Home
All posts
Wednesday, April 17, 2019
AJALI ZA MAJINI 300 HUTOKEA KILA MWAKA MKOANI MWANZA
Na.
OWM, MWANZA.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
John Mongella amebainisha kuwa takribani ajali za majini zaidi ya mia tatu huripotiwa kuwa zimetokea
mkoani humo. Ajali hizo ni zile ambazo huripotiwa rasmi tu katika mamlaka husika , aidha inasadikika zipo
ajali nyingi ambazo hutokea lakini huwa haziripitiwi kutokana na jiografia ya mkoa huo. Mkoa wa
Mwanza una visiwa zaidi ya 162 ambapo kati ya Visiwa hivyo vipo ambavyo watu
wanayo makazi ya kudumu na vingine watu huishi kwa muda mfupi.
Akiongea wakati akifungua Mafunzo kwa Kamati ya Usimamizi
wa maafa ya mkoa huo, yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara
ya Uratibu wa shughulii za maafa Leo, tarehe 17 Aprili, 2019, jiijini Mwanza,
Mongella amefafanua kuwa ajali za vyombo vya usafiri hasa vya majini zinaweza
kupunguzwa sana kama wamiliki na waendeshaji wa vyombo hivyo watazingatia
sheria na Kanuni zinazotawala uendeshaji
wa vyombo hivyo.
“Suala muhimu la Kuzingatia
ni kuhakikisha mamlaka zetu za serikali za mitaa zinaimarisha utawala bora
unaotoa nafasi kwa jamii kushiriki
katika kuzuia na Kupunguza madhara ya majanga, kujiandaa, kukabili na kurejesha
hali baada ya maafa kutokea ikiwa ni pamoja na kutoa elimu, taarifa za
tahadhari ya awali kwa wakati muafaka na kuandaa rasilimali zinazohiotajika ,
Ni wajibu wetu kuhakikisha sheria zinasimamiwa kikamilifu ili kuepuka maafa“
alisisitiza Mongella.
Naye Mkurugenzi wa Uratibu
wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali, Jimmy Matamwe, ameitaka
Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya mkoa huo
kuandaa Mkakati wa Kupunguza madhara ya maafa pamoja na Mpango wa kujiandaa na
kukabili maafa, Aidha, ameeleza kuwa Ofisi
ya waziri Mkuu imeendesha mafunzo hayo ili kuijengea uwezo kamati hiyo ambayo ni
chombo cha kisheria hapa nchini kwa ajili ya kutathimini na kutekeleza masuala
ya kitaalam kuhusu usimamizi wa maafa, kuzuia na kupunguza madhara ya majanga
ya aina zote katika mkoa.
“Upunguzaji wa madhara ya
maafa ni suala mtambuka linalohusika katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi
na kijamii sekta zote. Suala la usimamizi wa maafa linahitaji utashi wa kisiasa
na kuwajibika kitaalam, kisheria, uelewa wa umma, elimu ya kisayansi, mipango
makini ya maendeleo, ufanisi wa utekelezaji wa sera, mifumo ya tahadhari
inayojibu matakwa ya jamii” alisema
Kanali., Matamwe.
Mwaka jana, Mwezi
Septemba, mkoa wa Mwanza ulipata maafa makubwa baada ya Kivuko cha MV. Nyerere
kuzama na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 200 na wengine 40 waliokolewa.
Kufuatia maafa hayo Mkoa huo umeendelea na jitihada za kuzijengea uwezo kamati
za Usimamizi wa Maafa za mkoa huo
Mafunzo hayo
yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu wa shughuli za maafa,
yamehudhuriwa na wajumbe wote wa Kamati ya Usimamizi wa maafa kwa kuzingatia
Kifungu cha 13 cha sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 7 ya mwaka 2015.
Monday, April 15, 2019
MATUKIO KATIKA PICHA OFISI YA WAZIRI MKUU YAHAMIA RASMI MJI WA SERIKALI
![]() |
Muonekano wa jengo la Ofisi ya
Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) iliyopo katika Mji wa Serikali uliopo Kata ya
Mtumba, Jijini Dodoma.
|
![]() |
Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na
Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi
yake baada ya kumaliza majukumu yao kwa siku ya kwanza katika Ofisi zao mpya
zilizopo katika Mji wa Serikali.
|
TANZANIA YAKWANZA DUNIANI KUENDESHA MAFUNZO YA DHANA YA AFYA MOJA KWA NGAZI YA STASHAHADA NA ASTASHAHADA.
