Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi leo tarehe 16 Septemba, 2025 ameshiriki Mkutano wa Kimataifa wa Uendelezaji Miundombinu unaofanyika Jijini Seoul nchini Korea.
Katika Mkutano huo Dkt. Yonazi
amepata fursa ya kuwasilisha mada kuhusu hatua iliyofikiwa katika zoezi
lakuhamisha Makao Makuu na fursa za uendelezaji wa Jiji la Dodoma pamoja na Mji
wa Serikali.
Aidha, Dkt. Yonazi amekutana
na Mwenyekiti wa KFINCO na taasisi inayoratibu uendelezaji wa Mji wa Serikali
Korea (National Agency For Administrative City Construction of KOREA-NA ACC)
kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo
pamoja na utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano baina Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Bunge na Uratibu) na Taasisi ya NAACC.
Katika mkutano huo, Dkt. Jim
Yonazi ameongozana na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za
Serikali Bw. Paul Sangawe na wajumbe wengine kutoka Tanzania.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.