Imeelezwa kwamba jukumu la
Ufuatiliaji na Tathmini ni muhimu katika kuboresha utendaji wa Serikali kwa ujumla
hivyo kusaidia kutoa msukumo wa kuboresha Miundo na Mifumo kwaajili ya kuandaa
Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini Ili kuimarisha U&T ndani ya Serikali.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi
wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali kutoka Ofisi ya
Waziri Mkuu Bi. Sakina Mwinyimkuu alipomuwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi
ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. James Henry Kilabuko, katika Kikao
kazi cha wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini na Maafisa kutoka katika
Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya wizara kilichofanyika katika
Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa lengo la kupitia Taarifa ya Utendaji wa
Serikali (Government Performance Report kwa Mwaka wa Fedha 2023/24).
Alisema dhumuni kubwa ni
kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji huduma bora kwa wananchi hivyo wataalam
wa Vitengo mnapaswa kusimamia na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo
yaliyoainishwa katika mipango ya serikali.
Nitoe rai kwa wataalam
kutofanya kazi kwa mazoea, uoga au kutojiamini, kwani kwa kufanya hivyo
serikali haitafikia malengo nhivyo kupunguza umuhimu wa kuanzisha Vitengo vya
Ufuatiliaji na Tathmini. Hivyo
“ni vema kufanya ufuatiliaji na tathmini kuwa
nyenzo ya msingi ya kusaidia utendaji wa taasisi, sekta na nchi kwa ujumla,”alifafanua
Bi, Sakina
Ikumbukwe kwamba
Kikao kazi hicho kitafanyika
kwa siku mbili kuanzia tarehe 12 hadi 13 februari 2025 kimelenga kutoa mafunzo
ya Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini (U&T) katika taasisi za Serikali
yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.