Wednesday, November 30, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE AZINDUA PROGRAM YA EDUCTAION PLUS

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene azindua program ya education plus inayolenga kuhakisha vijana balehe (wasichana na wavulana) wanawezeshwa kuishi maisha salama, yenye afya, na tija - bila ukatili wa kijinsia, VVU na UKIMWI.

Akizindua program hiyo hii leo novemba 30, 2022 wakati wa halfa ya kuhitimisha wiki ya Vijana katika kuelekea siku ya UKIMWI Duniani Mkoani Lindi Waziri wa Nchi amesema amefarijika kwa jitihada za Taasisi ya TACAIDS pamoja na wadau katika utekelezaji wa afua za masuala ya UKIMWI.

Alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana wote nchini kuzingatia jitihada za Serikali katika mapambano haya ya VVU na UKIMWI kwa kuendelea kujilinda na kulinda wengine huku wakijiepusha na tabia hatarishi.

“Rai yangu kwa vijana wote nchini, hususani wasichana, fanyeni kila muwezalo ikiwa ni pamoja na kuzingatia maudhui ya kampeni mbalimbali ili kujikinga na maambukizi ya VVU. Wale mlio shuleni na vyuoni hakikisheni mnaweka mkazo katika Elimu na kujiepusha na tabia zote hatarishi zinazopelekea kupata maambukizi ya VVU.”alisema

Aidha, aliwasihi vijana walio nje ya shule na vyuo, kuzitumia fursa zilizopo katika kuviwezesha vikundi vya vijana kujiinua kiuchumi hii itasaidia kujiepusha na tabia za kukaa vijiweni na kushawishika kujiingiza katika vitendo vinavyopelekea kuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Akieleza hali ya maambukizi nchini Waziri Simbachawene alisema katika kuelekea lengo la sifuri ya maambukizo mapya, kama nchi maambukizo mapya yameendelea kushuka mwaka hadi mwaka, japokuwa sio kwa kasi ya kuridhisha. Kwani, hadi sasa takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 54,000 waliambukizwa VVU mwaka 2021 nchini. Hii ni sawa na takribani watu 4,500 kwa mwezi au watu 150 kwa siku.

“Vijana wenye umri wa miaka 15-24 ndio kundi ambalo linaonyesha kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizo mapya, kwani katika watu wote wanaopata maambukizo mapya ya VVU kila mwaka, takribani Asilimia 30 ni vijana wenye umri wa miaka 15-24 (yaani katika kila watu 10 wanaopata maambukizo mapya ya VVU watatu ni vijana wa umri huu),”alisisitiza

katika kundi la vijana wa miaka 15-24 wanaopata maambukizo mapya, takriban Asilimia 70 ni wasichana. Katika mwaka 2021, kulikuwa na maambukizi mapya 212 kila wiki kwa kundi la wasichana wa miaka 15 -24, Inamaanisha maambukizi mapya 30 kila siku.

 

 

Read More

Tuesday, November 29, 2022

SERIKALI YALENGA KUIMARISHA USAWA MAPAMBANO VIRUSI VYA UKIMWI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amepongeza Tume ya kudhibiti UKIMWI, Wizara ya Afya na Wizara ya TAMISEMI katika Mkakati wa kupambana na Ukimwi kama janga la kitaifa.

Hayo yamesemwa Waziri na Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene Jijini Dar es saalam, wakati wa uzinduzi wa taarifa ya hali ya UKIMWI duniani yenye Kauli Mbiu inayosema Dangerous Inequalities iliyotolewa Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi Duniani UNAIDS Bi, Winnie Byanyima.

“Serikali imedhamiria kuweka usawa wa kijografia usawa kimazingira usawa kati ya watoto na wakubwa na usawa wa kiuchumi ili kuhakikisha watu wote wanapata huduma sawa ili wasiathirike na wale walio athirika wapate huduma za matibabu lakini pia huduma sawasawa kuhakikisha wanaendesha maisha yao.”

Akitoa taarifa hiyo Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi Duniani UNAIDS Bi, Winnie Byanyima amesema Tanzania imejitahidi kupunguza Ongezeko la Maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kila Mwaka kwa miaka kumi mfululizo.

“Tanzania Imejitahidi kupunguza vifo vinavyosababishwa na UKIMWI na imekuwa ikifanya vizuri katika mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI.”

 

Read More

Monday, November 28, 2022

MHE. KATAMBI: JITIHADA ZA PAMOJA NI MUHIMU KATIKA KUTOKOMEZA VVU TANZANIA

 


NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi amesema, jitihada za pamoja kati ya Serikali, wadau mbalimbali nchini wakiwemo wananchi ni muhimu katika kutokomeza maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) nchini.

Mheshimiwa Katambi ameyasema hayo Novemba 28, 2022 katika Ukumbi wa Sea View Beach Resort mkoani Lindi wakati akifungua Kongamano la Kisayansi katika Wiki ya kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani.

