Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri
Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi amekutana na kufanya mazungumzo
na Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo - IFAD wanaosimamia
Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo na Uvuvi (AFDP) katika ukumbi wa Ofisi
hiyo leo 12 Septemba, 2024 Jijini Dodoma.
Thursday, September 12, 2024
DKT. YONAZI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA IFAD
Tuesday, September 10, 2024
MAONESHO YA MIFUKO YA UWEZESHAJI FURSA KWA WANANCHI SINGIDA
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu,
Mhe. William Lukuvi amefungua rasmi Maonesho ya Saba ya Mifuko na Programu za
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Mkoani Singida ambayo yanaratibiwa na Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)
Wakati
wa ufunguzi wa maonesho hayo, Mheshimiwa Lukuvi amesema kuwa maonesho hayo yatafungua
fursa za Kiuchimi kwa wafanyabiashara, wakulima na wafanyabiashara wa Singida
na Mikoa ya Jirani.
Waziri Lukuvi Aliongeza kuwa, Maonesho hayo yatawezesha wananchi kupata huduma za uwezeshaji ikiwemo mitaji, mikopo nafuu, dhamana za mikopo, vifaa, mashine au mitambo, urasimishaji ardhi,urasimishaji biashara, huduma za msimbomilia, ujuzi, ithibati ya bidhaa, huduma za sheria, huduma za ushirika, huduma za ushauri wa kitalaam, elimu rasmi na elimu ya ufundi stadi, kuunganisha wananchi na fursa,na ukaguzi wa bidhaa.
Mhe. Lukuvi alibainisha kuwa, Maonesho hayo ni muhimu kwa kuwa yanakutanisha wadau mbalimbali wa uwezeshaji wakiwemo, Wizara, Mikoa, Halmashauri; Taasisi zinazosimamia Mifuko na Programu za Uwezeshaji, Taasisi za Fedha, Wafanyabiashara, Kampuni, Taasisi za Elimu na Tafiti, Wakulima, Wafugaji,na Wajasiriamali.
Aliongeza kuwa, Maonesho hayo yana lengo la kuhakikisha kuwa washiriki wanabadilishana ujuzi, maarifa, uzoefu na teknolojia mbalimbali ambazo zinatumika katika kukuza ushiriki wa wananchi katika shughulli za kiuchumi.
“Nina imani kuwa, Maonesho haya yatatoa fursa nyingi kwa wananchi wa Mkoa wa Singida na Mikoa mingine.” Alisisitiza
Akiongea
kwa Niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Bunge naa Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, Mkurugenzi wa Idara ya
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi, Bw. Condradi
Milinga amesema kuwa pamoja na maonesho
hayo kutoa fursa mbalimbali kwa wajasailiamali, wananchi pia watapata mafunzo
na ujuzi kuhusu masuala mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Maonesho na kutoa
wito kwa wananchi kutembelea maonesho hayo.
Kwa Upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi (NEEC), Bi Beng’ Issa amesema kuwa kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa lengo la kujenga uchumi na kuwaondoa wananchi katika umaskini.
“Juhudi hizo ni pamoja na kuanzisha mifuko na program za uwezeshaji mbalimbali kwa lengo la kutoa mikopo au dhamana ya mikopo kwa wananchi kwa masharti nafuu, kutoa ruzuku pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi ili waweze kukopesheka au kuhudumiwa na wadau wengine.” Alibainisha
Aliendelea kufafanua kuwa, mpaka sasa Baraza linaratibu Jumla ya Mifuko ya Uwezeshaji na Programu 72 ambayo 62 ipo Serikalini na 10 ipo Sekta binafsi, hivyo Lengo kuu la Maonesho haya ni kutoa uelewa wa fursa za Mifuko kwa Wananchi ambapo ilionekana mifuko mingi haifahamiki kwa wananchi hivyo kuchelewesha kufikisha huduma za uwezeshaji kwa wananchi.
Maonesho
hayo ya siku Saba yaliyofunguliwa leo Mkoani Singida yana Kaulimbiu inayosema “Shiriki
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Unufaike na Fursa za Uwezeshaji”
Monday, September 2, 2024
INEC, VYAMA VYA SIASA KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amesema, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushauriana na vyama vyote vya siasa itaandaa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024.
Mhe. Nderiananga ameyasema hayo leo katika Mkutano wa 16 Kikao cha Tano, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Neema Lugangira ambapo alitaka kufahamu ni lini kanuni za maadili ya uchaguzi zitakuwa tayari baada ya makosa ya ukatili wa Kijinsia kuongezwa kwenye Sheria za Uchaguzi mwezi Februari, 2024.
“Kwa mujibu wa Kifungu cha 162 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024 kinaeleza kuwa, Tume baada ya kushauriana na vyama vyote vya Siasa itaandaa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi; aidha, kwa kuzingatia masharti ya kanuni ya 1.2 ya Kanuni za Maadili ya Uchaguzi za mwaka 2020, maadili ya Uchaguzi yatatumika katika Uchaguzi Mkuu na katika chaguzi ndogo,” alifafanua Mhe. Nderiananga.
Aidha, Naibu Waziri huyo alieleza kwamba, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushauriana na vyama vyote vya siasa itaandaa Kanuni hizo kwa kuwa maadili mpya ya uchaguzi huandaliwa katika kila mwaka wa uchaguzi Mkuu.
MITANDAO YA KIJAMII
Popular Posts
-
Na. OWM, Dodoma. Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, imefanya ukaguzi wa utekelezaji wa sheria Na.5 y...
-
Wataalamu wa Afya moja wakiwa katikapicha ya pamoja wakati wa mkutano wa wataalamu wa Afya moja uliojikita katika ulinzi na usalama...
-
Na. OWM, ARUSHA Wataalam wa sheria kutoka katika sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wameshauri...
-
Washiriki wa Mkutano wa mwaka wa Wataalamu wa Maabara wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano wa mwaka kwa wataalam wa maabara w...
-
TAMOBA wafanya wasilisho la mfumo maalum wa kielektroniki wa ulinzi na usalama wa Bodaboda na BajajiKampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaj Association (TAMOBA) imefanya wasilisho maaluum kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mfumo maalum wa ...