Wednesday, May 3, 2023

NEC YAANZA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU 2025


 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi ipo katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa kuzingatia utaratibu na vigezo.

Hayo  yamesemwa leo  Bungeni Jijini Dodoma na Naibu  Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga wakati akijibu  maswali  ya baadhi ya  wabunge walioomba majimbo yao  yagawanywe.

Amesema muda utakapofika, Tume itatoa tangazo rasmi kwa wadau wote wa uchaguzi juu ya kuanza kwa machakato wa ugawaji wa majimbo ili wadau wawasilishe maoni na maombi yao na hivyo kushughulikiwa kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa kikatiba.

Mhe. Ummy amesema majimbo mengi yameomba kugawanywa lakini mambo yanayotazamwa ni pamoja na ukubwa wa ukumbi wa jimbo, idadi ya wabunge wa viti maalumu na jiongrafia za maeneo yaliyoomba kugawanywa.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.