"Napenda kuwakumbusha kuwa pamoja na mafanikio makubwa tuliyoyapata katika mapambano dhidi ya UKIMWI nchini ambapo idadi ya maambukizi mapya ya VVU pamoja na vifo vinavyotokana na UKIMWI kupungua sana na idadi ya watu wanaoishi na VVU kupata tiba.

"Bado tunayo maeneo ambayo juhudi zaidi zinahitajika. Maeneo haya ni pamoja na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na tiba kwa watoto chini ya miaka mitano. Pia kuna baadhi ya makundi yako nyuma katika kufikiwa na huduma za VVU na UKIMWI kama wanaume,vijana na makundi maalumu yalio katika hatari kubwa ya maambukizi ya VVU,"amesema Mheshimiwa Katambi.

Pia amesema,kongamano hilo la kisayansi limekuwa likifanyika kwa miaka mingi toka mwaka 2016 kama sehemu ya maadhimishio ya kuelekea siku ya UKIMWI duniani.

 

Kupitia kongamano hili, jumuiya ya wanasayansi wanapata nafasi ya kuungana na jamii kubwa zaidi katika kutafakari na kubadilishana mawazo, uzoefu pamoja na mbinu mpya za kisayansi za kupambana na janga la UKIMWI,

"Hivyo, kongamano la mwaka huu ni muhimu sana kwa kuwa Dunia pamoja na Taifa letu limeweka muelekeo mpya wa mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambapo kwa pamoja tumeamua kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

"Ili kutekeleza azima hiyo Dunia kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa linalishughulikia UKIMWI (UNAIDIS) limeandaa mkakati Mpya wa kuelekea lengo hilo (Global AIDS Strategy 2021-2026). Nasi kama taifa pia tumeandaa mikakati mipya ya Kitaifa na kisekta (Mkakati wa Taifa wa Sekta zote NMSF V na Mkakati wa Sekta ya Afya HSHSP V) ili kutekeleza azimio hilo,"amefafanua Mheshimiwa Katambi.

Pia amesema, kongamano hilo linafanyika chini ya kauli mbiu ya Equalize (Imarisha Usawa) ambapo litatoa nafasi ya wadau kujadili mbinu mpya na namna bora ya kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI katika huo muktadha mpya.

"Nimefahamishwa kuwa kongamano hili la siku mbili litahusisha wataalamu mbalimbali wakiwemo wanasayansi, watoa huduma za VVU na UKIMWI, wawakilishi mbalimbali wa jamii zinazotumia huduma hizo,wasimamizi na wadau wa maendeleo pamoja na wajumbe toka sekta mbalimbali.

"Inatarajiwa jumla ya mawasilisho 26 yatatolewa kwa njia ya muhadhara na mengine mengi kama mchapisho. Mawasilisho yote yamegawanyika katika mada kuu nane. Mgawano huu utatoa nafasi ya mijadala kuelekezwa katika maeneo makuu ya muitikio wa VVU na UKIMWI nchini,"amesema Mheshimiwa Katambi.

Wakati huo huo, Mhesshimiwa Katambi amesema fursa hiyo itakuwa muhimu katika kuweka nguvu mpya kuhakikisha mafanikio yaliyokwishapatikana mpaka sasa yanaendelezwa na makundi yaliyoachwa nyuma yanafikiwa kwa haraka na kwa ufanisi zaidi ili kufikia malengo ya kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

 

"Ninatambua kwamba katika makongamano kama haya, huwa kunaweza kuwa na tofauti kubwa ya kiwango cha uelewa wa mada pamoja na tofauti ya mitizamo. Nina waomba watoa mada kutumia lugha nyepesi katika kutoa mada zao ili kurahisisha ujumbe kufikia wajumbe na kupata uelewa wa pamoja na pia kwa wajumbe kuwa wasikivu pia wavumilivu pale ambapo sayansi inaelekeza mambo ambayo ni tofauti na mitizamo yao.

"Kusikia mada ni jambo moja na kutekeleza maelekezo ya kisayansi ni jambo tofauti. Ninapenda kuwashauri kuwa, ili tuweze kufanya mageuzi katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kupata matokeo chanya, hatuna budi kuzingatia zaidi ushauri wa kisayansi.

"Ninawaomba wote tutakapomaliza kongamano hili kila mmoja wetu kupitia asasi yake kufanya mapitio ya pamoja ya jinsi mada zilizowasilishwa hapa zinaweza kuboresha utendaji kazi wao na kufanya marekebisho stahiki. Ushirikiano kati ya asasi zinazotekeleza afua zinazofanana ni fursa muhimu ya kuanza kutekeleza mambo yale tuliyojifunza katika kingamano hili,"amebainisha Mheshimiwa Katambi.

Read More

Sunday, November 20, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE, AHIMIZA MAFUNZO YA ITIFAKI KUWA ENDELEVU


Waziri wa Nchi wa Ofisi ya Waziri Mkuu sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema ipo haja, mafunzo ya itifaki na uratibu wa maadhimisho kufanyika kila mwaka.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene wakati akifunga mafunzo kwa watendaji wa serikali yaliyohusu itifaki ya viongozi wa kitaifa iliyowakutanisha Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa yaliyofanyika Mkoani Singida.

