Thursday, February 27, 2025

WAZIRI LUKUVI AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA SHIRIKA LA FAO

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu uliyopo katika Mtaa wa posta Jijini Dodoma.

Ujumbe huo kutoka FAO umefanya ziara ya wadau wa ufadhili wa Mfuko Nyumbulifu wa Uchangiaji kwa Hiari (Flexible Voluntary Contribution - FVC) iliyohusisha  Waheshimiwa Mabalozi wa Ubelgiji na Uswisi, Wawakilishi wa Kudumu FAO katika Umoja wa Mataifa, Rome, Washauri Waandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDC) na Viongozi Waandaamizi wa FAO Makao Makuu.

Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kuwezesha washirika (partners) kupata uelewa wa utekelezaji wa programu na miradi inayofadhiliwa kupitia Flexible Voluntary Contribution (FVC) nchini Tanzania, kuongeza uelewa, muonekano na fursa zinazopatikana kwenye FVC kama mfuko nyumbulifu wa utoaji misaada ili kuweza kufikia malengo ya kimkakati Kitaifa na Kimataifa kupitia FAO.



Read More

Wednesday, February 26, 2025

TAARIFA ZA AWALI ZA TAADHARI ZA MAAFA ZITOKE KWA WAKATI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi ameelekeza Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura kujiratibu vizuri katika kufikisha taarifa zote za taadhari ya maafa kwa wakati ili utekelezaji wake ufanyike mapema kabla ya madhara kutokea.

Kauli hiyo ametoa leo alipotembelea Kituo cha Ufuatiliaji wa Majanga Katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma.

" kwa nafasi mliyonayo na teknolojia mnazotumia mnaweza kujua na kutoa taarifa zote za tahadhari bila urasimu, ili kuepuka athari kubwa za maafa zinazoweza kutokea baadae."alisisitiza Waziri Lukuvi.

Aidha muangalie na uwezekano wa kurahisisha mawasialiano ya taarifa zote za tahadhari ziweze kupatikana kila siku kwa njia ya simu ili kila mtu anayeenda kwenye shughuli ajue na achukue tahadhari.

“huduma hii iwe bure na ipatikane muda wote ili wananchi waingie wasome na wachukue tahadhari, na tutakuwa tumefanya kazi yetu vyema,” alisema

Naye Mkurugenzi Msaizidizi anaye simamia  Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi: Jane Kikunya amelezea kuhusu ufanyaji kazi wa kituo hicho kwamba kinajukumu kubwa la kufuatilia majanga ikiwa ni pamoja kushirikiana na taasisi mbalimbali katika ngazi ya kitaifa katika kutoa taarifa za awali za tahadhari kwa ngazi mbalimbali.

Amefafanua kwamba katika Ngazi ya Mikoa kuna vituo vya maafa vinapaswa kuanzishwa na jukumu hilo limeainishwa katika sheria ya maafa ya mwaka 2022 ambayo imeeleza kila Mkoa, kuwa na kituo cha usimamizi wa maafa ili kufanya ufuatiliaji wa majanga yanayoweza kutokea katika eneo la Mkoa husika.

Hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu inafanya ufuatiliaji wa uanzishwaji wa vituo hivyo ambapo wameweza kukutana na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa ambao kisheria wamepewa jukumu la usimamizi wa vituo hivyo ili kujengeana uelewa wa miongozo na namna ya uanzishaji na usimamizi wa vituo hivyo.

“Vituo hivyo vya Mikoa vitaunganishwa na mifumo ya Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu ili waweze kufanya ufuatiliaji kwa karibu,” alibainisha Bi. Jane.



Read More

Saturday, February 22, 2025

WAZIRI LUKUVI AMSHUKURU RAIS SAMIA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi amesema Serikali ya Awamu ya Sita imekamilisha kiu na ndoto za Iringa kwa kuanza ujenzi bararaba ya kiwango cha lami kwenda Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na upanuzi wa ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Iringa.

Waziri ametoa Kauli hiyo wakati aliposhiriki katika tukio la kurejesha wa safari za ndege za shirika la ndege Tanzania (ATCL) Mkoani Iringa iliyoongozwa na Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa.

Amesema wazo la Ujenzi lilikuwa la Muda Mrefu tangu enzi za TANU lakini Mungu amemleta Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yote mawili utekelezaji wake umefanyika, hivyo hatuna budi kumshukuru.

