Friday, December 4, 2020

FAO yaanza na halmashauri 3 kujenga uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa

Mratibu Taifa Dawati la Afya Moja, Ofisi ya Waziri Mkuu, Harrison Chinyuka akifafanua umuhimu wa kutumia Dhana ya Afya moja wakati wa mafunzo wa Kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi hiyo pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Baadhi ya Washiriki kutoka Halmashauri za mikoa ya Arusha, Dar es salaam na Mwanza wakifuatilia mafunzo ya Kuwajengea Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi hiyo pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Mratibu wa Mafunzo kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Tanzania, Elibariki Mwakapeje, akieleza dhamira ya Shirika hilo katika Kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Shirika hilo pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu, mjini Morogoro, kuanziatarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Baadhi ya Washiriki kutoka Halmashauri za mikoaya Arusha, Dar es salaam na Mwanza wakifuatilia mafunzo ya Kuwajengea Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi hiyo pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanziatarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Mtaalumu wa masuala ya Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Gibonce Kayuni akifundisha namna ya kupambana na usugu huo kwenye sekta ya mifugo wakati wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Mtaalumu wa masuala ya Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kutoka Chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi- Muhimbili, Hussein Mohamed akifundisha namna ya kupambana na usugu huo kenye Nyanja ya afya ya binadamu,wakati wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana yaAfya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali RBA linalojihusisha na kuelimisha jamii kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa, Erick Venant, akifundisha namna kuishirikisha jamii wakati wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Baadhi ya washiriki wa Mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa wa kijadili mbinu za kupambana na usugu huo wa wakati wa mafunzo yaliyoratibiwa na Ofisiya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO),mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Mtaalumu wa masuala ya Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kutoka Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine, Abubakar Hoza akifundisha namna ya kupambana na usugu huo kwa kwenye nyaja ya mifugo wakati wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO),mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Baadhi ya washiriki wa Mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa wa kijadili mbinu za kupambana na usugu huo wa wakati wa mafunzo yaliyoratibiwa na Ofisiya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO),mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Katibu Tawala Msaidizi (Uchumi), Mkoa wa Dar es salaam, Elizabert Mshote akitoa uzoefu wa shughuli za uratibu kama mshiriki wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanziatarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Katibu Tawala Msaidizi (Uchumi), Mkoa wa Arusha, Hargeney Chitukuro akitoa uzoefu wa shughuli za uratibu kama mshiriki wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Wazir Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020.
Washiriki na wawezeshaji wa mafunzo ya kuzijengea Halmashauri Uwezo wa kupambana na Usugu wa vimelea vya Magonjwa dhidi ya Dawa kwa kutumia Dhana ya Afya moja wakiwa katika picha ya pamoja, Mafunzo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), mjini Morogoro, kuanzia tarehe 2 hadi 4 Desemba, 2020. F
Read More

Friday, November 27, 2020

TAARIFA KWA UMMA

Read More

Monday, November 16, 2020

JE UNAWAFAHAMU MAWAZIRI WAKUU WOTE KUANZIA MWAKA 1961 HADI SASA?

Read More

Thursday, November 12, 2020

RAIS MAGUFULI AMPENDEKEZA KASSIM MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU

Mpambe wa Rais Kanali Benard Paulo Masala Mulunga akimkabidhi spika wa Bunge Job Ndugai barua kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli yenye pendekezo la la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyemteua, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akionesha kwa wabunge barua kutoka kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli yenye pendekezo la la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyemteua, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akisoma kwa wabunge barua kutoka kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli yenye pendekezo la la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyemteua, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimpongeza Waziri Mkuu Mteule na Mbunge wa Ruangwa Kassim Majaliwa baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kusoma jina lake baada ya kupendekezwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimpongeza Waziri Mkuu Mteule na Mbunge wa Ruangwa Kassim Majaliwa baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kusoma jina lake baada ya kupendekezwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimpongeza Waziri Mkuu Mteule na Mbunge wa Ruangwa Kassim Majaliwa baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kusoma jina lake baada ya kupendekezwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

 Mpambe wa Rais Kanali Benard Paulo Masala Mulunga (katikati) akisindikizwa na wapambe wasaidizi wa Bunge kukabidhi barua kwa spika wa Bunge kutoka Rais, Dkt. John Pombe Magufuli,  yenye pendekezo la jina la Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.


