Friday, April 28, 2023

WAZIRI MHAGAMA KATIKA KIKAO CHA BUNGE CHA 15

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.  Pauline Gekul Wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa 11Kikao cha 15 Mjini Dodoma.

Read More

Wednesday, April 26, 2023

SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 59 YA MUUNGANO MWAKA HUU YAFANYIKA KILA MKOA


Kilele cha sherehe za Maadhisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Mwaka huu yamefanyika kiaina yake, ambapo kila mkoa unaadhimisha kwa kutelekeza maelekezo mahsusi ya Serikali.

Mkurugenzi wa Kitengo ya Maadhimisho na Sherehe za Kitaifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bw. Batholomeo Jungu ameyamesema hayo jana wakati ziara maalum ya Kamati ya Kitaifa ya maadhimisho hayo mwaka huu ilipotembelea na kukagua utekelezaji wa maelekezo mahsusi kwa Ofisi za Serikali Jijini Dodoma.

Bw. Jungu alisema kuwa kwenye mikoa ndipo kwenye wananchi hivyo shughuli hizi kufanyika katika mikoa zinaleta chachu ya uzalendo kwa wananchi sababu kila mtu anapata nafasi ya kushiriki kuanzia kwenye uzinduzi wa miradi, mashindano ya insha kwa wanafunzi, michezo mbalimbali, usafi wa mazingira na maswala mengine muhimu.

"Watu wapo katika kila mkoa, hivyo tukio hili la kushirikisha wananchi linaleta tija kwa jamii kwa kuona ni sehemu ya maadhimisho haya kwa vitendo,"alisisitiza Jungu.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Bi. Mary Maganga aliseme

Kila mwaka tarehe 26 mwezi Aprili hututumika kama kumbukumbu ya sherehe za Muungano wa Iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar, uliyofanya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo kaulimbiu ya Mwaka huu inasema “ Umoja wetu na Mshikamano ndiyo nguzo ya kukuza uchumi wetu.”

Katibu Mkuu Masanja alitumia fursa hiyo kueleza namna ofisi yake ilivyotekeleza maelekezo mahsusi ikiwemo kulipamba jengo la ofisi hiyo na kuweka picha za viongozi wakuu wa nchi pamoja na waasisi wa taifa leo

Read More

Tuesday, April 25, 2023

WAZIRI MHAGAMA KATIKA KIKAO CHA BUNGE CHA 13

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi Mhe. Dkt Angeline  Mabula na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja Wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa 11Kikao cha 13 Mjini Dodoma.

Read More

Monday, April 24, 2023

WAZIRI MHAGAMA KATIKA KIKAO CHA BUNGE CHA 12

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Feleshi Mwanasheria Mkuu wa Serikali Wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa 11Kikao cha 12 Mjini Dodoma.

Read More

Tuesday, April 18, 2023

WATAALAM WAJADILI KUHUSU MPANGO HARAKISHI WA UPATIKANAJI WA RASILIMALI WATU KATIKA SEKTA YA AFYA.



SERIKALI imefanya uwekezaji mkubwa na maboresho katika sekta ya Afya yanayokwenda sambamba na uwepo wa rasilimali watu itakayotoa huduma zenye ubora ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Hayo yameelezwa  na Mratibu wa Mipango ya Rasilimaliwatu katika sekta ya Afya Bw. Issa Mmbaga kutoka Wizara ya afya wakati wa mawasilisho yaliyohusu upatikanaji wa rasilimali watu katika sekta ya Afya, kwenye kikao cha wataalam kilichofanyika Jijini Dodoma.

Bw. Mmbaga alisema kuwa, baadhi ya maboresho yaliyofanywa katika kipindi cha miaka kumi iliyopita katika sekta hiyo ni pamoja na ujenzi wa hosptali mpya, ongezeko la vifaa tiba na kuboreshwa kwa miundombinu iliyopo katika eneo la huduma.

“Maboresho haya yamesababisha mahitaji ya ziada ya watumishi katika sekta hii hivyo serikali ina mikakati maalum ya kuhakikisha kunaupatikanaji wa kutosha wa wataalam ili kuwa na sekta ya afya yenye nguvu na uwezo wa kutoka huduma bora za afya”. Alisema Bw. Mmbaga.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Sera na Program Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Crispin Musiba, amesema kuwa, uzalishaji wa madaktari na wataalamu wengine katika sekta ya Afya umekuwa mkubwa zaidi kiasi kwamba, idadi kubwa ya wataalam hao wapo nje ya ajira.

