Friday, August 28, 2020

NAIBU KATIBU MKUU TAMISEMI AKUNWA NA MAFUNZO KAZINI YA OFISI YA WAZIRI MKUU

 

Ofisi ya Waziri Mkuu imefanya mafunzo ya kujenga uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa maafisa 36 kutoka idara na vitengo vya ofisi hiyo. Mafunzo hayo ya wiki moja yamefanyika kuanzia tarehe 24 hadi 28 Agosti 2020, Jijini Dodoma, ambapo Wakala wa Serikali ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) waliendesha mafunzo hayo kwa ufadhili wa Shirika la Chakula Duniani. 


Lengo la mafunzo hayo lilikuwa ni kujenga uwezo kwa maafisa wake katika maeneo ya Uchambuzi wa Sera, Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera na Uandishi wa taarifa. Mafunzo hayo pia yamewezesha maafisa hao kuongeza umahiri wa utekelezaji majukumu waliyokasimiwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara 52, ambapo jukumu la msingi la Ofisi hiyo ni kuratibu na kusimamia shughuli za Serikali katika sekta zote na Bungeni pamoja na majukumu mengine yaliyoainishwa kwenye Tangazo la Serikali Na. 144 Aprili 2016, lililofanyiwa mabadiliko tarehe 7 Oktoba 2017.


Akiongea wakati akifunga rasmi mafunzo hayo, leo tarehe 28 Agosti  jijini Dodoma,  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli hakusita kueleza furaha yake juu ya utaratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendesha mafunzo kwa watumishi yanayolenga kujenga uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa.


“Nimevutiwa sana na mbinu zilizotumika katika ufundishaji wa mafunzo haya. Nimeambiwa katika kuhakikisha mnapata mbinu na umahiri kwenye Tathmini na Ufuatiliaji wa Sera, mmepitia Mpango Jumuishi wa Kitaifa wa masuala ya Lishe. Naelewa Ofisi ya Waziri Mkuu ndiyo mratibu wa mpango huu na sisi TAMISEMI tunatekeleza. Nakusudia na mimi Kufanya mafunzo kama haya kwa watumishi wa wizara yangu” amesisitiza Mweli.


Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko amelishukuru Shirika la Chakula Duniani kwa ufadhili wa mafunzo hayo, ambapo   matokeo ya mafunzo hayo  ni Ofisi hiyo kuwa na mfumo bora wa uratibu wa shughuli za serikali kutokana na mamlaka iliyonayo kikatiba ya kuratibu shughuli zote za Serikali pamoja na masuala mtambuka ikiwemo masuala ya lishe.


“Mafunzo haya yatakuwa ni mwendelezo kwa   maafisa wote na menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, lengo ni kuongeza umahiri kwa uchambuzi bora wa sera, ufuatiliaji na tathmini ya sera pamoja na kuwa na  mfumo bora wa mawasiliano ya utekelezaji wa majukumu kwa idara zote ndani ya Ofisi, pia na mfumo bora wa uratibu wa shughuli za serikali” amesisitiza Mwaluko.


Awali akiongea kabla ya kufungwa kwa mafunzo hayo, Kaimu mkurugenzi mkuu wa Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), Dickson Mwanyika amefafanua kuwa mafunzo hayo yaliyoendeshwa kwa utaratibu wa mijadala washiriki walipata fursa ya kufahamu mbinu za kimkakati za uchambuzi wa Sera na kanuni za uratibu wa Sera, njia za kufanya ufutiliaji na tathmini, vigezo vya kuzingatia katika kufanya tathmini na ufuatiliaji pamoja na  namna ya kuandika taarifa na muundo wa taarifa.


Wakiongea kwa nyakati tofauti kwenye mafunzo hayo, baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, Frank Mwega na Elilanga Kaaya  wamebainisha kuwa mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa washiriki katika kuwajengea uwezo. Aidha, wameshauri uendelevu wa mafunzo ya namna hiyo yenye kuwajengea uwezo watumishi kwenye maeneo ya utendaji.