Read More

WABUNGE WAMTHIBITISHA MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU

 


*Apata asilimia 100 ya kura zote 350 zilizopigwa

*Amshukuru Rais na aahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii

 

 

SPIKA wa Bunge la 12 Job Ndugai amesema wabunge wamemthibitisha mbunge wa jimbo la Ruangwa mkoani Lindi, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kuwa Waziri Mkuu kwa miaka mitano mingine (2020-2025) kwa kupata kura zote 350 zilizopigwa na wabunge sawa na asilimia 100.

 

“Kura zote zilizopigwa ni 350 hakuna iliyoharibika, hakuna kura ya hapana. Kura zote 350 zimemthibitisha Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, kwa hiyo ndugu wabunge Mheshimiwa Majaliwa amethibitishwa na Bunge hili kuwa Waziri Mkuu kwa kura 350 sawa na asilimia 100.”

 

Spika Ndugai ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 12, 2020) Bungeni jijini Dodoma baada ya kupokea jina la Waziri Mkuu lililowasilishwa bungeni na Mpambe wa Rais na kisha wabunge kupiga kura kwa ajili ya kulithibitisha jina hilo.

 

Akizungumza baada ya kuthibitishwa Mheshimiwa Majaliwa amesema amepokea uteuzi huo kwa mikono miwili na anamshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameendelea kuwapa uhai wote na kushuhudia hayo, Pia ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyoionesha juu yake.

 

“Mheshimiwa spika naomba nitumie nafasi hii kwa dhati yangu ya moyo kumshukuru sana Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushindi mkubwa alioupata kutoka kwa Watanzania kupitia uchaguzi ambao ulifanyika hivi karibuni kwa kushinda kwa kishindo. Uchaguzi uliofanyika kwa uhuru na haki.”

 

 “Jambo hili si dogo, Mwenyezi Mungu ameliongoza, namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyonayo juu yangu na kuendelea kuniamini. Namshukuru sana na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa ushiriki wake katika kuridhia jina langu.”

 

“Pia, nampongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi huo na namna ambavyo Watanzania wameridhishwa na kazi aliyoifanya na imani waliyonayo kwamba viongozi hao wataendelea kuwatumikia vizuri zaidi.”

 

Ametumia fursa hiyo kumpongeza Spika wa Bunge Job Ndugai kwa kuchaguliwa bila kupingwa kuwa mbunge wa Kongwa pamoja na kurudi katika nafasi yake ya uspika baada ya kupigiwa kura nyingi na waheshimiwa wabunge, hakuna siri kwamba umefanya kazi nzuri miaka mitano iliyopita umeisaidia sana serikali na kuiwezesha kufanya mambo makubwa.

 

“Kazi uliyoifanya miaka mitano iliyopita tunaifahamu vizuri zaidi na Serikali itaendelea kukupa ushirikiano wa dhati. “Mheshimiwa spika niendelee kushukuru kwa kuwashukuru wabunge wenzangu, waheshimiwa wabunge wenzangu mmenifanyia jambo kubwa kwangu na familia yangu.”

 

“…idadi ya kura zenu mlizonipigia mmenipa changamoto sana. Haijawahi kutokea mmepiga kura kwa asilimia 100, haijawahi kutokea nawashukuru sana. Nitaendelea kushirikiana na wabunge wenzangu wote nikijua nyie ni wawakilishi wa Watanzania wanaotamani kupata maendeleo kupitia uwakilishi wenu. ”

 

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa jimbo la Ruangwa na mkoa wa Lindi, familia na CCM kwa ushirikiano alioupata katika kutekeleza majukumu yake katika kipindi cha miaka mitano na anaimani wataendelea kumpa ushirikiano katika kipindi cha miaka mitano mingine.

 

Awali, kabla ya kuthibitisha jina la Waziri Mkuu wabunge mbalimbali walizungumzia utendaji kazi wa Mheshimwa Majaliwa ambapo Mbunge wa Tunduma David Silinde alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumrudisha tena Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika nafasi hiyo.

