Friday, November 30, 2018

WAZIRI MKUU: TUTABORESHA MASLAHI YA WATUMISHI WOTE WA UMMA


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi wote wa umma wakiwemo wa kada ya afya kupitia Bodi ya Mishahara na Motisha baada ya kukamilisha uhakiki wa taarifa za kiutumishi.

Amesema kukamilika kwa uhakiki huo wa taarifa za kiutumishi kwa watumishi wa umma kutaiwezesha Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kupanga upya mishahara na motisha kwa watumishi.

Waziri Mkuu alitoa taarifa hiyo jana jioni (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na watumishi wa Kituo cha Afya cha Ushirombo wilayani Bukombe baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi mradi wa uboreshaji miundombinu wa kituo hicho uliogharimu sh. milioni 500.

Alisema Serikali inaendelea kushughulikia maslahi ya watumishi, hivyo aliwataka waendelee kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote. “Tunataka mwananchi akifika kwenye maeneo ya kutolea huduma apokelewe, asikilizwe na ahudumiwe.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali la kujenga Zahanati katika kila kijiji kwa kuwa wilaya hiyo imebakisha vijiji 2 kati ya 52 kumalizia ujenzi huo.

Waziri Mkuu alisema kwa sasa wananchi wa Ushirombo hawana sababu ya kusafiri umbali mrefu hadi Geita mjini au wilayani Kahama kwa ajili ya kufuata huduma za afya kwa kuwa huduma zote zitakuwa zikipatikana kituoni hapo.

Alizitaja huduma ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye Kituo cha Afya cha Ushirombo kuwa ni pamoja na za mama na mtoto, huduma za upasuaji wa aina zote mdogo na mkubwa, maabara, chumba cha kuhifadhia maiti.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bukombe, Dionis Myinga alisema ukarabati wa Kituo cha Afya cha Ushirombo ulianza Juni 22, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.

Alisema lengo la mradi huo ni kukiwezesha Kituo cha Afya cha Ushirombo kutoa huduma bora za upasuaji wa dharura kwa akinamama wajawazito pindi wapatapo matatizo yatokanayo na uzazi. Majengo yote ya kipaumbele yamekamilika kwa asilimia 99.

“Mradi huu ambao tunaujenga kwa kutumia force account, pamoja na lengo la kutatua matatizo yatokanayo na uzazi kwa akinamama mradi huu utakapokamilika, Kituo cha Afya cha Ushirombo kitaweza kuhudumia watu wapatao 54,271.”

Mkurugenzi huyo alisema mradi wa ukarabati wa kituo hicho cha afya unakadiriwa kutumia sh. milioni 436.933 hadi utakapokamilika na sh. milioni 63.066 zilizosalia kwenye ukarabati huo zitatumika kujenga njia za kuunganisha wodi na kukarabati majengo ya zamani.

 (mwisho)
Read More

Thursday, November 29, 2018

WAZIRI MKUU ACHUKIZWA NA WANAFUNZI KUKATISHWA MASOMO


*Ni baada ya wanafunzi 72 wa kike kupewa ujauzito wilayani Nyang’hwale

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amechukizwa na vitendo vya watoto wa kike kukatisha masomo yao kwa kupata ujauzito wilayani Nyang’hwale ambapo jumla ya wanafunzi 72 wamepata ujauzo katika kipindi cha miaka mitatu cha kuanzia mwaka 2016 hadi 2018.

Kutokana na wilaya hiyo kuwa na idadi kubwa ya watoto wa kike wanaokatisha masomo kutokana na ujauzito, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Hamim Gwiyama kufanya operesheni katika kila kijiji na kubaini waliowapa wanafunzi ujauzito na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumatano, Novemba 28, 2018) alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba,kijiji cha Kalumwa wilaya ya Nyang’hwale, akiwa katika ziara yake mkoani Geita.

“Jambo lingine litakalowawezesha kukabiliana na tatizo la ujauzito kwa wanafunzi wa kike ni kuanzisha miradi ya ujenzi wa mabweni ili watoto wa kike waweze kusoma bila ya kupata vishawishi vinavyosababisha wao kupata ujauzito.” 

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuacha jambo hilo likiendelea, hivyo aliwataka wananchi washirikiane katika kuwalinda watoto wa kike na Serikali itawachukulia hatua watendaji wote ambao katika maeneo yao watoto wa kike watabainika kuwa na ujauzito.

