Monday, September 29, 2025

DKT. YONAZI: TUIMARISHE LISHE, TUPUNGUZE MAGONJWA SUGU

 


KATIBU Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi amewataka wadau kushirikiana na Serikali katika kuimarisha hali ya lishe nchini ili kupunguza kasi ya kuenea kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Amesema ulaji usio faa na mitindo mibaya ya maisha vimechangia kuongezeka kwa magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza jambo linalohatarisha maendeleo ya Taifa.

Dkt. Yonazi ameyasema hayo jijini Dar es salaam leo katika Mkutano Mkuu wa 11 wa Wadau wa Lishe unaoendelea katika kituo cha mikutano cha APC Bunju.

 Dkt. Yonazi amesema tafiti zinaonesha kuwa uzito uliozidi na uliokithiri ni chanzo kikuu cha magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza yakiwemo  kisukari, moyo, figo na baadhi ya saratani.

“Napenda kukumbusha wadau, taasisi na wataalam kushirikiana na serikali kufanya tafiti zitakazosaidia kuleta majibu ya changamoto za lishe, pamoja na kusaidia watu kubadili tabia za ulaji na mtindo wa maisha ili kuzuia magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza yanayohusiana na ulaji usiofaa na ambayo ni tishio kwa Taifa letu,”alisema Dkt. Yonazi

Dkt.Yonazi ameongeza kuwa  Takwimu zinaonesha  licha ya hali ya lishe nchini kuendelea kuimarika bado kuna changamoto hususani kwenye uzito uliozidi na kiriba tumbo hii kutokana maendeleo tunayoyapata na mabadiliko ya mtindo wa maisha hususani  ulaji usiofaa hivyo jitihada za pamoja kati ya wadau na serikali zinahitajika ili kukabiliana na tatizo hili.

Akizungumza kuhusu mkutano huo Dkt. Yonazi amesema lengo ni kupokea na kujadili hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa afua za lishe kwa kipindi cha Mwaka wa Tatu 2024/2025 katika maeneo mahsusi yaliyoanishwa kwenye Mpango Jumuishi wa Kitaifa wa Lishe (2021/22-2025/26).

Vilevile amesema mkutano huo unatoa fursa kwa wadau wote wa lishe kujadili namna utekelezaji ulivyofanyika, changamoto na mikakati ya kufanikisha utekelezaji katika kipindi kilichobaki cha utekelezaji wa mpango huo hususan mwaka 2025/26.

Kwa mujibu wa Dkt. Yonazi mkutano huo unatazamiwa kuongeza msukumo mpya wa utekelezaji wa afua za lishe miongoni mwa wadau kama moja ya nguzo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

“Uwepo wenu hapa, ni uthibitisho tosha wa ushirikiano mlionao na utayari wenu katika kuhamasisha uboreshaji wa hali ya lishe kwa Watanzania, hususani makundi yanayoathirika zaidi ambayo ni watoto wadogo na wachanga, watu wenye mahitaji maalum, wanawake wajawazito na wale walio katika umri wa uzazi,”amesema Dkt. Yonazi.

Dkt. Yonazi amewashukuru  wadau wote walitoa mchango wa fedha na ushauri wa kitaalamu katika kufanikisha maandalizi ya mkutano huo na amewahakikishia kuwa serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za wadau ili kuhakikisha Taifa linapata mafanikio dhidi ya mapambano ya tatizo la utapiamlo.

 


Read More

Thursday, September 25, 2025

DKT. YONAZI ATOA WITO WATUMISHI KUBEBA MAONO YA DIRA YA TAIFA 2050

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, ametoa wito kwa Viongozi, Menejimenti na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kubeba malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 kama sehemu ya wajibu wao wa kitaifa ili kuweza kufikia maono yaliyopo kufikia mwaka 2050.

 Dkt. Yonazi ametoa wito huo wakati ufunguzi wa Kikao cha Mazingativu ya Menejimenti, Wakuu wa taasisi na Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu na taasisi zake kinachofanyika leo Jijini Arusha.

 “Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 tayari imeshazinduliwa, Dira hii ni ramani ya mustakabali wa nchi yetu, ikitupa taswira ya nchi ambayo tunaihitaji kuwa nayo katika ndani ya miaka 25 ijayo, ili kufanikisha maono haya kila mmoja wetu anawajibu na anajambo la kulifanya, ni wajibu wetu kujiuliza kwamba nitachangia nini kuhakikisha nchi yangu inafikia maono haya kufikia mwaka 2050” ameeleza Dkt. Yonazi.

