Sunday, January 21, 2024

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUREJESHA HALI KATIKA MIUNDO MBINU YA BARABARA ILIYOATHIRIKA NA MVUA

 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulika na Sera, Bunge na Uratibu Mhe, Ummy Nderiananga amepongeza Kamati ya Maafa ya Mkoa wa Dar es salaam kwa jitihada mbalimbali za kurejesha hali katika maeneo ambayo miundo mbinu ya barabara imeathirika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake leo Mkoani humo alipotemebelea na kujionea athari za mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia tarehe 20/ januari/2024 na kuathiri maeneo mabalimbali ya wilaya ya Kindondoni, Temeke, Kigamboni, Ubungo na Jiji la Ilala.

Naibu Waziri Ummy alisema anampongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.  Abert Chalamila kwa uongozi ambao wameuonesha katika kurejesha halina kazi waliyofanya.

“Naomba tufanye kazi hii usiku na mchana ili tuweze kurejesha hali mapema bila kuathiri shughuli za biashara na shughuli nyingine za uchumi zinazofanyika katika Mkoa wa Dar es saalam,” alihimiza.

Sisi kama serikali tunawahakikishia wana Dar es salamu kwamba tutafanya kazi hii ya urejeshaji wa hali kwa nguvu bila kuchoka,

Naye Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mhe. Saad Mtambule amesema kazi waliyofanya ni kusimamia usafishaji wa mitaro na usawishaji wa mito na hivyo kusaidia maji kutotuwama kwa muda mrefu.

“Tumeendelea kuwaeleza wananchi walio katika maeneo ya pembezoni mwa mito kama; Mto Nyakasangwa, Mto Mpiji, Mto Tegeta, Mto Mlalakuwa na Mto Ng’ombe kuhamia maeneo ya juu ili kuepeuka athari za mvua,”alibainisha

Ujenzi wa nyumba holela umesababisha Watu kujenga mpaka kwenye mapito asili ya maji na kusababisha maji kukosa sehemu za kupita na kuingia maeneo ya watu

“Lakini pia tuna kazi ya kuendelea kuwaelimisha wananchi ili wafuate misingi ya ujenzi wa maeneo kulingana na ramani ya mipango Miji,” alisisitiza

Akizungumza katika ziara hiyo Mkazi wa Ununio Bw. James Koyi ameishukuru serikali kwa kazi kubwa inayofanya ya urejeshajji wa hali katika maeneo yaliyoathirika mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoa wa Dar es salaam.

Hakuna aliyejua kama mvua itanyesha masaa ishirini na nne hata hivyo  serikali iendelee kufanya kazi katika kurejesha hali, alisema


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.