 “Watoto wa kike lazima waheshimiwe waachwe wasome bila ya usumbufu na atakayekatisha masomo adhabu yake ni kali. Tukikukuta umesimama na binti katika kona isiyoeleweka tutakukamata. Ole wenumtakaobainika kuwapa ujauzito wanafunzi, adhabu yake ni miaka 30 jela.”

Waziri Mkuu pia, alitoa onyo kwa wazazi au walezi watakaowaozesha watoto kike ambao bado ni wanafunzi na kwa upande wa wazazi watakaomsindikiza mtoto wao wa kiume kwenda kuoa mwanafunzi wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Katika kuoneshwa kuchukizwa na jambo hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mwita Waitara ambaye anashughulikia elimu, amemueleza Waziri Mkuu kwamba Novemba 30, 2018 yeye arudi wilayani hapo kwa  ajili ya kuwashughulia wote wanaokatisha masomo wanafunzi kike. Ametoa namba ya simu ili wananchi waanze kumpa taarifa za wahusika.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu alisemaSerikali imedhamiria kusambaza umeme katika vijiji vyote ambavyo bado havijaunganishiwa nishati hiyo nchini vitaunganishiwa katika awamu ya tatu ya Mradi wa Nishati Vijijini (REA).

“Rais wetu Dkt. John Magufuli anataka kuona nyumba ya kila Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu na ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”

Kuhusu suala la gharama za kulipia nguzo, Waziri Mkuu alisema wananchi hawatowajibika tena katika kulipia gharama za nguzo pamoja na zile za fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na Serikali.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Nyamigogo ambapo alikagua miundombinu ya kiwanda hicho na kisha aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda hicho, ambacho muwekezaji wake ni mzawa.
(mwisho)
Read More

MAAGIZO 5 YA WAZIRI MHAGAMA KWA KAMATI YA USIMAMIZI WA MENEJIMENTI YA MAAFA YA MKOA WA DAR ES SALAAM

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliye kuwa akimueleza juu ya ujenzi wa mfereji wa mto Ngo’mbe, wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza, Bibi, Nuru Damson, mkazi wa Dar es Salaam, aliye kuwa akimueleza  jinsi ujenzi wa mfereji wa mto Ngo’mbe, ulivyowasaidia kutopata athari za maafa ya mafuriko wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es Salaam. 
 NA MWANDISHI WETU:
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amefanya ziara ya siku moja mkoani Dar es salaam, lengo la ziara hiyo ni kukagua miundo mbinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko pamoja na kutaka kujua mikakati ya kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa mkoani humo ya kukabiliana na maafa hayo.

Katika ziara hiyo Waziri Mhagama emetembelea wilaya zote za mkoa wa Dar es salaam hususan katika maeneo ambayo mkoa huo umeboresha miundo mbinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko. Maeneo hayo ni Jangwani, Mto Mbezi, Mto Ng’ombe, Mto Bungoni na mfereji wa Mtoni kwa Azizi Ally.

Pamoja na kuridhishwa na jitihada zilizofanywa na mkoa wa Dar es salaam za kuboresha miundombinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko, pia na mikakati ya kukabiliana na maafa hayo waliyomueleza, Waziri Mhagama ametoa maagizo 5 kwa kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa ya mkoa huo kuyatekeleza  ili menejimenti ya maafa ya mafuriko mkaoni Dares salaam iwe endelevu.

“Nimeridhishwa na juhudi zilizofanywa na serikali kuu chini ya uongozi wa Dkt.Joh Pombe Magufuli za kuboresha miundo mbinu ya kakabiliana na maafa ya mafuriko, na nimeona jinsi serikali ya ngazi ya mkoa na wilaya zote zinavyo jitahidi kujenga uwezo   wa kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na maafa. Pamoja na jitihada hizo ninge penda kuishauri  na kuielekeza kamati na Mkuu wa mkoa ayasimamie maelekezo yangu.” Amesisitiza  Mhagama

Mhagama ameiagiza Kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa kusimamia suala la uharibifu wa mazingira hususani maeneo ya mito na mabondeni kwa mujibu wa sheria ya menejimenti ya maafa ya mwaka 2015. Aidha alifafanua kuwa Maafa mengi ya mafuriko mkoani humo yanatokana na uharibifu wa mazingira unaochangiwa na  ujenzi  katika maeneno yasiyo stahili kama kingo za mito na mabondeni hali ambayo huzuia maji kutiririka na kusababisha mafuriko.

