Monday, May 16, 2022

SERIKALI YAENDELEA KUHIMIZA WANACHI UWEKAJI ANWANI ZA MAKAZI





NA MWANDISHI WETU-LINDI

Naibu Katibu Mkuu Bwn. Kaspar Mmuya amehimiza wananchi ambao bado maeneo yao hayajatambuliwa kwenye zoezi uwekaji anwani za makazi kujitokeza kwenye Ofisi za serikali za Mitaa au Kijiji kueleza ili uongozi uwawekee namba.

Amezungumza hayo katika ziara yake ya kikazi Mkoa wa Lindi alipotembelea kujionea utekelezaji wa zoezi la anwani na makazi ambalo limeweza kutambua barabara na mitaa 7972 na majengo na viwanja 334771 vimeweza kutambuliwa na kuingizwa kwenye mfumo wa NAPA.

“ Mkoa wa Lindi umefaulu vizuri sana katika kuweka miundo mbinu hasa ya barabara na wamefanikiwa vizuri kuyatambua maeneo yake na kuyapa namba ikiwa inamaanisha nyumba na barabara nyingi kutambuliwa kwa majina alisema Naibu Katibu Mkuu “

Ameongeza kusema Mitaa ambayo haijabandikwa kibao na jina nimepewa mpango kazi na miundo mbinu inatengenezwa kwa kushirikiana vizuri na TANROAD pamoja TARURA katika barabara zinazohusu taasisi zetu hizi mbili. 

Uelewa wa wananchi katika kulipokea na kulitekeleza jambo hili ni mkubwa kwa sababu wameshirkishwa katika kutafuta majina hayo ya mitaa na wanajua umuhimu wa kuwepo kwa miundo mbinu hiyo.

“Wananchi walio wengi wamekubali kuzichora nyumba zao kwa kutumia rangi ya njano na kuweka namba katika nyumba kwa kutumia rangi nyeusi, ni wajibu wetu kama kanuni za anwani za makazi ambazo zimewekwa na TAMISEMI kanuni namba 20 ambayo inasema ni wajibu wa mwenye nyumba kuweka namba hiyo kwenye nyumba yake alisema, Naibu Katibu Mkuu”

Akihitimisha Kaimu Meneja wa TARURA Mkoa wa Lindi Injinia Dawson  Paschal amesema watawekwa nguzo na vibao 3042 katika Mkoa mzima wa Lindi. Vibao vitakavyotengenezwa vitafidia sehemu ambazo hazijawekwa ili kuhakikisha zoezi la uwekaji wa miundo mbinu linafanikiwa.


 

 

 

 

 

 



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.