MWISHO.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akisisitiza kuwa Ofisi hiyo itaendelea kutoa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) na kufungwa leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti, 2020.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko, akimshukuru Afisa Lishe kutoka Shirika la Chakula Duniani, Neema Shosho, kwa ufadhali wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa. Mafunzo hayo ya siku tano, yameendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) na kufungwa leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti, 2020.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli akisisitiza umuhimu wa ubora wa Uratibu wa shughuli za serikali wakati akifunga rasmi mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, kushoto kwake ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko na kulia ni  Kaimu mkurugenzi mkuu  wa Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) Dickson Mwanyika,  


Baadhi Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli wakati akifunga rasmi mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).

Mchumi Mwandamizi Ofisi ya Waziri Mkuu. Frank Mwenga, akieleza umuhimu wa  mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo wakati wa kufunga mafunzo hayo  leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).

Mchumi Ofisi ya Waziri Mkuu. Elilanga Kaaya, akieleza umuhimu wa  mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo wakati wa kufunga mafunzo hayo  leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu Gerald Mweli,   akimkabidhi cheti Afisa Habari Mwandamizi Ofisi ya Waziri Mkuu Isabela Katondo,  baada ya kuhitimu mafunzo ya Uchambuzi wa Takwimu, Ufuatiliaji  na Tathmini ya Sera na Uandishi wa Taarifa, leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu Gerald Mweli,   akimkabidhi cheti Afisa Utumishi Ofisi ya Waziri Mkuu Herman Chando, baada ya kuhitimu mafunzo ya Uchambuzi wa Takwimu, Ufuatiliaji  na Tathmini ya Sera na Uandishi wa Taarifa, leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).

Washiriki wa mafunzo ya Uchambuzi wa Takwimu, Ufuatiliaji  na Tathmini ya Sera na Uandishi wa Taarifa wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu,  Gerald Mweli (mwenye tai),  kulia kwake ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko, leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti  2020, Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA).


Read More

Tuesday, August 25, 2020

MAJALIWA AREJESHA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA RUANGWA

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Ruangwa, Frank Chonya ambaye ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo, fomu za kuwania Ubunge wa Jimbo la Ruangwa kupitia CCM,,wakati aliporejesha fomu hizo kwenye Ofisi ya Mukurugenzi huyo, Agosti 25,2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Ruangwa, Frank Chonya ambaye ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo, fomu za kuwania Ubunge wa Jimbo la Ruangwa kupitia CCM,,wakati aliporejesha fomu hizo kwenye Ofisi ya Mukurugenzi huyo, Agosti 25,2020.

Read More

Monday, August 24, 2020

MAAFISA OFISI YA WAZIRI MKUU WAPIGWA MSASA UTEKELEZAJI MAJUKUMU


Baadhi ya maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao(TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akisisitiza umuhimu wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Mtaalamu wa masuala ya Sera kutoka Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) Apronius Mbilinyi akiendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mafunzo hayo ya siku tano yanajikita katika namna ya kufanya Uchambuzi wa sera, Tathmini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa Sera hizo, utaalamu katika Uandishi wa Ripoti pamoja na namna bora ya  kutekeleza shughuli za Uratibu.  Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Baadhi ya maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo likiwa ni kutekeleza kwa ufanisi na weledi majukumu waliyokasimiwa. Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao, jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), Dickson Mwanyika akisisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kupata mafunzo ya kujenga uwezo kwa watumishi wa umma  lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo, jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.

Mchumi mwandamizi Ofisi ya Waziri Mkuu, Happiness Mugyabuso akipitia makabrasha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi hiyo, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa shughuli za serikali Paul Sangawe akisisitiza umuhimu wa ufanisi na weledi katika kutekeleza uratibu wa shughuli za serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu waliyokasimiwa maafisa wa Ofisi hiyo, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu na kuendeshwa na Wakala hiyo jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Afisa Tawala Mwandamizi  ofisi ya Waziri Mkuu Stephen Magoha akichangia juu ya masuala ya Uratibu wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko wakati akisisitiza umuhimu wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameratibiwa na Ofisi hiyo na kuendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA), jijini Dodoma leo tarehe 24 Agosti, 2020.
Read More

Friday, August 21, 2020

MAJALIWA ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE WA RUANGWA


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Ruangwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)  kutoka kwa Frank Chonya ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ruangwa, Agosti 21, 2020.