Aidha Mhagama ameitaka kamati hiyo  kusimamia suala la usafi wa mitaro, mifereji na mito iliyopo  jijini  Dares salaam, ambayo hujaa maji wakati wa msimu wa mvua kutokana  na uchafu na takataka zilizotupwa katika mifereji na mitaro hiyo hali ambayo husababisha maji kushindwa kutirirka kuelekea baharini na hatimaye mitaro hiyo hujaa na kusababisha mafuriko.

Ameitaka kamati hiyo kuwasiliana na sekta nyingine zenye miundmbinu katika mitaro na mifereji inayojengwa na kuondoa miundo mbinu hiyo ili uboreshaji wa miundo mbinu hiyo kuwa wa ufanisi. Mhagama alibainisha kuwa Mkoa umefanya  juhudi nzuri za kujenga mitaro na mifereji lakini ndani ya  miundo mbinu hiyo  kuna miundombinu mingine kama vile mabomba ya  maji safi,  hivyo,  sekta nyingine husika hazina budi kushrikishwa na kuhakikisha miundo mbinu hiyo inatolewa ili kulifanya zoezi la kuboresha miundombinu ya maafa ya mafuriko linakuwa bora na ufanisi.

Kamati imetakiwa kuhakikisha miradi yote inayolenga kuboresha miundombinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko ndani ya mkoa wa Dar es salaam inashirikiana katika hatua ya kupanga utekelezaji wake. Mhagama amefafanua kuwa Mkoa una miradi mingi ya kuboresha miundo mbinu ya kukabiliana na maafa hivyo ni vyema miradi hiyo ikae pamoja ili kujua ni namna gani ya kutekeleza malengo yake hususani kujua miundo mbinu husika inawekwa wapi bila kuathiri utekelezaji wa mradi mwingine.

Mhe.Mhagama ameitaka kamati kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya sheria ya menejimenti ya maafa ya mwaka 2015. Amebainisha kuwa kila mmoja katika jamii analojukumu la kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na maafa, hivyo jamii ikiwa na elimu ya kutosha juu ya menejimenti ya maafa hususani ya mafuriko jamii haitapata athari kubwa za uharibifu wa mali na vifo vitokanavyo  na maafa ya mafuriko.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akioneshwa ujenzi wa miundombinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es saaam na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu hiyo mkoani humo.

Read More

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA, MASUMBWE WILAYANI MBOGWE.

 Wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia Mkutano wa Hadhara kwenye Kiwanja cha Shule ya Msingi ya Masumbwe wilayani Mbogwe, Novemba 29, 2018.

Wananchi wakimshangilia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipoingia kwenye Kiwanja cha Shule ya Misngi ya Masumbwe wilayani Mbogwe kuhutubia Mkutano wa Hadhara, Novemba 29, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa Hadhara kwenye Kiwanja cha Shule ya Msingi ya Masumbwe wilayani Mbogwe, Novemba 29, 2018. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa Hadhara kwenye Kiwanja cha Shule ya Msingi ya Masumbwe wilayani Mbogwe, Novemba 29, 2018. 

Read More

SERIKALI KUWANUFAISHA WACHIMBAJI WADOGO-MAJALIWA


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali imeweka mikakati mizuri kuhakikisha wananchi hususani wachimbaji wadogo wadogo wananufaika na uwepo wa rasilimali hiyo.

Hivyo, Waziri Mkuu amewashauri wachimbaji wadogo wadogo wajiunge katika vikundi ili Serikali iweze kuwapatia misaada mbalimbali ikiwemo mkopo ili waongeze mitaji.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi jengo la halmashauri ya Mbogwe.

Amewahamasisha wachimbaji hao watumie taasisi mbalimbali za kifedha na kukopa fedha na kununua mitambo ya uchimbaji na uchenjuaji kwa lengo la kujiongozea tija.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Geita kwa ziara ya kikazi, amesema wachimbaji wadogo wadogo waendelee kuwa na imani na Serikali yao, kwa kuwa imewapangia mambo mazuri.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa wilaya hiyo kwamba Serikali imedhamilia kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama.

