Wednesday, April 17, 2019

WAZIRI MKUU ASHIRIKI KWENYE MSIBA WA MTOTO WA MTUMISHI WA OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima ya mwisho kwa mtoto wa Mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Cheka Kaviga, baada ya kufiwa na mtoto wake Samson Cheka,katika kanisa la Mchungaji Mwema Ipagala jijini Dodoma Aprili 17, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Cheka Kaviga, baada ya kufiwa na mtoto wake Samson Cheka,katika kanisa la Mchungaji Mwema Ipagala jijini Dodoma Aprili 17, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima ya mwisho kwa mtoto wa Mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Cheka Kaviga, baada ya kufiwa na mtoto wake Samson Cheka,katika kanisa la Mchungaji Mwema Ipagala jijini Dodoma Aprili 17, 2019. 

Read More

AJALI ZA MAJINI 300 HUTOKEA KILA MWAKA MKOANI MWANZA


Na. OWM, MWANZA.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amebainisha kuwa takribani ajali za majini  zaidi ya mia tatu huripotiwa kuwa zimetokea mkoani humo. Ajali hizo ni zile ambazo huripotiwa rasmi  tu  katika mamlaka husika , aidha inasadikika zipo ajali nyingi ambazo hutokea lakini huwa haziripitiwi  kutokana na jiografia ya mkoa huo. Mkoa wa Mwanza una visiwa zaidi ya 162 ambapo kati ya Visiwa hivyo vipo ambavyo watu wanayo makazi ya kudumu na vingine watu huishi kwa muda mfupi.
Akiongea wakati  akifungua Mafunzo kwa Kamati  ya  Usimamizi wa maafa  ya mkoa huo,  yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughulii za maafa Leo, tarehe 17 Aprili, 2019, jiijini Mwanza, Mongella amefafanua kuwa ajali za vyombo vya usafiri hasa vya majini zinaweza kupunguzwa sana kama wamiliki na waendeshaji wa vyombo hivyo watazingatia sheria na Kanuni  zinazotawala uendeshaji wa vyombo hivyo.
“Suala muhimu la Kuzingatia ni kuhakikisha mamlaka zetu za serikali za mitaa zinaimarisha utawala bora unaotoa nafasi kwa  jamii kushiriki katika kuzuia na Kupunguza madhara ya majanga, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali baada ya maafa kutokea ikiwa ni pamoja na kutoa elimu, taarifa za tahadhari ya awali kwa wakati muafaka na kuandaa rasilimali zinazohiotajika , Ni wajibu wetu kuhakikisha sheria zinasimamiwa kikamilifu ili kuepuka maafa“ alisisitiza Mongella.
Naye Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali, Jimmy Matamwe, ameitaka Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya mkoa huo  kuandaa Mkakati wa Kupunguza madhara  ya maafa pamoja na Mpango wa kujiandaa na kukabili maafa, Aidha, ameeleza kuwa  Ofisi ya waziri Mkuu imeendesha mafunzo hayo  ili kuijengea uwezo kamati hiyo ambayo ni chombo cha kisheria hapa nchini kwa ajili ya kutathimini na kutekeleza masuala ya kitaalam kuhusu usimamizi wa maafa, kuzuia na kupunguza madhara ya majanga ya aina zote katika mkoa.
“Upunguzaji wa madhara ya maafa ni suala mtambuka linalohusika katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii sekta zote. Suala la usimamizi wa maafa linahitaji utashi wa kisiasa na kuwajibika kitaalam, kisheria, uelewa wa umma, elimu ya kisayansi, mipango makini ya maendeleo, ufanisi wa utekelezaji wa sera, mifumo ya tahadhari inayojibu matakwa ya jamii” alisema  Kanali., Matamwe.
Mwaka jana, Mwezi Septemba, mkoa wa Mwanza ulipata maafa makubwa baada ya Kivuko cha MV. Nyerere kuzama na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 200 na wengine 40 waliokolewa. Kufuatia maafa hayo Mkoa huo umeendelea na jitihada za kuzijengea uwezo kamati za Usimamizi wa Maafa za mkoa huo
Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa, yamehudhuriwa na wajumbe wote wa Kamati ya Usimamizi wa maafa kwa kuzingatia Kifungu cha 13 cha sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 7 ya mwaka 2015.
Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri  Mkuu, Jimmy Matamwe akifafanua  umuhimu wa kuwa na Mkakati wa Kupunguza madhara ya maafa, katikati ni Mkuu wa  Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella, kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa huo, Christopher Kadio, wakati wa Mafunzo kwa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Mkoa huo, leo tarehe 17 Aprili, 2019, jijini Mwanza, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu , Idara ya Uratibu Maafa.
Mkuu wa  Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella  akifafanua umuhimu wa kuwa na Kamati za Usimamizi wa Maafa katika ngazi za serikali za mitaa wakati wa Mafunzo kwa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Mkoa huo, leo tarehe 17Aprili, 2019, jijini Mwanza., kulia ni Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri  Mkuu, Jimmy Matamwe, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu , Idara ya Uratibu Maafa.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati  wa Usimamizi wa Maafa ya Mkoa wa Mwanza wakifuatilia mafunzo ya Kuijengea Kamati hiyo uwezo wa Usimamizi wa Maafa , leo tarehe 17Aprili, 2019, jijini Mwanza, Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu , Idara ya Uratibu Maafa.
Mkuu wa  Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella akiwa katika picha ya pamoja na Baadhi ya Wajumbe wa Kamati  wa Usimamizi wa Maafa ya Mkoa wa Mwanza mara baada ya kufungua  mafunzo ya Kuijengea Kamati hiyo uwezo wa Usimamizi wa Maafa , leo tarehe 17Aprili, 2019, jijini Mwanza.Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu , Idara ya Uratibu Maafa.




