Monday, August 21, 2023

WAZIRI MHAGAMA AHIMIZA MASHIRIKIANO

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Mhe. Jenista Mhagama ameitaka Idara ya Ufutiliaji na Tathimini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini, (TAKUKURU) katika kutumia Mfumo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathimini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali, ili kuweza kuondoa upendeleo, Rushwa na kutoa huduma bora kwa wananchi katika utendaji Serikalini.

Kauli hiyo ameitoa leo Jijini Dodoma alipokuwa katika kikao kazi cha Mapitio kilichohusisha Wakurugenzi, wa Idara na Wakuu wa vitengo wa Ofisi hiyo ambapo, Mamlaka ya Serikali Mtandao imefanya wasilisho la Mfumo wa Taifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa shughuli za Serikali.

Waziri Mhagama Alisema kuwa, eneo la Ufuatiliaji na Tathmini ni eneo ambalo haliwezi kukwepeka “Leo Tumekutana hapa tumefanya kazi nzuri ya kufanya mapitio na kuangalia ramani hii ambayo inaanza na kuwa na mfumo wa Ufuatilia na Tathmini Nchini, kama nyenzo muhimu sana ya Utendaji kazi ndani ya Serikali.” Alisisitiza

Aliendelea kusema kuwa, Mfumo huu utasaidia kushauri namna ya kujipanga na namna ya kufanya kazi ndani ya Serikali ,“Mfumo huu utusaidie kuchakata  kila kitu na kutusaidia kupata matokeo sahihi kwa jambo sahihi na shughuli sahihi, katika kupima utendaji kazi na matokeo yake.” Alifafanua.

Aidha, Alisema pia kwa Mujibu wa Sheria kuna Taasisi ambazo zimekasimiwa majukumu ya kufanya, zinazofanana na Idara hii akitolea mfano Tume ya Taifa ya Mipango, na kusema ni lazima kukutana na Tume hii ya Mipango ili kila mtu afanye kazi kwa kufuata Sheria na Kuzingatia Mifumo iliyopo. “Ni lazima kufanya Tathmini na Ufuatiliaji wa matumizi sahihi ya fedha katika Utekelezaji wa Miradi na utendaji wa shughuli za Serikali, eneo hili kwenye mfumo liwekwe vizuri na liweze kutusaidia,” Alisema.

Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga, Alisema Mamlaka ya Serikali Mtandao (Ega) imefanya wasilisho zuri lenye kutoa muelekeo wa Utendaji wa Shughuli za Serikali Utakaosaidia Ofisi ya Waziri Mukuu kuratibu vizuri shughuli za utendaji Serikalini katika kuripoti na kufanya Tathmini.

Akiongea baada ya wasilisho hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bi. Sakina Mwinyimkuu alisema, Idara yake Itajitahidi kufuatilia kwa Ukaribu ukamilishwaji wa mfumo huo kwa wakati, ili Taasisi za Umma ziweze kushirikishwa na mfumo uweze kufanya kazi kwa wakati kwenye upimaji wa Utendaji wa Shughuli za Serikali.

Awali, Akiongea katika kikao kazi hicho, Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA cha Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Innocent Mboya alisema, Amepokea maelekezo ya kukamilisha mfumo huo ndani ya mwaka huu wa fedha 2023/2024.

 “Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao, tunaahidi kwamba ndani ya hizi wiki mbili, tutakuwa tumeandaa mpango kazi ambao utatupeleka kwenye ramani na utelekelezaji wa mfumo huu, na ndani ya miezi mitatu tutakuwa tumekamilisha mfumo huu kwa kufuata matakwa na maelekezo ya Serikali.”  Alisisitiza

Walisisho hili ni Sehemu ya Utekelezaji wa Maelekezo ya Mhe. Waziri Mhagama aliyoyatoa katika kikao cha mazingativu kilichofanyika Mkoani Arusha Mapema Mwezi huu.

Read More

Monday, August 14, 2023

NAIBU WAZIRI UMMY, ATOA WITO KWA WANANCHI KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII.



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga ametoa rai kwa wananchi, Taasisi na Wizara kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kutembelea vivutio vyetu vya utalii wa ndani.

Wito huo umetolewa wakati Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake, walipotembelea Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro baada ya kutoka katika Mkutano wa Mazingativu Mkoani Arusha.

"Tunamshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa alizozifanya katika sekta ya utalii kupitia filamu ya Royal tour," alibainisha.

"Tumefika Ngorongoro na tumejionea wageni wamefurika wamekuja kujionea vivutio vya utalii." Alisisitiza.

Aidha, alitoa shukrani nyingi Kwa Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kwa kutoa ruhusa ya kutembelea eneo hilo la Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Aliongeza Kwa kusema kuwa, ziara hiyo imeimarisha upendo, uongozi na urafiki kati ya viongozi na watumishi na itaongeza hari ya utendaji kazi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia na (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi amesema, ziara hiyo ni Maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu kwa lengo la kuhakikisha kwamba tuna viongozi wa kusimamia Sera na wanalifahamu eneo la utalii wanaloliratibu Sera zake katika Serikali.

"Tumekuja kuona Mazingira halisi ya Utalii pamoja na Mazingira halisi ya Utendaji kazi, Tumeona Utalii umekuwa kwa kiasi kikubwa wageni ni wengi na sisi kama Serikali tunawajibu wa kuhakikisha tunaweka sera bora za kuwasaidia wageni kuendelea kuja nchini," Alisisitiza

Aliendelea kusema kuwa, eneo la Ngorongoro ni zuri linavutia na Watanzania wana fursa ya kuja kujionea.

Read More

Friday, August 11, 2023

WAKULIMA WATAKIWA KUJIFUNZA MBINU BORA ZA KILIMO KUPITIA MAONESHO YA WAKULIMA NANENANE.


 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Muhagama amesema maonesho ya kilimo ya Nane Nane ni njia pekee ya wakulima kuweza kujifunza mbinu bora za kilimo cha  kisasa na matumizi ya zana bora za kilimo  zinazoweza kuleta  mafanikio katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara nchini.

 

Aliyasema hayo mapema , alilpokuwa katika Shehia ya Dole Kizimbani alipokuwa akifunga Maonesho ya wakulima Nane Nane yaliyo washirikisha wadau kutoka sekta binafsi na wakulima 275 wajasiriamali, taasisi binafsi na za Serikali.

 

“Serikali ya Mapinduzi ya Zanziba chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Hussen Ali Mwinyi inafanya   juhudi kubwa katika kuibadilisha nchi ili kuweza kuleta madiliko katika sekta za uzalishaji wa chakula na kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake” alibainisha.

