Saturday, February 22, 2025

WAZIRI LUKUVI AMSHUKURU RAIS SAMIA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi amesema Serikali ya Awamu ya Sita imekamilisha kiu na ndoto za Iringa kwa kuanza ujenzi bararaba ya kiwango cha lami kwenda Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na upanuzi wa ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Iringa.

Waziri ametoa Kauli hiyo wakati aliposhiriki katika tukio la kurejesha wa safari za ndege za shirika la ndege Tanzania (ATCL) Mkoani Iringa iliyoongozwa na Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa.

Amesema wazo la Ujenzi lilikuwa la Muda Mrefu tangu enzi za TANU lakini Mungu amemleta Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yote mawili utekelezaji wake umefanyika, hivyo hatuna budi kumshukuru.

“Tunatarajia ujenzi wa babarara ya Pawaga kuanzia Pawaga Kuja Mjin, tunategemea barabara hiyo ikikamilika tuanze kusafirisha mpunga unaozalishwa kutoka Pawaga  kusafirishwa na shirika la ndege la Tanzania (ATCL),” alibainisha.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.