 Aidha, amebainisha kuwa, kila mmoja mahali pake pa kazi anawajibu kwa kuhakikisha nchi ya Tanzania inakuwa nchi bora na mahali bora pa kuishi kwa kuweka misingi bora ifikapo mwaka 2050.

 Akizungumza kuhusu kikao hicho, Dkt. Yonazi amebainisha kuwa, kikao hicho ni sehemu ya utamaduni wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutenga muda kila mwaka kwa ajili ya kujitafakari, kujifunza na kujipanga upya kwa lengo la kuboresha utendaji katika kutekeleza majukumu ya Ofisi hiyo.

 Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA. Amos Makalla ametoa wito kwa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa wabunifu katika kufikiri na kutekeleza majukumu yao, ili kuweza kutoa huduma zinazokidhi mahitaji na matarajio ya wananchi kwa ufanisi zaidi.

“Dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kubwa na changamoto zake zinahitaji mbinu mpya za kuzikabili, ni wajibu wetu kuwa wabunifu katika kufikiri na kutekeleza majukumu yetu, ili tuweze kutoa huduma zinazokidhi mahitaji na matarajio ya wananchi kwa ufanisi zaidi. Hivyo, kubadilika kulingana na wakati ni muhimu ili kuendana na mabadiliko ya kidunia, kitaifa na kijamii, tukizingatia misingi hii, tutakuwa na Ofisi yenye weledi, inayothamini maendeleo endelevu na inayokabiliana na changamoto kwa mafanikio” alisema.

 Aidha, Mkuu wa Wilaya huyo amebainisha kuwa “Kwa kuwa jukumu la uratibu, ufuatiliaji na tathmini ya shughuli zote za Serikali lipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, nitumie fursa hii kutoa rai kuwa tuendelee kulitekeleza jukumu hili kwa ufanisi wa hali ya juu. Kila taasisi inapaswa kuonesha matokeo halisi katika maeneo yake ya utekelezaji, tuweke mkazo zaidi katika kuhakikisha kwamba kazi zetu zinajikita kwenye matokeo yanayogusa maisha ya wananchi, badala ya kuishia kwenye michakato au utekelezaji usioonesha matokeo”.

Mbali na hayo Mhe. Mkude ametoa wito wa kushiriki uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani kwani Uchaguzi huo ni fursa ya kipekee kushiriki katika kuimarisha misingi ya demokrasia na utawala bora.

 “Kila Mtanzania anatakiwa kutimiza haki na wajibu wake wa kikatiba kwa kupiga kura, ili kuchagua viongozi watakaoliongoza Taifa letu katika ngazi zote, aidha, ni wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha tunadumisha amani, mshikamano na utulivu katika kipindi chote cha uchaguzi, ili Tanzania iendelee kubaki kuwa mfano bora wa utulivu, mshikamano na demokrasia barani Afrika” ameongeza.

 Kikao hicho kinaendelea Jijini Arusha, na mada mbalimbali zitawasilishwa ikiwemo ikiwemo Matumizi ya Akili Unde (AI) mahala pa kazi na mustakabali wa ajira kutokana na maendeleo ya kasi ya sayansi na teknolojia, masuala ya afya ya akili, fursa za uwekezaji kwa watumishi na maandalizi ya maisha baada ya kustaafu, masuala ya itifaki na ustaarabu na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, ili kuweza kujiimarisha katika nyanja mbalimbali kitaaluma, kimaisha na kiutumishi.



Read More

Sunday, September 21, 2025

UBUNIFU UENDELEZAJI MAKAO MAKUU, MJI WA SERIKALI WAHITAJIKA- DKT. YONAZI

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi amesisitiza ubunifu katika uendelezaji wa Makao Makuu na Mji  Serikali ili kuweza kuvutia watalii wa ndani na nje.

Dkt. Yonazi ametoa msisitizo huo wakati wa ziara yake nchini Malaysia alipotembelea Mji Mkuu wa Utawala wa Malaysia uitwao Putrajaya.

"Ni muhimu wataalam kuzingatia masuala yanayofanya mji wa Serikali kuwa kivutio kwa wananchi na watalii kutoka nje. Masuala hayo ni ubunifu katika majengo, utunzaji wa mazingira na miundombinu na huduma muhimu hasa nyumba za ibada, huduma za fedha na maeneo ya kupumzika" amesema Dkt. Yonazi.

Aidha, Dkt.  Yonazi ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano na taasisi za Kimataifa ili kubadilishana uzoefu na kujifuza masuala ambayo yataongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Serikali kwa ujumla.

Katika ziara hiyo Dkt. Yonazi ameambata na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Mhe. Dkt. Mahadhi Maalim, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali Bw. Paul Sangawe, Wataalam kutoka Ubalozi wa Tanzania Nchini Malaysia na kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.


