Thursday, February 27, 2025

WAZIRI LUKUVI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA SHIRIKA LA FAO

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu uliyopo katika Mtaa wa posta Jijini Dodoma.

Ujumbe huo kutoka FAO umefanya ziara ya wadau wa ufadhili wa Mfuko Nyumbulifu wa Uchangiaji kwa Hiari (Flexible Voluntary Contribution - FVC) iliyohusisha  Waheshimiwa Mabalozi wa Ubelgiji na Uswisi, Wawakilishi wa Kudumu FAO katika Umoja wa Mataifa, Rome, Washauri Waandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDC) na Viongozi Waandaamizi wa FAO Makao Makuu.

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kuwezesha washirika (partners) kupata uelewa wa utekelezaji wa programu na miradi inayofadhiliwa kupitia Flexible Voluntary Contribution (FVC) nchini Tanzania, kuongeza uelewa, muonekano na fursa zinazopatikana kwenye FVC kama mfuko nyumbulifu wa utoaji misaada ili kuweza kufikia malengo ya kimkakati Kitaifa na Kimataifa kupitia FAO.



Read More

Wednesday, February 26, 2025

TAARIFA ZA AWALI ZA TAADHARI ZA MAAFA ZITOKE KWA WAKATI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi ameelekeza Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura kujiratibu vizuri katika kufikisha taarifa zote za taadhari ya maafa kwa wakati ili utekelezaji wake ufanyike mapema kabla ya madhara kutokea.

Kauli hiyo ametoa leo alipotembelea Kituo cha Ufuatiliaji wa Majanga Katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma.

" kwa nafasi mliyonayo na teknolojia mnazotumia mnaweza kujua na kutoa taarifa zote za tahadhari bila urasimu, ili kuepuka athari kubwa za maafa zinazoweza kutokea baadae."alisisitiza Waziri Lukuvi.

Aidha muangalie na uwezekano wa kurahisisha mawasialiano ya taarifa zote za tahadhari ziweze kupatikana kila siku kwa njia ya simu ili kila mtu anayeenda kwenye shughuli ajue na achukue tahadhari.

“huduma hii iwe bure na ipatikane muda wote ili wananchi waingie wasome na wachukue tahadhari, na tutakuwa tumefanya kazi yetu vyema,” alisema

Naye Mkurugenzi Msaizidizi anaye simamia  Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi: Jane Kikunya amelezea kuhusu ufanyaji kazi wa kituo hicho kwamba kinajukumu kubwa la kufuatilia majanga ikiwa ni pamoja kushirikiana na taasisi mbalimbali katika ngazi ya kitaifa katika kutoa taarifa za awali za tahadhari kwa ngazi mbalimbali.

Amefafanua kwamba katika Ngazi ya Mikoa kuna vituo vya maafa vinapaswa kuanzishwa na jukumu hilo limeainishwa katika sheria ya maafa ya mwaka 2022 ambayo imeeleza kila Mkoa, kuwa na kituo cha usimamizi wa maafa ili kufanya ufuatiliaji wa majanga yanayoweza kutokea katika eneo la Mkoa husika.

Hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu inafanya ufuatiliaji wa uanzishwaji wa vituo hivyo ambapo wameweza kukutana na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa ambao kisheria wamepewa jukumu la usimamizi wa vituo hivyo ili kujengeana uelewa wa miongozo na namna ya uanzishaji na usimamizi wa vituo hivyo.

“Vituo hivyo vya Mikoa vitaunganishwa na mifumo ya Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu ili waweze kufanya ufuatiliaji kwa karibu,” alibainisha Bi. Jane.



Read More

Saturday, February 22, 2025

WAZIRI LUKUVI AMSHUKURU RAIS SAMIA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi amesema Serikali ya Awamu ya Sita imekamilisha kiu na ndoto za Iringa kwa kuanza ujenzi bararaba ya kiwango cha lami kwenda Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na upanuzi wa ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Iringa.

Waziri ametoa Kauli hiyo wakati aliposhiriki katika tukio la kurejesha wa safari za ndege za shirika la ndege Tanzania (ATCL) Mkoani Iringa iliyoongozwa na Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa.

Amesema wazo la Ujenzi lilikuwa la Muda Mrefu tangu enzi za TANU lakini Mungu amemleta Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yote mawili utekelezaji wake umefanyika, hivyo hatuna budi kumshukuru.

“Tunatarajia ujenzi wa babarara ya Pawaga kuanzia Pawaga Kuja Mjin, tunategemea barabara hiyo ikikamilika tuanze kusafirisha mpunga unaozalishwa kutoka Pawaga  kusafirishwa na shirika la ndege la Tanzania (ATCL),” alibainisha.



Read More

Tuesday, February 18, 2025

WAZIRI LUKUVI AKUTANA NA WADAU WA SEKTA BINAFSI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa Sekta binafsi katika kikao kilichoratibiwa na Baraza la Taifa la Biashara (TNBC).