Amesema katika kumaliza tatizo la maji Serikali imetoa zaidi ya sh. bilioni moja kwa ajili ya  uchimbaji visima virefu 11 na visima vifupi 43 katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati ya kumaliza tatizo la maji nchini kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.

Waziri Mkuu amesema kampeni hiyo inalenga kuhakikisha wananchi katika maeneo yote wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yao ya makazi.

“Serikali imedhamiria kuhakikisha wananchi wote nchini wakiwemo na wa wilaya ya Mbogwe wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao.”

Kuhusua suala la wanafunzi kukatishwa masomo kwa kupata ujauzito wilayani Mbogwe, Waziri Mkuu ameitaka jamii kukemea vitendo hivyo. Wanafunzi 54 wamepata ujauzito.

Amesema katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu wanafunzi 20 wa shule za msingi na 34 wa sekondari wameacha shule baada ya kupata ujauzito.

“Hali ni mbaya, Mbogwe inatia aibu kwa kuwa na idadi kubwa ya watoto waliopewa ujauzito. Naagiza msiwaguse wanafunzi wa kike ni moto utawaunguza. Tukikukamata jela miaka 30.”

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko amesema wilaya ya Mbogwe inafanya vizuri katika sekta ya madini, ambapo ina viwanda 27 vya kuchenjulia dhahabu.

Amesema katika kuhakikisha wachimbaji wadogo wadogo wanawezeshwa kufanya shughuli zao vizuri, Serikali imetenga eneo la hekta 547.64 kwa ajili ya kuwagawia wachimbaji hao.

Akizungumzia kuhusu leseni za uchimbaji mkoani Geita amesema kuna jumla ya leseni 971 za uchimbaji mdogo wa madini na kati yake zinazofanyakazi ni leseni 184 tu.

Waziri huyo amewataka wachimbaji wadogo wadogo waendelee na shughuli zao za uchimbaji kwenye maeneo yao waliyopangiwa na kwamba hakuna atakayewaondoa.

Awali, Waziri Mkuu alikagua na kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Mbogwe katika kijiji cha Kasosobe. Ujenzi huo utagharimu sh. bilioni 4.3. Pia alikagua mradi wa uboreshaji miundombinu na kuzindua maabara ya Kituo cha Afya Masumbwe.
 (mwisho)
Read More

MAJALIWA AFUNGUA JENGO LA MAABARA LA KITUO CHA AFYA CHA MASUMBWE WILAYANI MBOGWE.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Ilembela wilayani Mbogwe akiwa katika ziara ya mkoa wa Geita, Novemba 29, 2018. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua jengo la Maabara ya Kituo cha Afya cha Masumbwe wilayani Mbogwe, Novemba 29, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wazazi waliolazwa kwenye Kituo cha Afya cha Masumbwe wilayani Mbogwe, Novemba 29, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Bibi Frola Samwel aliyelazwa katika Kituo cha Afya  cha Masumbwe wilayani Mbogwe akimuuguza mwanae  Mathias Paschal wakati alipofungua jengo la Maabara ya Kituo hicho, Novemba 19, 2018. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi, Robert Gabriel. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Bibi Frola Samwel aliyelazwa katika Kituo cha Afya  cha Masumbwe wilayani Mbogwe akimuuguza mwanae  Mathias Paschal wakati alipofungua jengo la Maabara ya Kituo hicho, Novemba 19, 2018. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi, Robert Gabriel. 

Read More

WAZIRI MKUU: TUTABORESHA MASLAHI YA WATUMISHI WOTE WA UMMA


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi wote wa umma wakiwemo wa kada ya afya kupitia Bodi ya Mishahara na Motisha baada ya kukamilisha uhakiki wa taarifa za kiutumishi.

Amesema kukamilika kwa uhakiki huo wa taarifa za kiutumishi kwa watumishi wa umma kutaiwezesha Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kupanga upya mishahara na motisha kwa watumishi.

Waziri Mkuu alitoa taarifa hiyo jana jioni (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na watumishi wa Kituo cha Afya cha Ushirombo wilayani Bukombe baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi mradi wa uboreshaji miundombinu wa kituo hicho uliogharimu sh. milioni 500.