Read More

Monday, April 15, 2019

MATUKIO KATIKA PICHA OFISI YA WAZIRI MKUU YAHAMIA RASMI MJI WA SERIKALI

Afisa Mipango Miji wa Jiji la Dodoma, Bw. William Alfayo (wa tatu kutoka kulia) akiwaonesha baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waliombatana na Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi (wa pili kutoka kushoto) maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za Balozi katika Mji huo. 
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwaeleza jambo Watumishi wa Ofisi yake kuhusu Miundombinu, huduma na mahitaji mbalimbali yatakayokuwa yanapatikana katika Mji huo wa Serikali uliopo Kata ya Mtumba, Jijini Dodoma. (Kushoto) ni Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe. 
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwa anatekeleza majukumu yake katika Ofisi yake Mpya iliyopo katika Mji wa Serikali Kata ya Mtumba, Jijini Dodoma ikiwa ni kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alilotoa tarehe 13 Aprili, 2019.
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akizungumza na baadhi Wakuu wa Idara na Vitengo wakati alipofanya kikao cha kuwakaribisha katika ofisi zao mpya zilizopo katika Mji wa Serikali Aprili 15, 2019.
Mkurugenzi wa Uwekezaji, Bw. Joseph Mramba (katikati) akieleza jambo kwa Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna (hayupo pichani) juu ya utayari wa kutekeleza majukumu yao wakati wa kikao hicho kilichofanyika Aprili 15, 2019 katika Mji wa Serikali, Jijini Dodoma. 
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwaonesha baadhi ya Watumishi wa Ofisi yake (hawapo pichani) namna Mji wa Serikali ulivyo walipofanya ziara ya kuzunguka kujua maeneo mbalimbali ya Wizara na huduma zilizopo katika Mji huo. 
Muonekano wa jengo la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) iliyopo katika Mji wa Serikali uliopo Kata ya Mtumba, Jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Madini, Bw. Msajigwa Kabigi (wa pili kutoka kulia) akimpa taarifa Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi (katikati) juu ya zoezi la kuamishia ofisi zao rasmi katika Mji huo wa Serikali uliopo Kata ya Mtumba, Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Naibu waziri wa Madini iliyopo katika Mji wa Serikali alipotembelea Wizara hiyo ambayo tayari imekwisha hamia Mji wa Serikali.
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi yake baada ya kumaliza majukumu yao kwa siku ya kwanza katika Ofisi zao mpya zilizopo katika Mji wa Serikali.


