Wednesday, December 21, 2022

MAWAZIRI WAKUTANA KUIMARISHA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA KWA WATOTO


 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene ahimiza ushirikishwaji wa wadau wote katika kuunganisha nguvu ili kupambana na ukatili wa kijinsia kwa watoto.

Kauli hiyo ameitoa wakati akiongoza kikao kilichowakutanisha Mawaziri wa kisekta kilichofanyika leo jijini Dar es salaam, kilicholenga kuimarisha mikakati ya kupambana dhidi ya ukatili wa kijinsia kwa watoto.

“Waziri Simbachawene, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge na Uratibu kwa kushirikiana na wataalamu waandae miongozo yote izungumze kwa pamoja kuhusu ukatili wa kijinsia na baada ya kikao cha Mawaziri ushauri upelekwe kwa Waziri Mkuu ili aridhie.”

Ili hatua za muda mfupi hatua za muda wa kati na hatua za muda mrefu ziweze kuchukuliwa katika kupambana na vita hii, binadamu wamekuwa waajabu kuliko wanyama matukio mengi ya ukatili wa kijinsia yanafanywa na ndugu wa karibu.

Katika kikao hicho amesema Mwaka 2021 viliripotiwa vitendo vya unyanyasaji wa watoto 110499 ni asilimia chache yawalioripoti.

“Uliongoza ni ukatili wa ubakaji 5899 na waliolawitiwa 1114 na waliopata mimba za utotoni ni 1677 na utafiti ukaonesha namba hizi uzigawe kwa 60, utaona asilimia 60 inafanyika nyumbani walipo baba na mama ndugu jamaa na marafiki na asilimia 40 ni nje ya nyumbani, wakiwa shuleni au wanapoenda shuleni.”

Lazima tuimarishe mifumo izungumze na uwajibikaji, sheria tunazo tayari tuna miongozo mbalimbali sasa tunahitaji mawasiliano yaanzie kwa Mawaziri yashuke kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, ishuke kwenye kata zetu, ishuke kwenye mitaa na vijiji.

“Mfumo wa mawasiliano uende kwenye kamati za mabaraza ya madiwani kwenye Halmashauri zetu, lakini kwenye vikao vya maendeleo vya kata ili viwe na nguvu ya kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto ili hata marekebisho ya sheria ndogo ndogo yaanzie kule chini,” alisema Waziri Gwajima.

 

Read More

Friday, December 9, 2022

MIAKA 61 YA UHURU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene  amesema nchi imepiga hatua kubwa katika ujenzi wa maendeleo ambayo ni shirikishi na yamelenga watu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu katika kilele cha maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanzania Bara kilichofanyika Kibakwe Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa.

“Katika ujenzi wa maendeleo ukisema ujenzi wa sekondari za kata, ujenzi wa vituo vya afya ujenzi wa barabara vyote vimetekelezwa kwa kushirikisha wananchi.”

Kauli mbiu ya miaka 61 ya uhuru ambayo inasema, Amani na Umoja ni nguvu ya maendeleo yetu.” Imetusaidia kutimiza shabaha zetu.

“Mabadiliko ya kisiasa, mabadiliko ya kiuchumi, Mhe. Rais amepeleka maendeleo hayo kwa watu na maendeleo ya watu yanahitaji rasilimali fedha,” alisema waziri .

Sisi watanzania tuna misingi yetu kila awamu inayoingia  inategemea misingi ya awamu iliyopita ndio maana tumefika hapa tulipofika.

 “Watanzania wanapenda furaha watanzania hawapendi hofu watanzania ni watii kwa mamlaka, tuendelee kuheshimiana na kuipenda nchi yetu.”

Hata wenye mawazo mbadala Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua mipaka ndio maana anazungumzia R-nne watu wawe na utaratibu wa maridhiano; maelewano, kujenga upya, na kuendelea mbele.

“Tunaiona Tanzania iliyobadilika sana kimaendeleo, lakini imebakia na misingi ile ile iliyoachwa na waasisi wa Taifa letu katika mioyo ya watu.”

Tulivyopata uhuru falsafa ya Baba wa Taifa alisema, Uhuru ni kazi ndio maana wananchi wamejikita katika kufanya kazi.

Awali Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime amesema nchi imepiga hatua kwenye miundo mbinu ya Mawasiliano.

“Ujenzi wa miundo mbinu ya afya, ujenzi wa miundo mbinu ya elimu, mabadiliko haya yameasisiwa na viongozi wetu kutokana  na Amani na utulivu uliojengwa na wazee wetu.”

Naye muwasilishaji mada Mwl Charles Malugu amesema serikali ya awamu ya sita imefanya ujenzi wa sekondari vyumba 20000, na ujenzi wa vyumba 3000 kwa shule shikizi  ambao utasaidia wanafunzi wa kidato cha kwanza na wanafunzi wa darasa la kwanza kuanza masomo bila kuwa na kikwazo cha aina yoyote.

“Serikali ya awamu ya sita imeruhusu wanafunzi walikatisha masomo kutokana na ujauzito, kuendelea na masomo ili wasikatize ndoto zao.”