 

Zanzibar imepiga hatua nzuri na matokeo ya Maonesho yatawezesha wakulima kujifunza vitu vipya na kwenda kuleta mapinduzi ya kilimo ambapo wakulima wataźalisha kwa wingi mazao ya biashara ambayo yataongeza mnyororo wa thamani wa mazao na kuweza kufanya baishara katika soko la ndani na nje ya nchi.

 

Akiongea katika maonesho hayo, katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwangiliaji, Maliasili na Mifugo amesema Maonesho hayo yenye lengo la kutoa elimu ya kilimo bora kwa wakulima yamedumu kwa siku 10 na kugharimu kiasi cha Shilingi  Milioni Mia Tano fedha za kitanzania.

 

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Umwangiliaji, Maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Shaame Khamis ameishukru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano kwa mashirikiano yao na kuyawezesha maonesho ya kilimo kwa mwaka 2023 kufanikiwa

 

Aidha aliwashukuru wadau na wananchi wote waliochangia na kuwaomba wakulima kuzidisha bidii na kuja na mbinu mpya za kilimo katika maonesho yajayo

Read More

WAZIRI MHAGAMA, AHIMIZA KUWEPO MUONGOZO NA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTENDAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, Ameitaka Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali, kuharakisha kutengeneza Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Utendaji wa Shughuli za Serikali Pamoja na kukamilisha na kuzindua haraka Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya nchi utakaotumika na Seriali kwa ujumla, Wizara, Taasisi na maeneo yote ya Utendaji kazi ndani ya Serikali.

 Ameyasema hayo Jijini Arusha, alipofungua Mkutano wa Mazingativu uliyohusisha, Viongozi, watumishi wa Ofisi hiyo Pamoja na Taasisi zake.

Sambamba na hilo, Pamoja na kuonesha Imani wa Mkurugenzi wa Idara hiyo mpya, Waziri Mhagama aliitaka pia idara hiyo kuwa na Ubunifu “Jaribuni kununua mifumo, miundo na taratibu za kufanya ufuatiliaji na Tathmini kutoka kwenye mataifa mengine, ili tuweze kuitangaza Taifa letu kwa kazi hili kuwa tunaweza kufanya vizuri” Alisisitiza Waziri Mhagama.

Aidha, Waziri Mhagama alisema anahitaji kupata taarifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Ofisi yake na Serikali kwa ujumla wa kila robo mwaka ikiwa ni katika kuboresha Eneo hilo.

Akizungumzia kuhusu Uchapishaji wa Nyaraka za Serikali, Waziri Mhagama alisema katika eneo hilo, katika mwaka huu Mpya wa Fedha 2023/2034, Serikali imejiwekea mkakati wa kuongeza Maduhuli na mapato ya yake kupitia Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambapo ujenzi wa Mradi wa Mkakati wa kiwanda kipya cha Mpigachapa Mkuu wa Serikali Umefikia asilimia 97% na “Tumeshaanza kufanya manunuzi ya mashine za kisasa, na tumeshafufua mashine ambazo zilikuwa zimehariba.

Nisisitize Chapa muendeshe kiwanda kwa Ubunifu, jengeni fikra mpya boresheni mifumo miundo na namna ya uhifadhi na uchapaji wa nyaraka za Serikali, nataraji kiwanda hiki kinaweza kikajiuza na kinaweza kikapata soko la nchi za kusini mwa Afrika SADC na katika na Soko la  nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, pale mnalo jambo na kazi kubwa ya kufanya, na mazingativu haya yawasaidie kujiongoza na kupata picha na fikra ambazo zitatuvusha.” Alisisitiza Waziri Mhagama

Akiongea katika Mkutano huo wa Mazingativu, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Dkt Jim Yonazi alisema kuwepo kwa Ofisi hiyo Jijini Arusha katika Mkutano huo  ni kutokana na nia ya Ofisi hiyo kuhakikisha kwamba inatenda majukumu yake kwa umakini na kwa utimilifu ikiwa ni pamoja na Uratibu wa shughuli za Serikali kwa ujumla na kwenye maeneo mengine.

“Tunaweza kujifunza kutoka hapa ndani ya nchi mambo mengi na tukatumia ubunifu na wataalam wa ndani katika utendaji na hakuna mtu anaweza kuwa mbunifu katika mazingira yenye stress, hivyo tunaweza kuweka mazingira wezeshi kwa watumishi na kukuza na kuongeza uelewa katika utendaji.”Alisema

 Kwa kutekeleza Agizo la Mhe. Waziri Mhagama, Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini wa Ofisi Hiyo Bi. Sakina Mwinyimkuu alisema, kikosi kazi kitakaa haraka ili kuweza kuandaa mwongozo wa ufuatiliaji na Tathmini na kuhusiana  na kuwa na Mfumo wa Ufuatiiaji na Tathmini, Mkurugenzi alisema kazi hii inafanyika kwa kushirikiana na Taasisi ya Serikali Mtandao (Ega) na maandalizi ya kujengwa kwa mfumo huo yanatarajiwa kuanza.

 Kwa Upande wake Mpigachapa Mkuu wa Serikali Bw. George Lugome alisema, kama Idara imejipanga hasa kwa watumishi kuhakikisha wanafanya kazi katika ubora wa hali ya juu na kuhakikisha, watumishi watapata mafunzo ya kuendesha mashine mpya za kisasa, kuongeza idadi ya watumishi wenye sifa na ueledi katika endeo hilo la uchapaji “Ili kuweza kuendana na mabadiliko ya teknolojia, ni lazima pia tuchape nyaraka za Serikali kwa kufuata Ubora na kuweka alama za usalama kulingana na teknolojia zilizopo,na tumeshaanza mikakati ya namna gani ya kushirikiana wenzetu wenye utaalam wa masuala ya usalama katika nyaraka mbalimbali.” Alifafanua

Mada mbalimbali  zinawalishwa katika Mkutano huu wa mazingativu ni Matarajio  ya washiriki wengi kuwa, mkutano huo utawasaidia, kuboresha utendaji wa kazi, kujifunza, kupata ubunifu  katika maeneo yao ya kazi, kuongeza bidii zaidi na hali ya utendaji katika kazi unaoendana na sayansi na teknolojia.

 

Read More

Thursday, August 3, 2023

MRADI WA UJENZI WA MJI WA SERIKALI MTUMBA, UMELETA AJIRA NA KUCHANGIA CHACHU YA UKUAJI WA UCHUMI.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, amesema mradi wa Ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba, pamoja na Miradi mingine ya kimkakati imeleta ajira na kuchangia kasi na chachu ya ukuaji wa uchumi hususan katika Jiji la Dodoma.