“Tunatarajia ujenzi wa babarara ya Pawaga kuanzia Pawaga Kuja Mjin, tunategemea barabara hiyo ikikamilika tuanze kusafirisha mpunga unaozalishwa kutoka Pawaga  kusafirishwa na shirika la ndege la Tanzania (ATCL),” alibainisha.



Read More

Tuesday, February 18, 2025

WAZIRI LUKUVI AKUTANA NA WADAU WA SEKTA BINAFSI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa Sekta binafsi katika kikao kilichoratibiwa na Baraza la Taifa la Biashara (TNBC).

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Magogoni Jijini Dar es salaam, kilicholenga kujadili ushiriki wa Sekta binafsi katika kuboresha mazingira ya biashara kwa kuangalia fursa za uchumi ikiwa ni pamoja na kupanga mikakati ya kutumia fursa hizo vizuri na kushauri Serikali katika maeneo yanayohitaji kuboreshwa.

Akizungumza katika kikao hicho Rais wa Shirikisho la Sekta Binafsi Bi. Angelina Ngalula amesema Sekta binafsi ndio injini ya kusukuma uchumi, inayochukua fursa zote zinazofunguliwa na serikali kama mabadiliko makubwa ya sheria na taratibu, kutolewa kwa tozo inalenga kutoa fursa kwa sekta binafsi kuwekeza na kupata mafanikio.

“Katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani umefanya kazi kubwa sana katika uwekezaji wa miundombinu ambayo imesaidia katika kuchochea biashara," alieleza Bi. Angelina

Akichangia kuhusu Sekta ya Kilimo Bi. Jacqueline Mkindi amesema sekta ya kilimo na mifugo imenufaika sana kwa sababu ya nguvu ya serikali kutangaza diplomasia ya uchumi na kueleza kuwa umeongeza uhitaji wa bidhaa za Tanzania nje ya Nchi.




Read More

Wednesday, February 12, 2025

WAKURUGENZI WA UFUATILIAJI NA TATHMINI NGAZI YA WIZARA WAKUTANA KUPITIA TAARIFA YA UTENDAJI WA SERIKALI



Imeelezwa kwamba jukumu la Ufuatiliaji na Tathmini ni muhimu katika kuboresha utendaji wa Serikali kwa ujumla hivyo kusaidia kutoa msukumo wa kuboresha Miundo na Mifumo kwaajili ya kuandaa Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini Ili kuimarisha U&T ndani ya Serikali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Sakina Mwinyimkuu alipomuwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. James Henry Kilabuko, katika Kikao kazi cha wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini na Maafisa kutoka katika Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya wizara kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa lengo la kupitia Taarifa ya Utendaji wa Serikali (Government Performance Report kwa Mwaka wa Fedha 2023/24).

Alisema dhumuni kubwa ni kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji huduma bora kwa wananchi hivyo wataalam wa Vitengo mnapaswa kusimamia na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyoainishwa katika mipango ya serikali.

Nitoe rai kwa wataalam kutofanya kazi kwa mazoea, uoga au kutojiamini, kwani kwa kufanya hivyo serikali haitafikia malengo nhivyo kupunguza umuhimu wa kuanzisha Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini. Hivyo

 “ni vema kufanya ufuatiliaji na tathmini kuwa nyenzo ya msingi ya kusaidia utendaji wa taasisi, sekta na nchi kwa ujumla,”alifafanua Bi, Sakina

Ikumbukwe kwamba

Kikao kazi hicho kitafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 12 hadi 13 februari 2025 kimelenga kutoa mafunzo ya Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini (U&T) katika taasisi za Serikali yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu



Read More

Saturday, February 8, 2025

WAZIRI LUKUVI AMPA KONGOLE MHE. WAZIRI MKUU

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa William Lukuvi amemshukuru na kumpongeza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa kwa kuendelea kusimamia na kuratibu shughuli za Serikali.

Waziri Lukuvi ametoa pongezi hizo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Ngome Jijini Dodoma.

Alisema kuwa kazi ya Waziri Mkuu kwa Mujibu wa Katiba ni kuratibu shughuli zote za Serikali na chini yake yupo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati na watendaji wa Ofisi yake ambayo wanatekeleza majukumu hayo kwa weledi na ufanisi mkubwa.