Read More

Tuesday, September 16, 2025

DKT. YONAZI ATANGAZA FURSA ZILIZOPO MAKAO MAKUU YA MJI WA SERIKALI DODOMA NCHINI KOREA.


 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi leo tarehe 16 Septemba, 2025 ameshiriki Mkutano wa Kimataifa wa Uendelezaji Miundombinu unaofanyika Jijini Seoul nchini Korea.

Katika Mkutano huo Dkt. Yonazi amepata fursa ya kuwasilisha mada kuhusu hatua iliyofikiwa katika zoezi lakuhamisha Makao Makuu na fursa za uendelezaji wa Jiji la Dodoma pamoja na Mji wa Serikali.

Aidha, Dkt. Yonazi amekutana na Mwenyekiti wa KFINCO na taasisi inayoratibu uendelezaji wa Mji wa Serikali Korea (National Agency For Administrative City Construction of KOREA-NA ACC) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano baina Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) na Taasisi ya NAACC.

Katika mkutano huo, Dkt. Jim Yonazi ameongozana na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali Bw. Paul Sangawe na wajumbe wengine kutoka Tanzania.



Read More

Saturday, September 6, 2025

AFDP YADHAMIRIA KUONGEZA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA NCHINI

 


Ujumbe wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kwa kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), umesema utaendelea kuwekeza katika uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora ili kuongeza tija kwa wakulima nchini.

Kauli hiyo imetolewa na kiongozi wa ujumbe huo, Bi. Nester Mashingaidze, alipozungumza na wakulima wa Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, alipokuwa akikagua utekelezaji wa programu hiyo inayolenga kuongeza uzalishaji wa mahindi, alizeti, maharage na mimea jamii ya mikunde.

“Tunalenga kuongeza upatikanaji wa mbegu bora kwa kushirikiana na taasisi kama TARI, ASA, na TOSCI ili kuwafikia wakulima wengi zaidi kwa wakati,” alisema Bi. Mashingaidze.

Kwa upande wake, Bw. Salum Mwinjaka – Mratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema AFDP inatekelezwa katika mikoa 11 ya Tanzania Bara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. Alibainisha kuwa programu inajikita katika kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, lishe na usawa wa kijinsia.

Naye, Mhandisi Enock Nyanda kutoka TAMISEMI, alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wizara za kisekta kufikisha huduma kwa wananchi kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo.

Wakulima waliopokea mafunzo kutoka kwenye programu hiyo wamesema imewasaidia kuachana na kilimo cha mazoea na kuhamia kwenye kilimo chenye tija kwa kutumia mbegu bora na za kisasa.



Read More

Tuesday, September 2, 2025

WAZALISHAJI WA MBEGU MKALAMA WAOMBA SERIKALI KUIMARISHA UFUNGASHAJI

 


Wazalishaji wa mbegu za alizeti katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida, wameiomba Serikali kuongeza juhudi katika kuwawezesha kuandaa vifungashio bora vya mbegu ili kuongeza thamani ya mazao yao sokoni. 

 Wito huo umetolewa  wakati wa ziara ya ujumbe wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kwa kushirikiana na wawakilishi kutoka IFAD katika Kijiji cha Ilunda, waliokuja kufuatilia utekelezaji wa programu hiyo. 

Bw. Athumani Ramadhani, mzalishaji wa mbegu aina ya Record, alisema: “Tunaomba Serikali itupe msaada wa kitaalamu kuandaa vifungashio bora vitakavyotangaza mbegu zetu na kuongeza thamani sokoni.” 

Naye Bi. Aziza Ramadhani aliongeza kuwa uzalishaji huo umeimarisha ushirikiano wao na taasisi za Serikali kama ASA na TOSCI, zinazopima ubora kabla ya mbegu kuingia sokoni. 

 Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mkalama, Bi. Asia, alisema Serikali inalenga kuifanya Mkalama kuwa mfano bora katika utekelezajiwa Programu ya Kilimo na Uvuvi (AFDP), huku akisisitiza umuhimu wa kuongezwa nguvu katika sekta hiyo.

 


Read More

Monday, September 1, 2025

DKT. KILABUKO: OFISI YA WAZIRI MKUU ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA IFAD

 


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko, amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika utekelezaji wa miradi ya kilimo na uvuvi nchini. 

Ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati wa kikao na ujumbe wa IFAD waliopo nchini kufuatilia utekelezaji wa mradi wa programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo na uvuvi (AFDP). 

