Monday, August 4, 2025

HELEN KELLER INTERNATIONAL KUSHIRIKIANA NA OFISI YA WAZIRI MKUU KUIMARISHA URATIBU WA LISHE NCHINI


Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Bi. Stella Mwaisaga, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Kimataifa la Helen Keller International, Bw. William “Bill” Toppeta.

Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na shirika hilo katika utekelezaji wa masuala ya lishe, ambapo Bw. Toppeta aliipongeza Serikali kwa juhudi kubwa katika kusimamia na kuratibu lishe, huku akisisitiza dhamira ya Helen Keller International kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora za lishe.

“Tunaishukuru Serikali ya Tanzania kwa usimamizi wake imara katika masuala ya lishe. Tutaendelea kuwa wadau wa karibu katika kusaidia juhudi hizi muhimu kwa afya ya wananchi,” alisema Bw. Toppeta.

Ujumbe huo wa Helen Keller International upo nchini kwa ziara ya kukagua na kutathmini utekelezaji wa miradi ya shirika hilo, hususan katika sekta ya lishe, ambapo Ofisi ya Waziri Mkuu ni mratibu mkuu wa kitaifa wa masuala hayo.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.