Ameyasema hayoalipokuwa katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Jengo la Mpigachapa Mkuu wa Serikali; Jengo la Kituo cha Taifa cha Usimamizi na Uratibu wa Maafa, Jengo la Wizara Mipango na Uwekezaji, na jengo la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu).

Waziri Mhagama alisema kuwa, ujenzi wa Mradi hiyo mikubwa ya kimkakati inayoendelea umewezesha vijana wengi kupata ajira katika maeneo hayo, na kujiongezea pato binafsi sambamba na kuchangia ukuajia wa uchumi kutokana na manunuzi ya bidhaa zinazotumika katika mradi hiyo kufanyika katika viwanda vilivyopo nchini.

Alipokuwa katika jengo la Mpigachapa Mkuu wa Serikali, Waziri Mhagama alisema kuwa mradi huo, mkubwa umefikia asilimia tisini na saba (97%) ambapo kiwanda hicho kitakapokamilika kitakuwa na hadhi na sifa ya kuwa ni kiwanda kikubwa kimojawapo cha Serikali,ambapo mashine mpya zimeagizwa na kiwanda hicho  kitafanya kazi za ndani ya nje na nchi za Afrika Mashariki (EAC) pamoja na ukanda wa nchi za  Kusini mwa Afrika (SADC).

"Sisi tumejipanga kwa matumizi ya ndani na nje pia, nimefarijika kuona ujenzi kwa awamu, hii ya kwanza umefikia hatua kubwa, na ujenzi wa Ofisi umeanza na unaenda kwa kasi." Alisisitiza Waziri Mhagama.

Alipokuwa katika kituo cha Taifa cha Uratibu na Usimamizi wa Maafa Mhe. Mhagama alisema, ujenzi wa awamu ya kwanza ya kituo hicho pia umekamilika kwa Asilimia tisini na nne (94%) na kufafanua kuwa maghala mawili makubwa na Ofisi za Watumishi zimeshakamilika.

"Tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba katika kituo hicho nchi inafikia malengo ya kitaifa na Maono na maelekezo ya Mhe. Rais, Dkt, Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa Ujumla" Alibainisha Waziri Mhagama.

Waziri Mhagama  Alisema kuwa katika kituo  hicho cha Maafa kutakuwa na vitu vingine vingi ambavyo vinajenga dhana nzima ya uratibu na usimamizi wa Maafa, ambapo kutakuwa na kiwanja ambacho, kitakuwa kinasaidia utuaji na uondokaji wa Helkopta ambazo zitaweza kwenda kwenye shughuli za maafa, kutakuwa na kituo cha tiba kitakachosaidia dharura za maafa hasa katika magonjwa ya milipuko na kitatumika pia katika masuala ya utafiti na tiba na kituo cha mafunzo kwa wataalam ambao watashughulika na usimamizi na uratibu huo wa dharura.

Waziri Mhagama pia alitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) pamoja na Jengo la Wizara ya Mipango na uwekezaji katika Mji wa Serikali Mtumba, na kuagiza kuongezeka kwa kazi ya ujenzi ili majengo hayo yaweze kukabidhiwa kwa wakati.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi Hiyo Bw. Anderson Mutatembwa, alisema Ofisi hiyo itasimamia kikamilifu maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri Mhagama, ikiwa ni pamoja na kuzifanyia kazi chagamoto zilizojitokeza na kuhakikisha zinatatuliwa kwa wakati.

Awali akizungumza katika ziara hiyo, Mwakilishi na Msimamizi Mkuu wa miradi ya Ujenzi kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi Mhandisi Anania Saudeni, Alikiri kuyapokea maagizo ya Mhe. Waziri Mhagama na kuyatekeleza kwa wakati, kimkataba na kukamilika katika ubora kulingana na maelekezo na kuhakikisha kazi zinafanyika usiku na Mchana na kuongeza  nguvu kazi ya kutosha na usimamizi madhubuti.

 

Read More

Thursday, July 27, 2023

Taasisi zinazotekeleza programu ya kuendeleza kilimo na uvuvi (AFDP) zatakiwa kufanya kazi kwa malengo

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na maswala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amezitaka taasisi zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kufanya kazi kwa malengo na kwa wakati ili kutekeleza mpango kazi ambao umewekwa katika programu hiyo.

Kauli hiyo ameitoa , alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kutembelea Shirika la Uvuvi la Nchini (TAFICO) Jijini Dar es Salaam, ambapo alisema (TAFICO) ni Moja ya taasisi za Serikali iliyopewa majukumu katika programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi, yenye lengo kubwa la kuongeza tija na faida katika mazao yatokanayo na Kilimo na uvuvi ikiwa ni pamoja na ukuzaji wa  mazao yatokanayo na viumbe maji kupitia teknolojia ya kisasa.

Akizitaja Wizara na Tasisi zinazotekeleza Programu hizo chini ya Uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu kuwa  ni pamoja na  Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, (TAFICO) na  (ZAFICO) Waziri Mhagama alitaka Taasisi hizo kuzingatia ubora, na thamani ya fedha katika mradi mzima “Natarajia kila senti itakayowekezwa  katika mradi huu itaenda kujibu na kuleta matokeo halisi tena yakiwa chanya na yatakayosaidia nchi yetu kusonga mbele na kupata maendeleo endelevu kwa wananchi na Taifa kwa Ujumla, Alisisita.”

Akizungumza katika Ziara hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi alisema, Serikali Imeweka mkazo katika kuhakikisha kwamba Nchi inanufaika na Rasilimali maji hasa katika eneo la uvuvi, kupitia mradi wa (AFDP) hivyo “Sisi kama watendaji tupo tayari kuweka msisitizo na kuhahakisha kwamba haya yote yanakamilika kwa wakati na kuleta Tija kwa Taifa letu.” Alisisitiza Dkt. Yonazi

 Kwa Upande wake Afisa Mtendaji mkuu wa Shirika hilo Bw. Dennis Simba alisema kuwa, (TAFICO) imejipanga na ipo tayari katika kuhakikisha kwamba inafungua njia ya kwenda katika uvuvi wa Bahari kuu na mnyororo mzima wa thamani, na kuongeza kuwa miradi kumi na moja (11) iliopo katika programu hii itatekelezwa kwa wakati na kwani Serikali imeonesha nia ya dhati ya kufungua uchumi wa Bluu.

Awali, Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya (TAFICO) Dkt. Eliamini Kasembe, alisema Serikali ya Awamu ya Sita imeamua kufufua Shirika hili kwani lina manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa kwa Ujumla, “Nia hii thabiti inaweza kufikia malengo ya uanzishwaji wa Shirika hili ikiwa ni pamoja na kutoa Ajira na kuchangia katika kuinua uchumi wa Taifa hili.” Alibainisha.

