Wazalishaji wa mbegu za alizeti katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida, wameiomba Serikali kuongeza juhudi katika kuwawezesha kuandaa vifungashio bora vya mbegu ili kuongeza thamani ya mazao yao sokoni.
Bw. Athumani Ramadhani, mzalishaji wa mbegu aina ya Record, alisema: “Tunaomba Serikali itupe msaada wa kitaalamu kuandaa vifungashio bora vitakavyotangaza mbegu zetu na kuongeza thamani sokoni.”
Naye Bi. Aziza Ramadhani aliongeza kuwa uzalishaji huo umeimarisha ushirikiano wao na taasisi za Serikali kama ASA na TOSCI, zinazopima ubora kabla ya mbegu kuingia sokoni.