Wednesday, July 30, 2025

SERIKALI KUWEKEZA KATIKA UVUVI WA BAHARI KUU

Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Paul Sangawe ameongoza Kikao cha Kamati ya Wataalamu kuhusu matokeo ya tathmini ya kazi ya tafiti juu ya kampuni zenye uwezo wa kujenga Meli kwa ajili ya Uvuvi katika Bahari Kuu.

Katika Kikao hicho, Bw. Sangawe alilisitiza juu ya utekelezaji wa maelekezo ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi kilichofanyika kabla ya kikao cha wataalam. Masuala yaliyosisitizwa ni pamoja na upatikanaji kampuni yenye uwezo wa kujenga Meli ya Uvuvi wa Bahari Kuu kwa viwango vinavyohitajika, na kupata meli hizo kwa wakati ili kuchochea uvuvi wa kisasa nchini.

Vikao hivyo vya Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi ( AFDP) vimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Bluu, Zanziba




 

Read More

Monday, July 28, 2025

JITIHADA ZA PAMOJA ZINAHITAJIKA KUPAMBANA NA UDUMAVU – DKT. YONAZI


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, ametoa wito kwa Serikali na wadau kushirikiana kwa karibu katika mapambano dhidi ya tatizo la udumavu nchini.

Akizungumza katika kikao cha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa Wadau wa Lishe nchini, kinachotarajiwa kufanyika Septemba 4–5, 2025 jijini Dar es Salaam, Dkt. Yonazi amesema juhudi za pamoja, tafiti, elimu na majukwaa ya kitaifa ni muhimu katika kutokomeza udumavu.

“Tunahitaji nguvu ya pamoja kati ya Serikali na wadau kuhakikisha tunapunguza kwa kiasi kikubwa viwango vya udumavu kupitia sera, elimu na programu zenye tija,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Germana Leyna, amesema mkutano wa mwaka huu utaambatana na Lishe Marathon, yenye lengo la kuhamasisha afya bora kwa jamii na kuongeza uelewa wa masuala ya lishe.

Mkutano huo wa kitaifa unatarajiwa kufunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.



Read More

Wednesday, July 23, 2025

KAMATI YA MAKATIBU WAKUU YARIDHISHWA NA UJENZI WA UWANJA MPYA WA MPIRA JIJINI ARUSHA

 


Kamati ya Makatibu Wakuu inayoongozwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, imekagua na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa wa mpira wa miguu katika eneo la Olmoti, jijini Arusha. Uwanja huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano ya AFCON 2027.

Dkt. Yonazi amesema maendeleo ya mradi huo ni ya kuridhisha na uwanja huo utakuwa si tu kituo cha michezo, bali pia kivutio cha utalii na maendeleo ya uchumi kwa wakazi wa Arusha.

“Tunaamini uwanja huu utakuwa fursa kwa wananchi kuwekeza kibiashara. Ujenzi huu unapaswa kutazamwa kama chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya michezo.

Naye Rais wa TFF, Wallace Karia, amesema uwanja huo utaongeza idadi ya matukio ya kimataifa nchini, Kutakuza vipaji vya ndani, na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia michezo.

Ujenzi wa uwanja huo ni sehemu ya maandalizi ya Tanzania kuandaa mashindano ya AFCON 2027, kwa ushirikiano na Kenya na Uganda



Read More

WAZIRI LUKUVI AWAPONGEZA MALIASILI KWA KUTEKELEZA MAONO YA MHE. RAIS SAMIA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kutekeleza kikamilifu maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa Wizara ya kwanza kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi na kuwezesha Idara na Vitengo vyake kuhamia Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.

Waziri Likuvi ametoa pongezi hizo leo alipotembelea Wizara hiyo kwa lengo la kukagua ujenzi wa Majengo ya Serikali ambao ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu ya Serikali kuhamia Dodoma.

Mhe. Lukuvi amesema kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii licha ya kukamilisha mapema ujenzi wa jengo hilo, inastahili pia kupongezwa kuwa wa kwanza kuhamia na kuwa mfano katika Matumizi ya samani za Ofisini zilizozalishwa hapa nchini kupitia mazao ya Misitu.

"Ninyi ni mabalozi wazuri wa Matumizi ya bidhaa zetu za hapa nchini zinazotokana na Misitu yetu, niimani yangu kuwa Wizara zote zitaiga mfano huu". Aliongeza Mhe. Lukuvi

Aidha Mhe. Lukuvi ametoa rai kwa watumishi wa Wizara hiyo kuhakikisha wanatunza vyema miundombinu na vifaa vilivyopo ili viweze kudumu kama ilivyo kusudiwa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi amemshukuru Waziri Lukuvi kwa ziara yake, na kuahidi kuwa Wizara itatekeleza vyema maelekezo aliyoyatoa hususani ya usimamizi mzuri wa Matumizi ya jengo na vifaa vilivyopo.