Read More

TANZANIA YAKWANZA DUNIANI KUENDESHA MAFUNZO YA DHANA YA AFYA MOJA KWA NGAZI YA STASHAHADA NA ASTASHAHADA.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki wa mafunzo ya  Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili,

Na. OWM, MOROGORO.

Mtandao wa Afya moja kwa nchi za Afrika mashariki, Kati na Magharibi (OHCEA) umeendesha mafunzo ya Dhana ya Afya moja kwa wanafunzi wa ngazi ya Stashahada na Astashahada  kutoka vyuo vya kwenye sekta za Afya ya Binadamu, Mifungo, Wanyamapori na Mazingira. Tanzania imekuwa nchi ya kwanza Duniani kufundisha Dhana hiyo katika ngazi hizo za taaluma,  kwa kuwa nchi nyingine  duniani hufundisha tu kwa ngazi ya Shahada na Shahada ya Uzamivu masuala ya  Afya moja.

Dhana ya Afya moja ambayo ni ushirikishwaji wa pamoja  sekta ya Afya ya Binadamu, Wanyamapori, Mifugo, Kilimo na  mazingira katika kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu ama kinyume chake. Wataalamu hao wamepata mafunzo hayo kwakuwa wapo karibu sana na jamii na  pindi utokeapo mlipuko wa ugonjwa ndio huwa kikosi kazi cha  kwanza na mstari wa mbele  kuwa eneo la tukio katika kufuatilia  na kukabili milipuko, kabla ya wataalamu wengine kushiriki kikamilifu.

Akiongea wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, tarehe 13 Aprili, Mjini Morogoro, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe alifafanua kuwa mafunzo hayo yanajenga kikosi kazi imara chenye kuchagiza shughuli za Afya moja hapa nchini.

“Katika kuimarisha Afya ya Binadamu pamoja na Afya ya mifugo na wanyamapori, kwa kutumia Dhana ya Afya moja, ninafarijika kwa  jitihada hizi za kuwajengea uwezo Wataalamu wa sekta za Afya katika ngazi ya Stashahada na Astashahada pamoja na wakufunzi wao, kwa kuwa tunaandaa rasilimali watu ya kuweza kuwa na uwezo wa kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa kwa Dhana ya Afya moja. Alisema Matamwe.

Wakiongea kwa nyakati tofauti waratibu wa mafunzo hayo  Profesa; Japheti Killewo na Profesa. Robinson Mdegela walifafanua kuwa tayari mitaala ya Afya moja kwa ngazi ya stashahada na astashahada imekamilika, lakini wakati taratibu za kuingiza  masuala ya Afya moja zitakamilika hivi karibuni katika mitaala ya ngazi  ya stashahada na Astashahada wameamua kufanya mafunzo hayo ili wakufunzi kujifunza kwa vitendo juu ya kufundisha masuala ya Afya moja lakini pia na kuwaandaa wanafunzi watakao fundishwa  kwa kutumia mitaala hiyo.

Aidha waratibu hao walibainisha kuwa wanafunzi hao wakiweza kuielewa vizuri dhana ya Afya moja watatumika vyema kuielimisha jamii juu ya masuala ya Afya Moja,  na nchi yetu itaweza kuzuia maambukizi ya magonjwa ya mlipuko hususani yale yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu na pia kupunguza usugu wa madawa kwa sababu wataweza kuongeza ushirikiano, mawasiliano na uratibu baina ya sekta husika.