“Kwa hivyo ili kupunguza muonekano wa wataalam hao kuwepo nje ya Ajira, tumeita kikao hiki ili kuweza kuwa accommodate wataalam hao katika kupata ajira, na kikao hiki kimetoka na maazimio nane (8) ambayo tumepeana muda wa mwezi mmoja ili yaweze kukamilishwa na kuwasilishwa katika ngazi za juu.” Alisisitiza

Naye Mkurugenzi wa Afya kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Ntuli Kapalagwe alisema, ipo haja ya kuendelea kuwa na program za elimu kwa umma kwa lengo la kuongeza uelewa kwa jamii hususan katika masuala ya huduma za kiafya ikiwemo zile za kibingwa zinazotolewa pamoja na kuwa na mikakati madhubuti ya tafiti mbalimbali zitakazoweza kusaidia kujua rasilimali iliyopo katika masuala ya afya.

“Maendeleo yaliyopo katika sekta ya afya, hayatazaa matunda ikiwa hatutaendelea kutoa elimu kwa umma kwa upana wake na kuwa na mikakati ya makusudi inayolenga kuboresha kada hii,”alisema Dkt. Ntuli

Kikao Hicho kilihusisha wataalam kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais Utumishi, Wizara ya Fedha na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu.

=MWISHO=


Read More

Sunday, April 16, 2023

SERIKALI YADHAMIRIA KUENDELEA KUZINGATIA MASUALA YA UTAWALA BORA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amesema serikali imeridhia kuwa kifungu maalumu cha bajeti kwa ajili ya kuendesha baraza la Vyama Vya Siasa ili kuweza kufanya shughuli zake kwa ufanisi.

Kauli hiyo imetoloewa wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Vyama Vya Siasa kilichofanyika Mjini Dar es salaam . Amesema serikali Imepitisha Bajeti ya shilingi Billioni Shilingi 1,586,662,000.00 kwa ajili ya kuendesha baraza la Vyama Vya Siasa kwa Mwaka wa fedha 2023/24.

“Kwa kuwa sasa Mhe. Rais Dkt. Samia Sulluhu Hassan ameamua kutenga fedha ya kuendesha baraza, naomba vikao vyote vya kikatiba vya baraza la vyama vya siasa vikae kwa kwa mujibu wa ratiba ikiwa ni pamoja na vikao vya kamati kwa kufuata kanuni na sheria.”

Ameongeza kusema baraza la vyama vya siasa lipewe nafasi ya kukutana serikali ili kujadiliana kuhusu mambo mabalimbali yanayohusu ustawi wa Demokrasia Nchini.

Iko miradi ya kimkakati hapa nchini, kuna kila sababu viongozi wa vyama vya siasa na baraza la vyama vya siasa wapate nafasi ya kuangalia miradihiyo , kwa sababu tunapofika kwenye masuala ya maendeleo ya nchi na ustawi nchi hakuna chama.

“kuna nafasi ya viongozi wa vyama vya siasa kutushauri vizuri zaidi kwa ustawi wa wananchi, “alisema Waziri Mhagama.

Aidha tunahitaji kutengeneza programu maalumu ya mafunzo kwa ajili ya viongozi wetu wa vyama vya siasa, ili tuendele kuimarisha  Demokrasia ya vyama vingi chini, hatuwezi kufanikiwa kama viongozi wetu hawataendana na mabadiliko yanayoyendelea kwenye ulimwengu wa sasa.

Katika hatua nyingine Waziri Mhagama ameomba migogoro ya vyama imalizwe ndani ya vyama, tunauwezo wa kuimaliza sisi wenyewe, tujenge uwezo wa kutizama matatizo yetu ndani ya chama na kuyamaliza ndani ya vyama vyetu.

Waziri amehimiza viongozi wa vyama vya siasa, kuzingatia sheria za matumizi na mapato ya fedha.

Waziri Mhagama ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania.

“Mhe. Rais alipoingia madarakani aliasisi ” 4r” ambazo ni (reconcilian, resiliance, reform and rebuilding) kwa kiswahili ni maridhiano, ustamilivu, mageuzi na mabadiliko hii ikiwa ni kwa lengo la kutoa mwongozo wa jinsi ambavyo siasa za nchi yetu zinapaswa kuwa.”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vyama Siasa Juma Ally Khatibu,  ameomba mfaunzo ya siku  tatu mara tu baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili kuwa na uelewa mkubwa kuhusu ” 4r”

Mafanikio ya kikosi kazi katika Mkutano ule uliofunguliwa  Mhe. Dkt,  Samia Suluhu Hassan Jijini Dodoma ambao ni zao la Baraza la Vyama Vya Siasa, ni pamoja na kufanyika kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa,  mafanikio mengine ni kuundwa kwa Tume ya  Rais ya  kuangalia namna ya  kuboresha Taasisi za Haki jinai.

 

 

 

Read More

Thursday, April 13, 2023

BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU IMEZINGATIA VIPAOMBELE MUHIMU KATIKA MASUALA YOTE YA URATIBU WA SHUGHULI ZA SERIKALI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista  Mhagama amesema Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia vipaombele muhimu katika maeneo yote yanayoratibiwa na Ofisi hiyo ili kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na tija kwa Taifa.

Ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya Mwaka wa fedha  2023/24 wakati wa Kikao cha Bunge la 12 Mkutano wa 11 Kikao cha sita Mjini Dodoma.