Read More

Tuesday, July 22, 2025

MIUNDOMBINU YA MICHEZO ZANZIBAR YAVUKA KIWANGO CHA KIMATAIFA KUELEKEA CHAN

Serikali imeridhishwa na maandalizi ya miundombinu ya michezo Zanzibar kuelekea Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), huku Uwanja wa Amaan Complex ukitajwa kuwa katika viwango vya kimataifa.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, mara baada ya kuongoza Kamati ya Makatibu Wakuu kukagua maandalizi ya CHAN katika visiwa vya Zanzibar.

 “Tumejionea hali halisi ya miundombinu, hasa Uwanja wa Amaan. Uko katika viwango vya kimataifa, na tunaamini Zanzibar ipo tayari kuwa sehemu ya mashindano haya muhimu kwa bara letu la Afrika,” amesema Dkt. Yonazi.

Aidha, Dkt. Yonazi alieleza kuwa hatua hiyo inaonesha utayari wa Taifa kuandaa mashindano ya kimataifa, huku akisisitiza kuwa mashindano ya CHAN ni fursa kubwa ya kuimarisha michezo na kukuza uchumi wa ndani.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (SMZ), Mhe. Fatma Hamad Rajab, alieleza kuwa Uwanja wa Aman Complex tayari umekidhi vigezo vyote vinavyohitajika na Zanzibar iko tayari kuwapokea wachezaji, mashabiki na wageni kutoka mataifa mbalimbali.

Kamati hiyo ya Makatibu Wakuu inafanya ziara katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Visiwani ili kukagua maandalizi ya CHAN na AFCON 2027. 

Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe 2 Agosti 2025 yakihusisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika.

 


Read More

Monday, July 21, 2025

TANZANIA YATANGAZA UTAYARI WA KUANDAA MASHINDANO YA CHAN


 Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, amesema kuwa Tanzania ipo tayari kwa ajili ya kuandaa Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), yatakayoanza rasmi Agosti 2, 2025.

Akizungumza mara baada ya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya michezo jijini Dar es Salaam, Dkt. Yonazi alisema maandalizi yamefikia hatua nzuri na viwanja viko tayari kwa mashindano hayo makubwa.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Makatibu Wakuu ya CHAN na AFCON, Dkt. Yonazi alitembelea viwanja vya Benjamin Mkapa, Isamuhyo, Shule ya Sheria na Gymkhana, akisisitiza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha miundombinu yote inakidhi viwango vya kimataifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Gerson Msigwa, ametoa wito kwa Watanzania kuonesha uzalendo kwa kujitokeza kwa wingi viwanjani kuishangilia Taifa Stars.

 

#CHAN2025 #TaifaStars #TanzaniaYapoTayari



Read More

Friday, July 18, 2025

DKT. YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kwa maendeleo ya Taifa.

Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo Ofisini kwake jijini Dodoma akikabidhiwa tuzo na Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Conrad Milinga iliyotolewa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati akifungua Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu kupokea tuzo kumeongeza motisha katika ushiriki wa maonesho yajayo makubwa ya Kimataifa ya Sabasaba na kutambua mchango wa Ofisi hiyo iliyoutoa kwa wananchi katika kipindi chote cha maonesho hayo na kutambua huduma ianayotolewa kwa wananchi.

“Ofisi ya Waziri Mkuu imefurahi sana kupokea tuzo hii kama ishara ya kutambua ushiriki wetu na mchango ambao Ofisi yetu inatoa kwa wananchi hivyo tunaamini ushiriki wetu unaofuata utakuwa wa viwango vya juu sana,” Alisema Dkt. Yonazi.

Pia aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazofanya chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambayo ndio mratibu wa Maonesho kwa  kuhakikisha maonesho hayo yanaleta tija na mageuzi makubwa katika sekta ya kiuchumi kwa wananchi na Kimataifa.

“Tunazishukuru sana Taasisi mbalimbali ambazo tumeshirikiana nazo na viongozi ambao wameendelea kutupa maelekezo yaliyowezesha kufanya vizuri katika maonesho hayo na tunaamini kwamba tutaendelea kuwa washindi au hata washindi wa jumla,”Alishukuru.

Ikumbukwe Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025 yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi tarehe 07 Julai, 2025 na kufungwa na Waziri Mkuu Mhe.  Kassim Majaliwa katika viwanja vya maonesho Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 13, 2025.



Read More

"KILA SEKTA IJIANDAE KUPOKEA WAGENI KUELEKEA CHAN", DKT. YONAZI

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amezitaka sekta zote kujianda kupokea wageni mbalimbali kuelekea Mashindano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) yanatayorajiwa kuanza Mwanzoni mwa mwezi wa Agosti 2025.