 

Read More

Thursday, December 8, 2022

RAIS WA JAMHURI YA WATU WA SAHRAWI ATEMBELEA MJI WA SERIKALI MTUMBA

 

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Sahrawi, Mhe. Brahim Ghali leo amefanya ziara ndogo katika mji wa Serikali  Mtumba ambapo alitembelea jengo la Ofisi ya Rais Menejiment na Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Katika ziara hiyo ndogo Mhe. Rais Brahim Ghali alikaribishwa na kuoneshwa Mji wa Serikali na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Uratibu Bwn. Omar S Ilyas, pamoja na Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Mji wa Serikali Bwn.  Meshack Bandawe, ambapo walipata nafasi ya kuonyeshwa kiwanja cha Ubalozi wa Taifa la watu wa Sahrawi.

Read More

Tuesday, December 6, 2022

DKT. GWAJIMA: ELIMU YA LISHE IPEWE KIPAUMBELE

Serikali imesisitiza utoaji wa elimu kwa jamii namna ya kuzingatia masuala ya lishe nchini ili kuwa na Taifa lenye afya bora na kujiletea maendeleo yake.

 

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt.Doroth Gwajima wakati akimwakilisha  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa  wakati wa Mkutano wa Nane wa Mwaka wa Wadau wa Lishe nchini uliofanyika uwanja wa shule ya Msingi Mukendo  Wilaya ya Musoma Mkoani Mara.

 

Akizugumza kuhusu Mkutano huo alisema, umewezesha washiriki kupata maelezo kuhusu utekelezaji wa afua za lishe kwa kipindi cha mwaka wa kwanza (2021/2022) wa utekelezaji wa Mpango Jumuishi wa Pili wa Kitaifa wa Lishe (2021/22 - 2025/26) na kusema kuwa tathmini hizo ni za muhimu kwani ndio kipimo cha kujua hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Mpango.

 

Kaulimbiu ya mkutano wa mwaka huu ni“KUONGEZA KASI KATIKA KUBORESHA HALI YA LISHE KWA MAENDELEO YA RASILIMALI WATU NA UCHUMI” .

 

Waziri alisema katika kutekeleza mpango Juishi wa Lishe suala la elimu lina umuhimu wa kipekee kwa kila mmoja ili kufikia malengo.

 

Alifafanua kuwa Serikali itaendelea kutoa kipaumbele juu ya jamii kupewa elimu ya namna ya kuzingatia lishe bora ili kuweza kuepukana na udumavu kwa watoto na kuwa na afya bora.

 

“Ili kupata matokeo chanya katika kuboresha hali ya lishe nchini ni muhimu kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya lishe. Pamoja na uhamasishaji kufanyika kabla ya mkutano na wakati wa  mkutano huu, natoa rai kwa Taasisi ya Chakula na Lishe na wadau wengine kuhakikisha tunabuni mikakati zaidi ya kufikisha elimu sahihi ya lishe kwa umma ili kusaidia jamii kuelewa changamoto,”Alisisitiza Dkt.  Gwajima

 

Aliekeza  kuwa,  upo  umuhimu  wa  kuwa  na  jitihada za makusudi ili kuhakikisha wadau wa sekta binafsi wanashirikishwa na kuwa na utaratibu mzuri wa kuchangia utekelezaji wa afua za lishe.

 

Aidha, Serikali chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kulipa umuhimu wa kipekee suala la lishe nchini ili kuifanya nchi yetu kuwa na uchumi imara kupitia maendeleo ya viwanda ambapo alieleza kuwa Maendeleo haya hayawezi kupatikana iwapo hatutaimarisha kasi ya kujenga na kulinda kizazi chenye nguvu, afya njema na uwezo wa kufikiri.

 

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde aliasema Wizara yake itaendelea kutoa kipaumbele katika kutenga fedha nyingi kwenye masuala ya lishe na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji ili kuchagiza ongezeko la upatikanaji wa chakula nchini.

 

"Uwekezaji katika kilimo utaleta matokeo chanya katika lishe, lazima tuwekeze katika uzalishaji wa mbegu, huduma za ugani, umwagiliaji na miundombinu ya uhifadhi wa mazao ili kufikia malengo kama yalivyotarajiwa," alisema Mhe. Mavunde

Naye, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega alisema kumekuwa na  chagamoto ya ulaji kwa kutozingatia  kauni za lishe bora inayosababisha changamoto za kifya kwa wengi.

“Takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha ulaji wa nyama kwa wastani wa mtu mmoja kwa mwaka ni kilo 15 wakati kiwango kinachopendekezwa na FAO kwa mtu mmoja kwa mwaka ni wastani wa kilo 50, upande wa ulaji wa samaki wastani wa kilo nane na nusu kwa mtu mmoja kwa mwaka, kiwango hichi kipo chini kulinganisha kiwango kinachopendekezwa cha kilo 23 kwa mtu mmoja kwa mwaka, aidha ulaji wa mayai na kuku bado si wa kuridhisha," alisisitiza Ulega.

Aidha  wizara imeendelea kutekeleza afua mbalimbali za kuhamasisha hali ya ulaji nchini ambapo wanahamasisha ulaji na utumiaji mazao ya mifugo kwa kushirikina na wadau mbalimbali sambamba na kuongeza uzalishaji nchini.

 

Read More

Monday, December 5, 2022

FEDHA ZA MAADHIMISHO YA UHURU KUJENGA MABWENI YA SHULE NANE

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema fedha zilizokuwa zimetengwa na Wizara na Taasisi kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe za Uhuru mwaka huu zitapelekwe Ofisi ya Rais – TAMISEMI nakutumika kujenga mabweni katika shule nane za Msingi za wanafunzi wenye mahitaji maalum hapa nchini.