Read More

Tuesday, August 18, 2020

WAZIRI MKUU: WATANZANIA TUBADILIKE, TUJIVUNIE VYETU

         *Akagua mradi wa kiwanda cha sukari na shamba la miwa Bagamoyo


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wabadilike na wajifunze kujivunia kilicho chao. "Lazima tubadilike Watanzania, tuwe wazalendo, tukisemee kitu chetu, tujivunie kitu chetu na tujivunie ujuzi tulionao," amesema.

 

Ametoa wito huo leo (Jumanne Agosti 18, 2020) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa na wafanyakazi wa kiwanda cha sukari cha Bagamoyo (BSL), katika kata ya Makurunge, wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

 

Waziri Mkuu ambaye alifika kiwandani hapo na kukagua ujenzi wa kiwanda unaoendelea, pia alikagua miundombinu ya mradi wa shamba la miwa ikiwemo vitalu vya mbegu, miche, maabara ya kupima maji na udongo na miundombinu ya umwagiliaji.

 

"Ninasema tubadilike sababu nimeenda kwenye maabara yao na kukuta wataalamu wetu wako vizuri, wanafanya utafiti wa udongo, maji na mbegu. Wameelezea vizuri utafiti wao na matokeo tumeyaona ni mazuri.”

 

“Rais wetu alisema Watanzania tunaweza, na leo nimethibitisha kwamba Watanzania tunao uwezo wa kazi lakini tatizo letu hatuwezi kujisemea wenyewe. Lazima tujisifu, tujisemee kuhusu umahiri tulionao. Ni kwa nini tujidharau?", alihoji.

 

"Nataka tubadilike sababu Watanzania tunaweza. Baadhi yao wanatoka hapa hapa Bagamoyo. Nimemuuliza ulisoma wapi, akajibu Chuo cha Kilimo Kaole, na hiki kiko Bagamoyo. Wengine wanatoka SUA (Chuo cha Kilimo cha Sokoine). Lazima turingie nchi yetu, lazima tuitangaze nchi yetu na ni lazima tuisemee nchi yetu," amesisitiza.

 

Waziri Mkuu amesema uamuzi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa eneo hilo lenye hekta 10,000 ili lilimwe miwa na kujenga kiwanda cha sukari, ulilenga kuongeza uzalishaji wa sukari nchini. "Tunahitaji kupata mashamba mengi ya miwa ili tuongeze uzalishaji wa sukari nchini".

 

“Hivi sasa mahitaji ya suakri nchini yamefikia tani 450,000 kwa sukari ya mezani. Ile sukari ya viwandani ambayo inatumika kutengeneza soda, biskuti na pipi mahitaji yake ni tani 165,000 ambayo hapa nchini hatuizalishi, kwa hiyo inabidi tuiagize kutoka nje ya nchi.”

 

Amesema uzalishaji wa sukari ya mezani kwa sasa unafikia tani 380,000 kwa viwanda vyote vilivyopo na kwamba bado kuna bakaa ya tani 70,000. Amesema mbali ya viwanda vilivyopo vya TPC, Kagera, Mtibwa, Kilombero, Manyara na Bagamoyo bado kuna maeneo ya kulima miwa huko Tarime na Kigoma. “Tunawaalika wawekezaji walime miwa na kuzalisha sukari zaidi.”

 

Akielezea kuhusu ujenzi wa kiwanda hicho, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na kazi inayofanyika na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutahakikisha sukari inapatikana kulekule na pia itatoa fursa ya kilimo cha miwa kwa wakazi wa maeneo jirani.

 

Amewataka maafisa kilimo waende wakatoe elimu kwa wananchi kuhusu kilimo cha miwa. “Wapeni uhakika wa soko ili wasisite kushiriki kwenye hiki kilimo. Wananchi watavutiwa wakijua kuna faida kwenye kilimo hicho lakini pia kiwanda kitapata tani za ziada na kuongeza uzalishaji wake,” amesisitiza.