Dkt. Yonazi ametoa rai hiyo wakati akiongoza Kikao cha Makatibu Wakuu cha Tathmini ya Maandalizi ya CHAN na AFCON kilichofanyika  leo katika Ukumbi wa Ofisi  ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

Aidha, ameeleza kuwa jukumu la Serikali ni kuleta fursa na kuweka miundombinu ili kila sekta inufaike na ugeni huu mkubwa na kusisitiza hii ni fursa ya kutuamsha katika kuandaa matukio makubwa.

Pia, Dkt. Yonazi amesisitiza umuhimu wa kutoa hamasa kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kila mtanzania aamasike na kushiriki katika mashindano haya ya CHAN.

Ikumbukwe Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kutimua vumbi kuanzia Agosti 2, 2025 ambapo timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itachuana na Timu ya Taifa ya Burkina Faso katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.



Read More

Wednesday, July 16, 2025

WAZIRI LUKUVI ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA 2025


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. William Lukuvi amefanya ukaguzi wa maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Mtumba – Dodoma.

Maadhimisho hayo yatapambwa na gwaride kutoka majeshi matano ya ulinzi na usalama na mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Katika ziara hiyo, Waziri Lukuvi aliambatana na viongozi waandamizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na maafisa kutoka JWTZ na Jeshi la Polisi.

Maandalizi yameelezwa kuendelea vizuri, huku tukio hilo likitarajiwa kuwa la kitaifa na kihistoria katika kutoa heshima kwa mashujaa wa Tanzania.




Read More

SERIKALI YAZINDUA MAFUNZO YA MTANDAO YA AFYA MOJA (ECHO)

 


SERIKALI imeanzisha mafunzo kwa njia ya mtandao ya Afya moja (ECHO) ili kuwajengea uwezo watoa huduma wa kada za afya ya binadamu, wanyama na mazingira kwa ngazi zote.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Dk.Jim Yonazi wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo tarehe 15 Julai, 2025 katika Kituo cha kurushia Mafunzo kwa njia ya mtandao (ECHO HUB) kilichopo katika jengo la Idara ya Utafiti na Mafunzo Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Amesema Serikali inaendelea kukabiliana na majanga na dharula zenye athari kwa afya ya binadamu, wanyama na mazingira hivyo imeona umuhimu wa kuwezesha wataalamu wake kuelewa kwa kina dhana ya Afya Moja.

“Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta na mradi wa USAID Usalama wa Afya Duniani unaotekelezwa na Shirika la CIHEB Tanzania, imeanzisha mafunzo ya mtandao ya Afya moja (ECHO) ili kujenga uwezo kwa watoa huduma wa kada za afya ya binadamu, wanyama na mazingira kwa ngazi zote,”amesema Dkt. Yonazi.

Aliongeza kuwa; “Naomba niwahamasishe viongozi na watumishi kutoka sekta mbalimbali kushiriki katika vipindi hivi. Wataalamu wabobezi watawasilisha mada mbalimbali zitakazojenga uwezo wetu katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kwa binadamu na wanyama, visumbufu vya mazao, usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, usalama wa chakula.

Awali akieleza lengo la uzinduzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Brigedia Generali Hosea Ndagala amesema,Mafunzo haya yanayolenga katika kuongeza ufanisi kwa wataalam katika kushughulikia magonjwa ya kizoonotiki, usugu wa vimelea dhidi ya dawa (AMR), hatari za kibailojia, usalama wa chakula na magonjwa yasiyoambukizwa ambayo ni maeneo muhimu yenye changamoto na yanapewa kipaumbele katika Sekta ya Afya nchini Tanzania.

 

Alifafanua kuwa, Mafunzo haya yatawahusu wataalamu wa Sekta ya Afya moja, Afya, mazingira, mifuko na uvuvi.

 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Afya na Lishe Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bi. Suzanne Nchalla  amesema mpango huo utasaidia watoa huduma ngazi ya msingi kupata uelewa wa Dhana ya Afya Moja na wakati wa utoaji huduma.

Amesema OR- TAMISEMI itashirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika kuhakikisha watumishi wa afya ya msingi wanashiriki kikamilifu katika mafunzo hayo.

“Tutawasimamia na kuwakumbusha viongozi wa Halmashauri kuhakikisha wanashiriki vipindi vilivyopangwa ili kupata matokeo chanya na kutimiza azma la mpango huu,”amesema Bi.Suzanne.

Naye Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Serikali Dkt.Otilia Gowelle alisema Wizara ya Afya inatambua umuhimu wa mashirikiano ya wadau na sekta mbalimbali katika kujiandaa pamoja na kukabiliana na matishio ya mara kwa mara ya magonjwa ya mlipuko pamoja na matukio yenye athari kwa afya ya binadamu.