 

Read More

Wednesday, July 19, 2023

WAZIRI MHAGAMA ATEMBELEA MNARA WA SHUJAA AHAMAD MZEE

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama ametembelea Mnara wa Shujaa UD 5826 L/CPL AHAMAD MZEE katika kata ya Kitaya Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba Mkoani Mtwara.

Waziri ametembelea mnara huo Nanyamba Mkoani Mtwara tarehe 17/07/2023 siku chache kuelekea siku ya Mashujaa ya kitaifa inayotarajiwa kufanyika tarehe 25/08/2023 katika Uwanja wa Mashujaa uliopo Mji wa serikali Mtumba Jijijni Dodoma.

Shujaa Ahmad Mzee alikuwa Muajiriwa wa Jeshi la Wananchi alipokuwa akitekeleza majukumu yake ya kikazi akiwa na umri wa Miaka 21 alipelekwa Mpakani mwa kijiji cha Kitaya akiwa na jukumu la Ulinzi wa Taifa la Tanzania katika nafasi ya Mpiga mzinga wa kuangusha ndege.

Katika kutekeleza Majukumu yake tarehe 14 April 1972 wakati ndege za Mreno zikitokea Msumbiji Helicopter na Jet Fighters zilipiga mabomu kijiji cha Kitaya na katika Mapambano hayo Shujaa Ahmad Mzee aliangusha Jet Fighter mbili, moja ilianguka ardhi ya Tanzania Mto Ruvuma na Nyingine ilianguka ardhi ya Msumbiji.

Kwenye Mapambano hayo Shujaa Ahamad Mzee alijeruhiwa baada ya Kupigwa na fighter na alichukuliwa na kukimbizwa Mtwara Ligula Hospitali na huko ndiko alikofia.

Read More

Tuesday, July 18, 2023

SERIKALI YATOA MSAADA WA KIBINADAMU, NANYAMBA NA TANDAHIMBA

 


Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) imetoa misaada ya kibinadamu kwa kaya 184 za kata ya Kitaya Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba na kaya 160 kwa kata ya Michenjele Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba.

Zoezi hilo limeongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe, Jenista Mhagama Mkoani Mtwara, amesema kwa kutumia sheria no 6 iliyotungwa mwaka 2022 ya usimamizi wa maafa, kazi yetu ni kufanya tathimini na kutoa Mkono wa pole kwenye Majanga yanayohusu binadamu mahali popote.

“Nitoe wito kila yanapotokea majanga na maafa, kwanza liwe jukumu letu kufarijiana kwa karibu; na kutoa taarifa za dalili za majanga yanapotokea, na kuangalia ni mambo gani ya msingi yafanyike ili kurudisha hali katika utaratibu wa kawaida” alihimiza.

Waziri Mhagama amesema, tumepokea tathimini iliyowakilishwa ikionesha madhara yaliyojitokeza kwa wananchi katika eneo hili katika maeneo kadha kwa kadha katika makazi, chakula,na  nyenzo za kufanyia shughuli za kiuchumi

Amefafanua kwamba Serikali imekuja kutoa Mkono ili tuweze kushirikiana na nyie katika kujibadilishia hali katika kipindi hiki chote, “nikweli Serikali imeendelea kuwa na nyie kwa nguvu kubwa na ya ziada zaidi,” alisema Mhe. Waziri

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassani kwa kutushika Mkono wananchi yanapotokea majanga ya kibindamu, yanapotokea mafuriko, na vinapotokea vimbunga, tunajisikia faraja.

Tumepokea magodoro 190 tumepokea ndoo kubwa 380, na ndoo kubwa za lita ishirini 190, tumepokea blanketi za watoto 190 na blanketi za watu wazima 380 na mikeka 380 na mabati 5700 na kaya zinazostahiki ni 184 zilizoordheshwa kwa sasa katika Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba.

Kanali Ahmedi ameongeza kusema Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba Ilipokea vifaa vya msaada wa kibinadamu kwa waathirika 160, tuna mabati 4800 kuna magodoro 160, mikeka 320 na mablanketi 320, ndoo kubwa za lita ishirini 320 na tayari zimeundwa kamati mbalimbali kwa ajili ya kuhakiki

Naye Mbunge wa Nanyamba Mhe. Abdallah Chikota amesema Tunashukuru kwa msaada wa kibinadamu na kipekee nimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa sababu asiyeshukuru kwa moja hata kumi hawezi kushukuru.

 

Read More

Saturday, July 15, 2023

KAMPENI YA KILL CHALLENGE 2023 KUCHAGIZA JITIHADA ZA KUZIFIKIA SIFURI TATU DHIDI YA VVU NA UKIMWI

 


Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete amepongeza kampeni maalum ya kuchangia fedha katika utekelezaji wa afua za masuala ya  UKIMWI nchini ya Kilimanjaro HIV  & AIDS  Challenge 2023 kwa kuzingatia mchango wake katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI nchini.

Ametoa pongezi hizo mapema wakati wa hafla ya kuwaaga wapanda Mlima Kilimanjaro na waendesha baiskeli kuzunguka mlima huo katika lango la Machame Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya kampeni hiyo kwa mwaka huu.

Mhe. Dkt. Kikwete alisema kampeni hiyo ina mchango mkubwa katika kufikia Kampeni ya Kitaifa ya kufikia malengo ya SIFURI TATU, yaani Sifuri ya maambukizo mapya ya Virusi vya UKIMWI, Sifuri ya Unyanyapaa na Ubaguzi kwa watu wanaoishi na VVU na Sifuri ya vifo vitokanavyo na UKIMWI kwa kuzingatia mchango wa kifedha unaopatikana na kusaidia utekelezaji wa afua za UKIMWI nchini.

“Kazi iliyofanywa na ndugu zetu GGM wameonesha njia wanastahili kuungwa mkono, hivyo basi, niziombe Jumuiya za wafanyabiashara, makampuni na sekta binafsi pamoja na Watanzania wote kwa ujumla, kuunga mkono kampeni ya Kill Challenge kwa miaka ijayo,”alisema

Akieleza uzoefu wa ushiriki wake katika kampeni hiyo alisema ni jambo muhimu kwa kuzingatia mchango wa tukio hilo katika masuala ya Afua za UKIMWI na linamatokeo mengi mazuri ikiwemo la kujijenga kiafya, kuchochea hali ya uzalendo kwa nchi yetu pamoja na kuimarisha mahusiano kati yetu na mataifa mengine kwani wapo washiriki wa mataifa mengine ikiwemo Afrika Kusini.

