea kuimarisha sekta ya biashara na viwanda nchini ili kuchochea maendeleo ya nchi kwa ujumla. Akielezea mafanikio ya Serikali katika kipindi cha miaka mitano, Waziri Mkuu amesema: “Jumla ya viwanda vipya 8,477 vimejengwa na kuchangia kuzalisha ajira mpya 482,601… mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa kwa mwaka 2019 ulikua kwa asilimia 8.5 ikilinganishwa na asilimia 8.05 mwaka 2018, sawa na ongezeko la asilimia 0.45.”

Amesema mchango huo, ni matokeo ya kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji wa bidhaa viwandani nchini ambao unaendelea kuimarika na kukua vizuri. Akitoa mfano, Waziri Mkuu amesema mwaka 2019, bidhaa za viwanda zilikuwa na thamani ya sh. trilioni 10.2 ikilinganishwa na sh. trilioni 9.6 mwaka 2018 ambao ukuaji wake ni sawa na asilimia 5.8.

Kuhusu viwanda vidogo na biashara ndogo, Waziri Mkuu amesema sekta hiyo inaendelea kutoa mchango mkubwa katika pato la taifa wa wastani wa asilimia 35 kwa mwaka. “Kwa mwaka 2019/2020, jumla ya miradi 304 inayohusiana na ujenzi wa viwanda imesajiliwa ambayo inatarajiwa kuongeza jumla ya ajira 11,793.”

Amesema SIDO imeratibu na kuhudumia viwanda vidogo vipya 1,400 vinavyotoa ajira 4,200. “Sekta hii muhimu imeajiri Watanzania zaidi ya milioni tisa ikiwa ni ya pili kwa sekta za kiuchumi katika kutoa ajira baada ya sekta ya kilimo,” ameongeza. 

Amesema maendeleo ya uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini yameongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo bidhaa za chuma, saruji, vigae, nguo na mavazi, ngozi na bidhaa za ngozi, kusindika nyama, chakula, mbogamboga na matunda, maziwa, mafuta ya kula, sukari, vifungashio, mbolea, dawa za binadamu, sabuni na sigara pamoja na ubanguaji wa korosho.  

Kwa upande wa biashara, Waziri Mkuu amesema utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reform to Improve Business Environment umewezesha maboresho ya tozo 173 ambapo kati ya tozo hizo, tozo 163 zimefutwa na tozo kero 10 zimepunguzwa viwango.

“Kati ya tozo zilizofutwa, 114 ni za sekta ya kilimo na mifugo, tano ni za Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), 44 za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka za Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), utalii, maji, uvuvi na iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).”

Amesema tozo zilizopunguzwa za GCLA, zimewezesha kuhamisha jukumu la usimamizi wa masuala ya chakula kutoka iliyokuwa TFDA kwenda TBS ili kuondoa muingiliano wa majukumu. “Maboresho hayo yamesaidia kuondoa urasimu na kupunguza gharama za kufanya biashara,” amesisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maonesho hayo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema kati ya mwaka 2015 na 2019, viwanda 8,477 vilianzishwa katika maeneo mbalimbali nchini ambapo kati ya hivyo, viwanda 201 ni vikubwa, 460 ni vya kati, 3,406 ni vidogo na 4,410 ni vidogo sana.

“Uwepo wa viwanda vyetu vya ndani, ulitusaidia hata wakati wa janga la corona tuliweza kutengeneza barakoa, mavazi ya watoa huduma, vitakasa mikono na bidhaa nyingine nyingi.”

Akisisitiza matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini, Waziri Bashungwa amesema: “Hakuna soko endelevu na lenye uhakika kama soko la ndani. Kwa hiyo, wazalishaji wa ndani wazalishe bidhaa zenye ubora, na Watanzania wapende kununua bidhaa za ndani. Kwa njia hiyo, tutaimarisha soko la ndani na kulinda viwanda vyetu,” alisisitiza.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TanTrade, Dkt. Ngw’anza Kamata alisema kutokana na changamoto ya COVID 19, mwaka huu idadi ya washiriki imepungua kiasi. “Washiriki wa ndani wamepungua kutoka 3,250 hadi 2,837 wakati wa washiriki wa nje nao wamepungua kutoka 520 hadi 43,” alisema.  

(mwisho)
Read More

MAJALIWA AFUNGUA MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DAR ES SALAAM

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipunga baada ya kukata utepe wakati alipofungua  Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya  Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda, Mhandisi Stella Manyanya, Waziri wa Biashara na Viwanda, Innocent Bashungwa,Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro na kulia ni Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mashine ya kuranda na kuweka urembo kwenye mbao wakati alipotembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO) kabla ya kufungua Maonyesho  ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya  Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020. Kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na wa tatu kulia ni Kaimu Mkurugenzi  wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO), Shoma Kibende.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kufungua Maonyesho  ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Nnee ya Dar es salaam, Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020.Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda, Mhandisi Stella Manyanay, Waziri wa Biashara na Viwanda, Innocent BashungwaNaibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro na kuliani Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya  Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya  Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Maonyesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya  Dar es salaam , Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam, Julai 3, 2020.


Read More