Wednesday, February 12, 2025

WAKURUGENZI WA UFUATILIAJI NA TATHMINI NGAZI YA WIZARA WAKUTANA KUPITIA TAARIFA YA UTENDAJI WA SERIKALI



Imeelezwa kwamba jukumu la Ufuatiliaji na Tathmini ni muhimu katika kuboresha utendaji wa Serikali kwa ujumla hivyo kusaidia kutoa msukumo wa kuboresha Miundo na Mifumo kwaajili ya kuandaa Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini Ili kuimarisha U&T ndani ya Serikali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Sakina Mwinyimkuu alipomuwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. James Henry Kilabuko, katika Kikao kazi cha wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini na Maafisa kutoka katika Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya wizara kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa lengo la kupitia Taarifa ya Utendaji wa Serikali (Government Performance Report kwa Mwaka wa Fedha 2023/24).

Alisema dhumuni kubwa ni kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji huduma bora kwa wananchi hivyo wataalam wa Vitengo mnapaswa kusimamia na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyoainishwa katika mipango ya serikali.

Nitoe rai kwa wataalam kutofanya kazi kwa mazoea, uoga au kutojiamini, kwani kwa kufanya hivyo serikali haitafikia malengo nhivyo kupunguza umuhimu wa kuanzisha Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini. Hivyo

 “ni vema kufanya ufuatiliaji na tathmini kuwa nyenzo ya msingi ya kusaidia utendaji wa taasisi, sekta na nchi kwa ujumla,”alifafanua Bi, Sakina

Ikumbukwe kwamba

Kikao kazi hicho kitafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 12 hadi 13 februari 2025 kimelenga kutoa mafunzo ya Miongozo ya Ufuatiliaji na Tathmini (U&T) katika taasisi za Serikali yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.