Tuesday, September 2, 2025

WAZALISHAJI WA MBEGU MKALAMA WAOMBA SERIKALI KUIMARISHA UFUNGASHAJI

 


Wazalishaji wa mbegu za alizeti katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida, wameiomba Serikali kuongeza juhudi katika kuwawezesha kuandaa vifungashio bora vya mbegu ili kuongeza thamani ya mazao yao sokoni. 

 Wito huo umetolewa  wakati wa ziara ya ujumbe wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kwa kushirikiana na wawakilishi kutoka IFAD katika Kijiji cha Ilunda, waliokuja kufuatilia utekelezaji wa programu hiyo. 

Bw. Athumani Ramadhani, mzalishaji wa mbegu aina ya Record, alisema: “Tunaomba Serikali itupe msaada wa kitaalamu kuandaa vifungashio bora vitakavyotangaza mbegu zetu na kuongeza thamani sokoni.” 

Naye Bi. Aziza Ramadhani aliongeza kuwa uzalishaji huo umeimarisha ushirikiano wao na taasisi za Serikali kama ASA na TOSCI, zinazopima ubora kabla ya mbegu kuingia sokoni. 

 Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mkalama, Bi. Asia, alisema Serikali inalenga kuifanya Mkalama kuwa mfano bora katika utekelezajiwa Programu ya Kilimo na Uvuvi (AFDP), huku akisisitiza umuhimu wa kuongezwa nguvu katika sekta hiyo.

 


Read More

Monday, September 1, 2025

DKT. KILABUKO: OFISI YA WAZIRI MKUU ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA IFAD

 


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika utekelezaji wa miradi ya kilimo na uvuvi nchini. 

Ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati wa kikao na ujumbe wa IFAD waliopo nchini kufuatilia utekelezaji wa mradi wa programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo na uvuvi (AFDP). 

“Nawahakikishia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ipo tayari kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha miradi mnayoitekeleza inaleta matokeo chanya,” amesema Dkt. Kilabuko.



Read More