Saturday, August 15, 2026

WAZIRI KABUDI, SERIKALI ITAENDELEA KUTHAMINI MCHANGO WA LUKUVI


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Prof, Palamagamba Kabudi amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kuthamini mchango wa kiuongozi uliotolewa na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu William Lukuvi.

Hayo ameyasema leo wakati wa maadhimisho ya  ibada ya Misa Takatifu ya kumaliza Msiba  iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Idodi Mkoani Iringa na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali.

Alisema, “Enzi za uhai wake Waziri Lukuvi alinisaidia kufahamu shughuli mbalimbali za Bunge na serikali na hivyo kupata weledi mzuri mambo mengi kutokana na uzoefu aliyokuwa nao,”

Aidha uwezo wake wa kusimamia nidhamu ipasavyo Bungeni ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na Bunge ilimfanya aendelee kuaminiwa katika kazi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.

Kwa Upande Mama Germana Lukuvi Mjane wa Marehemu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushikamana na familia tangu walipopata msiba.

Awali Mbunge wa Isimani Mhe, Emanuela Mtatifikolo alisema Marehemu Lukuvi ataendelea kuishi kwenye mioyo ya wananchi wa Isimani, kwa mageuzi makubwa ya maendeleo aliyoyafanya.

 “Uwakilishi wake kwa wananchi wa Jimbo la isimani na kwa kushirikiana na Serikali aliwezesha Jimbo la Isimani kunufaika na ujenzi wa barabara ya lami uimarishaji wa Huduma za afya na kuendelea kuboresha miundo mbinu ya elimu sambamba na umeme,” alibainisha

Read More

MJI WA SERIKALI MTUMBA WAIPA TANZANIA FURSA YA KUIMARISHA DIPLOMASIA


Balozi wa Serbia nchini, Mhe. Jovica Topalović, amesema, maendeleo ya Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, yanaipa Tanzania fursa ya kuimarisha mazingira ya shughuli za kidiplomasia na uhusiano na mataifa mbalimbali.

 Hayo yamejiri wakati wa ziara ya kukagua eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Ubalozi wa Serbia, ambapo alipongeza hatua za Serikali katika kuendeleza eneo hilo. Amesema anaamini ndani ya miaka 10 ijayo, balozi nyingi zitahamia Mtumba, jambo litakaloimarisha nafasi ya Dodoma kuwa kama kitovu cha shughuli za kidiplomasia nchini.

Aidha, amesema uwepo wa balozi nyingi katika eneo moja utarahisisha mwingiliano na ushirikiano wa kidiplomasia. Pia ameongeza kuwa, Serbia na Tanzania zina historia ndefu ya uhusiano na maeneo mbalimbali ya ushirikiano na akieleza matumaini ya kuimarika zaidi kwa uhusiano huo katika miaka minne ijayo.

Katika ziara hiyo, Mratibu wa Ujenzi na Uendelezaji wa Mji wa Serikali, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Noel Mlindwa, aliwasilisha taarifa kuhusu maendeleo ya ujenzi na uendelezaji wa eneo hilo. Ziara hiyo ilihudhuriwa pia na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Marekani kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Ellen Maduhu, pamoja na Maafisa wa Wizara na wataalamu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Read More

Wednesday, August 12, 2026

PROFESA KABUDI AHIMIZA MATUMIZI SAHIHI YA ALAMA ZA TAIFA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, amehimiza wananchi kuendelea kuzingatia matumizi sahihi ya alama za Taifa, hususan rangi na mwonekano wa Bendera ya Taifa, kwa mujibu wa sheria.

Prof. Kabudi ametoa kauli hiyo leo, jijini Dodoma, alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Serikali wa Uchapishaji Tanzania, ambapo alipongeza taasisi hiyo kwa kuendelea kuelimisha umma na kusimamia matumizi sahihi ya alama za Taifa, ikiwemo Bendera na Nembo ya Taifa.