“Binafsi ninafarijika kuendelea kuwa sehemu ya mafanikio haya, kwani leo ninashiriki kwa mara ya tatu tukio kama hili adhimu ambapo niliwahi kushiriki pia mara ya kwanza tarehe 2 Mei, 2014 na tarehe 21 Julai, 2016, hivyo naipongeza TACAIDS pamoja na Geita Gold Mining Limited ambao ndio waanzilishi na waratibu wa program hii ya Kilimanjaro Challenge Against HIV and AIDS, ni jambo la kuungwa mkono na kupongezwa, hongereni sana,”alisema.

Aidha aliipongea  Serikali katika kupambana na maambuzi ya VVU na UKIMWI ambapo kupitia program hii wadau wanapata fursa kuchangia fedha kwa ajili ya kusaidia jitihada za Serikali na wananchi katika mapambano haya.

“Kwa namna ya kipekee kabisa naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ilivyojipanga kuongeza nguvu ya mapambano haya kwa kuendelea kutenga fedha nyingi  kwa ajili ya utekelezaji wa afua za masuala ya UKIMWI Nchini.

Alitumia nafasi hiyo kuwaasa washiriki kutimiza malengo kwa kushikamana, upendo na kuwa na umoja katika zoezi hilo ili kukamilika kwa namna lilivyokusudiwa.

“Washiriki wote 61 ikiwemo wapanda mlima (Climbers) thelathini na sita na wanaouzunguka kwa baiskeli ishirini na tano mmeonesha ushujaa wa hali ya juu kwa kujitoa kwenu na kuwa tayari kupanda mlima na wengine kuendesha baiskeli mmefanya jambo kubwa na zuri la kuigwa,”.

Aliongezea kuwa, kushiriki zoezi hili ambalo si jepesi imedhihirisha kuwa bado ipo dhamira ya dhati miongoni mwa Watanzania na wadau ya kuendeleza mapambano haya, na yatafanikiwa iwapo pataendelea kuwa na dhamira ya dhati kwa kila mmoja wetu na ushirikiano wa pamoja kufikia ushindi unaoutarajia.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga alipongeza namna zoezi lilivyoratibiwa na kutoa wito kwa washiriki wote kuendelea kujitoa kwa kadiri inavyobidi huku akimshukuru Rais Mtaafu Dkt. Jakaya Kikwete kwa kukubali kuwa mgeni rasmi wa program hiyo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano na wadau mbalimbali wanaoshughulika na afua za masuala ya VVU na UKIMWI nchini.

Awali akieleza kuhusu kampeni hiyo Kaimu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Nchini Dkt. Jerome Kamwela alisema Tanzania imeendelea kuwa na mikakati madhubuti katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kueleza takwimu zinaonesha maambukizi yamepungua kufikia asilimia 4.7 ambapo ni ishara kuwa jamii imekuwa na mwamko na uelewa mpana kuhusu masuala haya.

 

Read More

Sunday, July 2, 2023

WAZIRI MHAGAMA AKABIDHIWA KIPANDE CHA SEHEMU YA UJENZI WA UWANJA WA MASHUJAA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, amekabidhiwa kipande cha sehemu ya ujenzi wa uwanja wa mashujaa, katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma mapema Julai 2, 2023.

Ujenzi huo unaotekelezwa na kampuni ya SUMA JKT,Umekamilisha kipande cha  sehemu ya kwanza ya ujenzi wa uwanja wa Gwaride ambao unategemewa kutumika katika Maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Mashujaa.

Akiwa kiwanjani hapo Waziri Mhagama alisema, Serikali pamoja na kuhamia Dodoma imejenga miundombinu yenye hadhi ya makao Mkuu ya Serikali, na jamii inashuhudia majengo ya Serikali makubwa na miondombinu mingine ikiendelea kukamilishwa.

Akiongelea Ujenzi wa Uwanja huo, Waziri Mhagama alisema, ujenzi utakapo kamilika utakuwa ni wa mfano Barani Afrika.

"Eneo hili ni sehemu ya kwanza ya ujenzi wa eneo la maadhimisho ya uwanja wa mashujaa, (Parade Ground) ambayo itakuwa na Mnara wa Mashujaa, wenye ubora na viwango vya juu kabisa.” Alieleza Mhe. Mhagama

Aliendelea kusema kuwa, awamu ya pili itakuwa na bustani kubwa, ambayo itakuwa na mvuto wa aina yake, na tayari Taasisi mbali mbali za Serikali zimeonesha nia ya kuwekeza na kushirikiana, kuhakikisha kutakuwa na bustani hiyo yenye migahawa, viwanja vya michezo na burudani mbalimbali, ambazo zitakuwa katika eneo hilo ambao leo amekabidhiwa kipande kidogo tuu kama sehemu ya kwanza ya ujenzi.

Alifafanua zaidi kuwa, sehemu ya tatu itahusisha ujenzi wa mnara mrefu wa zaidi mita 110 ambao utakuwa mnara wa kwanza Barani Afrika, ambao utakuwa ni kivutio kwa watalii na kuongeza pato la Taifa.

Kwa Upande Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Dkt. Jim Yonazi alisema uwanja huo utakapokamilika utaongeza uzuri na ubora wa Jiji la Dodoma na Serikali itahakikisha kwamba mnara pamoja na uwanja wake unakuwa wa kupendeza na kuwa na mvuto wa kipekee huku akizishuruku sekta nyingine zilizoonesha ushirikiano katika utekelezaji wa ujenzi huo na kuhakikisha miundombinu muhimu inapatikana kwa wakati.

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo, Katibu wa Kikosi kazi cha Taifa cha kuratibu Serikali kuhamia Dodoma Bw. Meshach Bandawe, alisema ujenzi huo umezingatia suala la mpango kabambe wa ujenzi wa Mji wa Serikali na kazi ya ubunifu wa awali ilifanywa kwa kina na wataalam kutoka chuo kikuu cha Ardhi, TPA, NHC  na SUMA JKT.

Naye Mwakilishi wa kampuni ya Ujenzi kutoka SUMA JKT kanda ya Kati Meja Samweli Jambo, alisema ujenzi huo umefuata taratibu zote za upimaji na viwango.

 “Tulifanya kazi usiku na mchana kuhakikicha tunatekeleza maelekezo ya Mhe. Waziri ya kukabidhi kipande hiki kwa wakati.” Alieleza Samweli

Read More

Tuesday, June 27, 2023

MUONGOZO WA UTEKELEZAJI WA DHANA YA AFYA MOJA WAJADILIWA

Mratibu wa Maafa kutoka Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Mololo Noah  akiongoza kikao cha Kuthibitisha Muongozo wa Utekelezaji wa  dhana ya Afya Moja. Kikao hiki kilihusisha washiriki kutoka sekta ya Afya, Mifugo, Mazingira, Wanyamapori, BAKITA na mashirika ya Umoja wa Kimataifa. Kikao kilifanyika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya regency  Mkoani Singida

Read More

Saturday, June 24, 2023

KATIBU MKUU DKT. YONAZI AHIMIZA WATUMISHI KUWA NA TABIA YA KUPIMA AFYA .