Taarifa hiyo na Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene katika mkutano wake na waandishi wa habari Mjini Dodoma.

“Shilingi Milioni 960,000,000/- (Tshs Milioni Mia Tisa Sitini)  zitatumika kujenga shule ya msingi Buhangija Shinyanga, Goweko Tabora, Darajani Singida, Mtanga Lindi, Songambele Lindi, Msanzi Rukwa,  Idofi Njombe, na Longido Arusha.”

Ni dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais wetu ya kuwajali na kuwajengea mazingira rafiki watu wenye mahitaji maalum hapa nchini. Hili ni jambo kubwa la kishujaa na la kupongezwa sana na Wananchi wote wa Tanzania.

Aidha Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara mwaka huu 2022 yatafanyika kwa Midahalo na Makongamano mbalimbali yatakayofanyika katika Wilaya zote hapa nchini kujadili, kutafakari kwa pamoja na kukumbuka tulikotoka, tulipo na tunakoelekea kuhusu Maendeleo Endelevu ambayo Nchi yetu adhimu Tanzania imeyafikia. Hivyo hakutakuwa na Gwaride na shughuli nyingine za Kitaifa.

 

Waziri amesema, Maadhimisho ya MIAKA 61 YA UHURU yataadhimishwa kwa Kauli mbiu inayosema  “AMANI NA UMOJA NI NGUZO YA MAENDELEO YETU”.

“Makongamano hayo yatatanguliwa na ratiba mbalimbali kwa Viongozi wa Mikoa na Wilaya kufanya shughuli za Kijamii kama vile kufanya usafi katika maeneo ya Hospitali, shule, nyumba za Wazee na makundi yenye mahitaji maalum”

Waziri ameelekeza Ofisi zote za Serikali hapa nchini kupambwa kwa mapambo ya rangi za Bendera ya Taifa pamoja na picha ya Mheshimiwa Rais.

Read More

MKUU WA WILAYA YA MUSOMA DKT. HAULE AHIMIZA UPANDAJI WA MITI

MKUU wa Wilaya ya Musoma Dkt. Khalifan Haule amehimiza wananchi kuendelea kuwa mstari wa mbele katika upandaji wa miti ya matunda ili kupata matunda na vivuli katika maeneo yao.

 

Ametoa kauli hiyo  wakati wa zoezi la upandaji miti ya matunda katika shule ya Msingi ya Mwisenge iliyopo mkoani Mara.Zoezi hili ni moja ya shughuli zinazoambatana na Mkutano Mkuu wa Nane wa mwaka wa Wadau wa Lishe.

 

Aidha jumla ya miti 300 imetolewa na kugawa katika shule sita ikiwemo; Mwisenge, Mtakuja, Nyarigamba A, Nyarigamba B, Nyabisare na Nyarugusu ambapo kila shule itapewa miti 50.

 

“Leo tunazindua upandaji wa miti hii kwenye shule ya Kihistoria aliyosoma Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyeyere ikiwa ni ishara ya kuunga mkono jitihada za kuhamasisha ulaji wa matunda kwa lengo la kuimarisha masuala ya lishe nchini,”aslisema Dkt. Haule

 

Aidha lengo la zoezi hilo ni kuimarisha utekelezaji wa masuala ya  lishe nchini kwa kuhamasisha ulaji wa matunda na mbogamboga katika jamii zetu.

 

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe nchini Dkt.Germana Leyna amesema taasisi yake imejithatiti kuhakikisha elimu ya masuala ya chakula na lishe bora inatolewa kwa makundi yote ikiwemo watoto waliopo mashuleni.

 

Aliongezea kuwa watu wengi wanakula kwa mazoea na si kula lishe bora hivyo jamii haina budi kubadilisha mitazamo juu ya masuala ya lishe na kuyapa kipaumbele.

 

"Hakuna mtu anayeweza kufanikiwa ikiwa anachamoto za kiafya zinazochangiwa na lishe duni, hivyo kila mmoja anajukumu la kuzingatia lishe bora kwa afya bora,"alisisitiza Dkt. Germana

 

Alitoa neno la Shukrani Mstahiki Meya wa Manispaa la Musoma Kapteni Mstaafu Patrick Gumbo alipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe pamoja na Mkoa kwa kuratibu zoezi hilo huku akitoa rai kwa kila shule kuhakikisha wanatunza miti hiyo ili kutimiza malengo yaliyokusudiwa.

 

"Ni jambo jema limefanyika leo, jukumu lililopo mbele yetu ni kuhakikisha miti inatunzwa na inaleta manufaa kama ilivyokusudiwa," alisema Patrick

 

Naye Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Sigawa Mwita alitoa shukrani kwa kuitumia shule hiyo yenye historia kubwa nchini kwa kuzingatia Rais wa Awamu ya Kwanza Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisoma hapo na kueleza zoezi hilo ni sehemu ya kumuenzi mwalimu kwa kuzingatia alikuwa kinara wa masuala ya upandaji wa miti.

