Friday, November 27, 2020
Monday, November 16, 2020
Thursday, November 12, 2020
RAIS MAGUFULI AMPENDEKEZA KASSIM MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU
WABUNGE WAMTHIBITISHA MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU
*Amshukuru Rais na aahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii
SPIKA wa Bunge la 12 Job Ndugai amesema wabunge wamemthibitisha mbunge wa jimbo la Ruangwa mkoani Lindi, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kuwa Waziri Mkuu kwa miaka mitano mingine (2020-2025) kwa kupata kura zote 350 zilizopigwa na wabunge sawa na asilimia 100.
“Kura zote zilizopigwa ni 350 hakuna iliyoharibika, hakuna kura ya hapana. Kura zote 350 zimemthibitisha Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, kwa hiyo ndugu wabunge Mheshimiwa Majaliwa amethibitishwa na Bunge hili kuwa Waziri Mkuu kwa kura 350 sawa na asilimia 100.”
Spika Ndugai ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 12, 2020) Bungeni jijini Dodoma baada ya kupokea jina la Waziri Mkuu lililowasilishwa bungeni na Mpambe wa Rais na kisha wabunge kupiga kura kwa ajili ya kulithibitisha jina hilo.
Akizungumza baada ya kuthibitishwa Mheshimiwa Majaliwa amesema amepokea uteuzi huo kwa mikono miwili na anamshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameendelea kuwapa uhai wote na kushuhudia hayo, Pia ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyoionesha juu yake.
“Mheshimiwa spika naomba nitumie nafasi hii kwa dhati yangu ya moyo kumshukuru sana Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushindi mkubwa alioupata kutoka kwa Watanzania kupitia uchaguzi ambao ulifanyika hivi karibuni kwa kushinda kwa kishindo. Uchaguzi uliofanyika kwa uhuru na haki.”
“Jambo hili si dogo, Mwenyezi Mungu ameliongoza, namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyonayo juu yangu na kuendelea kuniamini. Namshukuru sana na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa ushiriki wake katika kuridhia jina langu.”
“Pia, nampongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi huo na namna ambavyo Watanzania wameridhishwa na kazi aliyoifanya na imani waliyonayo kwamba viongozi hao wataendelea kuwatumikia vizuri zaidi.”
Ametumia fursa hiyo kumpongeza Spika wa Bunge Job Ndugai kwa kuchaguliwa bila kupingwa kuwa mbunge wa Kongwa pamoja na kurudi katika nafasi yake ya uspika baada ya kupigiwa kura nyingi na waheshimiwa wabunge, hakuna siri kwamba umefanya kazi nzuri miaka mitano iliyopita umeisaidia sana serikali na kuiwezesha kufanya mambo makubwa.
“Kazi uliyoifanya miaka mitano iliyopita tunaifahamu vizuri zaidi na Serikali itaendelea kukupa ushirikiano wa dhati. “Mheshimiwa spika niendelee kushukuru kwa kuwashukuru wabunge wenzangu, waheshimiwa wabunge wenzangu mmenifanyia jambo kubwa kwangu na familia yangu.”
“…idadi ya kura zenu mlizonipigia mmenipa changamoto sana. Haijawahi kutokea mmepiga kura kwa asilimia 100, haijawahi kutokea nawashukuru sana. Nitaendelea kushirikiana na wabunge wenzangu wote nikijua nyie ni wawakilishi wa Watanzania wanaotamani kupata maendeleo kupitia uwakilishi wenu. ”
Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa jimbo la Ruangwa na mkoa wa Lindi, familia na CCM kwa ushirikiano alioupata katika kutekeleza majukumu yake katika kipindi cha miaka mitano na anaimani wataendelea kumpa ushirikiano katika kipindi cha miaka mitano mingine.
Awali, kabla ya kuthibitisha jina la Waziri Mkuu wabunge mbalimbali walizungumzia utendaji kazi wa Mheshimwa Majaliwa ambapo Mbunge wa Tunduma David Silinde alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumrudisha tena Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika nafasi hiyo.
Amesema kuwa Waziri Mkuu Majaliwa ni kiongozi mwenye uwezo wa kusimamia maono ya Rais Dkt. Magufuli katika kuibadilisha nchi na pia anauwezo wa kuunganisha nchi yote kupitia Bunge na hivyo kufanya kazi ya rais kuwa nyepesi.
“Sifa kuu ya kiongozi ni unyenyekevu, kujishusha na kusikiliza na sifa hizo Mheshimiwa Majaliwa anazo, ninaamini wote tutampitisha kwa asilimia 100 ili kuliambia Taifa nini tunakwenda kukifanya kwa miaka mitano baada ya miaka mitano ya mafanikio ambayo imeleta ushindi wa kimbunga.”
Amesema anaamini kwamba katika kipindi cha miaka mitano Serikali inakwenda kufanya mabadiliko makubwa katika Taifa na dunia inajua kuwa viongozi wao ni mahiri na kila mahali wanatetemeka kusikia kazi inayofanywa na viongozi hao.
