Friday, August 11, 2023

WAZIRI MHAGAMA, AHIMIZA KUWEPO MUONGOZO NA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTENDAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama, Ameitaka Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Shughuli za Serikali, kuharakisha kutengeneza Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Utendaji wa Shughuli za Serikali Pamoja na kukamilisha na kuzindua haraka Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini ndani ya nchi utakaotumika na Seriali kwa ujumla, Wizara, Taasisi na maeneo yote ya Utendaji kazi ndani ya Serikali.

 Ameyasema hayo Jijini Arusha, alipofungua Mkutano wa Mazingativu uliyohusisha, Viongozi, watumishi wa Ofisi hiyo Pamoja na Taasisi zake.

Sambamba na hilo, Pamoja na kuonesha Imani wa Mkurugenzi wa Idara hiyo mpya, Waziri Mhagama aliitaka pia idara hiyo kuwa na Ubunifu “Jaribuni kununua mifumo, miundo na taratibu za kufanya ufuatiliaji na Tathmini kutoka kwenye mataifa mengine, ili tuweze kuitangaza Taifa letu kwa kazi hili kuwa tunaweza kufanya vizuri” Alisisitiza Waziri Mhagama.

Aidha, Waziri Mhagama alisema anahitaji kupata taarifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Ofisi yake na Serikali kwa ujumla wa kila robo mwaka ikiwa ni katika kuboresha Eneo hilo.

Akizungumzia kuhusu Uchapishaji wa Nyaraka za Serikali, Waziri Mhagama alisema katika eneo hilo, katika mwaka huu Mpya wa Fedha 2023/2034, Serikali imejiwekea mkakati wa kuongeza Maduhuli na mapato ya yake kupitia Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambapo ujenzi wa Mradi wa Mkakati wa kiwanda kipya cha Mpigachapa Mkuu wa Serikali Umefikia asilimia 97% na “Tumeshaanza kufanya manunuzi ya mashine za kisasa, na tumeshafufua mashine ambazo zilikuwa zimehariba.

Nisisitize Chapa muendeshe kiwanda kwa Ubunifu, jengeni fikra mpya boresheni mifumo miundo na namna ya uhifadhi na uchapaji wa nyaraka za Serikali, nataraji kiwanda hiki kinaweza kikajiuza na kinaweza kikapata soko la nchi za kusini mwa Afrika SADC na katika na Soko la  nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, pale mnalo jambo na kazi kubwa ya kufanya, na mazingativu haya yawasaidie kujiongoza na kupata picha na fikra ambazo zitatuvusha.” Alisisitiza Waziri Mhagama

Akiongea katika Mkutano huo wa Mazingativu, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Dkt Jim Yonazi alisema kuwepo kwa Ofisi hiyo Jijini Arusha katika Mkutano huo  ni kutokana na nia ya Ofisi hiyo kuhakikisha kwamba inatenda majukumu yake kwa umakini na kwa utimilifu ikiwa ni pamoja na Uratibu wa shughuli za Serikali kwa ujumla na kwenye maeneo mengine.

“Tunaweza kujifunza kutoka hapa ndani ya nchi mambo mengi na tukatumia ubunifu na wataalam wa ndani katika utendaji na hakuna mtu anaweza kuwa mbunifu katika mazingira yenye stress, hivyo tunaweza kuweka mazingira wezeshi kwa watumishi na kukuza na kuongeza uelewa katika utendaji.”Alisema

 Kwa kutekeleza Agizo la Mhe. Waziri Mhagama, Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini wa Ofisi Hiyo Bi. Sakina Mwinyimkuu alisema, kikosi kazi kitakaa haraka ili kuweza kuandaa mwongozo wa ufuatiliaji na Tathmini na kuhusiana  na kuwa na Mfumo wa Ufuatiiaji na Tathmini, Mkurugenzi alisema kazi hii inafanyika kwa kushirikiana na Taasisi ya Serikali Mtandao (Ega) na maandalizi ya kujengwa kwa mfumo huo yanatarajiwa kuanza.

 Kwa Upande wake Mpigachapa Mkuu wa Serikali Bw. George Lugome alisema, kama Idara imejipanga hasa kwa watumishi kuhakikisha wanafanya kazi katika ubora wa hali ya juu na kuhakikisha, watumishi watapata mafunzo ya kuendesha mashine mpya za kisasa, kuongeza idadi ya watumishi wenye sifa na ueledi katika endeo hilo la uchapaji “Ili kuweza kuendana na mabadiliko ya teknolojia, ni lazima pia tuchape nyaraka za Serikali kwa kufuata Ubora na kuweka alama za usalama kulingana na teknolojia zilizopo,na tumeshaanza mikakati ya namna gani ya kushirikiana wenzetu wenye utaalam wa masuala ya usalama katika nyaraka mbalimbali.” Alifafanua

Mada mbalimbali  zinawalishwa katika Mkutano huu wa mazingativu ni Matarajio  ya washiriki wengi kuwa, mkutano huo utawasaidia, kuboresha utendaji wa kazi, kujifunza, kupata ubunifu  katika maeneo yao ya kazi, kuongeza bidii zaidi na hali ya utendaji katika kazi unaoendana na sayansi na teknolojia.

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.