Alisema Serikali inaendelea kushughulikia maslahi ya watumishi, hivyo aliwataka waendelee kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote. “Tunataka mwananchi akifika kwenye maeneo ya kutolea huduma apokelewe, asikilizwe na ahudumiwe.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali la kujenga Zahanati katika kila kijiji kwa kuwa wilaya hiyo imebakisha vijiji 2 kati ya 52 kumalizia ujenzi huo.

Waziri Mkuu alisema kwa sasa wananchi wa Ushirombo hawana sababu ya kusafiri umbali mrefu hadi Geita mjini au wilayani Kahama kwa ajili ya kufuata huduma za afya kwa kuwa huduma zote zitakuwa zikipatikana kituoni hapo.

Alizitaja huduma ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye Kituo cha Afya cha Ushirombo kuwa ni pamoja na za mama na mtoto, huduma za upasuaji wa aina zote mdogo na mkubwa, maabara, chumba cha kuhifadhia maiti.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bukombe, Dionis Myinga alisema ukarabati wa Kituo cha Afya cha Ushirombo ulianza Juni 22, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.

Alisema lengo la mradi huo ni kukiwezesha Kituo cha Afya cha Ushirombo kutoa huduma bora za upasuaji wa dharura kwa akinamama wajawazito pindi wapatapo matatizo yatokanayo na uzazi. Majengo yote ya kipaumbele yamekamilika kwa asilimia 99.

“Mradi huu ambao tunaujenga kwa kutumia force account, pamoja na lengo la kutatua matatizo yatokanayo na uzazi kwa akinamama mradi huu utakapokamilika, Kituo cha Afya cha Ushirombo kitaweza kuhudumia watu wapatao 54,271.”

Mkurugenzi huyo alisema mradi wa ukarabati wa kituo hicho cha afya unakadiriwa kutumia sh. milioni 436.933 hadi utakapokamilika na sh. milioni 63.066 zilizosalia kwenye ukarabati huo zitatumika kujenga njia za kuunganisha wodi na kukarabati majengo ya zamani.

 (mwisho)
Read More

ZIARA YA MAJALIWA MKOANI GEITA


Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa akikagua ukarabati wa Kituo cha Afya cha ushirombo wilayani Bukombe, Novemba 29, 2018. 
 Wanakwaya wa Ushirombo wakiimba wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipohutubia Mkutano wa hadhara kwenye Stendi ya Ushirombo, Novemba 29, 2018.


Bibi Mageni Simon akiwa mwenye furaha baada  ya kujifungua katika mazigira safi na salama ya  hospitali ya wilaya ya Geita ya Nzera iliyokaguliwa na kuzinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Novemba 28, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   akiweka Jiwe la Msingi la Ukarabati wa Kituo cha Afya cha Ushirombo wilayani Bukombe, Novemba 29, 2018. Kulia ni Mbunge wa Bukombe na Naibu waziri wa Madini, Doto Biteko na wapili kushoto ni  Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.

Read More

Wednesday, November 28, 2018

ZAIDI YA SH. BILIONI TATU ZAPOTEA WILAYANI NYANGW’ALE

*Waziri Mkuu aagiza kuchukuliwa hatua kwa watumishi wote waliohusika

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyangw’ale waliohusika na ubadhilifu wa zaidi ya sh. bilioni tatu fedha ambazo zilitolewa na Serikali kugharamia miradi ya maendeleo wachukuliwe hatua.

Pia ameagiza kukamatwa na kuchukuliwa hatua kwa Mkaguzi wa Ndani wa halmashauri hiyo, Gavana Matesa kwa sababu ameshindwa kutoa kwa mamlaka husika kuhusu taarifa za wizi wa fedha za maendeleo zilizotafunwa.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumatano, Novemba 28, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Geita.

Miongoni mwa miradi ambayo fedha zake zimepotea ni pamoja na sh. bilioni 1.2 za ujenzi ofisi ya halmashauri hiyo, sh. milioni 400 za ukarabati wa kituo cha afya Nyangw’ale, sh. milioni 611.230 za miradi ya maji.

Nyingine ni sh. milioni 536.119 za mpango wa malipo kulingana na huduma (EP4R), sh. milioni 125.914 za ushuru wa huduma, sh. milioni 31 za ujenzi wa ofisi ya mbunge na sh. milioni 109 za mfuko wa barabara.

