Wednesday, September 30, 2020

KATIBU MKUU OWM BI. DOROTHY MWALUKO AKUTANA NA WAWAKILISHI WAKAAZI WA MASHIRIKA YA UMOJA WA MATAIFA(UN)

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Dorothy Mwaluko akutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa(UN) Ofisini kwake jijini Dodoma.

Viongozi aliokutana  nao ni Bw. Zlatan Milisre muwakilishi Mkazi wa  Umoja wa Mataifa(UN) aliyeambatana na wawakilishi wa mashirika mengine ndani ya Umoja wa Mataifa.

Ambao ni muwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP)  Bi. Christine Musisi, mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalo hudumia watoto(UNICEF) Bi. Shalia Batiguna na muwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wahamiaji(IOM) Bw. Qasim Sufi.

Wawakilishi hao wamashirika ya Umoja wa Mataifa wametoa misaada ya vifaa mbalimbali kwa Idara ya Uratibu wa Maafa ikiwemo vifaa vya teknolojia ya Habari na Mawasiliano ili viweze kusaidia kituo cha kujiandaa kukabiliana na Majanga yanayotokana na Maafa hapa Nchini.

Aidha,Katibu Mkuu Bi. Dorothy Mwaluko ameshukuru kwa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia Mashirika yake kwa kusaidia nyezo muhimu kwa Serikali ili mwananchi aweze kufikiwa na huduma kwa wakati pindi maafa yanapotokea.

Naye muwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Bw. Zlatan Milisre kwa niaba ya wawakilishi wenzake amesema Umoja wa Mataifa utaendelea kuwezesha Serikali hasa Idara ya Uratibu wa Maafa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu katika na yajazoite za vifaa na elimu kwa wataalamu iliwawezre kuhudyumia wananchi kikamilifu. 

Katibu mkuu Bi. Dorothy Mwaluko akimsikiliza muwakilishi Mkaazi washirika la umoja wa mataifa Bw. Zlatan Milisre(kulia) alipokuwa akitowa maelezo ya misaada iliyotolewa na (UN) kiushoto ni muwakilishi mkazi wa (UNDP) Christine Musisi.

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.