Saturday, April 13, 2019
WAZIRI MHAGAMA AZINDUA TAARIFA YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI WA MWAKA 2016 – 2017
Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
amezindua taarifa ya utafiti wa viashiria na matokeo ya ukimwi wa mwaka 2016 –
2017 (Tanzania HIV Impact Survey) tarehe 13 Aprili, 2019 Jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa hafla
hiyo alieleza kuwa utafiti huo ni kielelezo tosha kuwa Serikali imeendelea kupambana
na ugonjwa wa Ukimwi kwa kuonesha juhudi za kupungua kwa kiwango cha maambukizi mapya na kupungua kwa vifo
vinavyotokana na Ukimwi.
“Tafiti zinaonesha maambukizi
mapya ya VVU yamepungua kutoka watu 80,000 mwaka 2012 hadi kufikia watu 72,000
kwa mwaka katika mwaka 2017, vilevile takimu zinaonesha kupungua kwa vifo vinavyotokana
na Ukimwi kutoka watu elfu 70 kwa mwaka katika 2010 hadi kufikia vifo elfu 32
kwa mwaka katika kipindi cha mwaka 2017,” alieleza Mhagama
Alisema kuwa katika
kuthibitisha hilo, kiwango cha maambukizi ya Ukimwi nchini kinazidi kupungua
ambapo mwaka 2012 matokeo ya utafiti kama huo yalionesha kuwa kiwango cha
maambukizi kilikuwa ni asilimia 5.1 kwa watu wenye umri kati ya miaka 15 hadi
49 na matokeo ya mwaka 2016 – 2017 kiwango cha maambukizi kwa watu wenye umri
wa miaka 15 hadi 49 ni asilimia 4.7.
Waziri Mhagama alieleza kuwa
matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa watu waliopima afya zao kwa hiari wanaongezeka
kutoka tafiti moja hadi nyingine, kati ya watu hao wanawake waliopima ni wengi
kuliko wanaume.
Sambamba na hilo, amewapongeza
wanawake kwa ujasiri na moyo wa kujali afya zao, pia kuwahimiza wanaume kujitokeza
kwa wingi kupima ili wafahamu hali zao za kiafya.
Hata hivyo, Waziri Mhagama
ametaka kila Mkoa na Halmashauri zote nchini kujadili matokeo ya utafiti huo
kwa undani katika kamati za VVU na Ukimwi kuanzia ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata
na Vijiji ili kuelewa hali ilivyo katika maeneo yao na kuandaa mipango
madhubuti ya kudhibiti ongezeko la maambukizi mapya ikiwemo kuongeza upatikanaji
wa huduma stahiki kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).
Aidha, alitoa wito kwa
watanzania kujitokeza kwa wingi na kupima afya zao, pia jamii kuelimishwa na
kuhamasishwa juu ya umuhimu wa kutumia dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi kwa
watu wanaoishi na VVU (WAVIU).
Aliongeza kwa kuagiza
TACAIDS na Baraza la Watu wanaoishi na Ukimwi (NACOPHA) kuongeza jitihada dhidi
ya unyanyapaa na ubaguzi.
Kwa Upande wake Naibu Waziri
wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman alisema kuwa
taarifa ya utafiti huo itasaidia watunga sera na waratibu wa miradi kufuatilia
na kufanya tathmini ya miradi iliyopo kuandaa mikakati mipya kuhusiana na
masuala ya Ukimwi hapa nchini.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa
Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko alisema
kuwa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania imekuwa ikiratibu zoezi hilo la utafiti
kila baada ya miaka mine na tafiti tatu zimeshafanyika mwaka 2003 – 2004, 2007 –
2008 na 2011 – 2012.
Pia, Kaimu Mtakwimu Mkuu wa
Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema kuwa malengo ya msingi ya utafiti utafiti
huo yalikuwa ni kutoa makadirio ya mwaka ya Kitaifa ya maambukizi mapya ya VVU
miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 64, na kutoa makadirio ya hali
halisi ya upimaji wa VVU Kitaifa na Kimkoa.
“Utafiti wa aina hii ni wa
kwanza kufanyika hapa nchini kwa kuwa umeangalia vitu vingi na umeshirikisha
watu wa rika lote na viashiria vingine tofauti na tafiti nyingine zilizofanyika
hapo awali,” alisema Chuwa.
Utafiti wa Viashiria vya Ukimwi
na Matokeo yake wa Mwaka 2016 – 2017, ulitekelezwa kwa kushirikiana baina ya
Ofisi ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar na ICAP Tanzania,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Afya –
Zanzibar na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Zanzibar (ZAC), Maabara ya Taifa ya Afya
za Jamii, Uhakiki, Ubora na Mafunzo, Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi
(NACP), na Kitengo Shirikishicha Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma, Zanzibar
(ZIHTLP) kwa kushirikiana na wadau kutoka shirika lisilo la Kiserikali Centers
for Disease Control and Prevention (CDC).