“Wilaya ya Nyangw’ale ni mpya na Serikali imekuwa ikileta fedha nyingi lakini fedha zote zimetafunwa, Serikali ipo makini sana na moja kati ya vita kubwa ni dhidi ya mafisadi, wala rushwa ambayo ni endelevu hivyo tutashughulika na kila mmoja.

Tayari watu saba akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale, Carlos Gwamagobe na wenzake wamekamatwa. Wizi unatisha Nyangw’ale wilaya inatia aibu tutawaondoa watu wote waliohusika na tutaendelea kuwakamata.”

Hata hivyo Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa wilaya hiyo kwamba Serikali itahakikisha miradi yote iliyoahidiwa kujengwa kwenye wilaya hiyo ikiwemo ya maji itatekelezwa kama ilivyopangwa, waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

Kuhusua suala la watumishi, amesema wilaya hiyo lazima iwe na watumishi wasafi wenye weledi wa kufanya kazi na lazima wahakikishe fedha za miradi zinazotolewa katika halmashauri hiyo zinalingana na thamani halisi ya mradi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema atahakikisha watumishi wote wa umma waliohusika na wizi huo wanachukuliwa hatua stahili na kwamba tayari baadhi yao wameshafikishwa kwenye vyombo vya dola. 

Amesema halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale inaongoza kwa matumizi mabaya ya fedha za maendeleo kwa kuwa awali lilikuwa chaka kubwa la wizi, ambapo amesema ni bora watumishi wote wasiokuwa waadifu waondolewe na waletwe wengine.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Gabriel amesema tayari baadhi ya watumishi wanaotuhumiwa kuhusika katika ubadhilifu wa fedha za miradi mbalimbali wameshakabidhiwa kwa vyombo vya dola huku watumishi wengine wakiendelea kuchunguzwa.”Watumishi wote waliohusika na wizi huu watapata tabu sana”

 (mwisho)
Read More

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SOKO LA KALANGALALA

*Azitaka halmashauri zingine nchini ziige mfano wa Mji wa Geita

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaameweka jiwe la msingi mradi ujenzi wa soko kuu la  Kalangalala katika Mji wa Geita na kuzitaka halmashauri zingine nchini kuiga.

Pia, amesema wajasiriamali waliokuwa wakifanya shughuli zao katika eneo hilo kabla ya  ujenzi watakuwa wa kwanza kupewa maeneo ya kufanyia biashara.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 28, 2018) baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa soko la Mji wa Geita.

Amesema ni vema halmashauri zote zikaiga mfano wa Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kujenga masoko ya kisasa ili wajasiriamali wapate maeneo ya kufanyia kazi zao.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwaondolea wananchi kwa kuboresha na kuimarisha huduma za jamii.”

Hivyo, Waziri Mkuu amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel kwa kuwa mbunifu na msimamiaji mzuri wa miradi ya maendeleo.

Waziri Mkuu amesema Serikali inahitaji viongozi wa aina yake, ambao si wabadhilifu bali wanajali thamani na maslahi ya wananchi katika maeneo yao ya kazi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi  Gabriel ameahidi kulinda heshima ya wananchi wa mkoa huo kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. 

Amesema atasimamia kikamilifu ujenzi wa miradi ya maendeleo, ukiwemo ujenzi wa soko la kisasa ambalo litakapokamilika wajasiriamali watafanyakazi muda wote hadi usiku.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Geita, Adolf Ritte amesema ujenzi wa mradi huo umegawanyika katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa soko lenye majengo makubwa mawili yenye thamani ya sh. bilioni 1.9. 

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na wananchi watakaokuwa wanakwenda kununua bidhaa mbalimbali kwenye soko hilo. 

“Pia Halmashauri ya Mji nayo itanufaika kwa kuongezeka kwa mapato yake ya ndani. Ajira zitakazozalishwa sokoni hapo ni takribani 200. Faida nyingine ya mradi huu ni kumaliza mgogoro wa maeneo ya kufanyia biashara katika mji wetu.” 

Mapema leo Waziri Mkuu alikagua mradi wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Mji Geita kwenye eneo la Magogo na kisha alikwenda katika eneo la Bombambili kwa ajili ya kukagua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa ofisi za CCM mkoa wa Geita.