 

Mapema, Mkurugenzi wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Abubakar Bakhresa alimshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia shamba hilo na kuahidi kuendana na dhamira ya Serikali ya kupunguza tatizo la upatikanaji wa sukari nchini.

 

Akielezea hatua zilizofikiwa kwenye mradi huo, Mkurugenzi wa Mahusiano wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Hussein Sufian alisema gharama ya mradi huo ni dola za Marekani milioni 100 na kwamba hadi sasa wameshapata asilimia 70 ya mtaji.

 

“Benki ya Kilimo (TADB) imetukopesha dola za Marekani milioni 6.5, Benki ya CRDB wametukopesha dola za Marekani milioni 25, makampuni ya Bakhresa tumetoa dola za Marekani milioni 30 na benki ya Standard Chartered imetukopesha dola za Marekani milioni 10. Tunayashukuru mabenki za ndani kwa kukubali kutuunga mkono,” alisema.

 

Alisema kampuni yao mpaka sasa imetoa ajira kwa watu 600 ambapo 500 kati yao wanatoka kwenye vijiji jirani vinavyozunguka eneo la mradi na kwamba mara baada ya awamu ya kwanza kukamilika, uzalishaji utakapoanza wataweza kuajiri watu 1,500. “Awamu ya pili inatarajiwa kuwahusisha wakulima wa nje (outgrowers scheme) kwani mradi utawapa fursa ya kushiriki kilimo cha miwa na kupata soko la uhakika kutoka kiwandani,” alisema.

 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Japhet Justin alisema mbali ya kiwanda hicho cha sukari, wamelenga pia kuwanufaisha wakulima wadogo wa miwa. “Kwa kawaida wenye mabenki wanaamini ili aweze kumkopesha mkulima ni lazima aone eneo lake analomiliki.”

 

“Sisi tumeona fursa, na tumeamua wakulima watakaopata mikataba baina yao na kiwanda cha sukari Bagamoyo, tutachukua mikataba hiyo iwe dhamana ya kupata mikopo ya kuendeleza mashamba yao. Hii ni kwa sababu kuna vijiji vitano tayari vimefanyiwa upimaji na kuna uwezekano wa hekta 3,600 zitakazotumika kulima miwa.”

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo, alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kutoa eneo hilo ili BSL ianzishe kilimo cha miwa. “Tunamshukuru kwa sababu ametuongezea zao jingine la biashara.”

 

“Kabla ya hapo, tulikuwa na zao la korosho ambalo mwaka jana limewaingizia wakulima shilingi bilioni 60. Pia zao la ufuta liliwaingizia shilingi bilioni 19. Mwaka huu umetuita Tanga na kutuelekeza tuanzishe zao la mkonge, kwa hiyo kilimo cha miwa kimekuwa zao la nne mkoani kwetu na hivi sasa kuna kata tano ambazo ziko tayari kulima miwa.”

 

Read More

Monday, August 17, 2020

MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA VIONGOZI WA DINI

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full  Gospal Bibble Fellowship, Zakary Kakobe akizungumza katika  Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

Mufti  na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir  Ally  akizungumza katika  Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Abubakar Kunenge wakati alipowasili kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam kufungua Mkutano wa Viongozi wa Dini Kuelekea Uchaguzi Mkuu na Kuunga Mkono Juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika Ustawi wa Amani, Uzalendo na Kumtanguliza Mungu uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.  Wa pili kushoto ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum.

Read More

MAJALIWA AZUNGUMZA KATIKA MAHAFALI YA VYUO NA VYUO VIKUU JIJINI DAR ES SALAAM

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Mic Mdegela ambaye ni Mwanachuo wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anayesoma kozi ya Menejimenti ya  Rasilimaliwatu baada ya kuzungumza  na kutoa vyeti katika Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Kheri James.
MAJALIWA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Mic Mdegela ambaye ni Mwanachuo wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere anayesoma kozi ya Menejimenti ya  Rasilimaliwatu baada ya kuzungumza  na kutoa vyeti katika Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Kheri James.

Wanavyuo wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza katika  Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu vya  jijini Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika  Mahafali ya Vyuo na Vyuo Vikuu jijini vya Dar es salaam yaliyofanyika  kwenye kumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Agosti 17, 2020. 