“Nawahakikishia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ipo tayari kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha miradi mnayoitekeleza inaleta matokeo chanya,” amesema Dkt. Kilabuko.



Read More

Saturday, August 23, 2025

SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MGODI NYANDOLWA.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi, amemfikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, salamu za pole kufuatia ajali ya kufukiwa kwa mafundi katika Mgodi wa Dhahabu wa Nyandolwa, iliyotokea tarehe 11 Agosti 2025 katika Mkoa wa Shinyanga.

Waziri Lukuvi ameeleza kuwa Serikali imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za ajali hiyo, na kwa niaba ya Rais Samia, ametoa pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao katika tukio hilo la kusikitisha. Aidha, ameeleza kuwa Serikali itagharamia kikamilifu gharama za mazishi kwa waathirika wa ajali hiyo pamoja na matibabu kwa waliofikwa na tukio hilo.

Akizungumza na wanandugu wa marehemu na wale waliokwama mgodini, Mhe. Lukuvi amewatia moyo na kuwahakikishia kuwa Serikali ipo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu. Ametoa wito kwa timu za uokoaji kuongeza juhudi na kasi ya uokoaji ili kuwaokoa mafundi waliokwama kwa haraka na usalama zaidi.

“Tunaamini kuwa kazi kubwa imefanyika lakini bado tunahitaji jitihada zaidi. Serikali inatambua uzito wa tukio hili na itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa kuhakikisha kila jitihada zinafanyika kwa ufanisi,” amesema Lukuvi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mgodi huo, Fikiri, ameiambia Serikali kuwa ndani ya kipindi cha siku tatu hadi nne zijazo, zoezi la kuwaokoa wahanga waliokwama litakuwa limekamilika. Ameeleza kuwa vifaa vya kutosha vimeletwa eneo la tukio na wataalamu wanaendelea na kazi kwa umakini mkubwa kuhakikisha mafanikio ya haraka.

Kabla ya kuwasili katika eneo la mgodi, Mhe. Lukuvi alifanya ziara katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ambapo alipokea taarifa ya kina kuhusu maendeleo ya sekta ya madini katika mkoa huo pamoja na hali ya sasa ya shughuli za uokoaji zinazoendelea katika mgodi wa Nyandolwa.

Akizungumza kwa niaba ya ndugu wa wanasubiri waliofukiwa na kifusi Bw.Furaha Enock aliishukuru Serikali kwa namna ilivyoratibu zoezi na inavyowahudumia katika kipindi chote toka tukio kutokea na kueleza kuwa imefanya jambo la kipekee, la heshima na la uungwana kuwashika mkono na kuhudumia kwa hali na mali na kuwasihi wanandugu kuendelea kuwa na utulivu.

"Kipekee ninaipongeza Serikali Yetu imetufanyia wema na imetupa faraja kwa namna wanavyoratibu tukio zima, tunakosa neno zaidi ya Asante sana kwa Rais Dkt. Samia pamoja na uongozo wake wote," alisema Enock

AWALI

Ziara ya Waziri Lukuvi ni sehemu ya juhudi za Serikali za Uratibu na kutoa maelekezo kwa karibu katika kipindi hiki cha majonzi, huku ikilenga kuimarisha utendaji wa shughuli za uokoaji na kuhakikisha haki na heshima kwa waathirika wote wa ajali hiyo.

Read More

Thursday, August 21, 2025

SERIKALI YAENDELEA NA JITIHADA ZA UOKOAJI MGODI WA NYANDOLWA


Imeelezwa kuwa, jitihada za kuendelea kuokoa maisha baada ya ajali ya mgodi kutokea eneo la Nyandolwa Mkoani Shinyanga zinaendelea usiku na mchana ambapo hadi kufikia Leo Agosti 21,2025 mafundi 10 kati ya 25 waliokuwa wamekwama chini ya ardhi wameokolewa, huku wanne wakiwa hai, mmoja kati yao akifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini, na saba wakikutwa wamefariki dunia.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Mkoani humo ambapo amethibitisha taarifa hizo na kusema kuwa tukio hilo lilitokea takribani siku 10 zilizopita, likisababisha shughuli za uokoaji kuendelea kwa muda mrefu katika mazingira magumu.

Amesema ajali hiyo ilitokea baada ya ardhi kutitia ghafla na kusababisha kifusi kuporomoka katika mashimo (maduara) matatu tofauti yaliyokuwa yakikarabatiwa na mafundi ndani ya mgodi huo, unaomilikiwa na kikundi cha Wachapakazi chini ya leseni ya uchimbaji mdogo.

"Tunaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali kuhakikisha mafundi waliobaki wanatolewa salama. Hili ni tukio la huzuni kubwa kwa mkoa wetu na Taifa kwa ujumla," amesema Mhe. Mhita.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. James Kilabuko, ametoa wito kwa timu ya uokoaji kuongeza kasi na juhudi katika shughuli za uokoaji, akisisitiza kuwa kila sekunde ina maana katika kuokoa maisha ya waliobaki chini ya kifusi.

“Natoa pongezi kwa kikosi kizima cha uokoaji kwa moyo wao wa kujitolea, lakini ni muhimu sasa kuongeza kasi bila kuhatarisha usalama wa waokoaji wenyewe,” amesema Dkt. Kilabuko.

Naye, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo, amefika eneo la tukio na kutoa salamu za pole kwa familia za marehemu na wote walioathirika na ajali hiyo. Ametoa rai kwa waokoaji kuendelea kuwa na umakini mkubwa na kutanguliza usalama katika operesheni ya uokoaji.

“Hii ni ajali ya kusikitisha mno. Tume ya Madini inatoa pole kwa familia za wahanga, na tutaendelea kufuatilia kwa karibu kuhakikisha taratibu zote za usalama katika migodi zinasimamiwa ipasavyo ili kuepusha ajali kama hizi siku za usoni,” amesema Dkt. Lekashingo.

Aliongezea kuwa, Timu za uokoaji zinajumuisha maafisa kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Polisi, Tume ya Madini, Wizara ya Madini, wachimbaji wenzao, Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Serikali ya Mkoa na Wilaya ya Shinyanga, ambao wote wanaendelea kushirikiana kuhakikisha mafundi waliobaki wanatolewa salama.

Hadi sasa, juhudi za uokoaji bado zinaendelea katika eneo hilo la mgodi, huku matumaini yakiwa bado hayajapotea kwa familia na ndugu wa mafundi waliobaki chini ya kifusi. Serikali imeahidi kutoa usaidizi wa karibu kwa waathirika na kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika kubaini chanzo cha ajali hiyo.



Read More

SERIKALI YA ZAMBIA YAPATA MAFUNZO KUTOKA TANZANIA: YAPONGEZA UJENZI WA MJI WA SERIKALI DODOMA


Maofisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Zambia wametembelea Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, kwa lengo la kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa kutekeleza mradi mkubwa wa kitaifa wa kuhamishia shughuli za serikali katika mji huo.

Wakiwa katika ziara hiyo, maofisa hao walipokelewa na Mratibu wa Ujenzi wa Mji wa Serikali, Bw. Noel Mlindwa, ambaye alieleza kuwa Tanzania imeweka historia kwa kuanzisha na kutekeleza kwa mafanikio makubwa ujenzi wa mji wa serikali, chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Bw. Mlindwa alifafanua kuwa mji huo umejengwa kwa kuzingatia mipango bora ya kisasa, usimamizi makini wa rasilimali na matumizi ya teknolojia, hali iliyowavutia wageni hao kutoka Zambia.

Kwa upande wao, maofisa wa Zambia waliipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua kubwa ilizopiga na walisisitiza kuwa Mji wa Serikali Dodoma si tu ni kielelezo cha maendeleo, bali pia ni kivutio cha kiutalii na mfano wa kuigwa kwa mataifa mengine barani Afrika.



Read More

Saturday, August 16, 2025

UZINDUZI WA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI ZANZIBAR WAFANA


Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Nderiananga, ameshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa anuani za makazi, unaolenga kutoa huduma ya barua ya utambulisho wa mkazi kwa njia ya kidijitali.

Uzinduzi huo umefanyika leo katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, ukiongozwa na Mgeni Rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Ummy amepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa jitihada zao za kuimarisha huduma za kijamii kupitia mifumo ya kidijitali.

"Niwapongeze kwa kuendelea kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa urahisi zaidi kupitia teknolojia. Mfumo huu utarahisisha utambuzi wa makazi na uboreshaji wa utoaji wa huduma mbalimbali serikalini," alisema Mhe. Ummy.

Aidha, amezipongeza wizara zote za kisekta kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano wao uliowezesha utekelezaji wa mfumo huo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.



Read More

Thursday, August 14, 2025

MAKATIBU WAKUU WATETA MIKAKATI YA KUENDELEZA SAFARI CHANNEL YA TBC


Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. James Kilabuko, ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali kilichofanyika leo jijini Dodoma kwa lengo la kujadili namna bora ya kuimarisha uendeshaji wa Tanzania Safari Channel chini ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Kilabuko amesema chaneli hiyo imekuwa nyenzo muhimu ya kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia vivutio vya utalii vilivyopo nchini, hivyo ni muhimu kwa taasisi zote za serikali kushirikiana katika kuiendeleza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba Chacha, akiwasilisha taarifa kuhusu chaneli hiyo, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kusaini sheria mpya ya TBC, ambayo imefungua milango ya maboresho ya kiutendaji na kuimarisha utoaji wa huduma kwa umma.