“Wakati wa uratibu wa shughuli za Maafa watendaji mmefanya kazi kwa ushirikiano Mkubwa chini ya Uongozi wa Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mambo yameenda vizuri nchi nzima,” alisema Waziri Lukuvi

Aidha alifafanua kuwa kazi ya Ofisi ya Waziri Mkuu ni kuratibu Serikali ili kuwafahamisha namna Serikali inavyoendelea kutekeleza majukumu na kuhudumia wananchi.

"...kwa kuwa tuna nafasi ya kupata taarifa na kuzifanyia uchambuzi ili kujulisha umma kwa njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari basi tuendelee kuratibu vyema taarifa na kuzitoa kwa usahihi ndiyo jukumu letu kubwa na lamsingi lazima tujipange ili ziweze kutoka kwa wakati alisema,” Waziri Lukuvi.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi katika maneno ya utangulizi amesema Viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wamewatengeneza mazingira mazuri kwa watendaji kufanya kazi kwa furaha na amani.

Pia ameahidi kuimarisha ushirikiano miongoni mwao ili kuyafikia maelengo ya ofisi na Serikali kwa ujumla.

"Tuimarishe ushirikiano miongoni mwetu ili kazi zetu ziende kwa wepesi na ufanisi kwa kuamini kila mmoja ana mchango chanya kuhakikisha malengo yanatimia," alisema Dkt. Yonazi.

 


Read More

Tuesday, February 4, 2025

DKT. YONAZI AWAKUMBUSHA WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU KUENDELEA KUTEKELEZA MAJUKUMU KWA WELEDI



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya sera, bunge na uratibu Dkt. Jim Yonazi amewakumbusha watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ushirikiano, upendo, furaha na amani ili kuyafikia malengo ya ofisi hiyo.

Dkt. Yonazi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Watumishi Ofisi yake wakati wa mkutano wake na watumishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyopo Njedengwa Jijini Dodoma.

Dkt. Yonazi amesema ipo haja ya kila mtumishi kujifanyia tathmini katika utendaji wake wa kazi huku akizingatia miongozo na kanuni za utumishi wa umma na kusema kuwa, kila mtumishi anawajibika katika kuhakikisha ofisi inapata matokeo iliyoyakusudia na kwa ufanisi.

“Ni wakati sahihi kila mmoja kuilinda furaha aliyonayo awapo mahali pa kazi, isingefaa utoke nyumbani huna furaha na ufike eneo la kazi ukose furaha, ni vyema kuja eneo la kazi na kuipata furaha mara mbili  kwa kuzingatia mazingira yaliyorafiki katika kutekeleza majukumu,” alisema Dkt. Yonazi

Aliongezea kuwa kila mtumishi wa umma awe na desturi ya kuheshimu nafasi ya mwingine bila kujali tofauti zinazoweza kuwepo miongoni mwa watumishi hao.

“Ni vyema kila mtu akajali mwingine na ikumbukwe hakuna mtu mwenye uwezo mdogo wa kufanya kazi, jambo la msingi ni kuhakikisha ule uwezo uliopewa na Mwenyezi Mungu na Mafunzo mbalimbali unatumia vizuri na kuhakikisha unaleta matunda mazuri na kuleta maendeleo kwa Nchi yetu” alisema Dkt, Yonazi.

Sambamba na hilo aliwaeleza watumishi hao kuwa kila mmoja ni kiongozi katika eneo lake la kazi hivyo abebe dhamana hiyo kwa weledi na ufanisi mkubwa.

“.....kila mtumishi aliyepo hapa ndiye Katibu Mkuu kwenye eneo lake, kwa kubeba imani ya kwamba ni Katibu Mkuu anapaswa kuwa na nidhamu na bidii katika kazi ikiwa ni pamoja na kuwa mwaminifu,” alisema.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Dkt. James Kilabuko katika neno lake la utangulizi amewaasa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi na kuzingatia sheria za utumishi wa Umma huku akiwasihi kuimarisha umoja na mshikamano ili kuiletea Serikali maendeleo yake.

Naye Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Ofisi ya Waziri Mkuu Bi, Numpe Mwambenja ameomba watumishi kuendelea kujitathimini mienendo yao katika utumishi wa Umma kwa kufanya kazi vizuri na nidhamu na kuheshimu viongozi huku wakiheshimiana wao kwa wao.

Bi. Numpe alitumia nafasi hiyo kuupongeza uongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa namna unavyojali maslahi ya watumishi na ustawi wao kwa ujumla na kuwasihii watumishi kuendelea kutimiza wajibu kwa kuzingatia kauli ya “hakuna haki bila wajibu”.






Read More