Saturday, May 25, 2024

KAMPUNI YA SANKU, YAPONGEZWA KWA KUJIKITA KATIKA URUTUBISHAJI WA VYAKULA NCHINI



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama amesema mahitaji ya virutubishi vya chakula ni ajenda kubwa ambayo itachochea katika kuongeza ajira kwa wakulima wetu na kuwa na uhakika na virutubishi tunavyovitumia hapa nchini.

Waziri amesema hayo alipotemebelea na kukagua kiwanda cha Sanku kilichopo Mwenge Jijini Dar es salaam leo tarehe 25/12/2024 na kujionea maendeleo ya kiwanda hicho cha uchanganyaji wa virutubishi kwenye unga wa mahindi na ngano kwa bei nafuu.

Naomba muendeele kufanya ufutailiaji wa karibu katika kutoa elimu ili kuondoa matatizo mengine ya udumavu, utapiamlo na shida ya kupungukiwa vitamini A kwa wakinamama wajawazito.

“Hii kazi ni kazi yenye manufaa makubwa na itaweza kutusaidia sana kama nchi tuweze kusonga mbele na kusaidia kuitangaza nchi kwa kuwa na kiwanda kikubwa cha kuchanganya virutubishi,” alisema Waziri Mhagama

Kwa upande wake Meneja Muandamizi wa Sanku Bw. Gwao Omari Gwao amesema kampuni yao inasaidia wafanyabishara wadogo na wakati kufanya urutubishaji ambazo zimefunguliwa katika Mikoa 26 Tanzania Bara na katika Halmashauri 142 Tanzania Bara.

 

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.