Chaneli ya Tanzania Safari Channel imekuwa chombo mahsusi cha kuitangaza Tanzania kama nchi yenye vivutio vya kipekee duniani, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kimkakati kukuza sekta ya utalii.

Read More

Tuesday, August 12, 2025

ZANZIBAR YACHOTA UZOEFU DODOMA: YAJIANDAA KUJENGA MJI WA SERIKALI KISAKASAKA

 



Kamati ya wataalamu kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ikiingozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Dkt. Islam Seif Salum imetembelea miradi mikubwa jijini Dodoma ikiwemo Mji wa Serikali Mtumba na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, kujifunza utekelezaji wa Ujenzi wa Mji wa Serikali.

Ziara hiyo inalenga kuandaa mazingira ya ujenzi wa ofisi za Serikali na Baraza la Wawakilishi eneo la Kisakasaka, Zanzibar.

Viongozi hao wamempongeza Rais Dkt. Samia kwa kuimarisha maendeleo ya Makao Makuu ya Nchi kupitia miradi ya kimkakati.



Read More

Monday, August 4, 2025

HELEN KELLER INTERNATIONAL KUSHIRIKIANA NA OFISI YA WAZIRI MKUU KUIMARISHA URATIBU WA LISHE NCHINI


Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bi. Stella Mwaisaga, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Kimataifa la Helen Keller International, Bw. William “Bill” Toppeta.

Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na shirika hilo katika utekelezaji wa masuala ya lishe, ambapo Bw. Toppeta aliipongeza Serikali kwa juhudi kubwa katika kusimamia na kuratibu lishe, huku akisisitiza dhamira ya Helen Keller International kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora za lishe.

“Tunaishukuru Serikali ya Tanzania kwa usimamizi wake imara katika masuala ya lishe. Tutaendelea kuwa wadau wa karibu katika kusaidia juhudi hizi muhimu kwa afya ya wananchi,” alisema Bw. Toppeta.

Ujumbe huo wa Helen Keller International upo nchini kwa ziara ya kukagua na kutathmini utekelezaji wa miradi ya shirika hilo, hususan katika sekta ya lishe, ambapo Ofisi ya Waziri Mkuu ni mratibu mkuu wa kitaifa wa masuala hayo.

Read More

Wednesday, July 30, 2025

SERIKALI KUWEKEZA KATIKA UVUVI WA BAHARI KUU

Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Paul Sangawe ameongoza Kikao cha Kamati ya Wataalamu kuhusu matokeo ya tathmini ya kazi ya tafiti juu ya kampuni zenye uwezo wa kujenga Meli kwa ajili ya Uvuvi katika Bahari Kuu.

Katika Kikao hicho, Bw. Sangawe alilisitiza juu ya utekelezaji wa maelekezo ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi kilichofanyika kabla ya kikao cha wataalam. Masuala yaliyosisitizwa ni pamoja na upatikanaji kampuni yenye uwezo wa kujenga Meli ya Uvuvi wa Bahari Kuu kwa viwango vinavyohitajika, na kupata meli hizo kwa wakati ili kuchochea uvuvi wa kisasa nchini.

Vikao hivyo vya Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi ( AFDP) vimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Bluu, Zanziba




 

Read More

Monday, July 28, 2025

JITIHADA ZA PAMOJA ZINAHITAJIKA KUPAMBANA NA UDUMAVU – DKT. YONAZI


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, ametoa wito kwa Serikali na wadau kushirikiana kwa karibu katika mapambano dhidi ya tatizo la udumavu nchini.

Akizungumza katika kikao cha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa Wadau wa Lishe nchini, kinachotarajiwa kufanyika Septemba 4–5, 2025 jijini Dar es Salaam, Dkt. Yonazi amesema juhudi za pamoja, tafiti, elimu na majukwaa ya kitaifa ni muhimu katika kutokomeza udumavu.

“Tunahitaji nguvu ya pamoja kati ya Serikali na wadau kuhakikisha tunapunguza kwa kiasi kikubwa viwango vya udumavu kupitia sera, elimu na programu zenye tija,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Germana Leyna, amesema mkutano wa mwaka huu utaambatana na Lishe Marathon, yenye lengo la kuhamasisha afya bora kwa jamii na kuongeza uelewa wa masuala ya lishe.

