Thursday, June 22, 2017

WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WAASWA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU


Baadhi ya watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika Ukumbi wa Mikutano ofisi hiyo Dodoma ili kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea Barani Afrika.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Issa Nchansi akieleza kanuni za maadili kiutendaji kwa watumishi wa ofisi hiyo wakati wa kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma walipokutana na watumishi wote Dodoma ili kujadili masuala ya kiutumishi Juni 22, 2017.

Mchumi Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Novatus Tesha akisoma Kanuni za Maadili ya Utendaji Katika Utumishi wa Umma wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambapo ofisi hiyo imeadhimisha kwa kukutana na watumishi wake kujadili masuala ya msingi ya kiutumishi Juni 22, 2017.

Msaidizi wa Waziri Mkuu (Hotuba) Bw. Abdalah Mtibora akiuliza swali kwa Mwenyekiti wa mkutano (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma tarehe 22Juni, 2017.

Mhasibu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi.Kissa Mwakipesile akieleza hoja yake kwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu ofisi hiyo Bw.Issa Nchansi (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Juni 22, 2017 Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.

Afisa Tehama Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Innocent Mboya akifafanua jambo kwa washiriki wa mkutano wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Juni 22, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.