Wednesday, May 26, 2021

Waziri Mhagama ateta na Viongozi wa Plan International Tanzania


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Plan International – Tanzania, ofisini kwake jijini Dodoma.

 

Ujumbe huo umeongozwa na Mkurugenzi Mkazi wa Plan International – Tanzania Dkt. Mona Girgis, akiwa na Meneja Miradi wa Plan Interanational Tanzania, Peter Mwakabwale,  pamoja na Meneja wa Uchechemuzi  wa Plan International  Tanzania.

 

Kupitia kikao hicho, Viongozi hao wa Shirika hilo walipata fursa ya kueleza kwa kina mipango yao ya kushirikiana na serika kwenye shughuli wanazozifanya. Wamebainisha kuwa wanayo miradi wanayo tekeleza katika kuchochea maendeleo ya vijana pamoja na kujumuisha watu wenye Ulemavu kwenye shughuli za maendeleo.


Katika Mazungumzo hayo Mhe. Mhagama amewahakikishia kuwa serikali ipo tayari kuendelea kushirikiana nao katika mikakati ya maendeleo ya vijana na masuala ya watu wenye ulemavu. Amewaeleza kuwa  atawaelekeza Wataalamu wa Ofisi hiyo wakutane na Wataalamu wa shirika hilo ili wapange mipango mikakati ya kushirikiana nao.


Ofisi ya Waziri Mkuu, (Kazi,vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu) inaratibu masuala ya Vijana na watu wenye Ulemavu kwa Uhamasishaji wa vijana, malezi na uwezeshaji wa kiuchumi na kijamii, pia inaratibu masuala ya Watu wenye Ulemavu kwa kutoa utaalamu na huduma kwa watu wenye ulemavu. 

 

MWISHO

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, akiongea na viongozi wa Plan International – Tanzania, ofisini kwake jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, akiwa katika picha ya pamoja na  viongozi wa Plan International – Tanzania, ofisini kwake jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, akiongea na Mkurugenzi Mkazi wa Plan International – Tanzania Dkt. Mona Girgis mara baada ya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano na shirika hilo walipomtembelea , ofisini kwake jijini Dodoma.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.