Tuesday, February 21, 2017

MAJALIWA AZINDUA MADARASA NA KUHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA MJINI KATESH

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua madarasa ya Shule ya Msingi ya Mogitu wilayani Hanang Februari 21, 2017. Kulia kwake ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Eliakim Maswi na wapili kulia kwake ni Mbunge wa hanang, Dkt. Mary Nagu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Katesh wilayani Hanang, Februari 21, 2017.
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akimkabidhi zawadi ya Shilingi 500,000/= mzee Giloya Semhonda  ikiwa ni shukurani kwa usimamizi wake mzuri wa ujenzi na ukarabati wa madarasa ya shule ya msingi ya Mogitu wilayani Hanang baada ya uzindu madarasa hayo Februari 21, 2017.  Fedha hizo zilitolewa na Mkuuu wa Mkoa wa Manyara,  Dkt. Joel Bendera.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika apicha ya pamoja na Walimu wa Shule ya Msingi ya Mogitu wilayani Hanang baada ya kuzindua madarasa ya shule hiyo, Februari 21, 2017. Watatu kulia ni Mbunge wa Hanang, Dkt. Mary Nagu.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Walimu wa Shule ya Msingi ya Mogitu Wilayani Hanang baada ya kuzindua madarasa ya shule hiyo  Februari 21, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama ngoma ya asili ya kabila la Wanyaturu kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Katesh wilayani Hanang Februari 21, 2017.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.