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu amewakumbusha  watumishi wa ofisi yake kuwa na tabia ya kupima afya zao mara kwa mara ili kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa lengo la kuongeza ufanisi na kuyafikia malengo ya Serikali.

Ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao chake na watumishi wa ofisi hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Utumishi wa Umma.

Katibu Mkuu huyo amesema upo umuhimu wa kujizoeza kupima afya hususan kwa magonjwa sugu yasiyoambuiza kwani yameendelea kuwa changamoto hasa kwa watu wenye umri mkubwa.

“Ni muhimu tumepata fursa ya kukumbushwa kupima afya zetu, hii ni changamoto inayotukabili, hivyo ni muhimu kuzingatia ushauri wa afya na masharti ya namna ya kuboresha masuala yanayohusu afya zetu, “alisema Dkt. Yonazi

Pamoja na hilo aliwakumbusha watumishi kuwa na tabia ya kufanya mazoezi ili kuendelea kutekeleza majukumu wakiwa wenye afya na kuwa na matokeo chanya.

Aidha aliutumia mkutano huo kuwaasa watumishi hao kuongeza ubunifu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku huku wakizingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

“Mkutano huu ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo tulianza kuiadhimisha tarehe 16 Juni, 2023 na leo ndio kilele.Wiki hii tunaitumia kutafakari namna tunavyotekeleza majukumu yetu kwa kipindi kilichopita, kujadili namna ya kutoa huduma bora kwa jamii ya Watanzania, kujifunza mbinu mpya na kuibua changamoto zinazotukabili katika kutekeleza majukumu yetu kwa lengo la kuzitafutia ufumbuzi,”alisisitiza

Pia aliwahimiza Watumishi kuendela kufanya kazi kwa upendo na kuheshimiana kwani kwa kufanya hivyo wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa amani.

“Ni falsafa yangu kuona watu ninaowaongoza wanafanya kazi kwa upendo na kushirikiana, ni lazima kuhusiana na kuwa na mashirikiano mazuri, napenda kufanya kazi na watu wanaoheshimiana na wenye amani siamini kama mtu anaweza akafiri vizuri iwapo hana amani ndani”alisisitiza Dkt. Yonazi

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti ya TUGHE wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Numpe Mwambenja alipongeza uwepo wa mkutano huo huku akieleza kuwa ni nyenzo muhimu kwa kuongeza motisha kwa watumishi wa umma, na imeonesha kujali na kuendelea kuleta umoja kazini.

“Mkutano huu umekuja wakati sahihi na muda sahihi, tunawapongeza viongozi wetu kuendelea kutuweka pamoja na kutukumbusha kupendana, kushirikiana na kuishi kwa amani, hili tumelithamini sana na tunaahidi hatuta waangusha tutachapa kazi na kuendele kuhudumia jamii ya Watanzania na kuitumikia nchi yetu kwa ujumla,”alisema Numpe.

 

Read More

Tuesday, June 13, 2023

MEJA JENERALI MBUGE “TUIMARISHE USHIRIKIANO KUKABILI MAJANGA”

 


Serikali  kupitia  Ofisi  ya Waziri Mkuu imesema itaendelea kuimarisha ushirikiano na sekta mbalimbali katika kukabiliana na maafa ili kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama.

Kauli hiyo imetolewa   Mkoani Singida na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja  Jenerali  Charles Mbuge  wakati akifungua kikao kazi cha Watalam waliokutana kwa lengo la Kuhuisha na Kutafsiri Mwongozo wa Utekelezaji wa Dhana ya Afya Moja.

Meja Jenerali Mbuge amesema kumekuwa na ongezeko kubwa la mwingiliano wa binadamu, wanyama na mazingira ambao  husababisha  kutokea kwa magonjwa mbalimbali yanayotoka kwa wanyama na kwenda kwa binadamu hivyo ipo haja ya   kuwepo kwa ushirikiano wa sekta mbalimbali katika kujiandaa, kuzuia na kukabiliana  na majanga hayo.

“Tunahuisha mwongozo huu kwa sababu ya mabadiliko ya sheria na kanuni za usimamizi wa Maafa.   Mwongozo huu ni muhimu katika kurahisisha ushirikiano wa kisekta ili kujenga na kuimarisha ustahimilivu wa jamii dhidi ya milipuko ya magonjwa na dharura zingine zenye madhara kwa afya ya binadamu, wanyama na mazingira,” Amesema Meja Jenerali Mbuge.

Ameongeza kuwa kwa mujibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa husisitiza yakiwemo  Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO),  Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Wanyama (WOAH) na Programu ya Mazingira ya Umoja wa Mataifa (UNEP) kwa pamoja husisitiza ushirikiano wa sekta mbalimbali ili  kuwa na mikakati na sera za  pamoja katika kuimarisha afya ya wanadamu, wanyama na mazingira.

“Ili kutekeleza dhana ya Afya moja, ni muhimu kuwa na miongozo mbalimbali ili kurahishisha uratibu na utendaji katika ngazi zote. Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru FAO ambao walianzisha mchakato wa kutengeneza mwongozo huu ambao katika kikao hiki utauhuishwa na kutafsiriwa,” Ameeleza.

Aidha amebainisha kuwa   Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa ina  wajibu wa kuratibu utekelezaji wa dhana ya  Afya Moja kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Menejimenti ya Maafa ya 2004, Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya Mwaka 2022 na kanuni zake za mwaka 2022 pamoja na Mkakati wa Afya Moja 2022-2027.

Read More

Thursday, May 25, 2023

SERIKALI KUZINGATIA MAFUNGU MAALUM YA FEDHA KWA WAVIU KATIKA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2023/24



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, amesema utekelezaji wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/2024 pamoja na vipaombele vingine inazingatia pia mafungu ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) katika kila Wizara na Taasisi.

Ameyasema hayo mapema  katika Ukumbi wa Waziri Mkuu Bungeni Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA).

Mhe. Mhagama, aliendelea kusema kuwa hii ni namna ambavyo Serikali kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imedhamiria kwa dhati kusaidia utekelezaji wa Afua za masuala ya UKIMWI nchini, kwa kuzingatia maeneo muhimu ikiwemo masuala ya lishe bora, dawa za kupunguza makali ya virusi na kuhakikisha mambo mengine yanayochangia ustawi wao kupatikana.