“Kwa kuzingatia umuhimu wa mafunzo haya, Wizara imekwisha fanya uhamasishaji na itaendelea kuhakikisha wataalam wengi zaidi wanashiriki mafunzo haya wakiwemo wauguzi, madaktari, wafamasia, maafisa afya, wataalam wa maabara na wengineo waliopo katika vituo vya kutolea huduma na maeneo mengine mahsusi” alisisitiza Dkt. Gowelle.

Aliongezea kuwa Wizara ya Afya imekuwa mshiriki na mnufaika mkuu wa ushirikiano uliopo kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kila inapohitajika.



Read More

Friday, July 11, 2025

KITUO CHA DHARURA CHA SERIKALI CHAWA KIVUTIO AFRIKA KWA KUKINGA MAAFA



Uwekezaji wa Serikali ya Tanzania katika kuimarisha mifumo ya kukabiliana na majanga kupitia Kituo cha Ufuatiliaji wa Majanga na Tahadhari ya Mapema (Situation Room) umeanza kuzaa matunda, baada ya nchi mbalimbali za Afrika kuonesha kuvutiwa na namna kituo hicho kinavyofanya kazi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso yanayofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, alisema kituo hicho kimeongeza uwezo wa nchi kuchakata taarifa za viashiria vya majanga na kutoa taarifa za viashiria vya majanga na kutoa tahadhari mapema kwa wananchi.

“Uendeshaji wa kituo hiki unahusisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali wanaoshirikiana kuchakata taarifa kwa pamoja, jambo linalosaidia kutoa tahadhari kwa wakati,” alisema Brigedia Jenerali Ndagala.

Mkurugenzi Msaidizi wa kituo hicho, Bi. Jane Kikunya, alisema wageni kutoka nchi hizo tatu wameonesha kuvutiwa na mfumo wa ufuatiliaji wa majanga unaohusisha hadi ngazi za vijiji, na wamepanga kuiga mfumo huo katika nchi zao ili kuimarisha usimamizi wa maafa.

 “Wameonesha nia ya kuitumia mifumo waliyojifunza hapa kwenye nchi zao. Hili ni jambo kubwa kwa ushirikiano wa kikanda,” alieleza Kikunya.

Katika mafunzo hayo, washiriki walielezwa namna kituo hicho kinavyokusanya taarifa kutoka sekta mbalimbali kama hali ya hewa, maji, kilimo, na kijamii, kisha kuzichambua na kutoa taarifa rasmi kwa vyombo husika na kwa wananchi.

Miongoni mwa wageni, Simboou Akleso kutoka Togo alisema:  “Tumekuja Tanzania kubadilishana uzoefu kwa sababu mnafanya vizuri. Tumeshuhudia kwa macho namna taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuwasilishwa kwa wananchi.”




 

Read More

Thursday, July 10, 2025

UJENZI WA UWANJA MPYA ARUSHA WAFIKIA ASILIMIA 51

Mkurugenzi wa Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bw. Paul T. Sangawe, amefanya ziara ya ukaguzi katika uwanja wa mpira unaojengwa mkoani Arusha, ambapo ametoa wito kwa wananchi kuelimishwa kuhusu maendeleo ya mradi huo pamoja na fursa zinazotokana nao.

Akiwa katika eneo la mradi, Bw. Sangawe alipokea taarifa rasmi ya utekelezaji wa ujenzi huo, ambao kwa sasa umefikia asilimia 51 ya kazi zote, kiwango kinachozidi malengo ya mpango kazi wa asilimia 50 kwa kipindi hiki. 

Ziara hiyo ilifanyika Mkoa wa Arusha, ambapo mradi huo unatekelezwa kama sehemu ya miradi inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Taarifa ya maendeleo ya mradi ilitolewa na msimamizi wa mradi, Bw. Ruta Chakupewa, ambaye alieleza hatua zilizofikiwa na kazi zinazoendelea.

Mradi huu, unaotarajiwa kumalizika kwa wakati, unalenga kuongeza miundombinu ya michezo nchini na unatarajiwa kuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000. Kazi zinazoendelea ni pamoja na Ukamilishaji wa majukwaa, Ujenzi wa vyumba mbalimbali katika sakafu ya chini, Ufungaji wa miundombinu ya umeme, zimamoto, na TEHAMA 

Bw. Sangawe alisisitiza umuhimu wa kuwaeleza wananchi juu ya kazi zinazoendelea na kuhamasisha uelewa juu ya fursa za kiuchumi, ajira, na maendeleo ya Jamii zinazotokana na miradi kama hiyo

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha uwazi na ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati kwa manufaa ya Watanzania.





Read More

DKT. YONAZI AONGOZA KIKAO CHA TANZANIA NATIONAL COORDINATING MECHANISM (TNCM).