Amesema sheria inayosimamia matumizi ya alama za Taifa inaweka wajibu kwa Wakala wa Serikali wa Uchapishaji Tanzania kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa ipasavyo, ikiwemo kuzalisha Bendera za Taifa kwa niaba ya Serikali.

“Sheria ya Alama za Taifa inaeleza kuwa Bendera yetu ina ufito wa rangi ya dhahabu na siyo njano. Lazima tuzingatie sheria ilivyoelekeza na kuendelea kuelimisha umma kuhusu matumizi na rangi sahihi za Bendera ya Taifa,” amesisitiza Prof. Kabudi.

Aidha, Prof. Kabudi amesema mabadiliko ya Idara kuwa Wakala wa Serikali yanalenga kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Serikali, pamoja na kuiwezesha taasisi hiyo kuendelea kupanua shughuli zake kulingana na mabadiliko ya teknolojia, uchumi na mahitaji ya kimkakati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali wa Uchapishaji Tanzania, Bw. George Lugome, amesema Wakala unaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa mashine mpya na malighafi, kulingana na mahitaji ya uzalishaji.

Amesema uwekezaji huo unalenga kuimarisha uwezo wa Wakala katika uzalishaji na utoaji wa huduma kwa ufanisi, sambamba na kuendana na mahitaji ya sasa ya kiteknolojia.

 

 

Read More

Tuesday, August 11, 2026

WAZIRI KABUDI AHIMIZA KUKAMILIKA KWA UJENZI OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe, Prof. Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuhakikisha  umaliziaji ujenzi wa Jengo  la Ofisi hiyo unakamilika kwa wakati ili kusaidia kuendelea kutoa huduma bora za Ofisi.

Waziri amesema hayo alipotembelea kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hiyo leo Mtaa wa Kilimani Jijini Dodoma ambapo amepongeza kwa hatua za ujenzi uliofikiwa na kuelekeza Mkandarasi kuhakikisha anamaliza ujenzi wa Jengo hilo kwa wakati.

Waziri amesema, “ujenzi wa Ofisi za Umma lazima ujengwe kwa hadhi na uakisi matarajio ya muda mrefu ujao kulingana na mahitaji ya Ofisi, niwapongeze kwa kuzingatia hilo katika  ujenzi wa jengo lenu.”

Kwa upande wake Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Mstaafu Fransis Mutungi amemshukuru Waziri kwa maelekezo aliyotoa, ambapo amesema mipango ya Ofisi ni kuwa na watendaji wa wenye elimu ya siasa, wataalamu wa elimu jamii ambao watasaidi kuchakata na kutoa muongozo kulingana na mambo yanavyokwenda.

“Taasisi hii ni kitovu cha mambo ya siasa tunahitaji wataalamu wenye ujuzi tofauti watakaosaidia katika kufanya tafiti na kutoa taarifa zenye weledi zitakazosaidia taasisi kufanya kazi vizuri zaidi,” alieleza Jaji Mstaafu Mutungi

Awali Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Bw,Magohu Zonzo amesema ujenzi wa jengo hilo unatekelezwa na Kampuni ya Group Six Intenational na unasimamiwa na mshauri elekezi kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi kupitia kampuni tanzu ya (ARU) kwa ajlili usanifu na usimamizi wa mradi.

 

Read More

Saturday, August 8, 2026

KABUDI, AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA ZA KISASA KATIKA UZALISHAJI


Washiriki wa Maonesho ya nane watakiwa kuendelea kuzingatia ubunifu, teknolojia mpya katika shughuli zao za uzalishaji ili zisaidie katika kutatua changamoto zinazojitokeza wakati wa kazi.

Kauli hiyo Imetolewa leo  Mkoani Morogoro na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe, Prof. Palamagamba Kabudi wakati akifunga maonesho ya nanenane Kanda ya Mashariki.

 

Waziri amehimiza viongozi wa Mikoa kuhakikisha teknolojia zilizooneshwa kwenye viwanja vya Nanenane zinafikishwa kwa wananchi kupitia huduma za ugani na mashamba darasa. 

