Saturday, May 14, 2022

SERIKALI YAHIMIZA USHIRIKISHWAJI ZAIDI ANUANI ZA MAKAZI

 





Na Mwandishi wetu- Pwani

Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bwn. Kaspar Mmuya amehimiza Ofisi za Umma na Ofisi Binafsi kuweka anuani za makazi katika majengo ya Ofisi zao ili kuwa mfano kwa wananchi wengine. Anuani hizo zitasadia kuonesha jina la Ofisi yenyewe Mtaa iliyopo na eneo ambalo posti kodi hiyo ipo.

Naibu katibu Mkuu Mmuya amesema hayo katika ziara yake Mkoani Pwani tarehe 13 /05/2022 alipotembelea na kupokea taarifa ya Mkoa ya utekelezaji wa Anuani za makazi. Kwa sasa ngazi ya Taifa tumefikia 90% ya matarajio yetu lakini tunazidiana Mkoa na Mkoa.

Amepongeza Mkoa wa Pwani kwa kutekeleza vyema zoezi la uwekaji wa anuani za makazi na kufuata miongozo iliyowekwa katika utekelezaji wa anuani za makazi. “Ziara imelenga kujionea uhalisia ili mwezi huu, tutumie kurekebisha dosari chache tulizogundua kwa kupokea taarifa kwenye mfumo au kwa ziara mbalimbali tunazozifanya au taarifa tunazopatiwa alisema, Naibu Katibu Mkuu Mmuya”

“zoezi la anuani ya makazi ni endelevu, kila mmiliki mwenye eneo ambalo limejengwa au halijajengwa anapaswa kuwa na namba,alisema Naibu Katibu Mmuya”. Hiyo itasaidia kujua mahali eneo lilipo, wananchi wanahitaji kuelimishwa zaidi juu ya umuhimu wa  zoezi la uwekaji wa anuani za makazi na itaongeza dhana ushirikishwaji wa wananchi.

Akihitimisha Kaimu Injinia wa Tanroad Mkoa wa Pwani Meneja Heririsper Mollel amesema utekelezaji wa anuani za makazi umefika katika hatua nzuri ukamilishaji wake kwa sasa wamejikita katika kurekebisha vibao vilivyokosewa.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.