Read More

Thursday, August 13, 2020

MAJALIWA ASALIMIANA NA WANANCHI WA MTAMA AKIWA NJIANI KWENDA RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na wananchi wa Mtama waliojitokeza kumlaki barabarani wakiongozwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Nape Nnauye, Agosti 13,2020.  Mheshimiwa Majaliwa alikuwa akitoka Dar es salaam kwenda Ruangwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na wananchi wa Mtama waliojitokeza kumlaki barabarani wakiongozwa na Mbunge aliyemaliza muda wake, Nape Nnauye, Agosti 13,2020.  Mheshimiwa Majaliwa alikuwa akitoka Dar es salaam kwenda Ruangwa.

 

Read More

MAJALIWA AKAGUA UKARABATI WA BARABARA YA SOMANGA - MBWEMKURU KATIKA KIJIJI CHA MTANDI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ukarabati wa barabara ya Somanga – Mbwemkuru katika kijiji cha  Mtandi Kata ya Kiranjeranje wilayani Kilwa , Agosti 13, 2020. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Arch.Elius Mwakalinga.
 

Read More

Sunday, August 9, 2020

MAJALIWA AKAGUA UJENZI WA MELI MPYA MWANZA

 

*Aitaka mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa wiki ijayo meli inaanza kazi

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekagua ukarabati  mkubwa wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi tu na kuagiza mamlaka inayosimamia ihakikishe kuwa kuanzia wiki ijayo meli hiyo inaanza kazi ya kusafirisha abiria na mizigo kwa kuwa ukarabati umekamilika na sasa inaendelea kukaa tu  hali ambayo ni hasara kwa Serikali.

 

Pia, Waziri Mkuu ametoa siku mbili kwa mamlaka inayohusika na utoaji wa kibali cha kuanza kazi kwa meli hiyo ihakikishe inatoa kibali hicho haraka na  ratiba ya safari itangazwe kwa sababu  Watanzania wanahamu  ya kuanza kuhuduiwa na meli hiyo.

 

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) baada ya kukagua meli hiyo ambayo tayari imeshafanya safari ya majaribio  kwa  kusafirisha  abiria kutoka Mwanza hadi Bukoba mkoani Kagera ambako ilirudi na abiria na mizigo.

 

Maeneo aliyokagua kwenye meli hiyo ni pamoja na vyumba vya abiria vikiwemo vyumba maalumu kwa ajili ya huduma za mama na mtoto, chumba cha kuongozea meli, vyumba vya migahawa na chumba cha injini.

 

“Nimeona ukarabati mkubwa uliofanywa, nimeona injini mpya, meli imekamilika na ilishafanyiwa majaribio ya aina zote kubeba abiria na kubeba mizigo na wataalamu wamejiridhisha kuwa inauwezo wa kubeba abiria na mizigo.”

 

Waziri Mkuu ameongeza kuwa “Haya yote ni mawazo na mipango ya Rais Dkt. John Magufuli pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020. Tumetekeleza na tunaendelea kutekeleza.”

 

Baada ya kukagua meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa chelezo pamoja na meli mpya na alieleza kuwa ameridhishwa na kazi inayoendelea kufanyika na amewataka Watanzania waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

 

Awali, Meneja Miradi ya Kimkakati inayotekelezwa na Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Luteni Kanali Vitus Mapunda alisema miradi hiyo minne ya ukarabati mkubwa wa meli ya Mv Victoria Hapa Kazi Tu, MV Butiama Hapa Kazi Tu, ujenzi wa chelezo na ujenzi wa meli mpya inayojulikana kama MV Mwanza Hapa Kazi Tu itagharimu sh. 152,916,249,842.

 

Alisema ukarabati wa meli ya MV New Victoria Hapa Kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mizigo tano 400 umegharimu sh. 22,712,098,200. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini, Kemendo na Bukoba.

 

“MV Butiama itakayobeba abiria 200 na mizigo tani 100 ukarabati wake umegharimu sh. 4,897,640,000. Meli hiyo itatoa huduma ya usafirishaji wa abiria na mizigo kati ya bandari ya Mwanza Kaskazini na Nansio Ukerewe. Ukarabati wa chelezo umegharimu sh. 36,152,511,642 na ujenzi wa meli mpya utagharimu sh. 89,154,000,000.”