 

Amesema kuwa Waziri Mkuu Majaliwa ni kiongozi mwenye uwezo wa kusimamia maono ya Rais Dkt. Magufuli katika kuibadilisha nchi na pia anauwezo wa kuunganisha nchi yote kupitia Bunge na hivyo kufanya kazi ya rais kuwa nyepesi.

 

“Sifa kuu ya kiongozi ni unyenyekevu, kujishusha na kusikiliza na sifa hizo Mheshimiwa Majaliwa anazo, ninaamini wote tutampitisha kwa asilimia 100 ili kuliambia Taifa nini tunakwenda kukifanya kwa miaka mitano baada ya miaka mitano ya mafanikio ambayo imeleta ushindi wa kimbunga.”

 

Amesema anaamini kwamba katika kipindi cha miaka mitano Serikali inakwenda kufanya mabadiliko makubwa katika Taifa na dunia inajua kuwa viongozi wao ni mahiri na kila mahali wanatetemeka kusikia kazi inayofanywa na viongozi hao.

“Naomba wote tumpitishe ili aweze kuongoza tena.”

 

Naye, Mbunge wa Ismani, William Lukuvi amesema Mheshimiwa Majaliwa ni binadamu mwenye upendo, mchapakazi asiyekuwa na majivuno na kwa mara ya kwanza ameshuhudia Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM akizunguka kwenda kuwatetea wabunge nchi nzima. “Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ametutendea haki Watanzania Mheshimiwa Majaliwa anatosha sana kuwa Waziri Mkuu.”

 

Kwa upande wake, Kapten Mstaafu George Mkuchika amesema Mheshimiwa Majaliwa anamfahamu vizuri na amewahi kufanya kazi wakiwa Ofisi ya Rais –TAMISEMI kwamba ni mtu mstarabu kama Mheshimiwa Majaliwa ni mtu msikivu, asiyejikweza na hajipendekezi anatenda haki kwa kila mtu.

 

“Katika kipindi cha miaka mitano hakubagua wabunge katika uetekelezaji wa shughuli za bunge na ni mtu msikivu sana. Amesimamia sana katika kufufua uchumi hasa mazao ya biashara, amerejesha mamlaka ya mkonge mikononi mwa Serikali. Ameratibu vizuri shughuli za wizara zote.”

 

Naye, Mama Salma Kikwete Alisema Mheshimiwa Majaliwa hakuwa mbaguzi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na amefanya mambo makubwa, hivyo anampongeza Rais Dkt. Magufuli  kwa kuwarejeshea kwani anastahiki kuwa Waziri Mkuu na hakuna anayeweza kupinga jambo hilo.

 

Mbunge mwingine, Fakharia Shomari alisema anamshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa uteuzi alioufanya katika nafasi ya Waziri Mkuu kwa sababu ni uteuzi ambao walikuwa wanaufikiria ila hawakuweza kuamua kabla ya yeye kutamka. “Mheshimiwa Majaliwa amefanya ziara nchi nzima na alikuwa anafanya kazi na kila rika na jamii. “Nawaomba wabunge wenzangu tuibariki hoja ya mheshimiwa Rais.”

 

Kwa upande wake, Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba alisema Mheshimiwa Majaliwa ni kiongozi msikivu, muadilifu, mnyenyekevu, hodari, mchapakazi na ni kiongozi shupavu ambaye nafasi hiyo anaimudu na anaiweza na hakuna shaka yoyote kwamba nafasi hiyo kwamba ataitendea haki. “Kumpigia kura nyingi tunaonesha imani kwa ndugu yetu na imani na busara kwa rais.”

 

 

 (mwisho)

Read More

RAIS MAGUFULI AMPENDEKEZA KASSIM MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU

 

Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini, Kepteni Mstaafu George Mkuchika  akitoa pongezi kwa Waziri Mkuu Mteule Kassim Majaliwa baada ya jina lake kupendekezwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bungeni jijini Dodoma, Novemba 12, 2020

Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi  akitoa pongezi kwa Waziri Mkuu Mteule Kassim Majaliwa baada ya jina lake kupendekezwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bungeni jijini Dodoma, Novemba 12, 2020

Waziri Mkuu Mteule na mbunge wa jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa akitoa shukrani kwa Rais Dkt. Magufuli kwa kumpendekeza kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupitishwa na wabunge kwa asilimia mia moja, Bungeni jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Waziri Mkuu Mteule na mbunge wa jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa akitoa shukrani kwa Rais Dkt. Magufuli kwa kumpendekeza kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupitishwa na wabunge kwa asilimia mia moja, Bungeni jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Prof. Adelardus Kilangi akisoma wasifu wa Waziri Mkuu Mteule Kassim Majaliwa baada ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kumpendekeza kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 12, 2020.

