Friday, August 11, 2023

WAKULIMA WATAKIWA KUJIFUNZA MBINU BORA ZA KILIMO KUPITIA MAONESHO YA WAKULIMA NANENANE.


 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Muhagama amesema maonesho ya kilimo ya Nane Nane ni njia pekee ya wakulima kuweza kujifunza mbinu bora za kilimo cha  kisasa na matumizi ya zana bora za kilimo  zinazoweza kuleta  mafanikio katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara nchini.

 

Aliyasema hayo mapema , alilpokuwa katika Shehia ya Dole Kizimbani alipokuwa akifunga Maonesho ya wakulima Nane Nane yaliyo washirikisha wadau kutoka sekta binafsi na wakulima 275 wajasiriamali, taasisi binafsi na za Serikali.

 

“Serikali ya Mapinduzi ya Zanziba chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Hussen Ali Mwinyi inafanya   juhudi kubwa katika kuibadilisha nchi ili kuweza kuleta madiliko katika sekta za uzalishaji wa chakula na kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake” alibainisha.

 

Zanzibar imepiga hatua nzuri na matokeo ya Maonesho yatawezesha wakulima kujifunza vitu vipya na kwenda kuleta mapinduzi ya kilimo ambapo wakulima wataźalisha kwa wingi mazao ya biashara ambayo yataongeza mnyororo wa thamani wa mazao na kuweza kufanya baishara katika soko la ndani na nje ya nchi.

 

Akiongea katika maonesho hayo, katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwangiliaji, Maliasili na Mifugo amesema Maonesho hayo yenye lengo la kutoa elimu ya kilimo bora kwa wakulima yamedumu kwa siku 10 na kugharimu kiasi cha Shilingi  Milioni Mia Tano fedha za kitanzania.

 

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Umwangiliaji, Maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Shaame Khamis ameishukru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano kwa mashirikiano yao na kuyawezesha maonesho ya kilimo kwa mwaka 2023 kufanikiwa

 

Aidha aliwashukuru wadau na wananchi wote waliochangia na kuwaomba wakulima kuzidisha bidii na kuja na mbinu mpya za kilimo katika maonesho yajayo


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.