Waziri Mhagama amesema pamoja na mambo mengine, Bajeti ya Mwaka huu ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia masuala muhimu ikiwemo la Uratibu wa shughuli za Serikali kwa kueleza tayari ofisi hiyo umeunda  Idara ya ufuatiliaji na Tathimini ya utendaji wa serikaliambapo itawezesha kuwa na taarifa sahihi za utekelezaji wa Shughuki za Serikali.

Akizungumzia kuhusu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Waziri Mhagama amesema, Mamlaka imefanya   kazi ya kutosha katika maeneo yote manne ya kimkakati ya kupambana na dawa za kulevya, kupunguza uingizaji wa dawa za kulevya, kufanya ukaguzi katika maeneo yanayofanya biashara ya kemikali bashirifu na kufanya maboresho ya sheria na kuteketeza mashamba mengi ya bangi nchini.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Mamlaka imefanya vizuri katika kutoa elimu ya uelewa kuhusu matumizi ya madawa ya kulevya.

“Tumefanya vizuri katika kupunguza athari za madhara ya dawa za kulevya kwa waathirika, na huduma ya za kutibu urahibu wa dawa za kulevya na bado tunaendelea kufanya mashirikiano ya nchi, kikanda na kimataifa ili kukabiliana na jambo hili mtambuka.”Alisisitiza  

Kwa Upande wa suala la  Sera ya lishe, Waziri amesema Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, itakuja na Mkakati wa kuwa na Sera ya lishe, UKIMWI na Janga la matumizi ya Dawa za kulevya.

Pamoja na hilo, Waziri alieleza kuwa ofisi yale inasimamia Dawati la Afya Moja linaloshughulikia uratibu wa magonjwa ya mlipuko yanayoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, ili kuweza kukabiliana nayo na kuangalia usalama wa wananchi.

Aidha alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kwa falsafa yake ya kuliwezesha Taifa kuwa na ustahimilivu na kuleta mabadiliko makubwa ya kiuongozi, kidemokrasia, kiuchumi na mahusiano ya kimataifa na kuwataka  wabunge kuunga  mkono falsafa hiyo.

 

 

Read More

Friday, April 7, 2023

WAZIRI MHAGAMA NA SIMBACHAWENE WAKABIDHIANA OFISI


 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amewataka watumishi wa umma kutekeleza  majukumu yao ipasavyo  kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo wakati wa hafla ya makabidhiano  kati ya aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya uteuzi uliyofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia  Suluhu Hassan  Aprili 01 mwaka 2023.

Waziri  Mhagama  amesema dhamira ya mtumishi wa umma Nchini ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kikamilifu katika kuwahudumia wananchi mahali na kwa nafasi yoyote anayopangwa  kwa kuzingatia miongozo na taratibu  zilizopo.

“Mara zote dhamira ya mtumishi wa umma  Nchini ni kuhakikisha kila unapopangwa unafanya kazi kwa nguvu zako zote pamoja na utii  na kuwa tayari kutumikia Taifa mahali popote kwahiyo kurudi kwangu hapa najihesabu ni sehemu yenu pia kama mtumishi wa umma,” Amesema Mhe. Jenista.

Pia amebainisha kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo ina jukumu la kuratibu shughuli za Serikali haiwezi kufanikiwa ikiwa watumishi wake watashindwa kujidhatiti na kufanya kazi kwa moyo kwa kuzingatia mazingira husika.

“Msingi wa tija katika utendaji wa kazi Serikalini  unatutaka  kuwa na uratibu mzuri unaozingatia sera, miongozo na kanuni zilizopo kwa kuzingatia jukumu kubwa la Ofisi ya Waziri Mkuu ni kuratibu shughuli zote za Serikali na tuna jukumu la kusimamia Bunge kama mhimili mwingine ndani ya Nchi hivyo bila kuwa na ushirikiano hatutafikia malengo tunayokusudia,” Ameeleza.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amemshukuru  Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa  kumuamini na kumpa  fursa ya kulitumikia Taifa pamoja na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu  kwa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake.

“Nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniamini  kuendelea  kuwatumikia wananchi katika nafasi hii na watumishi pia nawashukuru kwa ushirikiano mlionipatia na kuwezesha kufanikisha shughuli za uratibu kwa kipindi chote,” Ameshukuru Mhe. Simbachawene.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amemshukuru Mhe. Simbachawene kwa utumishi wake mwema katika Ofisi hiyo.

Aidha ametumia nafasi hiyo kumkaribisha Mhe. Waziri Mhagama katika Ofisi ya Waziri Mkuu na kuahidi kumpa ushirikiano ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwatumikia wananachi.

Read More

Sunday, April 2, 2023

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT, SAMIA SULUHU HASSAN AMEWAPISHA MAWAZIRI WAWILI LEO BAADA YA KUFANYA MABADILIKO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Jenista Mhagama kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 02 Aprili, 2023

Read More