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Magogoni Jijini Dar es salaam, kilicholenga kujadili ushiriki wa Sekta binafsi katika kuboresha mazingira ya biashara kwa kuangalia fursa za uchumi ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati ya kutumia fursa hizo vizuri na kushauri Serikali katika maeneo yanayohitaji kuboreshwa.

Akizungumza katika kikao hicho Rais wa Shirikisho la Sekta Binafsi Bi. Angelina Ngalula amesema Sekta binafsi ndio injini ya kusukuma uchumi, inayochukua fursa zote zinazofunguliwa na serikali kama mabadiliko makubwa ya sheria na taratibu, kutolewa kwa tozo inalenga kutoa fursa kwa sekta binafsi kuwekeza na kupata mafanikio.

“Katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani umefanya kazi kubwa sana katika uwekezaji wa miundombinu ambayo imesaidia katika kuchochea biashara," alieleza Bi. Angelina

Akichangia kuhusu Sekta ya Kilimo Bi. Jacqueline Mkindi amesema sekta ya kilimo na mifugo imenufaika sana kwa sababu ya nguvu ya serikali kutangaza diplomasia ya uchumi na kueleza kuwa umeongeza uhitaji wa bidhaa za Tanzania nje ya Nchi.




Read More

Wednesday, February 12, 2025

WAKURUGENZI WA UFUATILIAJI NA TATHMINI NGAZI YA WIZARA WAKUTANA KUPITIA TAARIFA YA UTENDAJI WA SERIKALI



Imeelezwa kwamba jukumu la Ufuatiliaji na Tathmini ni muhimu katika kuboresha utendaji wa Serikali kwa ujumla hivyo kusaidia kutoa msukumo wa kuboresha Miundo na Mifumo kwaajili ya kuandaa Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini Ili kuimarisha U&T ndani ya Serikali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Sakina Mwinyimkuu alipomuwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. James Henry Kilabuko, katika Kikao kazi cha wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini na Maafisa kutoka katika Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya wizara kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa lengo la kupitia Taarifa ya Utendaji wa Serikali (Government Performance Report kwa Mwaka wa Fedha 2023/24).

Alisema dhumuni kubwa ni kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji huduma bora kwa wananchi hivyo wataalam wa Vitengo mnapaswa kusimamia na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyoainishwa katika mipango ya serikali.

Nitoe rai kwa wataalam kutofanya kazi kwa mazoea, uoga au kutojiamini, kwani kwa kufanya hivyo serikali haitafikia malengo nhivyo kupunguza umuhimu wa kuanzisha Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini. Hivyo

 “ni vema kufanya ufuatiliaji na tathmini kuwa nyenzo ya msingi ya kusaidia utendaji wa taasisi, sekta na nchi kwa ujumla,”alifafanua Bi, Sakina

Ikumbukwe kwamba

Kikao kazi hicho kitafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 12 hadi 13 februari 2025 kimelenga kutoa mafunzo ya Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini (U&T) katika taasisi za Serikali yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu



Read More

Saturday, February 8, 2025

WAZIRI LUKUVI AMPA KONGOLE MHE. WAZIRI MKUU

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amemshukuru na kumpongeza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu shughuli za Serikali.

Waziri Lukuvi ametoa pongezi hizo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Ngome Jijini Dodoma.

Alisema kuwa kazi ya Waziri Mkuu kwa Mujibu wa Katiba ni kuratibu shughuli zote za Serikali na chini yake yupo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati na watendaji wa Ofisi yake ambayo wanatekeleza majukumu hayo kwa weledi na ufanisi mkubwa.

“Wakati wa uratibu wa shughuli za Maafa watendaji mmefanya kazi kwa ushirikiano Mkubwa chini ya Uongozi wa Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mambo yameenda vizuri nchi nzima,” alisema Waziri Lukuvi

Aidha alifafanua kuwa kazi ya Ofisi ya Waziri Mkuu ni kuratibu Serikali ili kuwafahamisha namna Serikali inavyoendelea kutekeleza majukumu na kuhudumia wananchi.

"...kwa kuwa tuna nafasi ya kupata taarifa na kuzifanyia uchambuzi ili kujulisha umma kwa njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari basi tuendelee kuratibu vyema taarifa na kuzitoa kwa usahihi ndiyo jukumu letu kubwa na lamsingi lazima tujipange ili ziweze kutoka kwa wakati alisema,” Waziri Lukuvi.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi katika maneno ya utangulizi amesema Viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wamewatengeneza mazingira mazuri kwa watendaji kufanya kazi kwa furaha na amani.

Pia ameahidi kuimarisha ushirikiano miongoni mwao ili kuyafikia maelengo ya ofisi na Serikali kwa ujumla.

