Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala Sera, Bunge na Uratibu
Mheshimiwa William Lukuvi amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka
Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri
Mkuu uliyopo katika Mtaa wa posta Jijini Dodoma.
Ujumbe
huo kutoka FAO umefanya ziara ya wadau wa ufadhili wa Mfuko Nyumbulifu wa
Uchangiaji kwa Hiari (Flexible Voluntary Contribution - FVC) iliyohusisha Waheshimiwa Mabalozi wa Ubelgiji na Uswisi,
Wawakilishi wa Kudumu FAO katika Umoja wa Mataifa, Rome, Washauri Waandamizi wa
Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDC) na Viongozi Waandaamizi wa FAO Makao
Makuu.
Ziara
hiyo ilikuwa na lengo la kuwezesha washirika (partners) kupata uelewa wa
utekelezaji wa programu na miradi inayofadhiliwa kupitia Flexible Voluntary
Contribution (FVC) nchini Tanzania, kuongeza uelewa, muonekano na fursa
zinazopatikana kwenye FVC kama mfuko nyumbulifu wa utoaji misaada ili kuweza
kufikia malengo ya kimkakati Kitaifa na Kimataifa kupitia FAO.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.