Mafunzo hayo  yaliyowajumuisha zaidi ya wanafunzi 210, wa ngazi ya astashahada na ngazi ya cheti kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili, SUA, Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Morogoro, Chuo cha Afya cha Kilosa, Chuo cha Wanyamapori Pasiansi na Chuo cha Wanyamapori Mweka,

Aidha,  wakufunzi zaidi ya 30 wameshiriki kutoka Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine, Vyuo vya Afya Lindi, Mafinga, Kilosa, Mtwara, Singida, Kagemu, Mirembe, Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Morogoro, Temeke, Tengeru, Buhuri, pamoja na Vyuo vya Taaluma ya Wanyamapori , Pasiansi na Mweka.

Mafunzo hayo yameratibiwa na Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili  na Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine kwa kushirikiana na USAID, kupitia vyuo vikikuu vya  MINNESOTA na Tufs vya nchini Marekani
MWISHO.


Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe akisistiza jambo wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili.
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki wa mafunzo ya  Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili.
Baadhi ya Waratibu wa Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili, kulia ni Mratibu kutoka  Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili,  Profesa Japhet Killewo na kushoto ni Mratibu kutoka Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine, Profesa. Robinson Mdegela, katikati ni Rasi wa Ndaki ya Tiba za Wanyama na Sayansi za Afya Chuo kikuu Sokoine.  
Baadhi ya wanafunzi wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe (hayupo pichani) wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili.
Mratibu kutoka  Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili,  Profesa Japhet Killewo akisisitiza jambo wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili.
Mratibu kutoka Chuo Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine,  Profesa Robinson Mdegela akisisitiza jambo wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili
Baadhi ya wanafunzi wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada wa sekta za Afya ya Binadamu , wanyamapori, mifugo, kilimo na Mazingira wakifuatilia warsha ya kufunga mafunzo hayo ya  Afya Moja, mjini Morogoro tarehe 13 Aprili.





Read More

Saturday, April 13, 2019

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA TAARIFA YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016 – 2017

Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu amezindua taarifa ya utafiti wa viashiria na matokeo ya ukimwi wa mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) tarehe 13 Aprili, 2019 Jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo alieleza kuwa utafiti huo ni kielelezo tosha kuwa Serikali imeendelea kupambana na ugonjwa wa Ukimwi kwa kuonesha juhudi za kupungua kwa  kiwango cha maambukizi mapya na kupungua kwa vifo vinavyotokana na Ukimwi.  
“Tafiti zinaonesha maambukizi mapya ya VVU yamepungua kutoka watu 80,000 mwaka 2012 hadi kufikia watu 72,000 kwa mwaka katika mwaka 2017, vilevile takimu zinaonesha kupungua kwa vifo vinavyotokana na Ukimwi kutoka watu elfu 70 kwa mwaka katika 2010 hadi kufikia vifo elfu 32 kwa mwaka katika kipindi cha mwaka 2017,” alieleza Mhagama
Alisema kuwa katika kuthibitisha hilo, kiwango cha maambukizi ya Ukimwi nchini kinazidi kupungua ambapo mwaka 2012 matokeo ya utafiti kama huo yalionesha kuwa kiwango cha maambukizi kilikuwa ni asilimia 5.1 kwa watu wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 na matokeo ya mwaka 2016 – 2017 kiwango cha maambukizi kwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 49 ni asilimia 4.7.
Waziri Mhagama alieleza kuwa matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa watu waliopima afya zao kwa hiari wanaongezeka kutoka tafiti moja hadi nyingine, kati ya watu hao wanawake waliopima ni wengi kuliko wanaume.
Sambamba na hilo, amewapongeza wanawake kwa ujasiri na moyo wa kujali afya zao, pia kuwahimiza wanaume kujitokeza kwa wingi kupima ili wafahamu hali zao za kiafya.
Hata hivyo, Waziri Mhagama ametaka kila Mkoa na Halmashauri zote nchini kujadili matokeo ya utafiti huo kwa undani katika kamati za VVU na Ukimwi kuanzia ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na Vijiji ili kuelewa hali ilivyo katika maeneo yao na kuandaa mipango madhubuti ya kudhibiti ongezeko la maambukizi mapya ikiwemo kuongeza upatikanaji wa huduma stahiki kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).
Aidha, alitoa wito kwa watanzania kujitokeza kwa wingi na kupima afya zao, pia jamii kuelimishwa na kuhamasishwa juu ya umuhimu wa kutumia dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).
Aliongeza kwa kuagiza TACAIDS na Baraza la Watu wanaoishi na Ukimwi (NACOPHA) kuongeza jitihada dhidi ya unyanyapaa na ubaguzi.
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman alisema kuwa taarifa ya utafiti huo itasaidia watunga sera na waratibu wa miradi kufuatilia na kufanya tathmini ya miradi iliyopo kuandaa mikakati mipya kuhusiana na masuala ya Ukimwi hapa nchini.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko alisema kuwa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania imekuwa ikiratibu zoezi hilo la utafiti kila baada ya miaka mine na tafiti tatu zimeshafanyika mwaka 2003 – 2004, 2007 – 2008 na 2011 – 2012.
Pia, Kaimu Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema kuwa malengo ya msingi ya utafiti utafiti huo yalikuwa ni kutoa makadirio ya mwaka ya Kitaifa ya maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 64, na kutoa makadirio ya hali halisi ya upimaji wa VVU Kitaifa na Kimkoa.
“Utafiti wa aina hii ni wa kwanza kufanyika hapa nchini kwa kuwa umeangalia vitu vingi na umeshirikisha watu wa rika lote na viashiria vingine tofauti na tafiti nyingine zilizofanyika hapo awali,” alisema Chuwa.
Utafiti wa Viashiria vya Ukimwi na Matokeo yake wa Mwaka 2016 – 2017, ulitekelezwa kwa kushirikiana baina ya Ofisi ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar na ICAP Tanzania, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Afya – Zanzibar na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Zanzibar (ZAC), Maabara ya Taifa ya Afya za Jamii, Uhakiki, Ubora na Mafunzo, Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), na Kitengo Shirikishicha Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma, Zanzibar (ZIHTLP) kwa kushirikiana na wadau kutoka shirika lisilo la Kiserikali Centers for Disease Control and Prevention (CDC).
Baadhi ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) iliyofanyika Jengo la Takwimu tarehe 13 Aprili, 2019 Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiwa pamoja na viongozi wengine wakifuatilia ripoti fupi iliyokuwa ikiwasilishwa na mwakilishi kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) hayupo pichani. (Wa pili kutoka kushoto) ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri anayeshughulika masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stalla Ikupa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akionesha kitabu cha Taarifa ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) baada ya kuzindua taarifa hiyo, Jijini Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi kitabu cha Taarifa ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) Bi. Dorothy Mwaluko mara baada ya Kuzindua taarifa hiyo, Aprili 13, 2019 Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi na wadau wa maendeleo mara baada ya kuzindua Taarifa ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizindua Taarifa ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey). (Kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko, Naibu Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman. (Kulia) ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Dawa za Kulevya, Mhe. Osca Mukaza 
Naibu Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman akieleza namna Serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar zimekuwa zikishirikiana katika kukabiliana na Ugonjwa wa Ukimwi nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko akitoa maelezo mafupi kuhusu utafiti huo uliofanyika juu ya Viashiria na Matokeo ya Ukimwi wa Mwaka 2016 – 2017.

Read More

Wednesday, April 10, 2019

WAZIRI MKUU AMUENZI SOKOINE ATEMBELEA DAKAWA

Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa akioneshwa ramani na Kaimu Mhandisi wa Wilaya Silva Mkonda, wakati akikagua mradi wa ujenzi wa Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Steven Kebwe.
aziri  Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019.
aziri  Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019.

aziri  Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019.
aziri  Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019.
aziri  Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019.
Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. 

Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. 
Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. 
Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. 


Read More

Tuesday, April 9, 2019

WAZIRI MKUU: MIFUKO YA PLASTIKI MWISHO JUNI MOSI


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuanzia Juni mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuingiza, kuuza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za aina yoyote na matumizi yake yatakoma ifikapo Mei 31, 2019.