"Tuimarishe ushirikiano miongoni mwetu ili kazi zetu ziende kwa wepesi na ufanisi kwa kuamini kila mmoja ana mchango chanya kuhakikisha malengo yanatimia," alisema Dkt. Yonazi.

 


Read More

Tuesday, February 4, 2025

DKT. YONAZI AWAKUMBUSHA WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU KUENDELEA KUTEKELEZA MAJUKUMU KWA WELEDI



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya sera, bunge na uratibu Dkt. Jim Yonazi amewakumbusha watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ushirikiano, upendo, furaha na amani ili kuyafikia malengo ya ofisi hiyo.

Dkt. Yonazi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Watumishi Ofisi yake wakati wa mkutano wake na watumishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyopo Njedengwa Jijini Dodoma.

Dkt. Yonazi amesema ipo haja ya kila mtumishi kujifanyia tathmini katika utendaji wake wa kazi huku akizingatia miongozo na kanuni za utumishi wa umma na kusema kuwa, kila mtumishi anawajibika katika kuhakikisha ofisi inapata matokeo iliyoyakusudia na kwa ufanisi.

“Ni wakati sahihi kila mmoja kuilinda furaha aliyonayo awapo mahali pa kazi, isingefaa utoke nyumbani huna furaha na ufike eneo la kazi ukose furaha, ni vyema kuja eneo la kazi na kuipata furaha mara mbili  kwa kuzingatia mazingira yaliyorafiki katika kutekeleza majukumu,” alisema Dkt. Yonazi

Aliongezea kuwa kila mtumishi wa umma awe na desturi ya kuheshimu nafasi ya mwingine bila kujali tofauti zinazoweza kuwepo miongoni mwa watumishi hao.

“Ni vyema kila mtu akajali mwingine na ikumbukwe hakuna mtu mwenye uwezo mdogo wa kufanya kazi, jambo la msingi ni kuhakikisha ule uwezo uliopewa na Mwenyezi Mungu na Mafunzo mbalimbali unatumia vizuri na kuhakikisha unaleta matunda mazuri na kuleta maendeleo kwa Nchi yetu” alisema Dkt, Yonazi.

Sambamba na hilo aliwaeleza watumishi hao kuwa kila mmoja ni kiongozi katika eneo lake la kazi hivyo abebe dhamana hiyo kwa weledi na ufanisi mkubwa.

“.....kila mtumishi aliyepo hapa ndiye Katibu Mkuu kwenye eneo lake, kwa kubeba imani ya kwamba ni Katibu Mkuu anapaswa kuwa na nidhamu na bidii katika kazi ikiwa ni pamoja na kuwa mwaminifu,” alisema.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Dkt. James Kilabuko katika neno lake la utangulizi amewaasa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi na kuzingatia sheria za utumishi wa Umma huku akiwasihi kuimarisha umoja na mshikamano ili kuiletea Serikali maendeleo yake.

Naye Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Ofisi ya Waziri Mkuu Bi, Numpe Mwambenja ameomba watumishi kuendelea kujitathimini mienendo yao katika utumishi wa Umma kwa kufanya kazi vizuri na nidhamu na kuheshimu viongozi huku wakiheshimiana wao kwa wao.

Bi. Numpe alitumia nafasi hiyo kuupongeza uongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa namna unavyojali maslahi ya watumishi na ustawi wao kwa ujumla na kuwasihii watumishi kuendelea kutimiza wajibu kwa kuzingatia kauli ya “hakuna haki bila wajibu”.






Read More

Wednesday, January 8, 2025

WAZIRI LUKUVI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI JENGO JIPYA LA MAHAKAMA YA WILAYA MKOANI

 


Imeelezwa kwamba hali ya amani utulivu na ushirikiano unaosimamiwa na Viongozi Wakuu wa Nchi imesaidia katika kuleta chachu kubwa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi ametoa kauli hiyo leo  wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Mkoani ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Amefafanua kwamba uongozi wao bora; hatuna budi kuendelea kuwaombea viongozi wetu, kila mmoja kwa dini yake ili Mwenyezi Mungu awape afya na nguvu ya kuendelea kutuongoza kwa mshikamano.

Waziri Lukuvi amesema, “chini ya uongozi wao Tanzania Bara imetulia na Tanzania Visiwani imetulia na hivyo kuwezesha haya kufanyika na kuendelea kuchochea maendeleo makubwa, mwenye macho haambiwi tazama.”

Sote ni mshahidi wa hatua kubwa za maendeleo zinazoendelea kutekelezwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia uongozi wa awamu ya nane chini ya Mhe. Daktari Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Waziri Lukuvi amesema, mafanikio ya Serikali ya awamu ya nane yanaonekana wazi katika nyanja za siasa na utawala bora, uchumi, huduma za kijamii na namna utamaduni wa watu wa Visiwa vya Zanzibar unavyoenziwa na kuheshimika wakati wote.