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chombo kinachosimamia utekelezaji wa Programu zinazofadhiliwa na Mfuko wa Dunia (Tanzania National Coordinating Mechanism - TNCM) Dkt. Jim Yonazi ameongoza kikao cha wajumbe wa chombo hicho kwa ajili ya kupitisha Maboresho ya Bajeti ya Utekelezaji wa Programu za Malaria, Kifua Kikuu, UKIMWI ambayo ni mzunguko wa saba (GC7) kwa mwaka 2024 hadi 2026.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 10 Julai, 2025 katika Jengo la Tume ya Ushindani Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Medical Stores Department (MSD), Local Fund Agent (LFA), Sekretarieti ya TNCM, Asasi za Kiraia (Non State Actors - NSAs), Mashirika ya Kimataifa (WHO, UNAIDS), Wadau wa Maendeleo (US Government, British High Commission pamoja na wawakilishi kutoka Mfuko wa Dunia).


 

Read More

DKT. KILABUKO: USHIRIKIANO WA KIKANDA MUHIMU KUKABILI MAAFA YA KIBINADAMU

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko amehimiza ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na majanga ya kibinadamu yanayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa, kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kuimarisha vituo vya ufuatiliaji wa majanga na tahadhari ya mapema (Situation Room).

Akizungumza leo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum ya kubadilishana uzoefu, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na UNDRR na Kituo cha Sayansi cha Afrika Magharibi kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (WASCAL), Dkt. Kilabuko alisema mafunzo hayo ni sehemu ya kuimarisha uwezo wa kanda katika kukabili matukio ya majanga. Mafunzo hayo yalihusisha ujumbe kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso.

Dkt. Kilabuko alieleza kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa majanga, kupitia vituo vyenye uwezo wa kukusanya taarifa mbalimbali, zikiwemo za hali ya hewa, maji, kijamii na kiuchumi, jambo linalosaidia kukabili majanga kama vile ukame na mafuriko.

 “Tunauzoefu mkubwa wa kiutendaji ambao unasaidia kuhakikisha vituo vyetu vinafanya kazi kwa ufanisi kwa kuratibu taasisi mbalimbali kukabiliana na majanga,” alisema Dkt. Kilabuko.



 

Read More

Wednesday, July 9, 2025

MAMA JANETH MAGUFULI ATEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA

Mke wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, Mama Janeth Magufuli ametembelea banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (SABASABA) Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi wa ofisi hiyo.

Akiwa katika banda hilo, Mama Janeth alipokelewa na kutembelea kuona namna Ofisi ya Waziri Mkuu inavyohudumia wananchi kupitia Idara, Vitengo pamoja na Taasisi zake.

Aidha, miongoni mwa huduma zinazotolewa na ofisi hiyo ni pamoja na elimu ya masuala ya menejimenti ya maafa, shughuli za Wakala wa Kupigachapa Mkuu wa Serikali, Baraza la Taifa la Biashara, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, elimu ya masuala ya Vyama vya Siasa Nchini, Masuala ya VVU na UKIMWI, Usalama na Afya Mahala Pa Kazi, Masuala ya Watu Wenye Ulemavu, programu ya ASDP II, fursa za vijana pamoja na huduma zinazotolewa na  NSSF, PSSSF, WCF na CMA.

 

Read More

Tuesday, July 1, 2025

DKT. YONAZI ATOA WITO KWA WATUMISHI KUJENGA TABIA YA KUJIFUNZA ILI KUIMARISHA UWAJIBIKAJI SERIKALINI

 


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, amewataka watumishi wa umma kujenga tabia ya kujifunza kwa bidii ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu ya serikali.

Dkt. Yonazi ametoa wito huo leo jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa PEPMIS yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Ngome.

Akihimiza dhana ya kujifunza kwa kushiriki kikamilifu, Dkt. Yonazi alinukuu kauli maarufu ya Benjamin Franklin isemayo: “Niambie nisahau, nifundishe nitakumbuka, nishirikishe nijifunze.” 

Alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa kila mmoja akisema: “Tuchukue sehemu ya tatu ya kauli hiyo kwa sababu tunachohitaji ni kujihusisha ili tuweze kujifunza zaidi na kuimarisha utendaji wetu.”

Aidha, Dkt. Yonazi aliwataka watendaji wote kuchangamkia fursa hiyo ya mafunzo ya PEPMIS ili kupata maarifa mapya yatakayosaidia katika kutathmini na kuboresha utendaji kazi wao wa kila siku.

Kwa upande wake, Bw. Mutani Josephat Manyama – Mkufunzi wa Kitaifa wa Mfumo huo kutoka Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), alieleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa kuwajengea uwezo watumishi wa umma kuhusu utekelezaji na tathmini ya utendaji kazi wao.