Read More

Tuesday, November 10, 2020

WAZIRI MKUU MSTAAFU, KASSIM MAJALIWA AAPA KUWA MBUNGE WA RUANGWA

  Waziri Mkuu Mstaafu, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Iramba Magharibi Dkt. Mwigulu Nchemba, Bungeni Jijini Dodoma Novemba 10, 2020.

Waziri Mkuu Mstaafu, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akiapa kuwa mbunge wa Ruangwa, Bungeni Jijini Dodoma Novemba 10, 2020.

Waziri Mkuu Mstaafu, na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akipokea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kanuni za Kudumu za Bunge kutoka kwa Katibu wa Bunge Stephen Kagaigai wakati alipoapa Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 10, 2020.

 

Read More

Sunday, November 8, 2020

WAZIRI MKUU MSTAAFU, KASSIM MAJALIWA AWAJULIA HALI MZEE KING KIKI NA MKUU WA WILAYA YA MLELE.

Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Msanii mkongwe wa muziki wa dansi  Kikumbi Mwanza Mpango, maarufu kama (King Kiki) , wakati alipomjulia hali msanii huyo anayesumbuliwa na matatizo ya pingiri za mgongo, nyumbani kwake Temeke kwa Azizi Ali, Novemba 8, 2020.

Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa akimjulia hali Msanii mkongwe wa muziki wa dansi  Kikumbi Mwanza Mpango, maarufu kama (King Kiki) , anayesumbuliwa na matatizo ya pingiri za mgongo, nyumbani kwake Temeke kwa Azizi Ali, Novemba 8, 2020. 

Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, akimpa pole Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Rechal Kasanda ambaye amelazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu baada ya kupata ajali ya gari Wilayani Mlele, Mkoani Katavi alipokuwa kwenye ziara ya kikazi, Novemba 8, 2020. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera. 

 

Read More

Thursday, October 22, 2020

JKT YATEKELEZA PROGRAMU YA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO AWAMU YA PILI (ASDP II)

 


Na. OWM, Morogoro.

Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, kilichopo Wilayani Kilombero, Mkoani Morogoro kimeanza kutekeleza kwa vitendo Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) kwa kuanza ujenzi wa skimu ya umwagiliaji ambayo kwa awamu ya kwanza skimu hiyo itakuwa na urefu wa Km 2.3, ambayo hivi karibuni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo ameweka jiwe la msingi la kuizindua.


Programu ya ASDP II inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, malengo yake ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo (kilimo, mifugo na uvuvi) kupitia maeneo makuu manne ikiwemo eneo la Usimamizi Endelevu wa Matumizi ya Maji na Ardhi ambalo moja ya kipaumbele cha uwekezaji ni kuendeleza miundo mbinu ya umwagiliaji.


Akiongea mara baada ya kufanya ziara kwenye Kikosi cha Jeshi 837KJ Chita, tarehe 21 Oktoba, 2020, Wilayani Kilombero lengo likiwa ni kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo kwa wadau wa Programu ya ASDP II, Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde, amefafanua kuwa ujenzi wa skimu hiyo utasaidia Programu kulifikia lengo la Kitaifa kwa miaka mitano la kuwa na eneo la umwagiliaji la hekta milioni moja na laki mbili.


“Jeshi la kujenga Taifa ni mdau muhimu katika utekelezaji wa Programu ya ASDP II, na kwa kikosi hiki cha 837 KJ Chita, kuanza ujenzi huu wa skimu ya umwagiliaji itasaidia kuongeza eneo linalohitajika la kilimo cha umwagiliaji nchini ambapo kwa sasa eneo lililopo la kilimo cha umwagiliaji ni takribani hekta laki sita na alfu tisini na nne tu.