“Hivi karibuni nimemwagiza Waziri anayesimamia masuala ya mazingira ikiwemo kuzungumza na wadau mbalimbali, ikiwemo wenye viwanda vya kutengeneza mifuko ya plastiki kwa ajili ya kuhakikisha jambo hili linatekelezwa kwa haraka.”

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Aprili 9, 2019) Bungeni jijini Dodoma, kwenye mkutano wa 15 wakati akihitimisha hoja ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2019/2020.

“Kuanzia sasa tunatoa fursa ya viwanda kubadilisha teknolojia, wauzaji kuondoa mzigo uliopo, Ofisi ya Waziri wa Nchi, Makamu wa Rais itajiandaa kutumia kanuni chini ya Sheria ya Mazingira ili kulifanya katazo hili kuwa na nguvu ya kisheria. Tunachukua hatua hii ili kulinda afya ya jamii, wanyama, mazingira na miundombinu dhidi ya athari kubwa zinazotokana na taka za plastiki,” amesema.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua kwamba kuna baadhi ya bidhaa lazima zifungwe kwenye vifungashio vya plastiki na kwamba vifungashio kwa bidhaa hizo havitapigwa marufuku.

“Kwa msingi huo, katika hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, yatatolewa maelezo ya kina kuhusu katazo la vifungashio vya aina hii, hasa katika maeneo ya uzalishaji viwanda, sekta ya afya, na kilimo,” amesema.

Amesema ana imani kuwa utaratibu huo pamoja na kutunza mazingira, utatoa fursa ya kutengeneza ajira nyingi husasan za watu wa chini kupitia utengenezaji wa mifuko mbadala ya plastiki pamoja na kutumia kikamilifu fursa ya viwanda vya karatasi vilivyopo nchini ikiwemo cha Mgololo.

Amesema matumizi ya plastiki nchini yameendelea kuleta madhara makubwa ikiwemo vifo vya mifugo kwa kula plastiki, kuziba kwa mifereji, uchafuzi wa mazingira na kushindikana kwa kuozesha taka kwenye vituo vya kukusanya taka. 

Bunge lilikubali kupitisha sh. 148,886,523,581/- kwa ajili ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake kwa mwaka 2019/2020. Kati ya hizo, sh. 86,290,355,000/- ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. 62,596,168,581/- ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Vilevile, Bunge liliidhinisha sh. 124,182,537,600 kwa ajili ya Mfuko wa Bunge ambapo kati ya hizo 116,573,026,000/- ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. 7,609,511,600/- ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.


Read More

HABARI PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU BUNGENI LEO 09.04.2019

Makatibu Wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu wakiteta jambo mara baada ya kuhairishwa kwa vikao vya bunge vinavyoendelea Jijini Dodoma Aprili 09, 2019, kulia ni Bw. Andrew Massawe anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu na kushoto ni Bi. Maimuna Tarishi (Bunge na Waziri Mkuu) 
Sehemu ya Watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia michango wa Wabunge wakati wa kujadili Hoja ya Mhe.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (Mb) kuhusu mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi yake kwa Mwaka wa FEdha 2019/ 2020 Bungeni Dodoma Aprili 09, 2019. 
Sehemu ya Watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia michango wa Wabunge wakati wa kujadili Hoja ya Mhe.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (Mb) kuhusu mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi yake kwa Mwaka wa Fedha 2019/ 2020 Bungeni Dodoma Aprili 09, 2019. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiteta jambo na Mbunge wa Mikumi Mhe. Joseph Haule mara baada ya kuhairishwa kwa mkutano wa Bunge unaoendelea Jijini Dodoma Aprili 9, 2019.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde (wa kwanza kushoto) pamoja na Naibu Waziri Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndungulile (mwenye tai ya blue) wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Andrew Massawe (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) mwenye tai nyekundu na Bi. Maimuna Tarishi (Bunge na Waziri Mkuu) nje ya Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama  (mwenye blauzi nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Mawaziri na wabunge nje ya Ukumbi wa Bunge Dodoma, wa kwanza kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako.

Read More