Wednesday, April 10, 2019
WAZIRI MKUU AMUENZI SOKOINE ATEMBELEA DAKAWA
aziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
aziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
aziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
aziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
aziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua majengo ya shule ya Sokoine Memorial High School, wilayani Mvomero Morogoro akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mnara wa kumbukumbu ya Hayati Moringe Sokoine, uliopo Wami Dakawa wilayani Mvomero, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam Aprili 10, 2019. |
Tuesday, April 9, 2019
WAZIRI MKUU: MIFUKO YA PLASTIKI MWISHO JUNI MOSI
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amesema kuanzia Juni mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kutengeneza,
kuingiza, kuuza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za
aina yoyote na matumizi yake yatakoma ifikapo Mei 31, 2019.
“Hivi
karibuni nimemwagiza Waziri anayesimamia masuala ya mazingira ikiwemo
kuzungumza na wadau mbalimbali, ikiwemo wenye viwanda vya kutengeneza mifuko ya
plastiki kwa ajili ya kuhakikisha jambo hili linatekelezwa kwa haraka.”
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Aprili 9,
2019) Bungeni jijini Dodoma, kwenye mkutano wa 15 wakati akihitimisha hoja ya
bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka
2019/2020.
“Kuanzia sasa tunatoa fursa ya viwanda
kubadilisha teknolojia, wauzaji kuondoa mzigo uliopo, Ofisi ya Waziri wa Nchi,
Makamu wa Rais itajiandaa kutumia kanuni chini ya Sheria ya Mazingira ili
kulifanya katazo hili kuwa na nguvu ya kisheria. Tunachukua hatua hii ili kulinda afya ya jamii, wanyama,
mazingira na miundombinu dhidi ya athari kubwa zinazotokana na taka za plastiki,”
amesema.
Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua kwamba kuna baadhi ya bidhaa lazima zifungwe kwenye vifungashio
vya plastiki na kwamba vifungashio kwa bidhaa hizo havitapigwa marufuku.
“Kwa msingi
huo, katika hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, yatatolewa maelezo ya
kina kuhusu katazo la vifungashio vya aina hii, hasa katika maeneo ya
uzalishaji viwanda, sekta ya afya, na kilimo,” amesema.
Amesema ana
imani kuwa utaratibu huo pamoja na kutunza mazingira, utatoa fursa ya
kutengeneza ajira nyingi husasan za watu wa chini kupitia utengenezaji wa
mifuko mbadala ya plastiki pamoja na kutumia kikamilifu fursa ya viwanda vya
karatasi vilivyopo nchini ikiwemo cha Mgololo.
Amesema
matumizi ya plastiki nchini yameendelea kuleta madhara makubwa ikiwemo vifo vya
mifugo kwa kula plastiki, kuziba kwa mifereji, uchafuzi wa mazingira na
kushindikana kwa kuozesha taka kwenye vituo vya kukusanya taka.
Bunge
lilikubali kupitisha sh. 148,886,523,581/-
kwa ajili ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake kwa mwaka
2019/2020. Kati ya hizo, sh. 86,290,355,000/- ni kwa ajili ya matumizi ya
kawaida na sh. 62,596,168,581/- ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
Vilevile,
Bunge liliidhinisha sh. 124,182,537,600 kwa ajili ya Mfuko wa Bunge ambapo kati
ya hizo 116,573,026,000/- ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh.
7,609,511,600/- ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
HABARI PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU BUNGENI LEO 09.04.2019
Subscribe to:
Posts (Atom)
MITANDAO YA KIJAMII
Popular Posts
-
Na. OWM, Dodoma. Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, imefanya ukaguzi wa utekelezaji wa sheria Na.5 y...
-
Wataalamu wa Afya moja wakiwa katikapicha ya pamoja wakati wa mkutano wa wataalamu wa Afya moja uliojikita katika ulinzi na usalama...
-
Na. OWM, ARUSHA Wataalam wa sheria kutoka katika sekta ya Afya ya binadamu, Afya ya wanyamapori na mifugo pamoja na mazingira wameshauri...
-
Washiriki wa Mkutano wa mwaka wa Wataalamu wa Maabara wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano wa mwaka kwa wataalam wa maabara w...
-
TAMOBA wafanya wasilisho la mfumo maalum wa kielektroniki wa ulinzi na usalama wa Bodaboda na BajajiKampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaj Association (TAMOBA) imefanya wasilisho maaluum kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mfumo maalum wa ...
Formulir Kontak
Contributors
Powered by Blogger.