Aidha Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imechukua hatua za makusudi kuja na mradi wa ujenzi wa jengo hili la Mahakama ya Wilaya pamoja na majengo mengine ya Mahakama za Mikoa na Wilaya kule Unguja na hapa Pemba ili kukabiliana na changamoto za miundombinu ya majengo.

“Ujenzi wa jengo hili ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa majengo saba ambao ulipangwa kufanyika katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 alisema,” Waziri Lukuvi.

Kwa upande wake Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla, Jaji Mkuu wa Zanzibar amesema Rais. Mhe. Daktari Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amewaheshimisha kwa kuwajengea majengo saba ya Mahakama za Mkoa na wilaya katika visiwa vyote vya unguja na pemba.

“Tumekusudia kusogeza huduma kwa wananchi kwa kujenga mifumo imara ya usimamizi wa haki ili kuboresha huduma zetu za mahakama kuwa za kisasa ,” alisema Mhe, Jaji, Khamis.

Naye Mhe, Valentina Katema, Mrajis wa Mahakama Kuu Zanzibar, amesema miundo mbinu ya majengo ya mahakama ipo katika muundo zamani hivyo kusababisha kushindwa kuendesha shughuli zake katika mazingira ya kisasa.

”Ujenzi wa majengo mapya ya Mahakama itasaidia, kupunguza msongamano wakati wa utoaji wa huduma na kusaidia wananchi kupewa huduma kwa kuendana na  mahitaji ya kisasa,” alisema Mrajis.



Read More

Thursday, December 19, 2024

WANANCHI WA HANANG' WAMSHUKURU RAIS SAMIA

 


Wananchi waliokumbwa na athari za maafa ya Maporomoko ya tope na mawe kutoka Mlima Hanang wametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa wema aliowatendea kwa ujenzi wa nyumba za makazi zilizojengwa katika eneo la Waret Wilaya ya Hanang' Mkoa wa Manyara.

Wametoa salamu hizo katika kikao cha ndani walichokutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi leo katika ukumbi wa Halmashauri Hanang' ikiwa ni maandalizi ya kuwakabidhi wananchi nyumba 109 zilizojengwa na Serikali tukio litakaloongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

Bw, Kizito Joackimu Mkazi wa Katesh "A" amesema Serikali iliweka jitihada kubwa kusimamia urejeshaji wa hali wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama nchini na kazi imefanyika kwa ubora na weledi.

“Mama Samia ni zaidi ya Mama hakulazimishwa na mtu kututendea wema alioufanya kwa wananchi wa Hanang', angeweza kutoa salamu za pole lakini akaona haitoshi, atoe vyakula vya kutosha, magodoro, matibabu ndugu zetu wametibiwa kwa kiwango kikubwa,” alieleza Bw, kizito.

Alifafanua, kwamba Kuna wananchi nyumba zao zilizoharibika zikiangaliwa thamani yake hazilingani na hizi zilizojengwa kwa ubora na kwa kuzingatia upatikanaji wa huduma muhimu za kibinadamu.

"nyumba hizi zitatufaa sana na kimsingi kuna watu walikuwa hawana ndoto za kuwa na nyumba zilizokatika mtaa mmoja wenye maji wenye umeme na eneo la biashara, tumebebwa sana na Serikali lazima tuwe na moyo wa shukrani," alisisitiza.

Wakitoa neno la shukrani wakati wa kikao hicho Bi. Fausta Magasa Mkazi wa Katesh, "A"amesema jambo hilo limewaletea furaha katika maisha yao na kusema ni la neema na baraka ambalo hawakulitegemea kutokea.

“Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mbegu ya upendo aliyoipanda kwa watu 109 ambayo itazaa vizazi na vizazi" alieleza Bi, Magasa.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi amesema wananchi watakaopewa funguo za nyumba kesho wataamua wao wenyewe siku watakayohamia kwenye nyumba  zao walizojengewa na serikali.

“Nimepokea Salamu za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nitaziwasilisha lakini naamini muwakilishi wenu atasema salamu zenu pia kesho wakati mnapokea hati ya nyumba, funguo za nyumba zenu na majiko ya gesi" alieleza Waziri Lukuvi.





Read More

Monday, December 16, 2024

DKT. YONAZI AMPONGEZA MHE. BALOZI MUTATEMBWA

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt Jim Yonazi amempongeza Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Anderson Mutatembwa kwa Kuteuliwa kuwa Balozi.

Dkt. Yonazi Ametoa pongezi hizo wakati akimuaga Mhe. Balozi Mutatembwa na Kumakaribisha Naibu katibu Mkuu mpya Dkt. James Kilabuko.