 

Alisema kukamilika kwa miradi hiyo ya kimkakati kutafungua fursa nyingi za ajira binafsi na kupunguza gharama za usafirishaji sambamba na kuongeza tija katika shughuli za biashara hivyo kuwafanya wananchi wanyonge wengi kunufaika. Ujenzi wa Meli mpya unatarajiwa kukamilika Agosti 2021.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa nahodha wa meli ya  MV New Victoria – Hapa Kazi Tu, Bembele Samson Ng’wita (wa pili kulia)  wakati alipoikagua meli hiyo ambayo ukarabati wake umekamilika, kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa nahodha wa meli ya  MV New Victoria – Hapa Kazi Tu, Bembele Samson Ng’wita (wa pili kulia)  wakati alipoikagua meli hiyo ambayo ukarabati wake umekamilika, kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozwa na nahodha wa meli ya  MV  New Victoria – Hapa Kazi Tu,  Bembele Samson Ng’wita kukagua meli hilo ambayo ukarabati wake umekamilika , kwenye Bandari ya Mwanza South, Agosti 9, 2020.


 

Read More

Saturday, August 8, 2020

WAZIRI MKUU ATOA WIKI MOJA KWA WIZARA YA ELIMU

 

*Ni kuhusu ucheleweshwaji wa michango ya wanafunzi NHIF

 

 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa muda wa wiki moja kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kukutana na Wakuu wa Vyuo Vikuu nchini ili kubaini vyuo ambavyo vimeshindwa kuwasilisha michango ya wanafunzi katika Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) licha ya wanafunzi kulipa fedha hizo.

 

“Katibu Mkuu Wizara ya Elimu kashughulikie jambo hili tujue mifumo wanayotumia, pia nataka kujua ni wanafunzi wangapi ambao wamelipa na hawajapewa vitambulisho na kwa nini na nani amesababisha haya na hatua alizochukuliwa. Taarifa hiyo nataka niipate tarehe 16 mwezi huu, wiki moja inakutosha.”

 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Agosti 9, 2020) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kwanza kwa mwaka 2019/2020 wa Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi ya Elimu ya Juu Tanzania(TAHLISO) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

 

Ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanafunzi hao yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Peter Niboye ambaye alisema kwamba kumekuwepo na ucheleweshaji wa vitambulisho vya bima ya afya unaotokana na baadhi ya vyuo kuchelewa kufikisha fedha NHIF.

 

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuziagiza Menejimenti zote za vyuo vikuu nchini ziendelee kushirikiana kwa karibu na Serikali za Wanafunzi kwenye vyuo vyao ili waweze kushughulikia changamoto za wanafunzi kwa wakati.

 

Akizungumzia kuhusu wabunifu pamoja na wanafunzi bora, Waziri Mkuu amesema “Naiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia isimamie utambuzi wa masuala mbalimbali ya kitaaluma iwe ni kwenye teknolojia, afya na hawa wabunifu watambuliwe na waendelezwe. Tuwe na benki ya wabunifu waliobuni kazi ambazo zinaweza kusaidia jamii.”

 

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa taarifa ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia inaeleza kuwa tangu kufunguliwa kwa vyuo nchini tarehe 01 Juni, 2020 wanafunzi wote walioripoti wapo salama na wanaendelea vema na masomo yao.

 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAHLISO, Bw. Niboye  amesema wanajivunia kufanya kazi kwa karibu na Bodi ya Mikopo na Mfuko wa Bima ya Afya na imechangia kutokuwepo kwa migomo ya wanafunzi.

Akitoa tamko la jumuia hiyo katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu, amesema TAHLISO inamuunga mkono mlezi wao na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika uchaguzi huo na watahakikisha  anashinda kwa kishindo.

Mwenyekiti huyo amesema TAHLISO imefanya uamuzi huo baada ya kuridhishwa na utendajikazi wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. Magufuli ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama ya elimu, umeme, maji, miundombinu na afya.

 

OWM

Read More