Monday, August 14, 2023

NAIBU WAZIRI UMMY, ATOA WITO KWA WANANCHI KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII.



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga ametoa rai kwa wananchi, Taasisi na Wizara kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kutembelea vivutio vyetu vya utalii wa ndani.

Wito huo umetolewa wakati Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake, walipotembelea Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro baada ya kutoka katika Mkutano wa Mazingativu Mkoani Arusha.

"Tunamshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa alizozifanya katika sekta ya utalii kupitia filamu ya Royal tour," alibainisha.

"Tumefika Ngorongoro na tumejionea wageni wamefurika wamekuja kujionea vivutio vya utalii." Alisisitiza.

Aidha, alitoa shukrani nyingi Kwa Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kwa kutoa ruhusa ya kutembelea eneo hilo la Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Aliongeza Kwa kusema kuwa, ziara hiyo imeimarisha upendo, uongozi na urafiki kati ya viongozi na watumishi na itaongeza hari ya utendaji kazi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia na (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi amesema, ziara hiyo ni Maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu kwa lengo la kuhakikisha kwamba tuna viongozi wa kusimamia Sera na wanalifahamu eneo la utalii wanaloliratibu Sera zake katika Serikali.

"Tumekuja kuona Mazingira halisi ya Utalii pamoja na Mazingira halisi ya Utendaji kazi, Tumeona Utalii umekuwa kwa kiasi kikubwa wageni ni wengi na sisi kama Serikali tunawajibu wa kuhakikisha tunaweka sera bora za kuwasaidia wageni kuendelea kuja nchini," Alisisitiza

Aliendelea kusema kuwa, eneo la Ngorongoro ni zuri linavutia na Watanzania wana fursa ya kuja kujionea.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.