Wednesday, March 21, 2018

WAZIRI MKUU AMUWAKILISHA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI KATIKA MKUTANO WA AU-RWANDA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais John  Pombe Magufuli leo 21/03/2018 akisaini mkataba wa makubaliano ya kulifanya Bara la Afrika kuwa eneo  hururu la Biashara . Utiaji saini huo umefanyika Jijini Kigali Rwanda

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa .kwaniaba ya Raisi John  Pombe Magufuli leo 21/03/2018 akisaini mkataba wa makubaliano ya kulifanya Bara la Afrika Kuwa eneo  hururu la Biashara . Utiaji saini huo umefanyika Jijini Kigali Rwanda

Read More

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu Bi. Maimuna Tarishi ameongoza Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo na kuwaasa wajumbe wa baraza kutoa maoni yatakayosaidia kufanikisha mchakato wa maandalizi ya Bajeti ya mwaka 2018/2019.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao hicho Tarishi amesema kuwa Watumishi wote katika Ofisi hiyo wanao wajibu wakushiriki kikamilifu katika mchakato wa maandalizi ya bajeti ili kufanikisha azma ya Serikali kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

“Bila kujali nafasi zenu ni lazima mtambue kuwa mnao wajibu sawa katika kutoa maoni yatakayosaidia katika mchakato wa maandalizi ya bajeti” alisisitiza Bi.  Tarishi.

Akifafanua Tarishi amesema kuwa Ofisi yake imekuwa ikizingatia maoni ya wajumbe wa baraza hilo katika maandalizi ya bajeti hivyo ni wakati mwingine tena kwa watumishi hao kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu katika kikao cha baraza hilo kwa kutoa mchango utakaosaidia katika utendaji wa Ofisi hasa katika kipindi hiki cha maandalizi ya bajeti.

Aliongeza kuwa Baraza hilo linafanyika ikiwa ni utekelzaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanayotaka Ofisi zote za Serikali kuwapa  nafasi watumishi wake kutoa maoni yao kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo bajeti kupitia kwenye baraza la Wafanyakazi hali inayochochea maendeleo na tija katika utoaji wa huduma.

Naye Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma Bw. John Mchenya alieleza kuwa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wanapaswa kuwa kielelezo katika uwajibikaji na utekelezaji wa majukumu yao ili kuwa mfano wa kuigwa hususan katika kukilinda na kuhakikisha uhai wa chama cha Wafanyakazi kwa kutenda haki kwa mujibu wa sheria zilizopo.

“Ni vyema kila mmoja wenu akawa wakili mzuri katika utendaji kuzingatia Ofisi hii ndiyo mtendaji Mkuu wa Shughuli za Serikali bila kuacha kuzingazita uwepo wa TUGHE kwa kuwa ipo kwa mujibu wa Sheria namba 6 inayoeleza masuala ya ajira na usajiri wa vyama vya Wafanyakazi”.Alisema Bw.Mchenya

Kwa upande wake mmoja wa wajumbe wa Baraza hilo Bw.Yona Mwakilembe  amesema kuwa  maoni ya watumishi katika Ofisi hiyo yamekuwa yakizingatiwa kwa ukamilifu  hali inayoongeza morali kwa watumishi wa Ofisi hiyo.

“Tangu nimehamia hapa nimeshuhudia kwa kiwango kikubwa kwamba maoni tunayotoa kupitia baraza la wafanyakazi yanazingatiwa hivyo ni jambo la kujivunia na tunapongeza kwa hatua hii” Alisisitiza

Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu linafanyika mjini Dodoma leo Machi 21, 2018 ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa uliowekwa na Serikali kupitia Wizara,  Mikoa,  Wilaya, Idara, Wakala, Taasisi na Mashirika ya Umma kuwapa nafasi watumishi kutoa maoni yao kupitia baraza la wafanyakazi ili kuongeza tija na uwajibikaji katika Taasisi husika.
Read More

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akimsikiliza Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Ofisi hiyo Bw.Packshard Mkongwa mara baada ya kufunga kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi hiyo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi (katikati) akisisitiza jambo wakati akifungua Kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu lililofanyika tarehe 21Machi, 2018 mjini Dodoma.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano pamoja na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Ofisi hiyo leo mjini Dodoma kabla ya kufungua Kikao hicho.


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi  wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano  leo mjini Dodoma kabla ya kufunguliwa  kwa Kikao  cha baraza hilo .


Katibu wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Waziri Mkuu Bi.Flora Bilauri akifafanua jambo wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akifurahia jambo na Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma Bw. John Mchenya mara baada ya kufungua kikao cha Baraza hilo mjini Dodoma.


Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Ernajoyce Hallo akiuliza swali wakati wa mkutano wa baraza hilo lililofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu)Bi. Maimuna Tarishi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Ofisi hiyo  leo mjini Dodoma  baada  ya kufungua Kikao hicho

Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Packshard Mkongwa akiwasilisha mada ya Bajeti ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2018/19 wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi hiyo


Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Alex Ndimbo akiuliza swali wakati wa mkutano wa baraza hilo lililofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.

Read More

Tuesday, March 20, 2018

SERIKALI YATEKELEZA MAOMBI 5 YA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO WILAYANI LONGIDO

Baadhi ya mifugo wakiwa katika eneo la kunywa maji kablaya kuuzwa katika Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido amablo limejengwa kwa  ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF)

Sehemu ya kunyweshea mifugo iliyojengwa katika ​​Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido kwa ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).

Muonekano wa Soko la Kimkakati la Longido,  Wilayani Longido baada ya kupata nishati ya mwanga kwa ufadhili wa  Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
Serikali kupitia, Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), imetekeleza maombi 5 ambayo yanawasaidia wafugaji hao  kuongeza thamani ya mifugo yao  kupitia Soko la Kimkakati la mifugo Longido lililojengwa na Program hiyo.
Mwishoni mwa mwaka 2017, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  (Sera, Bunge, Ajira ,Kazi,  Vijana na Watu wenye Ulemavu ) Mhe.Jenista Mhagama, alikuwa na ziara ya kukagua  ujenzi wa soko hilo wilayani humo, ambapo  baada ya ukaguzi alikutana na wafanyabiashara ya mifugo, ambao  waliwasilisha maombi  5,  ambayo yangeweza kuongeza Thamani Biashara za Mifugo na kutatua  kero zote  za wafanyabiashara wa mifugo wilayani humo.
“Serikali ya awamu ya tano imeamua kuwasikiliza watu wanyonge na ambao wanajituma kuchapa kazi, lakini pia lengo la Program ya MIVARF ni kuongeza kipato kwa  wananchi hasa waishio vijijini, kwa mantiki hiyo nilimuelekeza Mratibu wa Program Kutekeleza maombi yao haraka sana ili wafugaji hawa wapate tija ya ufugaji kupitia soko hili”alisema Mhagama
Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Mifugo wilayani Longido, Saruni Laizer amesema maombi waliyowasilisha serikalini ili waweze kupata tija ya mifugo kupitia soko la Kimkakati la Mifugo Longido yamefanyiwa kazi na Program ya MIVARF ndani ya miezi mitatu tangu wayasilishe, ikiwa ni; Mizani ya kupima mifugo, Maji ya kunyweshea mifugo, machinjio, Josho, pamoja na  umeme.
“Tulihitaji maji hapa ili mifugo isije ikafa wakati inasubiri kuuzwa kwa kukosa maji, lakini umeme hapa ni muhimu kwani biashara zetu zinafanyika usiku, tayari hadi jenereta imeletwa kwa ajili ya kuhakikisha biashara haikwami kwa dharura yoyote ile, lakini mizani itasaidia kutowauza mifugo kwa kuangalia kwa macho bali kwa uzito wao” alisema Laizer
Mhagama alitoa maagizo hayo baada ya kukagua  Soko la kimkakati lililojengwa na Serikali kupitia Ofisi Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).
Soko hilo litawanufaisha wananchi wapatao 14,2000  wa wilayani Longido ambapo asilimia 95 ni wafugaji na wanaojishughulisha na biashara za mifugo.
Soko  hilo la kimkakati ambalo halijafunguliwa rasmi , tayari halmashauri ya wilaya hiyo imeweza kukusanya mapato ya kiasi cha shilingi milioni 106 kwa mwaka  2016/2017 ambapo kwa makusanyo hayo yamewezesha halmashauri hiyo kuvunja rekodi ya miaka kumi iliyopita kwa kukusanya shilingi bilioni 1.3 kwa mara ya kwanza  kwani awali mapato yake yalikuwa chini ya bilioni moja.
MIVARF;  ni Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko na Huduma za Kifedha Vijijini  iliyobuniwa  na serikali ya Tanzania  kwa  kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo yaani (IFAD) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB).   Programu hii inatekelezwa  katika mikoa 29 ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani  tangu mwaka 2011.

Read More

WAZIRI MKUU AMKABIDHI MSAADA BIBI TACLA HAMIDU (MLEMAVU)

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemkabidhi Bibi Tecla Hamidu ambaye ni mlemavu wa miguu sh. milioni tano ili aweze kuongezea katika mtaji wake. Ametoa fedha hizo leo (Jumanne, Machi 20, 2018) ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake aliyoitoa Februari 22, 2018 kwenye Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemkabidhi Bibi Tecla Hamidu ambaye ni mlemavu wa miguu sh. milioni tano ili aweze kuongezea katika mtaji wake.Ametoa fedha hizo leo (Jumanne, Machi 20, 2018) ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake aliyoitoa Februari 22, 2018 kwenye Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes).


Read More