Aliongeza kuwa mafunzo hayo yatawawezesha viongozi na wasimamizi kufanya tathmini sahihi ya watendaji, jambo litakalosaidia maamuzi bora ya kiutumishi na kuongeza tija katika utumishi wa umma.



Read More

Thursday, June 26, 2025

WAZIRI LUKUVI AITAKA BODI YA ATF KUFIKIA MALENGO KUTOKOMEZA UKIMWI 2030


 

Serikali inategemea Bodi ya Mpya ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI italeta fikra mpya, mbinu mpya, na weledi wa hali ya juu ili kuhakikisha Mfuko huo unakuwa chombo madhubuti cha kuhakikisha Tanzania inafikia malengo yake ya kutokomeza UKIMWI ifikapo Mwaka 2030.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi (MB) wakati akizinduza Bodi ya Tatu ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund - ATF) jijini Dodoma.

 Waziri Lukuvi ameeleza kuwa, Bodi hiyo inapaswa kutambua kuwa dunia ipo katika hatua mpya na muhimu ya kimkakati katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambapo Tanzania kama sehemu ya jumuiya ya kimataifa imesaini na inatekeleza ahadi na makubaliano mbalimbali ya kimataifa na kikanda.

 “Tumejidhatiti kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs 2030), hasa lengo la tatu linalohusu kuhakikisha afya njema na ustawi kwa wote, vilevile, tunaitekeleza kwa dhati Ajenda ya Umoja wa Afrika ya 2063, pamoja na Azimio la Kisiasa la Umoja wa Mataifa la mwaka 2021 kuhusu UKIMWI” amefafanua Waziri Lukuvi.

Aidha, Mhe Lukuvi ameitaka Bodi hiyo kutambua kwamba kwa sasa dunia inashuhudia mabadiliko makubwa katika namna ya kufadhili mapambano dhidi ya UKIMWI.

 “Wahisani wakuu wa Kimataifa kama PEPFAR na Global Fund wameshaanza kupunguza kwa awamu michango yao huku wakisisitiza umuhimu wa nchi kuchukua umiliki wa ndani na kuhakikisha uendelevu wa kifedha kwa juhudi zake. Mwelekeo huu unatutaka sisi kama Taifa kuongeza uwezo wetu wa ndani wa kifedha ili kuhakikisha mwitikio wa VVU na UKIMWI unaendelea kwa nguvu, kasi, na mafanikio makubwa”.

“Katika muktadha huu, Mfuko wa Udhamini wa UKIMWI (ATF) ni nyenzo muhimu sana katika kuhakikisha Taifa linakuwa na uhakika wa kifedha na usalama wa afya ya wananchi wake” amebainisha Waziri Lukuvi.

 Vilevile ameeleza kuwa, Mfuko huo ni alama ya dhamira ya kweli ya Serikali kuhakikisha kuwa huduma za VVU na UKIMWI zinadumu, hata katika mazingira ambapo michango ya wahisani inapungua.

 “Kupitia Mfuko huu, tunasisitiza umiliki wa kitaifa ambapo Serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia, taasisi za dini, vijana, watu wanaoishi na VVU na jamii kwa ujumla wanashiriki kikamilifu katika juhudi hizi. Mfuko huu pia unaleta msukumo mkubwa wa uwajibikaji wa kisera na kifedha kwa kuhakikisha matumizi ya fedha yanazingatia uwazi na matokeo yanayoonekana” ameongeza.

 Akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Dkt. James Kilabuko kwa niaba ya Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Dkt. Jim Yonazi amesema kuwa, “mfuko huu ni jitihada za kujenga misingi imara ya uendelevu wa kifedha wa mapambano dhidi ya UKIMWI ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakitegemea zaidi wahisani kutoka nje, tukio hili linaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita  ya kuhakikisha kuwa uendelevu wa mwitikio wa UKIMWI unajengeka kwa msingi wa uhimilivu wa ndani na ushirikiano mpana wa wadau wote wa maendeleo yaa taifa letu”.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw. Sabasaba Mushingi amemshukuru Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumuamini na kumchagua yeye kuwa Mwenyekiti pamoja na wajumbe wake na hivyo kuahidi kuisimamia na kuingoza bodi hiyo ili kuweza kutimiza malengo ya majukumu waliyopewa.



 

 

 

 

Read More

Tuesday, June 24, 2025

MAAMBUKIZI MAPYA VVU YAENDELEA KUSHUKA


 Imeelezwa kwamba takwimu za maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI katika kipindi cha miaka mitano imeendelea kushuka kulingana na matokeo ya utafiti yaliyofanywa hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Catherine Joachim leo Jijini Dodoma wakati akifungua Kikao cha Wakurugenzi wa Sera na Mipango kutoka katika Wizara za Kisekta na Taasisi ili kuangalia mpango  uendelevu wa mwitikio wa UKIMWI.