Ameongeza kuwa mradi huo pia umezingatia kuongeza thamani ya zao la mpunga kwa kuanza ujenzi wa ghala la kuhifadhi mpunga sambamba na kuwa na mpango wa  kujenga kiwanda cha kusindika mpunga huo ambapo hatua hiyo inaongeza wigo wa Kikosi hicho kuwekeza kwenye eneo kuu la tatu la Programu ya ASDPII ambalo ni kukuza Biashara na Kuongeza Thamani.


Kwa upande wake Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni Nyakohanda Rusuhi ameeleza kuwa ujenzi wa skimu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya ASDP II pamoja na mipango ya JKT inayosimamiwa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Charles Mbuge, ambapo Programu hiyo inawataka wadau wake kufanya mageuzi kwenye sekta ya kilimo kwa kulima kilimo chenye tija.


“Awali wakati tunategemea kilimo cha mvua tulikuwa tunavuna gunia sita kwa hekari moja, lakini baada ya kukamilisha ujenzi wa skimu hii tunatarajia kuvuna takribani ya gunia 35 kwa hekari moja. Tukifanikiwa kupata mavuno haya tutakuwa tumezalisha chakula cha kutosha lakini pia tutakuwa tumefanikiwa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyelitaka Jeshi la kujenga Taifa kujilisha.” Amesisitiza Rusuhi.


Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Kanda ya juu Kusini -Mbeya, ambao wanashirikiana na JKT kujenga skimu hiyo, Mhandisi Elibariki Mwendo ameeleza kuwa tayari wameanza kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa kuanza na ujenzi wa awali wa ekari 2,500 kati ya ekari 12,000 zinazolengwa kujengwa.


Mhandisi Mwendo ameongeza kuwa ujenzi wa skimu hiyo utakuwa na ujenzi wa mifereji katika mito mitatu tofauti, ujenzi wa mifereji mikuu mama mitatu yenye urefu wa mita 1,716 pamoja na vivushamaji kupita kwenye reli ya TAZARA, pia ujenzi wa mabanio matatu, mifereji midogo ya kutoa maji shamba ipo 155, matuta mawili ya kuzuia mafuriko yenye kina cha wastani wa mita mbili.


Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) ilizinduliwa rasmi mwaka 2018 na inaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo inatekelezwa na wadau wakuu wa tatu ambao ni Serikali, Sekta Binafsi na Washirika wa maendeleo.


Malengo makuu ya Programu ya ASDP II ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo (kilimo, mifugo na uvuvi) ili kuongeza uzalishaji na tija, kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara zaidi na kuongeza pato la wakulima wadogo kwa ajili ya kuboresha maisha yao, usalama wa chakula na lishe.


Mbali na maeneo makuu ya ASDPII ambayo Kikosi cha JKT Chita kimeanza kutekeleza maeneo mengine ni Kuongeza Tija na Faida kwa lengo la kuongeza uzalishaji wenye tija hasa kwenye mazao ya kipaumbele; na Kuweka Mazingira Wezeshi ya Kuendeleza Sekta ya kilimo kwa kuwezesha uratibu, ufuatiliaji na kufanya tathmini ya sekta ikiwa ni pamoja na kuimarisha taasisi na kuweka mazingira wezeshi ya uratibu. Ni wazi kuwa Jeshi la Kujenga Taifa lipo kwenye nafasi kubwa ya kutekeleza Programu ya ASDPII kwenye maeneo yote makuu ya Programu hiyo.

MWISHO.

 

Sehemu ya ujenzi wa Vibanio vya maji inayojengwa kwenye mifereji mikuu mama kwenye skimu ya umwagiliaji inayojengwa na Jeshi la kujengaTaifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero, Morogoro, Ujenzi wa skimu hiyo ni katika kutekeleza Programu ya ASDP II ambayo moja ya kipaumbele cha uwekezaji ni kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji. Kwasasa eneo lililopo la kilimo cha umwagiliaji ni takribani hekta laki sita na alfu tisini na nne tu.

Sehemu ya Shamba la Mpunga la Jeshi la kujengaTaifa (JKT) kikosi cha 837KJ Chita, WilayaniKilombero, Morogoro.Kikosi hicho kimeanza kuboresha miundombinu ya umwagiliaji kwa kuanza na ujenzi wa awali wa ekari 2,500 kati ya ekari 12,000 zinazo lengwa kujengwa, Ujenzi wa miundombinu hiyo ni katika kutekeleza Programu ya ASDP II inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.