 

"Shule yetu inajumuisha na wanafunzi wenye mahitaji maalum na imendelea kuwa na ufaulu mzuri sana hii imetupa hamasa na kuonesha mnajali na mnatambua mchango wa shule hii," alisema Mwalimu Mwita

 

Read More

Saturday, December 3, 2022

SERIKALI KUJA NA MAELEKEZO KUIMARISHA UTENDAJI KAZI OFISI ZA KONGA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema serikali itatoa maelekezo kwa Halmashauri kuweka mipango maalumu ya kuziwezesha ofisi za vikundi vya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (Konga) katika maeneo ya usimamizi, ruzuku na mikopo. Ili kuwa imara na endelevu na kuwa na mchango mkubwa katika kufikia malengo ya kitaifa na dunia kuhusu UKIMWI.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene wakati wa uzinduzi wa magari nane ya mradi wa HEBU TUYAJENGE uliofanyika katika Ofisi za NACOPHA Mbezi Beach Dar es salaam.

“Serikali inatambua umuhimu wa mifumo ya kijamii kwa sababu ina mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa. Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI itaendelea kuhakikisha Uratibu wa Sera na miongozo unatoa fursa ya kuziwezesha Konga za WAVIU”

Aidha, katika hotuba yake, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo mahususi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia TACAID, Wizara ya Afya na wadau wengine kuweka jitihada na mikakati madhubuti katika kuzuia maambukizi mapya ili tuweze kufikia hatua ya kutokomeza kabisa.

 Ikiwa ni pamoja na Kuimarisha huduma za upimaji wa VVU na matumizi ya ARV ili kutokomeza vifo vitokanavyo na UKIMWI, kuweka mikakati ya kutokomeza ubaguzi na unyanyapaa kwa WAVIU.

“Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itayatekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa haraka ikiwa ni pamoja na kuziratibu Wizara husika na Wadau katika kuhakikisha maelekezo haya yanatekelezwa kwa wakati, alisema Waziri.”

Naye Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya amewapongeza NACOPHA kwa kazi nzuri ya kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

“Kuhamasisha watu kujitokeza na kupima afya zao ni njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.”

Akitoa taarifa Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) Bi, Leticia Mourice Kapela, amesema baraza limeneemeka kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwa upande wa vijana, wanawake na WAVIU kwa ujumla.

“Uwezeshi huu katika fursa za mafunzo, mitaji ya kifedha, vifaa vya kuanzia shughuli za ujasiriamali, umesaidia vijana WAVIU kupata ujasiri wa kukabiliana na kuziepuka changamoto mbalimbali zinazowaweka katika hatari ya kupata maambukizi, ikiwemo kuanza ngono katika umri mdogo, kuwa na mahusiano na watu wenye umri mkubwa  na ulevi wa kupindukia”

Naye Mkurugenzi TACAIDS Bi. Audrey Njelekela, amesema Konga ziko kwenye Halmashauri 184 na Afua zote zinatekelezwa kwa kushirikiana na Halmashauri.

“Kupata magari kutasaidia kuongeza kasi na ufanisi katika kuhakikisha muitikio wa kitaifa unatekelezwa”

Read More

Wednesday, November 30, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE AZINDUA PROGRAM YA EDUCTAION PLUS

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene azindua program ya education plus inayolenga kuhakisha vijana balehe (wasichana na wavulana) wanawezeshwa kuishi maisha salama, yenye afya, na tija - bila ukatili wa kijinsia, VVU na UKIMWI.

Akizindua program hiyo hii leo novemba 30, 2022 wakati wa halfa ya kuhitimisha wiki ya Vijana katika kuelekea siku ya UKIMWI Duniani Mkoani Lindi Waziri wa Nchi amesema amefarijika kwa jitihada za Taasisi ya TACAIDS pamoja na wadau katika utekelezaji wa afua za masuala ya UKIMWI.

Alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana wote nchini kuzingatia jitihada za Serikali katika mapambano haya ya VVU na UKIMWI kwa kuendelea kujilinda na kulinda wengine huku wakijiepusha na tabia hatarishi.

“Rai yangu kwa vijana wote nchini, hususani wasichana, fanyeni kila muwezalo ikiwa ni pamoja na kuzingatia maudhui ya kampeni mbalimbali ili kujikinga na maambukizi ya VVU. Wale mlio shuleni na vyuoni hakikisheni mnaweka mkazo katika Elimu na kujiepusha na tabia zote hatarishi zinazopelekea kupata maambukizi ya VVU.”alisema

Aidha, aliwasihi vijana walio nje ya shule na vyuo, kuzitumia fursa zilizopo katika kuviwezesha vikundi vya vijana kujiinua kiuchumi hii itasaidia kujiepusha na tabia za kukaa vijiweni na kushawishika kujiingiza katika vitendo vinavyopelekea kuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Akieleza hali ya maambukizi nchini Waziri Simbachawene alisema katika kuelekea lengo la sifuri ya maambukizo mapya, kama nchi maambukizo mapya yameendelea kushuka mwaka hadi mwaka, japokuwa sio kwa kasi ya kuridhisha. Kwani, hadi sasa takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 54,000 waliambukizwa VVU mwaka 2021 nchini. Hii ni sawa na takribani watu 4,500 kwa mwezi au watu 150 kwa siku.

“Vijana wenye umri wa miaka 15-24 ndio kundi ambalo linaonyesha kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizo mapya, kwani katika watu wote wanaopata maambukizo mapya ya VVU kila mwaka, takribani Asilimia 30 ni vijana wenye umri wa miaka 15-24 (yaani katika kila watu 10 wanaopata maambukizo mapya ya VVU watatu ni vijana wa umri huu),”alisisitiza

katika kundi la vijana wa miaka 15-24 wanaopata maambukizo mapya, takriban Asilimia 70 ni wasichana. Katika mwaka 2021, kulikuwa na maambukizi mapya 212 kila wiki kwa kundi la wasichana wa miaka 15 -24, Inamaanisha maambukizi mapya 30 kila siku.