Dkt. Yonazi amempongeza Balozi Mutatembwa kwa kufanya kazi ya ushauri kwa utulivu aliyotokana hekima aliyojijengea na kujaliwaa na Mwenyezi Mungu kuwa nayo “Na ndiyo maana Mhe. Rais ameweza kukuamini na kukuteuwa katika nafasi ya Ubalozi ili uweze kumuwakilisha yeye pamoja na Nchi katika maeneo ambayo atakayoona inampendeza.” Alifafanua

Aliendelea kusema kuwa, nafasi ya ubalozi ni nafasi nyeti na adhimu sana na ni fursa inayopatikana kwa watu wachache sana, “umepata fursa nyeti sana ya kuitumikia Taifa naamini utaendelea kufanya kazi kama ambavyo umekuwa ukifanya hapa na utakaoenda kufanya nao kazi watafaidika na kufurahia kama tulivyo faidika sisi.” Alibainisha Dkt. Yonazi

Akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu mpya Dkt. James Kilabuko, Katibu Mkuu Dkt. Yonazi alisema Ofisi ya Waziri Mkuu ni Ofisi yenye majukumu mazito yenye watumishi wachapakazi wenye kutizama tija katika utendaji wa majukumu yao ya kila siku.

Naibu Katibu Mkuu, Dkt. James Kilabuko Alimshukuru Mhe. Rais kwa kumteuwa katika nafasi hiyo na kuona kwamba anaweza kumsaidia Katibu Mkuu Kiongozi katika nafasi hiyo, aliendea kusema kuwa anategemea kupata ushirikiano kutoka kwa Watumishi na Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika kumsaidia Katibu Mkuu Dkt. Jonazi kiutendaji na kufikia malengo yanayotegemewa na mamlaka za juu.

Kwa Upande wake Mhe. Balozi Anderson Mutatembwa, alimshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea Kumuamini na kumteuwa katika nafasi hiyo.

Aidha, Ameishukuru Menejimenet ya Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu pamoja na watumishi wa Ofisi hiyo kwa ushirikiano waliomupatia wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ofisini hapo, aliendelea kusema kuwa ni sehemu ambayo atapakumbuka kwani amefanya kazi kwa amani na Utulivu wa hali ya juu.

 

Read More

Saturday, December 14, 2024

MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHMNI KWA WIZARA, IDARA ZINAZOJITEGEMEA, WAKALA WA SERIKALI NA MASHIRIKA YA UMMA YAFANYIKA JIJINI TANGA

 


Afisa Muandamizi wa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw.Charlton Charles Meena amewataka washiriki wote wa mafunzo ya awamu ya kwanza ya ufuatiliaji na tathmni yaliyoshrikisha wizara, idara zinazojitegemea, wakala wa serikali na mashirika ya umma kuwa na mundelezo mzuri wa mafunzo ya awamu zote tatu ili kuweza kujipambanua vizuri katika utendaji wa kazi zao.

Kauli hiyo ameitoa Jijini Tanga wakati wa kuahirisha mafaunzo ya ufutiliaji na tathimini yaliyofanywa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kupitia kitengo chake maalumu cha ushauri wa kitaalam na kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) pamoja na washirika wengine Ofisi ya Msajili wa Hazina, yaliyofanyika katika ukumbi wa New Kiboko Hall Jijini Tanga kwa muda wa siku tatu.

Ameeleza kwamba Mafunzo yameshirikisha watumishi wa umma zaidi ya 200, na yamewawezesha washiriki kujifunza kutofautisha na kutumia ipasavyo aina tofauti za Ufuatiliaji na Tathmini, kuamua jinsi ya kufuatilia na kutathmini miradi, mipango ya kimaendeleo na sera ikiwa ni pamoja na kuweka bayana matokeo muhimu katika ngazi ya programu kwa kutumia mfumo wa kimantiki (Logical Framework) au miundo ya nadharia ya mabadiliko (Theory of Change).

Bw, Meena, alisema “mafunzo yamelenga kuunda viashiria sahihi (SMART), kwaajili Ufuatiliaji na Tathmini, kutumia zana mbalimbali za Ufuatiliaji na Tathmini kwaajili ya ukusanyaji na uchanganuzi wa takwimu, kubuni na kusimamia Tathmini kwa kutumia kanuni za Kiafrika za Tathmini na vigezo vya OECD-DAC na kuandaa ripoti bora za Ufuatiliaji na Tathmini kwaajili ya matumizi ya Serikali, Idara, Wizara, Mashirika na Wakala za Serikali.

Aidha kutokana na umuhimu wa mafunzo hayo, Chuo Kikuu Huria kitaendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, pamoja na Msajili wa Hazina kuandaa awamu nyingine ya mafunzo ya awamu ya kwanza ili kuweza kuzifikia baadhi ya Wizara, Idara zinazojitegemea, mashirika na wakala za serekali ambazo zilishindwa kuleta watumishi kwenye awamu hii ya kwanza ya mafunzo.

“ni vyema kujenga uelewa wa pamoja  sasa,  kwasababu kutakua na awamu ya pili na ya tatu ambazo zitawezesha  watumishi kubobea katika eneo la Ufuatiliaji na Tathmini wa shughuli za Serikali na hivyo kuboresha utendaji kazi wa serikali na utoaji huduma kwa wananchi,” alibainisha.