 

Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisiya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde,akifafanua umuhimu wa skimu ya umwagiliaji inayojengwa na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero, Morogoro wakati waziara ya kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo inayoratibiwa na Ofisi hiyo. Kulia kwake ni Mhandisi wa Mradi, Meja Mbaraka Magogo na kushoto kwake ni Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni Nyakohanda Rusuhi na Mratibu Msaidizi Programu Ofisi ya Waziri Mkuu, MethewMwinuka.



Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde, akiongozwa na Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni Nyakohanda Rusuhi kukagua ujenzi wa skimu ya umwagiliaji inayojengwa na kikosi hicho Wilayani Kilombero, Morogoro wakati waziara ya kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo inayoratibiwa na Ofisi hiyo.


Sehemu ya ujenzi wa mifereji midogo inayojengwa kwenye skimu ya umwagiliaji inayojengwa na Jeshi la kujengaTaifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero, Morogoro. Skimu hiyo kwa awamu ya kwanza itakuwa na urefu wa mita 2300 ambapo Ujenzi wa skimu hiyo ni katika kutekeleza Programuya ASDP II inayoratibiwa na Ofisiya Waziri Mkuu.

Mhandisi wa Mradi,  Meja Mbaraka Magogo (mwenyemiwani) akiwaeleza waratibu wa Programu ya ASDP II, Ofisi ya Waziri Mkuu,juu ya ramani ya eneo la shamba la Mpunga la kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero, Morogoro.Ujenzi wa skimu ya umwagiliaji, utasaidia Programu kulifikia lengo la Kitaifa kwa miaka mitano la kuwa na eneo la umwagiliaji la hekta milioni moja na laki mbili.

Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde,akisisitiza umuhimu wa skimu ya umwagiliaji inayojengwa na Jeshi la kujengaTaifa (JKT) kupitia kikosi cha 837KJ Chita, Wilayani Kilombero, Morogoro mara baada ya kukagua ujenzi wa skimuhiyo ambayo ni katika kutekeleza Programu hiyo inayoratibiwa n aOfisi ya Waziri Mkuu.

Mratibu wa Programu ya ASDP II Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Salim Nandonde,akimkabidhi Afisa Utawala wa Kikosi cha 837 KJ Chita, Kapteni Nyakohanda Rusuhi nyaraka za Programu ya ASDP II, mara baada kukagua ujenzi wa skimu ya umwagiliaji. Ambayo ni katika kutekeleza Programu hiyo inayoratibiwa na Ofisiya Waziri Mkuu.
Read More

Wednesday, September 30, 2020

MKURUGENZI WA SERA NA MIPANGO OFISI YA WAZIRI MKUU ASTAAFU UTUMISHI WA UMMA

 

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Packshard Mkongwa akipokea zawadi kutoka kwa Bi. Dorothy Mwaluko,Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Wakati wa sherehe fupi ya kuagwa rasmi na Uongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Bwana Mkongwa amestaafu rasmi Utumishi wa umma kuanzia tarehe 30.09.2020.

 

 


Read More

KATIBU MKUU OWM BI. DOROTHY MWALUKO AKUTANA NA WAWAKILISHI WAKAAZI WA MASHIRIKA YA UMOJA WA MATAIFA(UN)

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Dorothy Mwaluko akutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa(UN) Ofisini kwake jijini Dodoma.

Viongozi aliokutana  nao ni Bw. Zlatan Milisre muwakilishi Mkazi wa  Umoja wa Mataifa(UN) aliyeambatana na wawakilishi wa mashirika mengine ndani ya Umoja wa Mataifa.

Ambao ni muwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP)  Bi. Christine Musisi, mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalo hudumia watoto(UNICEF) Bi. Shalia Batiguna na muwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wahamiaji(IOM) Bw. Qasim Sufi.

Wawakilishi hao wamashirika ya Umoja wa Mataifa wametoa misaada ya vifaa mbalimbali kwa Idara ya Uratibu wa Maafa ikiwemo vifaa vya teknolojia ya Habari na Mawasiliano ili viweze kusaidia kituo cha kujiandaa kukabiliana na Majanga yanayotokana na Maafa hapa Nchini.

