Sunday, January 29, 2023

DKT.JINGU: MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YATUMIKE KATIKA MIPANGO YA MAENDELEO.

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Utatibu Dkt. John Jingu ameeleza ni muhimu kuyatumia matokeo ya sensa ya watu na maakazi ya mwaka 2022 katika mipango mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu.

Ameyasema hayo wakati akiongoza kikao cha 9 cha Kamati ya Ushauri ya Taifa ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kwa ajili ya kupitia baadhi ya ripoti za matokeo ya Sensa zilizo kamilika kabla ya kuzinduliwa.Kikao kilifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Dar es Salaam.

Jukumu kubwa la Kamati hiyo ni kuishauri Kamati Kuu ya Taifa ya Sensa inayoongozwa na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar namna bora ya utekelezaji wa masuala ya sensa.

=MWISHO=


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.