“Naomba wote tumpitishe ili aweze kuongoza tena.”
Naye, Mbunge wa Ismani, William Lukuvi amesema Mheshimiwa Majaliwa ni binadamu mwenye upendo, mchapakazi asiyekuwa na majivuno na kwa mara ya kwanza ameshuhudia Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM akizunguka kwenda kuwatetea wabunge nchi nzima. “Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ametutendea haki Watanzania Mheshimiwa Majaliwa anatosha sana kuwa Waziri Mkuu.”
Kwa upande wake, Kapten Mstaafu George Mkuchika amesema Mheshimiwa Majaliwa anamfahamu vizuri na amewahi kufanya kazi wakiwa Ofisi ya Rais –TAMISEMI kwamba ni mtu mstarabu kama Mheshimiwa Majaliwa ni mtu msikivu, asiyejikweza na hajipendekezi anatenda haki kwa kila mtu.
“Katika kipindi cha miaka mitano hakubagua wabunge katika uetekelezaji wa shughuli za bunge na ni mtu msikivu sana. Amesimamia sana katika kufufua uchumi hasa mazao ya biashara, amerejesha mamlaka ya mkonge mikononi mwa Serikali. Ameratibu vizuri shughuli za wizara zote.”
Naye, Mama Salma Kikwete Alisema Mheshimiwa Majaliwa hakuwa mbaguzi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na amefanya mambo makubwa, hivyo anampongeza Rais Dkt. Magufuli kwa kuwarejeshea kwani anastahiki kuwa Waziri Mkuu na hakuna anayeweza kupinga jambo hilo.
Mbunge mwingine, Fakharia Shomari alisema anamshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa uteuzi alioufanya katika nafasi ya Waziri Mkuu kwa sababu ni uteuzi ambao walikuwa wanaufikiria ila hawakuweza kuamua kabla ya yeye kutamka. “Mheshimiwa Majaliwa amefanya ziara nchi nzima na alikuwa anafanya kazi na kila rika na jamii. “Nawaomba wabunge wenzangu tuibariki hoja ya mheshimiwa Rais.”
Kwa upande wake, Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba alisema Mheshimiwa Majaliwa ni kiongozi msikivu, muadilifu, mnyenyekevu, hodari, mchapakazi na ni kiongozi shupavu ambaye nafasi hiyo anaimudu na anaiweza na hakuna shaka yoyote kwamba nafasi hiyo kwamba ataitendea haki. “Kumpigia kura nyingi tunaonesha imani kwa ndugu yetu na imani na busara kwa rais.”
(mwisho)
RAIS MAGUFULI AMPENDEKEZA KASSIM MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU
Tuesday, November 10, 2020
WAZIRI MKUU MSTAAFU, KASSIM MAJALIWA AAPA KUWA MBUNGE WA RUANGWA
Waziri Mkuu Mstaafu, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Iramba Magharibi Dkt. Mwigulu Nchemba, Bungeni Jijini Dodoma Novemba 10, 2020. |
Waziri Mkuu Mstaafu, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akiapa kuwa mbunge wa Ruangwa, Bungeni Jijini Dodoma Novemba 10, 2020. |
Sunday, November 8, 2020
WAZIRI MKUU MSTAAFU, KASSIM MAJALIWA AWAJULIA HALI MZEE KING KIKI NA MKUU WA WILAYA YA MLELE.
Thursday, October 22, 2020
JKT YATEKELEZA PROGRAMU YA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO AWAMU YA PILI (ASDP II)
Na. OWM, Morogoro.
Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, kilichopo
Wilayani Kilombero, Mkoani Morogoro kimeanza kutekeleza kwa vitendo Programu ya
Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) kwa kuanza ujenzi wa skimu
ya umwagiliaji ambayo kwa awamu ya kwanza skimu hiyo itakuwa na urefu wa Km 2.3, ambayo
hivi karibuni Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo ameweka jiwe la msingi la kuizindua.
Programu ya ASDP II inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, malengo yake
ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo (kilimo, mifugo na uvuvi) kupitia
maeneo makuu manne ikiwemo eneo la Usimamizi Endelevu wa Matumizi ya Maji na
Ardhi ambalo moja ya kipaumbele cha uwekezaji ni kuendeleza
miundo mbinu ya umwagiliaji.
Akiongea mara baada ya kufanya ziara kwenye Kikosi cha Jeshi 837KJ
Chita, tarehe 21 Oktoba, 2020, Wilayani Kilombero lengo likiwa ni kufuatilia
utekelezaji wa Programu hiyo kwa wadau wa Programu ya ASDP II, Mratibu wa
Programu ya ASDP II Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde, amefafanua kuwa ujenzi
wa skimu hiyo utasaidia Programu kulifikia lengo la Kitaifa kwa miaka mitano la
kuwa na eneo la umwagiliaji la hekta milioni moja na laki mbili.