Aidha,Katibu Mkuu Bi. Dorothy Mwaluko ameshukuru kwa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia Mashirika yake kwa kusaidia nyezo muhimu kwa Serikali ili mwananchi aweze kufikiwa na huduma kwa wakati pindi maafa yanapotokea.

Naye muwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Bw. Zlatan Milisre kwa niaba ya wawakilishi wenzake amesema Umoja wa Mataifa utaendelea kuwezesha Serikali hasa Idara ya Uratibu wa Maafa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu katika na yajazoite za vifaa na elimu kwa wataalamu iliwawezre kuhudyumia wananchi kikamilifu. 

Katibu mkuu Bi. Dorothy Mwaluko akimsikiliza muwakilishi Mkaazi washirika la umoja wa mataifa Bw. Zlatan Milisre(kulia) alipokuwa akitowa maelezo ya misaada iliyotolewa na (UN) kiushoto ni muwakilishi mkazi wa (UNDP) Christine Musisi.

 

Read More

Monday, September 21, 2020

SEKTA BINAFSI WAIJADILI TAARIFA YA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA SERA YA TAIFA YA UWEKEZAJI YA MWAKA 1996. • Waridhishwa na ushirikiano kutoka sekta ya umma kwenye masuala ya uwekezaji




Na. OWM, DAR ES SALAAM.

Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Maendeleo ya Uwekezaji imekutana na wadau wa uwekezaji wa sekta Binafsi kwa lengo la kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996. Wadau hao kupitia Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Baada ya kupokea rasimu ya taarifa hiyo,wameridhishwa kwa jinsi serikali imekuwa ikiishirikisha sekta binafsi katika masuala ya uwekezaji nchini.

Akiongea wakati wa kufungua mkutano huo kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu na Uwekezaji) Dorothy Mwaluko,  Mkurugenzi Idara ya Mipango na Bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu, Packshard Mkongwa amewahakikishia wadau wa Sekta Binafsi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao katika kukuza uwekezaji na biashara nchini.

Serikali imekuwa ikitekeleza sera za mageuzi ya uchumi kuanzia miaka ya 1980 kwa lengo la kuimarisha na kuiwezesha sekta binafsi kuwa mhimili wa ukuaji wa uchumi. Ili kutimiza azma hii, Serikali imekuwa ikitunga Sera na Sheria kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya kukuza uwekezaji na biashara nchini. Kwa mantiki hii tunakutana na nyie sekta binafsi ili muweze kutoa maoni yenu kuhusu rasimu ya taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996” Amesisitiza Mkongwa.

Ameongeza kuwa ili kuiwezesha Sekta Binafsi kuwa yenye nguvu na ushindani nchini amewataka wadau hao kuendelea kushirikiana na serikali katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara kwenye nyanja za Uratibu wa Masuala ya Uwekezaji, Utangazaji wa Fursa za Uwekezaji na Uwezeshaji Uwekezaji. Moja ya mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Sera hiyo  ni pamoja na Tanzania kufikia lengo la kuwa na Uchumi wa kipato cha Kati, Ukuaji wa Uchumi usioteteleka na kudhibiti mfumuko wa bei.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Zachy Mbenna akielezea maoni ya wadau na amefafanua kuwa mkutano huo wa  kuijadili rasimu ya  taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996 ni muendelezo wa  juhudi za  serikali katika kuweka mazingira bora na wezeshi ya biashara na uwekezaji nchini.

“Sisi wadau wa sekta Binafsi tungependa Sera ya Taifa ya Uwekezaji iwe kwenye mtazamo wa Kuhamasisha uwekezaji, kwa maneno, utekelezaji wake pamoja na sheria zinazo husiana na masuala ya uwekezaji zioneshe zinalenga kuhamasisha uwekezaji wa hapa nchini, kikanda na kimataifa. Sawa tunatengeneza Sera ya Uwekezaji ya Tanzania lakini lazima iwe imezingatia masuala yanayohusu uwekezaji ya kikanda na kimataifa” Ameeleza Mbenna.

