Tuesday, July 18, 2023

SERIKALI YATOA MSAADA WA KIBINADAMU, NANYAMBA NA TANDAHIMBA

 


Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) imetoa misaada ya kibinadamu kwa kaya 184 za kata ya Kitaya Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba na kaya 160 kwa kata ya Michenjele Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba.

Zoezi hilo limeongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe, Jenista Mhagama Mkoani Mtwara, amesema kwa kutumia sheria no 6 iliyotungwa mwaka 2022 ya usimamizi wa maafa, kazi yetu ni kufanya tathimini na kutoa Mkono wa pole kwenye Majanga yanayohusu binadamu mahali popote.

“Nitoe wito kila yanapotokea majanga na maafa, kwanza liwe jukumu letu kufarijiana kwa karibu; na kutoa taarifa za dalili za majanga yanapotokea, na kuangalia ni mambo gani ya msingi yafanyike ili kurudisha hali katika utaratibu wa kawaida” alihimiza.

Waziri Mhagama amesema, tumepokea tathimini iliyowakilishwa ikionesha madhara yaliyojitokeza kwa wananchi katika eneo hili katika maeneo kadha kwa kadha katika makazi, chakula,na  nyenzo za kufanyia shughuli za kiuchumi

Amefafanua kwamba Serikali imekuja kutoa Mkono ili tuweze kushirikiana na nyie katika kujibadilishia hali katika kipindi hiki chote, “nikweli Serikali imeendelea kuwa na nyie kwa nguvu kubwa na ya ziada zaidi,” alisema Mhe. Waziri

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassani kwa kutushika Mkono wananchi yanapotokea majanga ya kibindamu, yanapotokea mafuriko, na vinapotokea vimbunga, tunajisikia faraja.

Tumepokea magodoro 190 tumepokea ndoo kubwa 380, na ndoo kubwa za lita ishirini 190, tumepokea blanketi za watoto 190 na blanketi za watu wazima 380 na mikeka 380 na mabati 5700 na kaya zinazostahiki ni 184 zilizoordheshwa kwa sasa katika Halmashauri ya wilaya ya Nanyamba.

Kanali Ahmedi ameongeza kusema Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba Ilipokea vifaa vya msaada wa kibinadamu kwa waathirika 160, tuna mabati 4800 kuna magodoro 160, mikeka 320 na mablanketi 320, ndoo kubwa za lita ishirini 320 na tayari zimeundwa kamati mbalimbali kwa ajili ya kuhakiki

Naye Mbunge wa Nanyamba Mhe. Abdallah Chikota amesema Tunashukuru kwa msaada wa kibinadamu na kipekee nimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa sababu asiyeshukuru kwa moja hata kumi hawezi kushukuru.

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.