 

 

Read More

Tuesday, November 29, 2022

SERIKALI YALENGA KUIMARISHA USAWA MAPAMBANO VIRUSI VYA UKIMWI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amepongeza Tume ya kudhibiti UKIMWI, Wizara ya Afya na Wizara ya TAMISEMI katika Mkakati wa kupambana na Ukimwi kama janga la kitaifa.

Hayo yamesemwa Waziri na Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene Jijini Dar es saalam, wakati wa uzinduzi wa taarifa ya hali ya UKIMWI duniani yenye Kauli Mbiu inayosema Dangerous Inequalities iliyotolewa Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi Duniani UNAIDS Bi, Winnie Byanyima.

“Serikali imedhamiria kuweka usawa wa kijografia usawa kimazingira usawa kati ya watoto na wakubwa na usawa wa kiuchumi ili kuhakikisha watu wote wanapata huduma sawa ili wasiathirike na wale walio athirika wapate huduma za matibabu lakini pia huduma sawasawa kuhakikisha wanaendesha maisha yao.”

Akitoa taarifa hiyo Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi Duniani UNAIDS Bi, Winnie Byanyima amesema Tanzania imejitahidi kupunguza Ongezeko la Maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kila Mwaka kwa miaka kumi mfululizo.

“Tanzania Imejitahidi kupunguza vifo vinavyosababishwa na UKIMWI na imekuwa ikifanya vizuri katika mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI.”

 

Read More

Monday, November 28, 2022

MHE. KATAMBI: JITIHADA ZA PAMOJA NI MUHIMU KATIKA KUTOKOMEZA VVU TANZANIA

 


NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi amesema, jitihada za pamoja kati ya Serikali, wadau mbalimbali nchini wakiwemo wananchi ni muhimu katika kutokomeza maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) nchini.

Mheshimiwa Katambi ameyasema hayo Novemba 28, 2022 katika Ukumbi wa Sea View Beach Resort mkoani Lindi wakati akifungua Kongamano la Kisayansi katika Wiki ya kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani.

"Napenda kuwakumbusha kuwa pamoja na mafanikio makubwa tuliyoyapata katika mapambano dhidi ya UKIMWI nchini ambapo idadi ya maambukizi mapya ya VVU pamoja na vifo vinavyotokana na UKIMWI kupungua sana na idadi ya watu wanaoishi na VVU kupata tiba.

"Bado tunayo maeneo ambayo juhudi zaidi zinahitajika. Maeneo haya ni pamoja na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na tiba kwa watoto chini ya miaka mitano. Pia kuna baadhi ya makundi yako nyuma katika kufikiwa na huduma za VVU na UKIMWI kama wanaume,vijana na makundi maalumu yalio katika hatari kubwa ya maambukizi ya VVU,"amesema Mheshimiwa Katambi.

Pia amesema,kongamano hilo la kisayansi limekuwa likifanyika kwa miaka mingi toka mwaka 2016 kama sehemu ya maadhimishio ya kuelekea siku ya UKIMWI duniani.

 

Kupitia kongamano hili, jumuiya ya wanasayansi wanapata nafasi ya kuungana na jamii kubwa zaidi katika kutafakari na kubadilishana mawazo, uzoefu pamoja na mbinu mpya za kisayansi za kupambana na janga la UKIMWI,

"Hivyo, kongamano la mwaka huu ni muhimu sana kwa kuwa Dunia pamoja na Taifa letu limeweka muelekeo mpya wa mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambapo kwa pamoja tumeamua kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

"Ili kutekeleza azima hiyo Dunia kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa linalishughulikia UKIMWI (UNAIDIS) limeandaa mkakati Mpya wa kuelekea lengo hilo (Global AIDS Strategy 2021-2026). Nasi kama taifa pia tumeandaa mikakati mipya ya Kitaifa na kisekta (Mkakati wa Taifa wa Sekta zote NMSF V na Mkakati wa Sekta ya Afya HSHSP V) ili kutekeleza azimio hilo,"amefafanua Mheshimiwa Katambi.

Pia amesema, kongamano hilo linafanyika chini ya kauli mbiu ya Equalize (Imarisha Usawa) ambapo litatoa nafasi ya wadau kujadili mbinu mpya na namna bora ya kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI katika huo muktadha mpya.

"Nimefahamishwa kuwa kongamano hili la siku mbili litahusisha wataalamu mbalimbali wakiwemo wanasayansi, watoa huduma za VVU na UKIMWI, wawakilishi mbalimbali wa jamii zinazotumia huduma hizo,wasimamizi na wadau wa maendeleo pamoja na wajumbe toka sekta mbalimbali.

"Inatarajiwa jumla ya mawasilisho 26 yatatolewa kwa njia ya muhadhara na mengine mengi kama mchapisho. Mawasilisho yote yamegawanyika katika mada kuu nane. Mgawano huu utatoa nafasi ya mijadala kuelekezwa katika maeneo makuu ya muitikio wa VVU na UKIMWI nchini,"amesema Mheshimiwa Katambi.