 

Read More

Friday, November 29, 2024

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA USAMBAZAJI WA RIPOTI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI 2022-2023

 


Waziri Afya Mheshimiwa Jenista Mhagama amezindua Usambazaji wa Ripoti ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI 2022-2023 Mkoani Ruvuma.

 Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma alieleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika juhudi za kudhibiti maambukizi ya UKIMWI nchini Tanzania ambapo imeelezwa kuwa kiwango cha Maambukizi Mapya kimepungua huku akipongeza juhudu zinazofanywa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Nchini

"Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kiwango cha maambukizi ya UKIMWI nchini kimepungua kwa kiasi kikubwa kutoka asilimia 7 mwaka 2022 hadi asilimia 4.4 mwaka 2023. Aidha, juhudi za kupunguza maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto zimezaa matunda, ambapo kiwango cha maambukizi kimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2010 hadi asilimia 8.1 mwaka 2023," alisema Waziri Mhagama

Waziri Mhagama alieleza kuwa mafanikio haya yametokana na juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, sekta binafsi, na jamii katika kuimarisha programu za utoaji elimu, upimaji wa hiari, na matumizi ya dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI (ARVs).

Alisisitiza umuhimu wa kuendelea na juhudi hizi ili kufikia malengo ya kumaliza maambukizi mapya ya UKIMWI, hasa kwa watoto, ifikapo mwaka 2030. Vilevile, aliwahimiza wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na maambukizi na kufuata ushauri wa kitaalamu.

Aidha alitoa wito kwa jamii kuunga mkono mikakati ya kitaifa ya kupambana na UKIMWI ili kuhakikisha maendeleo ya afya ya jamii na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga, amesema Watanzania wamepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU)ambapo asilimia 98 ya Watanzania wanaohitaji dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo (ARVs) sasa wanatumia dawa hizo, hatua ambayo imevuka malengo yaliyowekwa kitaifa na kimataifa.

Mhe. Ummy alibainisha kuwa mafanikio haya ni matokeo ya jitihada za serikali chini ya Mhe. Dkt . Samia Suluhu Hassan, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwemo utoaji wa elimu ya afya, upimaji wa hiari, na utoaji wa dawa kwa urahisi katika vituo vya afya.

Pia ametumia nafasi hiyo kuhimiza wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuendelea kutumia dawa kwa walioambukizwa ili kuboresha maisha yao na kupunguza maambukizi mapya.

Serikali inaendelea kuweka mikakati imara kuhakikisha kila Mtanzania anayehitaji huduma za matibabu anazipata kwa wakati.

Maadhimisho ya Wiki ya UKIMWI Duniani yanaadhimishwa Kitaifa mkoani Ruvuma yenye kauli Mbiu isemayo "Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI"



Read More

Thursday, November 21, 2024

DKT. YONAZI ASHUKURU MICHANGO INAYOENDELEA KUTOLEWA, AFAFANUA NAMBA SAHIHI YA KUTUMA MICHANGO MAAFA KARIAKOO

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera,Bunge na Uratibu  Dkt. Jim Yonazi amewashukuru wadau mbalimbali wanaoendelea kujitolea na kutoa michango kwa ajili ya maafa ya Kuporomoka kwa ghorofa eneo la Kariakoo kusema ni moyo wa upendo unaoneshwa kwa matendo mbalimbali walioguswa na maafa hayo.

Ametoa shukrani hizo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu hatua zinavyoendelea katika eneo lililopatwa na ajali ya kuporomoko kwa jengo la ghorofa mtaa wa Agrey Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Yonazi ametumia nafasi hiyo kutangaza “Control Number” kwa ajili ya kuwawezesha wananchi ambao wataguswa na maafa hayo kwa kutuma michango yao kwa ajili ya kuendelea kusaidia katika hatua baada ya kutokea maafa hayo.

" Control number ni 987320001709 ambapo namba hii inatumika kwa mitandao yote ,mwananchi anaweza kuchangia kuanzia 1000 na kuendelea na fedha hizi zinaingia moja kwa moja kwenye akaunti ya Maafa au kuchangia kupitia akaunti ya National Relief Fund yenye namba 9921159801 ambayo ipo Benki Kuu ya Tanzania,” amesema Dkt.Yonazi.

Kwa hatua nyingine Dkt. Yonazi amepokea msaada kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) lililokabidhi kiasi cha shilingi za Kitanzania Milioni Ishirini kwa lengo la kusaidia kufuatia maafa hayo.

Akizungumza kabla ya kukabidhi hundi hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA, Jenerali mstaafu George Waitara amesema kuwa tukio hilo limesababisha maafa makubwa ikiwemo vifo,uharibifu wa mali pamoja na matatizo ya kisaikolojia kwa waathirika wa tukio hilo.