Aidha, ameeleza kuwa Sera ya Uwekezaji haina budi kuangalia namna ya kutoa mwongozo wa kuwafanya wawekezaji wa ndani na nje wanao wekeza nchini juu ya namna wanaweza kuhimili majanga endapo yanatokea na kuweza kuathiri shughuli za uwekezaji. Mfano mzuri wa ugonjwa wa homa ya COVID-19 ulivyo athiri shughuli zao za uwekezaji. Amesisitiza pia kuwa ni vyema kuwa sera ikazingatia kuwa inawezesha kutumika kuchagiza maendeleo ya ukuaji wa uchumi nchini.

Mbenna amefafanua kuwa wangependa sheria za kisekta kwenye masuala ya uwekezaji na Biashara ioneshe namna zinavyounga mkono sheria mama ya uwekezaji. Pia tusiruhusu jitihada zinazo kinzana katika kuendeleza uwekezaji bali ziwe na uwiano mzuri, vile vile amesema katika uwiano huo, Sera za Zanzibar na Tanzania bara hazina budi kuzingatia hilo. Pia amebainisha kuwa Sera ni vyema itambue makundi yanayoibuka kama vijana yanaweza kuchukua nafasi katika masula ya uwekezaji.

Sera ya Taifa ya Uwekezaji imebainisha malengo mahsusi sita (6) na malengo nane (8) ya kisekta. Baadhi ya malengo hayo ni kuhamasisha uzalishaji wa ndani wa bidhaa kwa ajili ya mauzo ya nje; Kuvutia uwekezaji kutoka nje ya nchi; Kuhimiza na kuvutia matumizi ya teknolojia za kisasa katika uwekezaji; Kuweka mfumo mzuri na wa wazi wa kisheria; na kuondoa urasimu katika taratibu za upatikanaji wa vibali vya uwekezaji.

Mkutano huo uliowashirikisha  wadau wa sekta binafsi ni wa pili baada ya ule wa kwanza uliofanyika tarehe 11 Septemba, 2020 jijini Dodoma ambao ulihusisha wadau wa sekta ya umma kwa maana ya Wizara na Taasisi za Serikali. Mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maendeleo ya Uwekezaji kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

(MWISHO).

Mkurugenzi Idara ya Mipango na Bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu, Packshard Mkongwa akiwahakikishia wadau wa sekta Binafsi kuwa serikali itaendelea kushirikiana nao katika kukuza uwekezaji na biashara nchini wakati wa mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa sekta Binafsi wakifuatilia mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam. Mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Zachy Mbenna akisisitiza jinsi serikali inavyowapa ushirikiano wa kutosha kwenye masuala ya uwekezaji na biashara wakati wa mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam.

Baadhi ya wadau wa sekta Binafsi wakifuatilia mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam. Mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Mratibu wa Masuala ya Uwekezaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Jumanne Gomera, akiwasilisha wasilisho la taarifa ya Tathmini ya sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, wakati wa Mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Mshiriki wa mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya Mwaka 1996, akichangia wakati wa mkutano huo leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam. Mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Mratibu wa Masuala ya Uwekezaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Biveline Mushumbusi, akichangia wakati wa mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Mkurugezi wa Idara ya Maendeleo ya Uwekezaji, Aristides Mbwasi akieleza umuhimu wa wadau  wa Sekta Binafsi kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020,  Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).
Mkurugenzi Idara ya Mipango na Bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu, Packshard Mkongwa (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Dkt. Godwill Wanga (wa pili kutoka kulia), Mkurugezi wa Idara ya Maendeleo ya Uwekezaji, Aristides Mbwasi (wa kwanza kulia) na Mtaalamu wa Utafiti wa masuala ya sheria ya uwekezaji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dkt. Saudin Mwakaje wakifuatilia mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020, Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).
Mtaalamu wa Utafiti wa masuala ya sheria ya uwekezaji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dkt. Saudin Mwakaje akisisitiza  umuhimu wa wadau  wa Sekta Binafsi kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020,  Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Dkt. Godwill Wanga akifafanua jinsi Baraza hilo linavyshirikiana na Sekta Binafsi wakati wa mkutano wa kuijadili rasimu ya taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996, leo tarehe 21 Septemba 2020 Dar es Salaam, mkutano huo umeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya maendeleo ya Sekta Binafsi kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Read More