 

“tuendelee kutumia Jukwaa la Business-to-Business (B2B) ili liweze kkuweka malengo yanayopimika katika biashara, uwekezaji na masoko” alihimiza Waziri Kabudi

 

Aidha  taasisi  nyingine kama ( TBS), (SIDO) ziendelee kujikita katika kuwasaidia wajasiriamali wadogo kufikia viwango vinavyohitajika kushindana katika soko la ndani na nje ya nchi.

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa utumishi wake wa kipekee katika taifa na kwa wananchi.

 

Mkuu wa Mkoa alieleza, “Maonesho ya Mwaka yamefanyika yakiwa katika utekelezaji wa mwaka wa kwanza wa dira ya taifa 2050, nasi tumeondoka katika mafanikio ya maonesho kwa kuangalia idadi ya mabanda na sasa tumeweka vigezo maalumu kwa kuangalia elimu iliyotolewa na teknolojia iliyochukuliwa na muunganiko wa biashara iliyopatikana.”

 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Batlida Burian amempongeza Mhe, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kusainiwa kwa mkataba wa kiwanda cha Usafishaji Mafuta Mkoani Tanga. 

 

“Mhe, Rais ameshaacha tabasamu kabla ya kufika mwaka 2030 mradi huo mkubwa utawezesha kunufaisha Tanga na kanda nzima ya Mashariki, tumejipanga kuhakikisha kila mtu ananufaika na fursa hii ya ujengwaji wa kiwanda ambayo imetolewa,”alibainisha

 

 

Read More

Thursday, July 23, 2026

TNCM YAPITISHA OMBI LA TANZANIA LA FEDHA KUTOKA MFUKO WA DUNIA 2027 HADI 2029


 Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu na Kusimamia Fedha za Mfuko wa Dunia nchini Tanzania (Tanzania National Coordinating Mechanism – TNCM), imeidhinisha rasmi Ombi la Tanzania la Ufadhili wa Mzunguko wa Nane wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Grant Cycle 8 – GC8) kiasi cha dola za Marekani milioni 538.6 kwa ajili ya kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI, Kifua Kikuu (TB) na Malaria, pamoja na kuimarisha Mifumo Thabiti na Endelevu ya Afya (RSSH), katika kipindi cha utekelezaji kuanzia Januari 2027 hadi Desemba 2029.

Uidhinishaji huo umefanyika jijini Dar es Salaam katika kikao maalum cha TNCM kilichoongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa TNCM.

Dkt. Yonazi amesema kuwa, mchakato wa maandalizi ya Ombi la GC8 ulianza rasmi tarehe 13 Machi, 2026 na umeendelea kwa zaidi ya miezi minne, ukihusisha mashauriano ya kina, majadiliano ya kitaifa, upangaji wa vipaumbele, uandishi wa andiko, mapitio ya kitaalamu na uhakiki wa nyaraka za maombi.

Aidha, alifafanua kuwa, mchakato huu umejengwa katika msingi wa ushirikishwaji mpana wa wadau, uwazi, uwajibikaji na umiliki wa kitaifa ambapo zaidi ya wadau 270 walishiriki kwa uwakilishi wa makundi mbalimbali, yakiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara, Idara na Taasisi zake; Washirika wa Maendeleo, Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi, Mashirika ya Dini, watu wanaoishi na VVU, jamii zilizo katika hatari kubwa ya maambukizi na zilizoathiriwa na magonjwa hayo; pamoja na wataalamu wa sekta ya afya.

Dkt. Yonazi ameeleza kuwa uwekezaji wa Mfuko wa Dunia umeendelea kutoa mchango mkubwa katika juhudi za Serikali za kuboresha afya na ustawi wa Watanzania, na kusema utekelezaji wa GC8 utatoa fursa kwa Nchi kuendela kuzuia maambukizi mapya ya VVU, kuongeza upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya VVU (ARV), kuimarisha kinga, uchunguzi na matibabu ya Malaria, pamoja na kuboresha ugunduzi wa mapema na matibabu ya Kifua Kikuu.

