Tuesday, September 1, 2020

MAJALIWA AVUNJA MAKUNDI CCM BABATI

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa  na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Babati Mjini Pauline Gekul (katikati) na   Esther Mahawe (kushoto) wakati alipowaasa  wanaCCM wote waliotia nia ya kugombea ubunge wa Jimbo hilo  waondoe tofauti zao  na wamuunge mkono mgombea aliyeteuliwa na CCM . Alikuwa akizindua Kampeni za CCM katika Mkoa wa Manyara kwenye uwanja wa Kwaraa mjini Babati, Septemba 1, 2020.

Mgombea ubunge wa Jimbo la Babati Mjini, Pauline Gekul akikumbatiana na  Esther Mahawe, mmoja wa wanaCCM waliotia nia ya kuomba uteuzi wa Chama wa kuwania ubunge katika Jimbo hilo katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CCM mkoani Manyara kwenye uwanja wa Kwaraa mjini Babati, Septemba 1, 2020.

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.