Dkt. Catherine amebainisha kuwa, nchi imefanya vizuri kwa takwimu za maambukizi mapya zilizotoka mwaka (2023-2024) ambapo maambukizi mapya yalikuwa watu 60000 kwa mwaka ukilinganisha na kipindi cha miaka mitano iliyopita ambapo maambukizi haya yalikuwa watu 72000 kwa mwaka.

“Halikadhalika ukiangalia vifo vitokanavyo na UKIMWI kwa Matokeo ya Utafiti ya Mwaka (2023-2024) watu 24000 walifariki kulinganisha na watu 28000 waliokuwa wamefariki mwaka (2016-2017),” aliongeza Dkt. Catherine.

Ameongeza kusema, ubaguzi na unyanyapaa kwa WAVIU umepungua kutoka 14% hadi kufikia 5%, hatua ambayo ni muhimu kwa sababu inaongeza muitikio wa watu kupima na kujua afya zao.

Aidha, ilikuendelea kuimarisha mapambano, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania imekutana na Wakurugenzi wa Sera na Mipango kutoka katika Wizara za kisekta na Taasisi ili kuangalia mkakati wa  usimamizi na utawala kutoka ngazi ya msingi mpaka ngazi ya Taifa kwa kuangali gharama ya fedha za UKIMWI kulingana na mikakati ya Serikali katika kuongeza fedha za ndani ya Nchi na kutoka kwenye Sekta Binafsi.

 Vilevile, Dkt. Catherine alisema “tutaangalia namna ya kuimarisha utoaji wa huduma na mifumo ya afya na kuongeza uwajibikaji wa wananchi wenyewe katika muitikio”.



 

 

 

 

Read More

Monday, June 23, 2025

ELIMU KUHUSU OWM SERA, BUNGE NA URATIBU KUENDELEA KUTOLEWA

Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Conrad Milinga amesema, maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yamewezesha Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) kutoa elimu juu ya fursa mbalimbali za kiuchumi kupitia mikopo na mifuko ambayo iko katika sekta mbalimbali zinazohusiana na uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Mkurugenzi Milinga ametoa kauli hiyo leo wa kilele cha Maadhimisho Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali park Jijini Dodoma.

Ameeleza, Ofisi ya waziri Mkuu imetumia maadhimisho ya wiki hiyo kueleza wananchi na wadau mbalimbali kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi hiyo ikiwemo Uwezeshaji wananchi kiuchumi, namba ya kujikinga na maafa na Alama za Taifa ambazo ni Wimbo wa Taifa, Ngao ya Taifa na Bendera ya Taifa.

 “Tumeweza kuelimisha wananchi kuhusu mfumo unaotumiwa na Idara ya Menejimenti ya Maafa unaoweza kutambua majanga mapema kabla hayajatokea ili kuwapa wananchi tahadhari ya kujiandaa kabla hayo majanga hayajatokea, tumetoa uelewa kwa wananchi kuweza kufahamu maatumizi sahihi ya Alama za Taifa ikiwemo Ngao sahihi ya Taifa , Beti za wimbo wa Taifa ambapo wimbo huo unatakiwa kuimbwa beti zote mbili na rangi sahihi za Bendera ya Taifa”, amebainisha Bw. Milinga

 Aidha, ameongeza kuwa, Ofisi imeweza kutoa elimu kwa umma kuhusu Idara ya Ufutiliaji na Tathimini ya shughuli za Serikali inavyohusika katika kutoa taarifa za utekelezaji wa miradi mabalimbali inayotekelezwa hapa nchini.

Mbali na hayo, Mkurugenzi Milinga ametoa wito kwa wananchi kujitokeza katika Maonesho ya Kimataifa ya Sababa ambapo Ofisi ya Waziri Mkuu itashiriki maonesho hayo yanayotarajiwa kuanza tarehe 28 Juni, 2025 Jijini Dar Es Salaam.

“Katika maonesho hayo Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na taasisi zetu zote itanatarajia kushiriki hivyo niwasihi wananchi kutembelea maonesho hayo ili kuweza kupata elimu kuhusu shughuli zote zinazofanya na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Madhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yalianza tarehe 16 Juni, 2025 mpaka tarehe 23 Juni, 2025 chini ya kauli mbiu isemayo “Himiza Matumizi ya Mifumo ya Kidigiti ili Kuongeza Upatikanaji wa Taarifa na Kuchagiza Uwajibikaji”



Read More

Saturday, June 21, 2025

SERIKALI YATOA MFUMO WA RAMANI KUONESHA MAENEO YENYE VIASHIRIA VYA MAJANGA

 


Serikali imeandaa mfumo wenye ramani inayoonesha maeneo yenye viashiria vya majanga katika mikoa na maeneo yake ili kuweka mikakati ya kukabiliana nayo yanapotokea.