Wakati huo huo, Mhesshimiwa Katambi amesema fursa hiyo itakuwa muhimu katika kuweka nguvu mpya kuhakikisha mafanikio yaliyokwishapatikana mpaka sasa yanaendelezwa na makundi yaliyoachwa nyuma yanafikiwa kwa haraka na kwa ufanisi zaidi ili kufikia malengo ya kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

 

"Ninatambua kwamba katika makongamano kama haya, huwa kunaweza kuwa na tofauti kubwa ya kiwango cha uelewa wa mada pamoja na tofauti ya mitizamo. Nina waomba watoa mada kutumia lugha nyepesi katika kutoa mada zao ili kurahisisha ujumbe kufikia wajumbe na kupata uelewa wa pamoja na pia kwa wajumbe kuwa wasikivu pia wavumilivu pale ambapo sayansi inaelekeza mambo ambayo ni tofauti na mitizamo yao.

"Kusikia mada ni jambo moja na kutekeleza maelekezo ya kisayansi ni jambo tofauti. Ninapenda kuwashauri kuwa, ili tuweze kufanya mageuzi katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kupata matokeo chanya, hatuna budi kuzingatia zaidi ushauri wa kisayansi.

"Ninawaomba wote tutakapomaliza kongamano hili kila mmoja wetu kupitia asasi yake kufanya mapitio ya pamoja ya jinsi mada zilizowasilishwa hapa zinaweza kuboresha utendaji kazi wao na kufanya marekebisho stahiki. Ushirikiano kati ya asasi zinazotekeleza afua zinazofanana ni fursa muhimu ya kuanza kutekeleza mambo yale tuliyojifunza katika kingamano hili,"amebainisha Mheshimiwa Katambi.

Read More

Sunday, November 20, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE, AHIMIZA MAFUNZO YA ITIFAKI KUWA ENDELEVU


Waziri wa Nchi wa Ofisi ya Waziri Mkuu sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema ipo haja, mafunzo ya itifaki na uratibu wa maadhimisho kufanyika kila mwaka.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene wakati akifunga mafunzo kwa watendaji wa serikali yaliyohusu itifaki ya viongozi wa kitaifa iliyowakutanisha Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa yaliyofanyika Mkoani Singida.

“Mafunzo haya yanapaswa kuongezwa mada na kuongeza namba ya washiriki ili kujenga uelewa wa pamoja”

Ambao utasaidia kupata ufahamu na ujuzi muhimu wa namna ya uandaaji wa Maadhimisho yanayohusu Idara na Taasisi za Serikali kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na kuzijua kanuni za kiitifaki ambazo mtazitumia katika uendeshaji wa shughuli mbalimbali kwenye taasisi zenu.

Awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya amesema mafunzo yamelenga kuwa na utaratibu ambao umekubaliwa, ambao unaleta matokeo chanya na watu wote kuheshimu.

“Watendaji waliopokea mafunzo sasa watasaidia katika maeneo yao; kitengo cha maadhimisho Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa sababu ndio Ofisi inayosimamia itifaki za viongozi”.

Naye Mtendaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Profesa Elisante Ole Gabriel  aliyekuwa mtoa maada wa huduma bora kwa mteja; ameshukuru serikali kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo yamesaidia kuwajenga watendaji kwenda kwa muelekeo unaolengwa na nchi.

“Huu ni uwekezaji  wa kifikira unaofaa, watendaji wakitoa huduma bora kwa wananchi na kwa viongozi, mashauri yatapungua kwa sababu ya huduma kuwa nzuri.”

 

Read More

Tuesday, November 15, 2022

MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI KUFANYIKA LINDI.

 


Waziri wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema maadhimisho ya siku ya UKIMWI yanatarajiwa kufanyika Mkoani Lindi katika Uwanja wa Ilulu.

Mhe. Simbachawene ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome, Jijini  Dodoma.

Amesema kuwa maadhimisho hayo yataambatana na maonesho ya shughuli mbalimbali kutoka kwa wadau wa UKIMWI zikiwemo  huduma ya upimaji wa hiari wa virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine  itakayotolewa kuanzia   Novemba  24 hadi Desemba  01, 2022.

 

“Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Imarisha Usawa’ ambayo imetafsiriwa kutoka kauli mbiu ya kimataifa equalize, kaulimbiu hii inahimiza kutilia mkazo uimarishaji wa usawa kutoa huduma za UKIMWI kwa makundi yote ya wananchi na katika maeneo yote ya kijeografia kwa kuondoa vikwazo vinavyoondoa usawa katika kufikia dira ya kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.”Amesema Mhe. Simbachawene.

 

Pia ameeleza kwamba maadhimisho hayo yatatumika  kutathimini hali halisi na muelekeo wa kudhibiti virusi vya UKIMWI, Kitaifa na Kimataifa pamoja na kuhamasisha viongozi na jamii kuendelea kwa mapambano  ya kudhibiti virusi vya UKIMWI ili  kujumuisha katika mipango yao ya maendeleo.

“Maadhimisho haya yatatumika kama sehemu ya kuwaenzi wahanga wanaoishi na virusi vya UKIMWI na kuwakumbuka wale waliopoteza maisha  kutokana na UKIMWI pamoja na kujali yatima  ambao wametokana  na vifo vilivyosababishwa na ugonjwa huo.

Vilevile  Waziri Simbachawene ameiagiza  Mikoa yote nchini kuandaa na kuadhimisha siku hiyo kwa kushirikiana na wadau wengine katika  Mikoa na katika ngazi ya Wilaya.