“Kuidhinishwa kwa Ombi hili la Ufadhili ni matokeo ya kazi kubwa na ushirikiano wa wadau wetu ambao wamewekeza muda, utaalamu na rasilimali kuhakikisha kuwa vipaumbele vilivyoainishwa vinazingatia mahitaji ya nchi pamoja na sauti za jamii na makundi yanayoathiriwa na magonjwa hayo”.Alisema Dkt. Yonazi.

Aliongezea kuwa,hatua hiyo ni mafanikio muhimu yanayoonesha dhamira ya Tanzania ya kuendeleza mapambano dhidi ya magonjwa hayo matatu, sambamba na kujenga mfumo wa afya ulio imara, jumuishi na endelevu.

Dkt. Yonazi ameshukuru Sekretarieti ya Mfuko wa Dunia iliyopo Geneva (Global Fund Country Team), wajumbe wa TNCM pamoja na wadau wote walioshiriki katika maandalizi na ukamilishaji wa maombi hayo, amepongeza jitihada zao akisema zimekuwa na mchango muhimu kuwezesha kufikia hatua hii.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TNCM, Bw. Kent Pius, ametoa shukrani maalum kwa Mwenyekiti wa TNCM, Mfuko wa Dunia, wajumbe na wadau wote kwa ushirikiano na uwajibikaji mkubwa katika kuhakikisha kuwa zoezi hili limefanyika kwa ufanisi na ubora uliokusudiwa na kusema kuwa, hatua hii ni matokeo ya dhamira ya dhati na juhudi za pamoja.

“TNCM itaendelea kuratibu ushirikiano kati ya Serikali, jamii, Asasi za Kiraia, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na wadau wa kimataifa katika kuhakikisha uwekezaji wa Mfuko wa Dunia unachangia katika kufikia malengo ya Kitaifa na Kimataifa ya kutokomeza UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria kama vitisho vya afya ya jamii,” alisema Kent.

 

 

Read More

PROF. KABUDI: TUMEPIGA HATUA UTOAJI HUDUMA ZA AFYA

 


Huduma za afya ya mama na mtoto katika ngazi ya Kata, Wilaya, Mkoa na Taifa zimeendelea kuimarika ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika ununuzi wa vifaa tiba na kutoa mafunzo kwa watoa huduma ikiwemo madaktari na wauguzi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi wakati akizindua jengo la mama na mtoto katika Hospitali ya Vijimbweni Kigamboni Jijini Dar es salaam.

 Alisema, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alianza kusimamia jambo hili tangu akiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndio maana Umoja wa Afrika ulimteua kuwa kinara wa afya ya mama na mtoto katika Bara la Afrika.

 Aidha, Prof. Kabudi, alifafanua “Maendeleo haya katika kipindi cha Miaka 65 ya Uhuru ni hatua kubwa ukilinganisha na kipindi ambacho Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere anaichukua nchi kutoka kwa mkoloni, hali ilikuwa na tofauti na sasa, ni lazima tujivunie maendeleo tuliyofikia”.

Awali Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mhe. Mikaya Tumaini Dalmia ameishukuru serikali kwa kuendelea kuimarisha miundombinu ya ya afya akisema awali wananchi wa Kigamboni walikuwa wanafuata huduma katika Hospitali ya wilaya ya Temeke na Mhimbili.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mhe. Haran Sanga ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwarahisishia wananchi wa kigamboni kupata huduma karibu na maeneo wanayoishi.