“Mafunzo haya yanapaswa kuongezwa mada na kuongeza namba ya washiriki ili kujenga uelewa wa pamoja”

Ambao utasaidia kupata ufahamu na ujuzi muhimu wa namna ya uandaaji wa Maadhimisho yanayohusu Idara na Taasisi za Serikali kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na kuzijua kanuni za kiitifaki ambazo mtazitumia katika uendeshaji wa shughuli mbalimbali kwenye taasisi zenu.

Awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya amesema mafunzo yamelenga kuwa na utaratibu ambao umekubaliwa, ambao unaleta matokeo chanya na watu wote kuheshimu.

“Watendaji waliopokea mafunzo sasa watasaidia katika maeneo yao; kitengo cha maadhimisho Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa sababu ndio Ofisi inayosimamia itifaki za viongozi”.

Naye Mtendaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Profesa Elisante Ole Gabriel  aliyekuwa mtoa maada wa huduma bora kwa mteja; ameshukuru serikali kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo yamesaidia kuwajenga watendaji kwenda kwa muelekeo unaolengwa na nchi.

“Huu ni uwekezaji  wa kifikira unaofaa, watendaji wakitoa huduma bora kwa wananchi na kwa viongozi, mashauri yatapungua kwa sababu ya huduma kuwa nzuri.”

 

Read More

Tuesday, November 15, 2022

MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI KUFANYIKA LINDI.

 


Waziri wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema maadhimisho ya siku ya UKIMWI yanatarajiwa kufanyika Mkoani Lindi katika Uwanja wa Ilulu.

Mhe. Simbachawene ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome, Jijini  Dodoma.

Amesema kuwa maadhimisho hayo yataambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali kutoka kwa wadau wa UKIMWI zikiwemo  huduma ya upimaji wa hiari wa virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine  itakayotolewa kuanzia   Novemba  24 hadi Desemba  01, 2022.

 

“Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Imarisha Usawa’ ambayo imetafsiriwa kutoka kauli mbiu ya kimataifa equalize, kaulimbiu hii inahimiza kutilia mkazo uimarishaji wa usawa kutoa huduma za UKIMWI kwa makundi yote ya wananchi na katika maeneo yote ya kijeografia kwa kuondoa vikwazo vinavyoondoa usawa katika kufikia dira ya kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.”Amesema Mhe. Simbachawene.

 

Pia ameeleza kwamba maadhimisho hayo yatatumika  kutathimini hali halisi na muelekeo wa kudhibiti virusi vya UKIMWI, Kitaifa na Kimataifa pamoja na kuhamasisha viongozi na jamii kuendelea kwa mapambano  ya kudhibiti virusi vya UKIMWI ili  kujumuisha katika mipango yao ya maendeleo.

“Maadhimisho haya yatatumika kama sehemu ya kuwaenzi wahanga wanaoishi na virusi vya UKIMWI na kuwakumbuka wale waliopoteza maisha  kutokana na UKIMWI pamoja na kujali yatima  ambao wametokana  na vifo vilivyosababishwa na ugonjwa huo.

Vilevile  Waziri Simbachawene ameiagiza  Mikoa yote nchini kuandaa na kuadhimisha siku hiyo kwa kushirikiana na wadau wengine katika  Mikoa na katika ngazi ya Wilaya.

“Maadhimisho haya yatatumika kuhamasisha masuala mabalimbali muhimu ikiwemo  utekelezaji wa azimio la umoja wa mataifa  la kutokomeza UKIMWI katika kuhakikisha  afua za kiafya  zinapewa rasilimali za kutosha na mifumo ya kiafya inaimarishwa”Amebainisha.

Aidha amesema kuendelea kuwepo kwa siku hiyo muhimu kutasaidia  upatikanaji wa dawa za kufubaza VVU, kuendeleza utafiti wa kutafuta chanjo, kuimarisha afua za kinga dhidi ya maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI na kuendelea kutekeleza afua za UKIMWI kwa kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu.

Read More

Sunday, November 13, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE, AMPONGEZA MAMA TUNU PINDA

 


Kuimba kuna nguvu kubwa; kuimba ni kusali mara mbili, wenzetu mmekuewa watumishi wa Mungu kwa njia ya uimbaji na kazi mnayoifanya ya utume inawasaidia mpate neema na baraka kubwa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene wakati wa uzinduzi wa Albamu ya Mtakatifu Theresia,  wa Mtoto  Yesu inayoitwa Mungu asiye shindwa iliyofanyika katika Parokia ya Nzinje Mjini Dodoma.

“Kwaya hii ya Mtakatifu Theresia, Mtoto yesu ndio anayoimbia Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda, amechagua jambo zuri sana la kufanya baada ya Kustaafu”.

Read More