(mwisho)
Read More

MAJALIWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA HOSPITALI YA WILAYA YA GEITA YA NZERA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wanawake waliojifungua katika Hospitali ya Wilaya  ya Geita ya Nzera baada ya kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali hiyo, Novemba 27, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijadili jambo na Mbunge wa Geita Vijijini, Jioseph Msukuma  wakati alipotembelea Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Geita, Novemba 27, 2018.

Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Geita  ya Nzera, Novemba 27, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mwita Waitara .  Watatu kulia ni Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma  na  wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nzera wilayani Geita, Novemba 27, 2018.

Read More

Tuesday, November 27, 2018

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA JENGO LA MAKTABA LA TAASISI YA MAENDELEO YA JAMII TENGERU ARUSHA.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Jengo la Maktaba ya kisasa katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tengeru mkoani Arusha.kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Dkt.Bakari George na kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.John Jingu Novemba 27, 2018.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akisalimiana naMkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Patrick Golwike wakati wa shughuli ya Uzinduzi wa Jengo la Maktaba la Chuo cha Tengeru Arusha Novemba 27, 2018.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama pamoja naKatibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.John Jingu wakizindua jiwe la msingi la Jengo la Maktaba ya Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru wakati wa uzinduzi huo.

Mkutubi wa Chuo cha Tengeru Bw.Joseph Athanas akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama  kuhusu eneo la mapokezi la Jengo la Maktaba ya chuo hicho mara baada ya uzinduzi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.John Jingu akizungumza na washiriki ikiwemo wanafunzi wa chuo cha Tengeru (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi huo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akihutubia kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa wakati wa ghafla ya uzinduzi wa Jengo jipya la Maktaba ya Taasisi ya Maendeleo ya Jamii ya Tengeru Arusha.
Bw. Nelgan Sigara ambaye ni rais wa Chuo cha Tengeru akimkabidhi zawadi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama kwa niaba ya wanafunzi wa chuo hicho wakati wa uzinduzi huo.


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro akizungumza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama wakati wa uzinduzi huo

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro akizungumza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama wakati wa uzinduzi huo

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe.Jerry Muro akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama wakati wa uzinduzi wa Jengo la Maktaba ya Chuo cha Tengeru.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tengeru mara baada ya uzinduzi wa Jengo la Maktaba ya chuo hicho Novemba 27, 2018.

Read More

WAZIRI MKUU AAGIZA MRADI WA MAJI CHATO UKAMILIKE KWA WAKATI

*Ni wa Imalabupina/Ichwankima wenye thamani ya sh. bil. 8.28

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaameweka jiwe la msingi mradi wa maji wa Imalabupina/Ichwankima wilayani Chato ambao una thamani ya sh. bilioni 8.28 na amewaagiza viongozi wa wilaya hiyo wahakikishe unakamilika kwa wakati.

Waziri Mkuu amesemaSerikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yao ya makazi.
Ameyasema hayo leo (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye kijiji cha Nyamirembe baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa maji wakati akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Geita.

Amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha wananchi wote nchini wakiwemo na wa wilaya ya Chato mkoani Geita wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao, hivyo amewataka waendelee kuwa na imaji na Serikali yao.

“Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwenye maeneo mbalimbali nchini vikiwemo na vijiji vya wilaya ya Chato ili kuwawezesha wananchi kupata maji.”
Waziri Mkuu ameagiza mradi huo ukamilike kwa wakati kwa kuwa Serikali inahitaji kuona wananchi wakinufaika na huduma hiyo. Mradi huo ulianza kujengwa Mei, 2017 na ulitakiwa ukamilike Mei, 2018 ila kutokana na changamoto mbalimbali unatarajiwa kukamilika Februari 2019.
Awali,Mkuu wa wilaya ya Chato Mhandisi, Mtemi Simeon alisema mradi huo unatarajiwa kuhudumia watu takribani 59,609 katika vijiji 11 vilivyopo kwenye kata nne za Nyamirembe, Ichwankima, Kachwamba na Kasenga.
“Vijiji vitakavyonufaika na mradi huu ni Nyamirembe, Kalebezo, Nyambiti, Busalala, Imalabupina, Ichwankima, Kachwamba, Ipandikilo, Idoselo, Igagula na Mwangaza. Tayari vituo 240 vya kuchotea maji vimeshakamilika na matenki nane kati ya tisa yamekamilika pamoja na mabirika 10 ya kunyweshea mifugo.”
(mwisho)
Read More