"TANAPA ni sehemu ya wananchi wa Tanzania,hivyo janga hili tumetugusa tukaona tutoe chochote kusaidia uokoaji wa maafa haya na Watanzania wasiwe na taharuki kwani tumeona shughuli za uokoaji zinakwenda vizuri, kikubwa wawe wanafuatilia taarifa kupitia mamlaka husika na si vyanzo vingine " amesema Jenerali Mstaafu Waitara.











Read More

Tuesday, November 19, 2024

SERIKALI YAONGEZA SAA 24 ZA ZIADA ZA UOKOZI KARIAKOO

Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Thobias Makoba, amesema zoezi la uokoaji wa watu walionasa kwenye jengo lililoporomoka Jumamosi ya Novemba 16, 2024 Kariakoo kwenye Mtaa wa Congo na Mchikichi Jijini Dasr es Salaam, litaendelea tena kwa saa 24 za ziada baada ya saa 72 za kawaida za kiwango cha kimataifa kumalizika.

Bw. Makoba ameyasema hayo, wakati akizungumza na waandishi wa habari Kariakoo kwenye eneo la tukio, ambapo amesema kuongezeka kwa saa hizo 24 za ziada, ni agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, alilolitoa kupitia kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa, katika kikao cha tathmini kuhusu zoezi hilo la uokoaji ambapo amelitaka jeshi la zimamoto na uokoaji, kuendelea na shughuli hiyo ili kunusuru uhai wa watu ambao bado wamekwama kwenye jengo hilo.

“Tukiwa kwenye kikao cha tathmini cha kazi inayoendelea, moja ya ajenda iliyozungumzwa ni kuhusiana na utaratibu wa uokoaji, kulianza kutokea maneno kwenye mitandao ya kijamii kwamba baada ya masaa 72 kwa kawaida kwa viwango vya kimataifa, zoezi la uokoaji kwenye maeneo kama haya linabadilika, na wanaanza kutumia mashine pale inapolazimu, sasa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan muda huu ametoa maelekezo kupitia kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, na maelekezo hayo yaje kwa kikosi chetu cha Zimamoto na Uokoaji kwamba zoezi hili liendelee kwa saa zingine 24 za ziada, ni kwamba wasisitishe, kabla ya kubadili hatua yoyote, kwa hiyo zoezi hili linaendelea, halitasitishwa kama ambavyo wananchi wengine wameanza kuwa na hofu” amesema Bw. Makoba.

Amesema lengo ni kuhakikisha maisha ya watu walioko kwenye jengo hilo yanalindwa na kwamba hakuna kifusi kitakachowaangukia.

“Imempendeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba, tutaendelea kutumia mbinu ambazo zilikuwa zikitumika za weledi na ustadi zaidi katika kuhakikisha kwamba, kwanza tunaridhika kwamba hakuna ambaye aliyepo hai atasumbuliwa au ataangushiwa kifusi huko chini, au kwa namna yoyote ile itamkuta ili kumsababishia kupoteza maisha, baada ya masaa 24 tutatangaza utaratibu unaofuata” amesema Bw. Makoba.

Zoezi la uokoaji wa watu walionaswa kwenye jengo lililoporomoka linaendelea kwa kasi kubwa kwa siku ya nne sasa ambapo Serikali inafanya jitihada zote kuhakikisha hakuna madhara yatakayowapata watu walionasa kwenye jengo hilo.

 

Read More

NAIBU WAZIRI UMMY AWASHUKURU RED CROSS NA TPA KWA MISAADA YA VIFAA SAIDIZI MAAFA KARIAKOO


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga amewashukuru wadau kutoka Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross Tanzania) pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA kwa kutoa misaada ya vifaa saidizi kwa ajili ya kuendelea kusaidia katika zoezi la uokoaji linaloendelea kufuatia janga la kuporomoka jengo la ghorofa eneo la Congo na Mchikichi Kariakoo Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam.

Ametoa shukrani hizo hii leo na kueleza kuwa miongoni mwa vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na machela tisa (9) mashuka 100 kutoka Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross Tanzania) Pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA, reflectors pamoja na  cover white.

Naibu Waziri huyo ameendelea kutoa rai kwa wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza kuchangia huku akipongeza namna zoezi la uokoaji linavyoendelea kwa kushirikiana na wadau.








 

Read More

Monday, November 18, 2024

MAPITIO YA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP), YAWAKUTANISHA WATAALAMU PAMOJA NA UJUMBE KUTOKA- (IFAD) MJINI ZANZIBAR

 


Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Paul Sangawe ameongoza Kikao cha Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), wakurugenzi wa sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu pamoja na timu ya wataalamu.

Pamoja na mambo mengine kikao hicho pia kimehusu mapitio ya Mipango na Bajeti ya Programu kwa kipindi cha miaka minne ya utekelezaji iliyobakia.

Kikao  hicho kimefanyika Zanzibar, katika ukumbi wa Mkutano wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi.



