Wednesday, July 19, 2023

WAZIRI MHAGAMA ATEMBELEA MNARA WA SHUJAA AHAMAD MZEE

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama ametembelea Mnara wa Shujaa UD 5826 L/CPL AHAMAD MZEE katika kata ya Kitaya Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba Mkoani Mtwara.

Waziri ametembelea mnara huo Nanyamba Mkoani Mtwara tarehe 17/07/2023 siku chache kuelekea siku ya Mashujaa ya kitaifa inayotarajiwa kufanyika tarehe 25/08/2023 katika Uwanja wa Mashujaa uliopo Mji wa serikali Mtumba Jijijni Dodoma.

Shujaa Ahmad Mzee alikuwa Muajiriwa wa Jeshi la Wananchi alipokuwa akitekeleza majukumu yake ya kikazi akiwa na umri wa Miaka 21 alipelekwa Mpakani mwa kijiji cha Kitaya akiwa na jukumu la Ulinzi wa Taifa la Tanzania katika nafasi ya Mpiga mzinga wa kuangusha ndege.

Katika kutekeleza Majukumu yake tarehe 14 April 1972 wakati ndege za Mreno zikitokea Msumbiji Helicopter na Jet Fighters zilipiga mabomu kijiji cha Kitaya na katika Mapambano hayo Shujaa Ahmad Mzee aliangusha Jet Fighter mbili, moja ilianguka ardhi ya Tanzania Mto Ruvuma na Nyingine ilianguka ardhi ya Msumbiji.

Kwenye Mapambano hayo Shujaa Ahamad Mzee alijeruhiwa baada ya Kupigwa na fighter na alichukuliwa na kukimbizwa Mtwara Ligula Hospitali na huko ndiko alikofia.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.