Tuesday, October 18, 2022

WATENDAJI WAASWA KUTUNZA VITENDEA KAZI VYA OFISI



Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya ametoa rai kwa watendaji wa serikali kutunza vizuri vyombo vya usafiri walivyopewa ili viweze kuwasaidia katika utendaji wa kazi na  kudumu kwa muda mrefu.

Wito huo umetolewa wakati wa kukabidhi bajaji mbili kwa watumishi wa Ofisi ya Mpiga chapa wa serikali jijini Dar es saalam katika kuwajengea Mazingira mazuri watu wenye ulemavu ya utendaji wa kazi.

“Ofisi ya Waziri Mkuu moja ya jukumu lake ni kuwezesha watu wenye ulemavu kwa kusimamia Sera ya Watu wenye Ulemavu na Miongozo ya watu wenye Ulemavu”

Akitoa neno la shukrani Bwn. Ophin Malley ameshukuru  serikali kwa kuwatambua watu wenye ulemavu katika mazingira waliyonayo mahala pa kazi.

“Tunaomba kama itafaa tuweze kupatiwa baiskeli maalumu ili zituwezeshe kuturahisishia kutoka sehemu moja kwenda nyingine wakati wa utendaji wa Kazi”

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.