Akizungumzia suala la Sera ya Taifa ya UKIMWI ya mwaka 2001 Mhe. Mhagama alisema kuwa kuna kila Sababu ya Sera hiyo kufanyiwa mapitio na maboresho kwani ni ya muda mrefu na kuona, namna gani sekta zote zinaweza kushiriki katika suala hili ili kuweza kuyafikia malengo ya dunia ya kupunguza vifo, maambukizi na unyanyapaa ifikikapo 2030.” Niwahakikishie kwamba sisi kama Serikali tunaweza kusimamia kufikia malengo haya ya dunia”Alisisitiza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa NACOPHA Mwalimu Leticia Mourice alimpongeza Mhe. Waziri Jenista kwa uteuzi wake na pia kumshukuru kwa juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya UKIMWI, aidha aligusia kuhusiana na maandalizi ya Mdahalo wa Kitaifa kuhusu uhimilivu wa mwitikio wa jamii katika mwitikio wa Taifa wa UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

Sambamba na hilo alizungumzia kuhusu, uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Taifa, ambao unalenga utekelezaji wa NMSF5 (Mpango Mkakati wa Tano wa Kitaifa wa Kudhibiti UKIMWI) na alisisitizia umuhimu wa ushirikiano, katika kujenga mwitikio wa kijamii katika mapambano dhidi ya UKIMWI, akitolea mfano maeneo kadhaa muhimu ikiwemo Uhimilivu wa Kisera.

Awali, akizungumza katika mkutano huo Afisa Mtendaji Mkuu wa NACOPHA Bw. Deogratius Rutatwa, aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuipongeza Serikali ya watu wa Marekeni (PEPFAR/USAID) kwa mchango wake mkubwa katika kufanikisha shughuli za mwitikio wa UKIMWI za NACOPHA na wadau wote wanaotekeleza suala la UKIMWI na kusema kuwa kuna haja ya kuwepo kwa mkakati endelevu na uhimilivu.

Read More

Wednesday, May 17, 2023

WAZIRI MHAGAMA KATIKA KIKAO CHA BUNGE CHA 27


Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Dkt Selemani Jafo wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa 11 wa Bunge la Bajeti linaloendelea Jijini Dodoma.

Read More

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA KATIKA KIKAO CHA BUNGE CHA 27


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja Wakati wa Bunge la 12 Mkutano 11 wa Bunge la Bajeti linaloendelea Jijini Dodoma.

Read More

Saturday, May 13, 2023

WILAYA YA IGUNGA KUNUFAIKA NA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI. AFDP



Halmashauri ya Wilaya ya IGUNGA iliyopo Mkoani Tabora imetajwa kuwa miongoni mwa Wilaya nchini itakayonufaika na programu ya kuendeleza Kilimo na uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa kuendeleza Kilimo IFAD.

Hayo yameelezwa mapema leo na Mratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Bw. Salim Mwinjaka alipokuwa na mazungumzo na kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya IGUNGA, wataalam pamoja na ujumbe kutoka AFDP ulipokuwa katika ziara ya kikazi ya kutembelea maeneo yatakayoteleza programu hiyo.

Bw. Mwinjaka alisema kuwa Wilaya ya IGUNGA ni miongoni mwa Wilaya itakayopata fedha za utekelezaji wa  programu hiyo kupitia wizara ya Kilimo Kwa mwaka wa fedha 2324, "na Kwa mwaka wa fedha unaofuata Kwa kuzingatia maandali ya Mpango wa mapato na matumizi ya bajeti kuwekwa vizuri, fedha hizo zitakuja Moja Kwa Moja katika Wilaya husika."Alifafanua

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa ushirika wa umoja wa wafugaji wa samaki Igunga (UWASAI) uliopo katika kata ya Mwamapuli Bw. Francis Mgaragu, ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya Uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Kwa kuwaletea mradi huo "mradi tumeupokea Kwa mikono miwili tunahaidi ushirikiano, na tunahaidi kuwa tutatekeleza mradi Kwa malengo yaliyokusudiwa." Alisema

Read More

Friday, May 12, 2023

MRADI WA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI KUTATUA CHANGAMOTO ZA UFUGAJI VIUMBEMAJI CHATO.

 


Imeelezwa kuwa Mradi wa kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) unakwenda kutatua changamoto wanazokumbana nazo wafugaji VIUMBEMAJI katika kituo Cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato,mkoani Geita.

Hayo yameelezwa Leo na Dkt. Nazaeli Madala, Mkurugenzi wa ukuzaji viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Dkt. amesema kituo Cha Rubambagwe kipo katika UJENZI ambapo, Nia na madhuni ya kituo hiki ni kuhamasisha, kuendeleza na kusimamia ukuzaji viumbe Maji,Kwa maana Ufugaji wa samaki kwa mabwawa na vizimba katika ukanda wa ziwa Victoria.

Alisema kuwa, kituo kitakwenda kutoa mafunzo ya utengenezaji wa chakula cha samaki,Ufugaji na ulishaji sahihi wa samaki, wafugaji watafundishwa pia namna ya kutengeneza chakula Cha samaki Kwa kutumia malighafi za asili, kutakuwa na majengo ambayo yatawezesha wafugaji wanaotoka mbali kukaa hapo wakati wa mafunzo, sambamba na hilo, kutakuwa na kiwanda kidogo Cha kutengeneza chakula cha samaki.

Aliongeza kusema kuwa kituo pia kitazalisha vifaranga vya samaki ili kuweza kutatua changamoto ambazo wafugaji wanakutana nazo "kutakuwa na kitotoleshi ambacho kitakuwa na uwezo mkubwa sana wa kuzalisha vifaranga ambavyo vitakwenda kuwezesha vitotoleshi vya sekta binafsi kupata wazazi "Alifafanua

Akiongea na ujumbe huo, Bi. Sifa Buguni  mmoja wa wafugaji wa samaki Rubambagwe Chato alibainisha changamoto kubwa mbili  walizokumbana nazo kabla ya mradi huu kukamilika kuwa ni pamoja na uhaba wa upatikanaji wa mbegu na chakula cha kulisha samaki.

Awali, ujumbe huu wa IFAD ulifika ofisini Kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Prof. Godius Kahyarara ambapo alisema ni wakati sasa kwa wakazi wa Mkoa wa Geita kujikita katika katika shughuli za kilimo na ufugaji wa viumbemaji na kwa uwekezaji wa uhakika kuweza kuwekeza katika sekta hizo kama wanavyowekeza katika sekta ya madini.