Mkutano huo wa kitaifa unatarajiwa kufunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.



Read More

Wednesday, July 23, 2025

KAMATI YA MAKATIBU WAKUU YARIDHISHWA NA UJENZI WA UWANJA MPYA WA MPIRA JIJINI ARUSHA

 


Kamati ya Makatibu Wakuu inayoongozwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, imekagua na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa wa mpira wa miguu katika eneo la Olmoti, jijini Arusha. Uwanja huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano ya AFCON 2027.

Dkt. Yonazi amesema maendeleo ya mradi huo ni ya kuridhisha na uwanja huo utakuwa si tu kituo cha michezo, bali pia kivutio cha utalii na maendeleo ya uchumi kwa wakazi wa Arusha.

“Tunaamini uwanja huu utakuwa fursa kwa wananchi kuwekeza kibiashara. Ujenzi huu unapaswa kutazamwa kama chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya michezo.

Naye Rais wa TFF, Wallace Karia, amesema uwanja huo utaongeza idadi ya matukio ya kimataifa nchini, Kutakuza vipaji vya ndani, na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia michezo.

Ujenzi wa uwanja huo ni sehemu ya maandalizi ya Tanzania kuandaa mashindano ya AFCON 2027, kwa ushirikiano na Kenya na Uganda



Read More

WAZIRI LUKUVI AWAPONGEZA MALIASILI KWA KUTEKELEZA MAONO YA MHE. RAIS SAMIA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kutekeleza kikamilifu maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa Wizara ya kwanza kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi na kuwezesha Idara na Vitengo vyake kuhamia Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.

Waziri Likuvi ametoa pongezi hizo leo alipotembelea Wizara hiyo kwa lengo la kukagua ujenzi wa Majengo ya Serikali ambao ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu ya Serikali kuhamia Dodoma.

Mhe. Lukuvi amesema kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii licha ya kukamilisha mapema ujenzi wa jengo hilo, inastahili pia kupongezwa kuwa wa kwanza kuhamia na kuwa mfano katika Matumizi ya samani za Ofisini zilizozalishwa hapa nchini kupitia mazao ya Misitu.

"Ninyi ni mabalozi wazuri wa Matumizi ya bidhaa zetu za hapa nchini zinazotokana na Misitu yetu, niimani yangu kuwa Wizara zote zitaiga mfano huu". Aliongeza Mhe. Lukuvi

Aidha Mhe. Lukuvi ametoa rai kwa watumishi wa Wizara hiyo kuhakikisha wanatunza vyema miundombinu na vifaa vilivyopo ili viweze kudumu kama ilivyo kusudiwa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi amemshukuru Waziri Lukuvi kwa ziara yake, na kuahidi kuwa Wizara itatekeleza vyema maelekezo aliyoyatoa hususani ya usimamizi mzuri wa Matumizi ya jengo na vifaa vilivyopo.



Read More

Tuesday, July 22, 2025

MIUNDOMBINU YA MICHEZO ZANZIBAR YAVUKA KIWANGO CHA KIMATAIFA KUELEKEA CHAN

Serikali imeridhishwa na maandalizi ya miundombinu ya michezo Zanzibar kuelekea Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), huku Uwanja wa Amaan Complex ukitajwa kuwa katika viwango vya kimataifa.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, mara baada ya kuongoza Kamati ya Makatibu Wakuu kukagua maandalizi ya CHAN katika visiwa vya Zanzibar.

 “Tumejionea hali halisi ya miundombinu, hasa Uwanja wa Amaan. Uko katika viwango vya kimataifa, na tunaamini Zanzibar ipo tayari kuwa sehemu ya mashindano haya muhimu kwa bara letu la Afrika,” amesema Dkt. Yonazi.

Aidha, Dkt. Yonazi alieleza kuwa hatua hiyo inaonesha utayari wa Taifa kuandaa mashindano ya kimataifa, huku akisisitiza kuwa mashindano ya CHAN ni fursa kubwa ya kuimarisha michezo na kukuza uchumi wa ndani.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (SMZ), Mhe. Fatma Hamad Rajab, alieleza kuwa Uwanja wa Aman Complex tayari umekidhi vigezo vyote vinavyohitajika na Zanzibar iko tayari kuwapokea wachezaji, mashabiki na wageni kutoka mataifa mbalimbali.

Kamati hiyo ya Makatibu Wakuu inafanya ziara katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Visiwani ili kukagua maandalizi ya CHAN na AFCON 2027. 

Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe 2 Agosti 2025 yakihusisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika.