Hayo yalibainishwa jijini Dar es Salaam jana na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi, katika kikao kilichohusisha Kamati ya Wataalamu ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa kilocholenga kujadili Mfumo wa Ramani ya Majanga; Mwongozo wa Utumiaji wa Ramani ya Viatarishi vya majanga nchini; na Mkakati wa Taifa Ugharamiaji wa viatarishi vya Maafa, pamoja na Mwongozo wa Uhawilishaji Fedha za Misaada ya Kibinadamu. 

Dkt. Yonazi Alisema, Tanzania inaendelea kuweka mikakati mahsusi kuhakikisha kuwa jamii ya Kitanzania inazuia majanga na inajandaa ipasavyo kukabiliana na majanga yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi.

“Serikali imeandaa mfumo mahsusi ambao una ramani mbalimbali zinazoonesha viashiria vya hatari za majanga katika mikoa na maeneo yake. Mfumo huu unasaidia Sekta zote, Mikoa na Halmashauri zote kujipanga na kuweka mikakati ya namna bora ya kukabiliana na vihatarishi vya majanga katika maeneo yao.” Taarifa za vihatarisha katika ramani hiyo, zitasaidia kila mdau katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo mipango ya matumizi wa ardhi.  alisema.

Aliongeza kuwa: “Mfumo huu utatusaidia kujenga uwezo wa kukabiliana na majanga ndani na nje ya nchi.”

Vilevile, Dkt. Yonazi alisema kikao hicho cha Kamati ya Kitaifa kimepitisha miongozo mbalimbali ya kukabiliana na majanga. Aidha, alieleza miongozo iliyopitishwa itatekelezwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kitaifa na kimataifa.

Alieleza kuwa kikao hicho kilihusisha Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa ambao wajumbe wake ni Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi zinazohusika zinazohusika na Usimamizi wa Maafa.

Kwa mujibu wa Dkt. Yonazi, lengo ni kuhakikisha kuwa miongozo ya kukabiliana na majanga inapitiwa na kupelekwa katika sekta zote na kusimamiwa ili iweze kutekelezwa

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na  Uvuvi Profesa. Riziki Shemdoe, alisema  ramani hizo zina mchango mkubwa katika kusaidia sekta ya mifugo na uvuvi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Alibainisha kuwa kupitia matumizi ya ramani hizo, nchi itaweza kupanga kwa ufanisi maeneo ya shughuli za uvuvi na ufugaji kwa kuzingatia maeneo yasiyo na hatari kubwa ya majanga kama ukame, mafuriko au mmomonyoko wa ardhi.

"Ramani hizo zitasaidia kuonesha maeneo yaliyo hatarini kwa mabadiliko ya tabia nchi hivyo kutusaidia katika upangaji wa maeneo kwa ajili ya mifugo, malisho, na miundombinu ya maji.



 

 

 

Read More

Wednesday, June 18, 2025

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA SEKTA YA KILIMO KUPITIA ASDP II

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu, Bw. Omary Ilyas, ameongoza kikao maalum cha Wakurugenzi wa Wizara na Taasisi zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo awamu ya pili (ASDP II).

Kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma kimejadili utekelezaji wa programu hiyo kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, sambamba na kuanza maandalizi ya mpango wa mwaka ujao wa 2025/2026.

Bw. Ilyas amesema ASDP II inalenga kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza tija kwa wakulima na kusaidia ukuaji wa uchumi wa vijijini kupitia ushirikiano wa kisekta.

Kikao kimehusisha wadau kutoka sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, pamoja na taasisi za fedha na maendeleo, ili kuhakikisha utekelezaji wa pamoja unaolenga mafanikio ya mkakati wa Taifa wa kilimo.

Read More

Tuesday, June 17, 2025

DKT. YONAZI AMEONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA TAIFA YA USHAURI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022


 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi (mwenyekiti wa kikao) cha Kamati ya Taifa ya Ushauri ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kilichofanyika tarehe 17 Juni, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere JIjini Dar es Salaam.

 Kikao hicho kimeudhuriwa na Matibu Wakuu wa Wizara za Kisekta, Makamisaa wa Sensa pamoja na baadhi ya wakuu wa Taasisi.Lengo la kikao hicho ni kupokea na kujadili ripoti mbalimbali za utekelezaji wa Awamu ya Tatu na ya Mwisho ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

 Aidha miongoni mwa ripoti hizo ni pamoja na ile ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kwa kipindi cha kuanzia Desemba 2024 hadi Mei 2025, na Hali ya Utekelezaji wa Anwani za Makazi.

 Pia kikao kimejadili na kupokea Rasimu za Ripoti Tano za kina za Matokeo ya Sensa, na Ripoti ya Makadirio ya Idadi ya Watu kuanzia mwaka 2023 hadi 2050 ngazi ya Mikoa.





Read More