Read More

TNCM YAPITISHA OMBI LA TANZANIA LA FEDHA KUTOKA MFUKO WA DUNIA 2027 HADI 2029


 Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu na Kusimamia Fedha za Mfuko wa Dunia nchini Tanzania (Tanzania National Coordinating Mechanism – TNCM), imeidhinisha rasmi Ombi la Tanzania la Ufadhili wa Mzunguko wa Nane wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Grant Cycle 8 – GC8) kiasi cha dola za Marekani milioni 538.6 kwa ajili ya kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI, Kifua Kikuu (TB) na Malaria, pamoja na kuimarisha Mifumo Thabiti na Endelevu ya Afya (RSSH), katika kipindi cha utekelezaji kuanzia Januari 2027 hadi Desemba 2029.

Uidhinishaji huo umefanyika jijini Dar es Salaam katika kikao maalum cha TNCM kilichoongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa TNCM.

Dkt. Yonazi amesema kuwa, mchakato wa maandalizi ya Ombi la GC8 ulianza rasmi tarehe 13 Machi, 2026 na umeendelea kwa zaidi ya miezi minne, ukihusisha mashauriano ya kina, majadiliano ya kitaifa, upangaji wa vipaumbele, uandishi wa andiko, mapitio ya kitaalamu na uhakiki wa nyaraka za maombi.

Aidha, alifafanua kuwa, mchakato huu umejengwa katika msingi wa ushirikishwaji mpana wa wadau, uwazi, uwajibikaji na umiliki wa kitaifa ambapo zaidi ya wadau 270 walishiriki kwa uwakilishi wa makundi mbalimbali, yakiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara, Idara na Taasisi zake; Washirika wa Maendeleo, Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi, Mashirika ya Dini, watu wanaoishi na VVU, jamii zilizo katika hatari kubwa ya maambukizi na zilizoathiriwa na magonjwa hayo; pamoja na wataalamu wa sekta ya afya.

Dkt. Yonazi ameeleza kuwa uwekezaji wa Mfuko wa Dunia umeendelea kutoa mchango mkubwa katika juhudi za Serikali za kuboresha afya na ustawi wa Watanzania, na kusema utekelezaji wa GC8 utatoa fursa kwa Nchi kuendela kuzuia maambukizi mapya ya VVU, kuongeza upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya VVU (ARV), kuimarisha kinga, uchunguzi na matibabu ya Malaria, pamoja na kuboresha ugunduzi wa mapema na matibabu ya Kifua Kikuu.

“Kuidhinishwa kwa Ombi hili la Ufadhili ni matokeo ya kazi kubwa na ushirikiano wa wadau wetu ambao wamewekeza muda, utaalamu na rasilimali kuhakikisha kuwa vipaumbele vilivyoainishwa vinazingatia mahitaji ya nchi pamoja na sauti za jamii na makundi yanayoathiriwa na magonjwa hayo”.Alisema Dkt. Yonazi.

Aliongezea kuwa,hatua hiyo ni mafanikio muhimu yanayoonesha dhamira ya Tanzania ya kuendeleza mapambano dhidi ya magonjwa hayo matatu, sambamba na kujenga mfumo wa afya ulio imara, jumuishi na endelevu.

Dkt. Yonazi ameshukuru Sekretarieti ya Mfuko wa Dunia iliyopo Geneva (Global Fund Country Team), wajumbe wa TNCM pamoja na wadau wote walioshiriki katika maandalizi na ukamilishaji wa maombi hayo, amepongeza jitihada zao akisema zimekuwa na mchango muhimu kuwezesha kufikia hatua hii.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TNCM, Bw. Kent Pius, ametoa shukrani maalum kwa Mwenyekiti wa TNCM, Mfuko wa Dunia, wajumbe na wadau wote kwa ushirikiano na uwajibikaji mkubwa katika kuhakikisha kuwa zoezi hili limefanyika kwa ufanisi na ubora uliokusudiwa na kusema kuwa, hatua hii ni matokeo ya dhamira ya dhati na juhudi za pamoja.