Ujumbe kutoka IFAD, wataalam na Mratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bw. Salim Mwinjaka wapo katika ziara ya ukaguzi wa maeneo yanayotekelezwa mradi huo

 

Read More

Thursday, May 11, 2023

PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI ITACHANGIA KULETA UHAKIKA NA USALAMA WA CHAKULA NCHINI - DKT. BATILDA

 


Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani amesema, Programu ya AFDP itasaidia upatikanaji wa mbegu za mazao zinazoweza kuhimili na kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi. Aidha mkuu huyo wa mkoa ameeleza kuwa Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi nchini AFDP italeta uhakika wa usalama wa Chakula upatikanaji wa ajira katika maeneo inapotekelezwa programu hiyo, pamoja na kuinua pato la mwananchi mmoja mmoja na Taifa Kwa ujumla.

Mheshimiwa Balozi Dkt. Batilda ameyasema hayo mapema alipokutana na ujumbe kutoka IFAD walipokuwa katika ziara ya Usimamizi wa utekelezaji wa programu hiyo ya kuendeleza Kilimo na uvuvi (AFDP).

Akielezea kuhusu sekta za kilimo na ufugaji Mheshimiwa Balozi Dkt Batilda ameelezakuwa mkoa wa Tabora ni maarufu kwa kilimo Cha zao la Tumbaku na Ufugaji wa nyuki.

Kwa Upande wake mtaalamu wa Tathmini na Ufuatiliaji wa programu hiyo Bw. Bernard Ulaya  akielezea utekelezaji wa Programu hiyo mkoani Tabora, programu hiyo ameeleza kuwa programu hiyo inaendeleza kituo cha kuzalisha vifaranga vya samaki kilichopo Mwamapuli wilayani Igunga, shamba la kuzalisha mbegu za mazao ya kilimo la Wakala wa Mbegu (ASA) )lililoko Kilimi katika wilaya ya Nzega, na Wilaya ya  Uyui itapewa nafasi ya kuendeleza mnyororo ya Alizeti, Mahindi na maharage.

Read More

Thursday, May 4, 2023

VIONGOZI WATAKIWA KUSIMAMIA KWA WELEDI UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA KILIMO NA UVUVI

KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewataka watendaji wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri kusimamia vizuri utekelezaji wa Programu ya Kilimo na Uvuvi katika maeneo yao kwani ni sekta muhimu katika uchangiaji wa uchumi na usalama wa chakula nchini.

Ameyasema hayo mapema leo Jijini Dodoma, katika warsha ya  utambulisho na uelewa  wa Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi kwa watendaji wa Mikoa na Halmashauri.

Dkt. Yonazi amesema kuwa Serikali imeona kuna ulazima wa kuwepo kwa usalama wa mbegu katika kilimo hivyo kupitia Wakala wa Mbegu za Kilimo nchini ASA imeweza kuwekeza mbegu kwa wingi ili kuyafikia maono ya serikali.

“Serikali imeendelea kusimamia uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora ambapo hadi kufikia Aprili 2023, jumla ya tani 49,962.35 za mbegu bora zimepatikana sawa na asilimia 26.68 ya mahitaji ya tani 187,197 kwa mwaka,”alisema Dkt. Yonazi.

 

Aliongezea kuwa, serikali imejitahidi kuweka nguvu katika upatikanaji wa mbegu hizo ili  kuhakikisha uwepo wa usalama wa chakula nchini, na kwa upande wa sekta ya uvuvi imehakikisha kunakuwa na manufaa ya rasilimali zilizopo katika sekta hiyo kwani bado hazijatumika vizuri.

Aliongeza kwa kusema kuwa Serikali ina mpango wa kununua meli zitakazotumika katika uvuvi wa kina kirefu cha bahari na hivyo kuweza kuongeza lishe na hatimaye nchi kunufaiika na rasilimali za uvuvi.

Aliendelea kufafanua kuwa, Programu hii pia, itahusisha ujenzi, upanuzi na ukarabati wa miundombinu mingine ikiwa ni pamoja na upanuzi wa vituo vya uzalishaji wa vifaranga vya samaki cha Kingolwira Morogoro.

“Lazima tushirikishe wadau ili tupeleke elimu ya kuweza kuzalisha vifaranga na kujenga mabwawa, natoa msisitizo kwa viongozi wa mkoa kuwa kuna jukumu la usimamizi, tuhakikishe tunasimamia vizuri mradi huu, kushauri na kuutekeleza kwa wakati.” Alisisitiza Dkt. Yonazi

Awali, akiongea wakati wa Ufunguzi wa Warsha hiyo Bw. Paul Sangawe Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, alisema lengo la programu hii kwa upande wa sekta ya uvuvi, ni kuendeleza ufugaji wa viumbe maji pamoja na kuanza uvuvi wa bahari kuu.

“Tunatazamia katika program hii meli zitanunuliwa kwa matumizi ya pande zote mbili za Muungano na kuwezesha nchi yetu kwa mara ya kwanza kufanya uvuvi katika bahari kuu ili kuweza kutumia rasilimali tulizonazo kwa ufanisi, lakini vile vile uzalishaji wa mbegu pamoja na usambazaji, na kuhakikisha fedha ambazo za mkopo ambazo tumepewa kutoka shirika la IFAD takribani dola 58.8 milioni,zinatumika kwa ufanisi na kuleta tija katika utelezaji wa program hii.” Alisisitiza

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchumi na Uzalishaji toka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Afisa Kilimo Mkuu Dkt. Rehema Mdendemi amesema programu hii ya maendeleo ya kilimo na uvuvi itaenda kuboresha maisha ya wakulima na wavuvi , na kujitosheleza kwa usalama wa chakula na kuleta ajira hivyo program hii ni ya muhimu kwa serikali na wanachi kwa ujumla.

Read More

Wednesday, May 3, 2023

NEC YAANZA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU 2025


 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi ipo katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa kuzingatia utaratibu na vigezo.

Hayo  yamesemwa leo  Bungeni Jijini Dodoma na Naibu  Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga wakati akijibu  maswali  ya baadhi ya  wabunge walioomba majimbo yao  yagawanywe.

Amesema muda utakapofika, Tume itatoa tangazo rasmi kwa wadau wote wa uchaguzi juu ya kuanza kwa machakato wa ugawaji wa majimbo ili wadau wawasilishe maoni na maombi yao na hivyo kushughulikiwa kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa kikatiba.

Mhe. Ummy amesema majimbo mengi yameomba kugawanywa lakini mambo yanayotazamwa ni pamoja na ukubwa wa ukumbi wa jimbo, idadi ya wabunge wa viti maalumu na jiongrafia za maeneo yaliyoomba kugawanywa.

Read More