Read More

MISAADA KWA AJILI YA WAATHIRIKA WA KUPOROMOKA KWA JENGO KARIAKOO ITOLEWE KWENYE AKAUNTI MOJA- DKT. YONAZI

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amesema msaada wa kifedha kwa ajili ya kusaidia walioathirika na kuporomoka kwa jengo la ghorofa Kariakoo Jijini Dar es Salaam unatolewa kwa akaunti maalum ya maafa ya 9921159801 ambayo ipo Benki Kuu ya Tanzania na kushughulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu hali inayoendelea katika zoezi la uokoaji.

Amesema akaunti hiyo ni pekee nchini ambayo inakusanya misaada ya kifedha kwa ajili ya maafa.

"Kuna watu wana nia njema kabisa ya kuwasaidia Watanzania, lakini naomba tujizuie kabisa kukusanya michango ya kifedha kutoka kwa mtu yeyote bila kupitia akaunti hii". Amesema Dkt. Yonazi.

Aidha amesema akaunti hiyo ni maalumu imethibitishwa na serikali ili kuweza kuhakikisha misaada inawafikia walengwa na inatimiza malengo ya kutoa misaada hiyo.

Amesema kwa sasa operesheni inaendelea mpaka pale watakapokamilisha zoezi la kuokoa baadhi ya watu ambao bado hawajaokolewa.



Read More

Sunday, November 17, 2024

KATIBU MKUU WA CCM DKT. EMMANUEL NCHIMBI AFIKA KARIAKOO, AUNGANA NA VIONGOZI WENGINE WAKATI WA ZOEZI LA UOKOAJI

 


Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Emmanuel Nchimbi afika Kariakoo Leo Novemba 17,2024 na kushuhudia zoezi la uokoaji akiwa ameongozana na viongozi wa Serikali na kujionea zoezi hilo linaloendelea  mara baada ya  kuporomoka kwa jengo la ghorofa Kariakoo kwenye mtaa wa Congo na Mchikichi Jijini Dar es Salaam.

Mawaziri hao ni pamoja na  Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godfrey Mollel, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga.



Read More

MAWAZIRI WAHAMIA KARIAKOO; KAZI YA UOKOZI INAENDELEA

 


Mawaziri wa kisekta wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi Leo Novemba 17,2024 wamekutana kwa ajili ya kuendelea na zoezi la uokoaji wa watu waliokwama kwenye jengo lililoporomoka Kariakoo kwenye mtaa wa Congo na Mchikichi Jijini Dar es Salaam.

Mawaziri hao ni pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godfrey Mollel, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Khamis na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga.



Read More

Thursday, November 14, 2024

TANZANIA YAVUTIA MATAIFA UWEPO WA KITUO CHA UFUATILIAJI WA MAJANGA

 

 

TANZANIA imeendelea kutolewa mfano wa kuwa na Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura (National Emergency Operation and Communication Center Situation Room) na kuelezwa kuwa nchi nyingine ziendelee kuiga mfano wa Tanzania na kuendelea kuwekeza katika mifumo ya tahadhali za mapema -early warning systems kwa kutumia vyanzo vya ndani, kushirikisha jamii na sekta binafsi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ameyasema hayo 13 Novemba, 2024 wakati wa Mkutano wa 29 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP-29) unaoendelea mjini Baku, nchini Azerbaijan.

Dkt. Yonazi amesema kuwa,Tanzania imeendelea kuwa kinara katika masuala ya menejimenti ya maafa hususan katika kuzuia, kupunguza kujiandaa na kukabili maafa pindi yanapotokea, huku akitaja mafanikio ya uwepo wa kituo cha ufuatiliaji wa majanga (situation room) ikiwemo ya kurahisisha ufuatiliaji wa mwenendo wa janga lililotabiriwa na kufanya uchambuzi wa kiwango cha madhara kwa jamii, miundombinu na mazingira.

Pia kituo hicho kimesaidia kuandaa taarifa za tahadhari ya mapema ya hatua za kuchukua ili kuzuia, kujiandaa na kukabili maafa, kuandaa taarifa ya mwenendo wa tukio na kusambaza kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya kusaidia uratibu na utekelezaji wa shughuli za kukabili na kurejesha hali pindi maafa yanapotokea.

Aidha alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wadau kuwezesha utekelezaji wa afua za usimamizi wa maafa katika eneo la mifumo ya tahadhali ya mapema.

Dkt. Yonazi ametumia jukwaa hilo kuyakaribisha Mataifa mbalimbali kuja kujifunza Tanzania namna Kituo hicho kinavyofanya kazi katika kuratibu mwenendo wa majanga kwa umahiri wa hali ya juu.

“Uwepo wa kituo hiki umewavutia wadau wengi kuja kujifunza huku wengine wakiahidi kuunga mkono juhudi za Tanzania katika masuala ya menejimenti ya maafa,” alisema Dkt. Yonazi






Read More