“Jeshi la kujenga Taifa ni mdau muhimu katika utekelezaji wa Programu
ya ASDP II, na kwa kikosi hiki cha 837 KJ Chita, kuanza
ujenzi huu wa skimu ya umwagiliaji itasaidia kuongeza eneo linalohitajika la
kilimo cha umwagiliaji nchini ambapo kwa sasa eneo lililopo la kilimo cha
umwagiliaji ni takribani hekta laki sita na alfu tisini na nne tu.
Ameongeza kuwa mradi huo pia umezingatia kuongeza thamani ya zao la
mpunga kwa kuanza ujenzi wa ghala la kuhifadhi mpunga sambamba na kuwa na
mpango wa kujenga kiwanda cha kusindika
mpunga huo ambapo hatua hiyo inaongeza wigo wa Kikosi hicho kuwekeza kwenye
eneo kuu la tatu la Programu ya ASDPII ambalo ni kukuza Biashara na Kuongeza
Thamani.
Kwa upande wake Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni
Nyakohanda Rusuhi ameeleza kuwa ujenzi wa skimu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa
Programu ya ASDP II pamoja na mipango ya JKT inayosimamiwa na Mkuu wa Jeshi la
Kujenga Taifa, Meja Jenerali Charles Mbuge, ambapo Programu hiyo inawataka wadau wake kufanya
mageuzi kwenye sekta ya kilimo kwa kulima kilimo chenye tija.
“Awali wakati tunategemea kilimo cha mvua tulikuwa tunavuna gunia sita
kwa hekari moja, lakini baada ya kukamilisha ujenzi wa skimu hii tunatarajia
kuvuna takribani ya gunia 35 kwa hekari moja. Tukifanikiwa kupata mavuno haya
tutakuwa tumezalisha chakula cha kutosha lakini pia tutakuwa tumefanikiwa
kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyelitaka Jeshi la
kujenga Taifa kujilisha.” Amesisitiza Rusuhi.
Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Kanda ya juu Kusini -Mbeya,
ambao wanashirikiana na JKT kujenga skimu hiyo, Mhandisi Elibariki Mwendo
ameeleza kuwa tayari wameanza kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa kuanza
na ujenzi wa awali wa ekari 2,500 kati ya ekari 12,000 zinazolengwa kujengwa.
Mhandisi Mwendo ameongeza kuwa ujenzi wa skimu hiyo utakuwa na ujenzi
wa mifereji katika mito mitatu tofauti, ujenzi wa mifereji mikuu mama mitatu
yenye urefu wa mita 1,716 pamoja na vivushamaji kupita kwenye reli ya TAZARA,
pia ujenzi wa mabanio matatu, mifereji midogo ya kutoa maji shamba ipo 155,
matuta mawili ya kuzuia mafuriko yenye kina cha wastani wa mita mbili.
Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) ilizinduliwa
rasmi mwaka 2018 na inaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo inatekelezwa na
wadau wakuu wa tatu ambao ni Serikali, Sekta Binafsi na Washirika wa maendeleo.
Malengo makuu ya Programu ya
ASDP II ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo (kilimo, mifugo na uvuvi) ili
kuongeza uzalishaji na tija, kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara zaidi na
kuongeza pato la wakulima wadogo kwa ajili ya kuboresha maisha yao, usalama wa
chakula na lishe.
Mbali na maeneo makuu ya ASDPII
ambayo Kikosi cha JKT Chita kimeanza kutekeleza maeneo mengine ni Kuongeza Tija
na Faida kwa lengo la kuongeza uzalishaji wenye tija hasa kwenye mazao ya
kipaumbele; na Kuweka Mazingira Wezeshi ya Kuendeleza Sekta ya kilimo kwa
kuwezesha uratibu, ufuatiliaji na kufanya tathmini ya sekta ikiwa ni pamoja na
kuimarisha taasisi na kuweka mazingira wezeshi ya uratibu. Ni wazi kuwa Jeshi
la Kujenga Taifa lipo kwenye nafasi kubwa ya kutekeleza Programu ya ASDPII kwenye
maeneo yote makuu ya Programu hiyo.
MWISHO.
Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisiya
Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde,akifafanua umuhimu wa skimu ya umwagiliaji inayojengwa
na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero,
Morogoro wakati waziara ya kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo inayoratibiwa
na Ofisi hiyo. Kulia kwake ni Mhandisi wa Mradi, Meja Mbaraka
Magogo na kushoto kwake ni Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni
Nyakohanda Rusuhi na Mratibu Msaidizi Programu Ofisi ya Waziri Mkuu,
MethewMwinuka.
Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisi ya
Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde, akiongozwa na Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni Nyakohanda Rusuhi kukagua ujenzi wa skimu ya umwagiliaji inayojengwa
na kikosi hicho Wilayani Kilombero, Morogoro wakati waziara ya kufuatilia utekelezaji
wa Programu hiyo inayoratibiwa na Ofisi hiyo.