“Maadhimisho haya yatatumika kuhamasisha masuala mabalimbali muhimu ikiwemo  utekelezaji wa azimio la umoja wa mataifa  la kutokomeza UKIMWI katika kuhakikisha  afua za kiafya  zinapewa rasilimali za kutosha na mifumo ya kiafya inaimarishwa”Amebainisha.

Aidha amesema kuendelea kuwepo kwa siku hiyo muhimu kutasaidia  upatikanaji wa dawa za kufubaza VVU, kuendeleza utafiti wa kutafuta chanjo, kuimarisha afua za kinga dhidi ya maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI na kuendelea kutekeleza afua za UKIMWI kwa kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu.

Read More

Sunday, November 13, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE, AMPONGEZA MAMA TUNU PINDA

 


Kuimba kuna nguvu kubwa; kuimba ni kusali mara mbili, wenzetu mmekuewa watumishi wa Mungu kwa njia ya uimbaji na kazi mnayoifanya ya utume inawasaidia mpate neema na baraka kubwa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene wakati wa uzinduzi wa Albamu ya Mtakatifu Theresia,  wa Mtoto  Yesu inayoitwa Mungu asiye shindwa iliyofanyika katika Parokia ya Nzinje Mjini Dodoma.

“Kwaya hii ya Mtakatifu Theresia, Mtoto yesu ndio anayoimbia Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda, amechagua jambo zuri sana la kufanya baada ya Kustaafu”.

Read More

Tuesday, October 18, 2022

WATENDAJI WAASWA KUTUNZA VITENDEA KAZI VYA OFISI



Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya ametoa rai kwa watendaji wa serikali kutunza vizuri vyombo vya usafiri walivyopewa ili viweze kuwasaidia katika utendaji wa kazi na  kudumu kwa muda mrefu.

Wito huo umetolewa wakati wa kukabidhi bajaji mbili kwa watumishi wa Ofisi ya Mpiga chapa wa serikali jijini Dar es saalam katika kuwajengea Mazingira mazuri watu wenye ulemavu ya utendaji wa kazi.

“Ofisi ya Waziri Mkuu moja ya jukumu lake ni kuwezesha watu wenye ulemavu kwa kusimamia Sera ya Watu wenye Ulemavu na Miongozo ya watu wenye Ulemavu”

Akitoa neno la shukrani Bwn. Ophin Malley ameshukuru  serikali kwa kuwatambua watu wenye ulemavu katika mazingira waliyonayo mahala pa kazi.

“Tunaomba kama itafaa tuweze kupatiwa baiskeli maalumu ili zituwezeshe kuturahisishia kutoka sehemu moja kwenda nyingine wakati wa utendaji wa Kazi”

 

Read More

Wednesday, October 12, 2022

SERIKALI YAOMBA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA

 


Serikali imetoa rai kwa viongozi wa dini kuendelea  kuhimiza jamii kuepuka uraibu wa matumizi ya dawa za kulevya na kujenga uelewa kuhusu madhara ya madawa ya kulevya.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti katika kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka 2022/23 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya Mjini Dodoma.

 “Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana Dawa za kulevya, itaendelea kushirikiana na Wizara nyingine katika kuona namna nzuri ya kuandaa maudhui ya mtandaoni ili kuelimisha vijana kuhusu athari ya dawa za kulevya kama ambavyo Tume ya Kudhibiti   UKIMWI inavyofanya”.

Tupo kwenye utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo imetoa maelekezo mahususi kuhusu kushughulikia dawa za kulevya, Amesema Naibu Waziri.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya Dkt. Alice Karungi ameipongeza serikali kwa kiwango cha fedha kilichopelekwa kwenye Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kinachoendana na kwa kiwango cha fedha kilichokadiriwa wakati wa bajeti.

“Zoezi la kuwasaidia vijana wetu waliopata nafuu ya uraibu wa dawa za kulevya kwa kupatiwa mafunzo ya kukuza ujuzi; kama sehemu ya jitihada za Mamlaka, katika  kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya, liwe endelevu”.

Naye Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila amesema mamlaka imeweka msukumo mkubwa katika kukabiliana dawa zinazotoka nje ya nchi, Heroin, Cocaine na Methamphetamine.

 “Bangi imekuwa ikitumika kwa wingi kwa sababu inapatikana kwa bei nafuu na zinalimwa katika maeneo ya kujificha sana”.

Tamaa ya kupata fedha imekuwa ikichochea wananchi kulima bangi kulinganisha na mazao mengine hata hivyo udhibiti unaendelea.

“Tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Klimo waweze kushauri Mwananchi badala ya kulima bangi walime zao gani ambalo litawasaidia kupata fedha nyingi.”

Naye Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Dkt. Leonard Maboko ameihakikishia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya kwamba fedha za Global Fund zitatoka robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/23.

 

“Mradi wa Umoja wa Mataifa wa Kuhusisha UKIMWI kwenye Mpango wa Maendeleo wa Taifa katika bajeti 2022/23 iliyoidhinishwa ya shilingi 2,132,610,000.00, tayari kiasi cha shilingi 1,090,849,597.00 zimepokelewa. Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (ATF) katika bajeti 2022/23 iliyoidhinishwa ya shilingi 1,880,000,000.00 fedha za ndani, tayari kiasi cha shilingi 469,992,000.00  zimepokelewa mwishoni mwa mwezi Septemba 2022 hivyo zitatumika katika robo ya pili ya mwaka (Oktoba – Desemba, 2022)”.