“TNCM itaendelea kuratibu ushirikiano kati ya Serikali, jamii, Asasi za Kiraia, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na wadau wa kimataifa katika kuhakikisha uwekezaji wa Mfuko wa Dunia unachangia katika kufikia malengo ya Kitaifa na Kimataifa ya kutokomeza UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria kama vitisho vya afya ya jamii,” alisema Kent.

Read More

Tuesday, July 21, 2026

KAMATI YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA MAAFA YAIDHINISHA MPANGO WA DHARURA WA TAIFA WA KUKABILIANA NA MADHARA YA EL NIÑO


 Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu ya Usimamizi wa Maafa imeidhinisha Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Niño na kuzielekeza Wizara, Idara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri kuongeza kasi ya maandalizi ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za El Niño zinazotabiriwa kudumu hadi mwisho wa mwaka 2026.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi, ameelekeza kila sekta kutenga rasilimali zitakazowezesha hatua za kuzuia, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali katika eneo lake na pia kuandaa mipango ya dharura ya manunuzi. Pia amesisitiza umuhimu wa kutambua mapema maeneo hatarishi, kufanya tathmini za vihatarishi na kuwahamasisha wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kuhamia maeneo salama.

Aidha, Dkt. Yonazi ameelekeza wananchi kupewa elimu kuhusu namna ya kupunguza madhara ya mvua hizo kwa kuweka akiba ya chakula, kulima mazao yanayostahimili mvua nyingi na kutumia fursa zitokanazo na mvua katika kilimo, uvunaji wa maji, ufugaji na uvuvi. Vilevile, amezitaka taasisi husika kuandaa mipango ya kuzuia milipuko ya magonjwa kwa binadamu, mifugo na mimea.

Kamati hiyo pia imeagiza ukaguzi na uboreshaji wa miundombinu muhimu ikiwemo barabara, maji na umeme, kuimarisha usimamizi wa mazingira, kuhakikisha vifaa vya uokoaji, huduma za dharura na mifumo ya mawasiliano vinakuwa tayari wakati wote, pamoja na kuhuisha mipango ya utekelezaji katika maeneo hatarishi.

Aidha, Wizara, Taasisi, Mikoa na Halmashauri zimeelekezwa kufuatilia kwa karibu utabiri na maelekezo ya kitaalamu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili hatua zote za maandalizi na kukabiliana na athari za El Niño zichukuliwe kwa wakati.

 

Read More

Monday, July 20, 2026

WATENDAJI MANISPAA YA UBUNGO WAPONGEZWA UBUNIFU WA UNUNUZI WA MITAMBO


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe, Prof. Palamagamba Kabudi amepongeza watendaji wa Manispaa ya Ubungo kwa ubunifu wa ununuzi wa mitambo ya kutengeneza barabara itakayosaidia mageuzi ya uimarishaji wa mtandao wa barabara na kuchochea shughuli za maendeleo na kasi ya ukuaji wa uchumi kwa wananchi.

Prof. Kabudi ameitoa pongezi hizo leo Jijini Dar es Salaam wakati aliposhiriki katika uzinduzi wa mitambo ya malori ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo itakayosaidia katika kuboresha miundombinu ya bararaba katika halmashauri hiyo.

“Maamuzi haya si mepesi kufanywa na baraza la madiwani, kwa sababu imelenga kutatua changamoto za barabara zinazotukabili kwa sasa, ni lazima mitambo hii isimamiwe sawasawa ili kuleta tija kwa wananchi na kila mtendaji aone anajukumu la kuilinda mitambo hii” ameeleza Prof. Kabudi

Aidha, Prof. Kabudi amesema, “ubunifu wa namna hii unahitajika sana, kufanywa katika maeneo mengine ili Halmashauri kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini (TARURA) na kwa kutumia nyenzo uwe wa faida kwa wananchi na mambo haya yanawekewa mkazo kwenye dira ya Taifa.”

Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Albert Chalamila amesema malengo ya Mkoa wake ni kutoka kwenye kuwaza mambo madogo na kuwaza mambo makubwa yenye tija kwa taifa.

