Tuesday, May 17, 2022

TUKUSANYE TAARIFA ZA KIJOGRAFIA KWA KILA NYUMBA TUNAYOITAMBUA

 


NA MWANDISHI WETU

Naibu katibu mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya amekemea tabia ya wachukua taarifa wasio waadilifu wanaochukua taarifa za kijiografia  (GPS) za sehemu moja kutolea taarifa kwenye eneo jingine. Jambo hilo linaharibu kazi data na linasababisha mfumo kutoa taarifa zisizosahihi.

“Watendaji mkagaue na kujiridhisha kuhusu taarifa za kijiografia (GPS), hasa pale inapotokea taarifa hizo kufanana eneo moja na jingine allisema Naibu Katibu Mkuu Mmuya.”

Hayo yamesemwa katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa operesheni ya anwani za makazi katika wilaya ya Kilwa na Rufiji. lazima tukusanye taarifa za kijiografia kwa kila nyumba ambayo inaenda kutambuliwa kwa sababu taarifa hizo za kijografia  zinatofautiana.

ninawapongeza wananchi wa Kilwa na Rufiji kwa uelewa na muitikio wao katika kutekeleza Operesheni ya anwani za makazi, na umuhimu wake kwa Sensa ya watu na makazi. Tuendelee kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa operesheni ya anwani za makazi.

“Ninatoa wito kwa wananchi wote, kujiwekea namba ya kudumu kwenye mageti au milango ni jukumu lao alisema Naibu Katibu Mkuu Mmuya.”

Akihitimisha Injinia wa Tarura Agatha Mtwangambate amesema kwa awamu ya kwanza  idadi ya vibao vya barabara ni kwa ajili ya barabara zote zilizosajiliwa, na vitawekwa katika mwanzo wa barabara na mwisho wa barabara. Kadri operesheni ya anuani za makazi inavyoendelea tutaanza kuzitambua barabara mpya na kuziwekea vibao.

 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.