Naye Mhe. Asia Halamga ameomba serikali kubadili baadhi ya Sheria zinazowazuia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya iweze kufanya kazi zake kikamilifu.

“Fedha tunazotumia kutibu ni vyema tukazitumia kudhibiti ili tusiendelee kuumiza taifa na hasa vijana”.

 

Read More

MKUU WA WILAYA KOROGWE BASILLA: ELIMU YA MAAFA IPEWE KIPAUMBELE


 Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Basilla Mwanukuzi ameziasa Kamati za Maafa kuendelea kutoa elimu katika maeneo yao ili kujiandaa na kukabili maafa pindi yanapotokea na kuweka mkazo katika maafa yanayoathiri maeneo ya Wilaya hiyo.

 

Ametoa kauli hiyo wakati akifungua semina ya siku 5 ya kujenga uelewa juu ya upunguzaji wa madhara ya maafa katika jamii kwa wajumbe wa Kamati za Maafa Wilaya hiyo iliyohusisha Kata sita zinazoathiriwa na maafa ikiwemo Magoma, Foroforo, Kalalani, Dindira, Bungu na Kizara zilizopo Korogwe mkoani Tanga.

 

Semina hiyo iliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IMO) imewafikia zaidi ya wajumbe 50 kutoka katika Kata hizo ikiwemo Viongozi wa dini, Wazee Mashughuli pamoja na Watendaji wa Kata na Vijiji wa Wilaya hiyo.

 

Mkuu wa Wilaya aliwaasa wajumbe hao kuendeelea kuwa mabalozi wazuri katika kutoa elimu juu ya kujikinga na madhara yatokanayo na maafa ili kiuendelea kuwa na jamii iliyosalama

 

“Yatumieni mafunzo haya kama nyenzo muhimu katika maeneo yenu kuhakikisha mnajilinda na maafa yanayoweza kujitiokeza katika maeneo yenu, kukabili maafa kunahitaji kujitolea kwa mtu mmoja mmoja ili kuwa na mazingira salama,”alisisitiza Mhe. Mwanukuzi

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Luteni Kanali Selestine Masalamado akieleza lengo la semina hiyo ni kutoa elimu ya masuala ya maafa kuanzia ngazi ya Halmashauri hadi Kijiji ikiwa ni moja ya jukumu la idara hiyo ili kuwa na uelewa mpana kuhusu masuala ya menejimenti ya maafa.

 

“Idara ya Menejimenti ya maafa imekuwa ikiendesha semina hizo katika maeneo mbalimbali nchini ili kuendelea kuwajengea uelewa wananchi kuhusu mzingo mzima wa menejimenti ya maafa unaohusisha kuzuia, kujiandaa kukabili, kukabiliana, kurejesha hali pindi maafa yanapotokea katika maeneo yao,”alisema Kanali Masalamado.

 

Aliongezea kuwa miongoni mwa maeneo yaliyofikiwa ni pamoja  na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe kwa kuzingatia imekuwa ikikabiliwa na maafa mbalimbali yakiwemo ya uhalibifu wa mazao unaosababishwa na uvamizi wa wanyamapori(tembo), ukame, pamoja na mafuriko.

 

Naye Afisa Afya kutoka Wilaya ya Korogwe Bw. Majaliwa Tumaini alieleza mada kuhusu ugonjwa wa ebola aliiasa jamii kuona umuhimu wa kujilinda na kulinda wengine kwa kuzingatia madhara yatokanayo na ugonjwa huu.

 

“Lazima tuchukue tahadhari zote muhimu kwani ugonjwa huu upo nchi jirani, kila mmoja awe mlinzi wa wenzake huku tukifuatilia maelekezo yanayotolewa na Wizara husika na wataalam wa afya,” alieleza

Read More

Tuesday, October 11, 2022

WADAU WA MAENDELEO WAHIMIZWA KUCHANGIA VIFAA VYA MISAADA YA KIBINADAMU WAKATI WA MAAFA.

 


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa.

Mhe. Ummy aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa Kanda ya Kaskazini  lililopo maeneo ya Chekereni, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.

Alisema uungwaji mkono wa serikali kutoka kwa wadau unasadia wananchi kufikiwa na huduma kwa haraka kutokana na majanga yaliyojitokeza ambayo husabababisha madhara kama vifo, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na miundombinu.

“Nitoe wito kwa wadau na watu mbalimbali ambao wanaguswa kushirikiana na serikali kwa kutoa vifaa wafanye hivyo pengine ngaji ya Wilaya, Mkoa na hata kijiji ili tuwe navyo vya kutosha ili yanapotokea tunatoa msaada kwa haraka,” alihimiza Mhe. Ummy.

Pia Mhe. Ummy alisisitiza utunzwaji wa magahala hayo hatua itakayosaidia vifaa hivyo kudumu kwa muda mrefu na kuwa tayari kutumika pindi vinapohitajika katika maeneo yenye maafa.

Aidha aliupongeza uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa utayari wa kutoa msaada wa kibinadamu kwa wananchi wanaokumbwa na maafa kwa lengo la kuwasaidia kurejea katika hali yao ya awali.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni Afisa Mifugo katika Mkoa huo  Bwa. James Shao alisema ghala la Kanda ya Kasikazini linahudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.

 

Read More