“Ili kufikia matarajio hayo tumeainisha kwamba maendeleo lazima yawe yanahusu watu, maendeleo yanayoweza kuchangiwa na watu na yawe maendeleo yao wenyewe,” ameeleza Mkuu wa Mkoa.

 Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando amesema, msukumo wa kununua mitambo hiyo ulitokana na kulenga kukarabati barabara zinazoharibika wakati wa masika na hasa barabara za mtaani ambazo ziko katika utaratibu wa kusajiliwa na Wakala wa Barabara vijijini na Mjini (TARURA).

“Imani yetu kwa ngazi ya wilaya ni kuendelea kuwekeza zaidi kwa kujipanga kununua seti nyingine ya mitambo  ili kusaidia kila jimbo kuwa na mitambo yake ili kupata matokeo mazuri,” alifafanua Mhe. Msando.

Read More

Sunday, July 12, 2026

MKUU WA MKOA WA TANGA ATOA WITO WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA OWM SABASABA

 

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kupata elimu ya masuala mbalimbali katika Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Ametoa wito huo hii leo (12 Julai, 2026) alipotembelea na kujionea namna ofisi hiyo inavyoendelea kutoa huduma kwa wananchi na kuwasihi waendelee kujitokeza kwa wingi na kupata taarifa na huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake.

Dkt. Batilda amepongeza namna Ofisi ya Waziri Mkuu ilivyojipanga na kuhakikisha inawafikia wananchi kwa utoaji wa huduma bora na kuzingatia viwango huku wakiendelea kutatua changamoto mbalimbali kwa jamii kupitia maonesho hayo.

Aidha amewakumbusha watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kuwa na program mbalimbali za elimu kwa umma ili kuifikia jamii kwa ukumbwa wake na kuendelea kutangaza huduma zinazotolewa.

Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanaendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu isemayo, "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba ni Fahari ya Tanzania," yakilenga kukuza biashara, uwekezaji na ubunifu, nchini.

 

Read More

Saturday, July 11, 2026

WITO WATOLEWA KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KITAIFA KULINDA AMANI


SERIKALI imewataka Watanzania kuendelea kulinda na kudumisha amani ya nchi kwa kutambua kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa, huku ikisisitiza kuwa jukumu hilo linamhusu kila mwananchi bila kujali dini, kabila au itikadi za kisiasa.

Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, profesa Palamagamba Kabudi, wakati wa Ibada ya Siku Maalumu ya Wanaume (AMO Big Day) iliyofanyika katika Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA), Mwenge, tarehe 11 Julai, 2026 jijini Dar es Salaam.

Dkt. Nchemba alisema ulinzi wa amani unapaswa kupewa kipaumbele na kuwa ajenda namba moja ya kitaifa kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, unaowezesha wananchi kuishi kwa utulivu, kufanya kazi kwa bidii na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.

Alisema kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda amani kwa kuheshimu sheria za nchi, kuimarisha mshikamano wa kitaifa na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama na utulivu wa nchi.

“Suala la ulinzi wa amani lipewe kipaumbele na kwa kila mmoja liwe ajenda namba moja ya kitaifa. Watanzania wote tutambue kuwa tunao wajibu wa kulinda amani yetu,” alisema.Aidha, Dkt. Nchemba aliwataka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhamasisha wananchi kudumisha amani, upendo, mshikamano na maadili mema kupitia mafundisho yao.

Alisema viongozi wa dini wana nafasi muhimu katika kujenga jamii yenye umoja na mshikamano, hivyo wanapaswa kuendelea kuhubiri ujumbe wa amani na kuhimiza wananchi kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa taifa.

“Viongozi wa dini endeleeni kuhubiri kuhusu umuhimu wa kudumisha amani na upendo miongoni mwa wanajamii. Ninawasihi sana katika hili, shirikianeni na Serikali kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa na amani na utulivu. Suala la ulinzi wa amani halina mbadala; sote kwa pamoja tuendelee kuweka msisitizo katika kulinda amani ya nchi,” alisema.