 


Read More

Monday, July 21, 2025

TANZANIA YATANGAZA UTAYARI WA KUANDAA MASHINDANO YA CHAN


 Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, amesema kuwa Tanzania ipo tayari kwa ajili ya kuandaa Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), yatakayoanza rasmi Agosti 2, 2025.

Akizungumza mara baada ya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya michezo jijini Dar es Salaam, Dkt. Yonazi alisema maandalizi yamefikia hatua nzuri na viwanja viko tayari kwa mashindano hayo makubwa.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Makatibu Wakuu ya CHAN na AFCON, Dkt. Yonazi alitembelea viwanja vya Benjamin Mkapa, Isamuhyo, Shule ya Sheria na Gymkhana, akisisitiza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha miundombinu yote inakidhi viwango vya kimataifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Gerson Msigwa, ametoa wito kwa Watanzania kuonesha uzalendo kwa kujitokeza kwa wingi viwanjani kuishangilia Taifa Stars.

 

#CHAN2025 #TaifaStars #TanzaniaYapoTayari



Read More

Friday, July 18, 2025

DKT. YONAZI AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU MAONESHO SABASABA

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kwa maendeleo ya Taifa.

Dkt. Yonazi ameyasema hayo leo Ofisini kwake jijini Dodoma akikabidhiwa tuzo na Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw. Conrad Milinga iliyotolewa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati akifungua Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu kupokea tuzo kumeongeza motisha katika ushiriki wa maonesho yajayo makubwa ya Kimataifa ya Sabasaba na kutambua mchango wa Ofisi hiyo iliyoutoa kwa wananchi katika kipindi chote cha maonesho hayo na kutambua huduma ianayotolewa kwa wananchi.

“Ofisi ya Waziri Mkuu imefurahi sana kupokea tuzo hii kama ishara ya kutambua ushiriki wetu na mchango ambao Ofisi yetu inatoa kwa wananchi hivyo tunaamini ushiriki wetu unaofuata utakuwa wa viwango vya juu sana,” Alisema Dkt. Yonazi.

Pia aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazofanya chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) ambayo ndio mratibu wa Maonesho kwa  kuhakikisha maonesho hayo yanaleta tija na mageuzi makubwa katika sekta ya kiuchumi kwa wananchi na Kimataifa.

“Tunazishukuru sana Taasisi mbalimbali ambazo tumeshirikiana nazo na viongozi ambao wameendelea kutupa maelekezo yaliyowezesha kufanya vizuri katika maonesho hayo na tunaamini kwamba tutaendelea kuwa washindi au hata washindi wa jumla,”Alishukuru.

Ikumbukwe Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam Sabasaba 2025 yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi tarehe 07 Julai, 2025 na kufungwa na Waziri Mkuu Mhe.  Kassim Majaliwa katika viwanja vya maonesho Sabasaba jijini Dar es Salaam Julai 13, 2025.



Read More

"KILA SEKTA IJIANDAE KUPOKEA WAGENI KUELEKEA CHAN", DKT. YONAZI

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amezitaka sekta zote kujianda kupokea wageni mbalimbali kuelekea Mashindano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) yanatayorajiwa kuanza Mwanzoni mwa mwezi wa Agosti 2025.

Dkt. Yonazi ametoa rai hiyo wakati akiongoza Kikao cha Makatibu Wakuu cha Tathmini ya Maandalizi ya CHAN na AFCON kilichofanyika  leo katika Ukumbi wa Ofisi  ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

Aidha, ameeleza kuwa jukumu la Serikali ni kuleta fursa na kuweka miundombinu ili kila sekta inufaike na ugeni huu mkubwa na kusisitiza hii ni fursa ya kutuamsha katika kuandaa matukio makubwa.

Pia, Dkt. Yonazi amesisitiza umuhimu wa kutoa hamasa kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kila mtanzania aamasike na kushiriki katika mashindano haya ya CHAN.

Ikumbukwe Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kutimua vumbi kuanzia Agosti 2, 2025 ambapo timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itachuana na Timu ya Taifa ya Burkina Faso katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.



Read More

Wednesday, July 16, 2025

WAZIRI LUKUVI ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA 2025


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. William Lukuvi amefanya ukaguzi wa maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Mtumba – Dodoma.

Maadhimisho hayo yatapambwa na gwaride kutoka majeshi matano ya ulinzi na usalama na mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Katika ziara hiyo, Waziri Lukuvi aliambatana na viongozi waandamizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na maafisa kutoka JWTZ na Jeshi la Polisi.

Maandalizi yameelezwa kuendelea vizuri, huku tukio hilo likitarajiwa kuwa la kitaifa na kihistoria katika kutoa heshima kwa mashujaa wa Tanzania.




Read More