Alisema Tanzania imeendelea kujijengea heshima ndani na nje ya nchi kutokana na historia yake ya amani, umoja na mshikamano, hali iliyowezesha kuvutia uwekezaji, kukuza biashara, kuboresha utoaji wa huduma za jamii na kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Nchemba aliwapongeza waumini wa Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA) Mwenge kwa kukamilisha ujenzi wa jengo la kisasa la ibada, akisema ni ushahidi wa imani yao, mshikamano na kujitoa katika kazi ya Mungu.

“Hili ni jambo la kujivunia. Ni alama ya imani yenu thabiti, mshikamano wenu wa kijamii na bidii yenu ya kujitoa kwa kazi ya Mungu,” alisema.

 

Read More

PROF. NAGU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA BANDA JUMUISHI LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya katika Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Tumaini Nagu, ametembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, na kupongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Akiwa katika ziara hiyo, Prof. Nagu amepata fursa ya kutembelea sehemu mbalimbali za banda hilo na kupokea maelezo kuhusu huduma na mifumo mbalimbali inayowezesha wananchi kupata taarifa na huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake.

Amesema banda hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuwaelimisha wananchi kuhusu utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za kijamii, hususan katika sekta ya afya, elimu, utawala bora na maendeleo ya serikali za mitaa.

Prof. Nagu amewapongeza watumishi wanaohudumu katika banda hilo kwa kujituma, kutoa elimu kwa ufasaha na kuhakikisha kila mwananchi anayefika anapata huduma na taarifa sahihi zinazomwezesha kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu.

Aidha, amewataka kuendelea kutumia maonesho hayo kama fursa ya kusikiliza maoni ya wananchi, kupokea changamoto zao na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu huduma zinazotolewa, ili kuongeza uelewa na kuimarisha uhusiano kati ya Serikali na wananchi.

"Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu limeendelea kuvutia maelfu ya wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba, ambapo wamekuwa wakipata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi hii pamoja na taasisi zake kwa lengo la kuboresha ustawi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya Taifa, hivyo wananchi endeleeni kuitumia fursa ya uwepo wa ofisi hii katika maonesho haya," alisema Dkt. Nagu

Aidha,ametumia nafasi hiyo kuipongeza Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) pamoja na Taasisi nyingine zilizowezesha mafanikio ya maonesho hayo huku akiiasa jamii kuendelea kutembelea banda hilo na kupata elimu.

Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanaendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu isemayo, "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba ni Fahari ya Tanzania," yakilenga kukuza biashara, uwekezaji na ubunifu nchini.

Miongoni mwa Taasisi za Ofisi ya Waziri Mkuu zilizoshiriki ni pamoja na PSSSF, WCF, NSSF, OSHA, NEEC, TNBC, CMA, TACAIDS, DCEA,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, DART, TARURA, Chuo cha Serikali za Mitaa(LGTI) pamoja na Shirika la Masoko Kariakoo.

Read More

Thursday, July 9, 2026

SERIKALI YAAHIDI KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI LICHA YA KUPUNGUA KWA MISAADA YA WAHISANI


Serikali imehakikisha kuwa mapambano dhidi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) yataendelea kupewa kipaumbele, huku huduma za kinga, matibabu na upatikanaji wa dawa muhimu zikiendelea kutolewa bila kukwama licha ya changamoto zinazotokana na kupungua kwa misaada kutoka kwa wahisani wa maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa leo, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, alipokutana na Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Winnie Byanyima, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, jijini Dar es Salaam.

Prof. Kabudi alisema Serikali imeendelea kuwekeza katika sekta ya afya kupitia vyanzo vya ndani vya mapato ili kuhakikisha huduma zote muhimu zinazohusiana na mapambano dhidi ya UKIMWI zinaendelea kutolewa kwa wananchi bila kuathiriwa na mabadiliko ya ufadhili kutoka nje.




Read More