Thursday, May 19, 2022

TAARIFA ZA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI, KUTUMIKA KWENYE MAWASILIANO

 


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bwn. Kaspar Mmuya ameshauri watendaji kuanza kutumia taarifa za mfumo wa Anwani za makazi Postikodi kwenye barua za ofisi ili kurahisha mawasiliano kwa watu kujua eneo zinapopatikana Ofisi

“Watendaji tuanze kujitambulisha kwenye mikutano kwa mfumo wa Anwani za makazi ili kutoa hamasa zaidi kwa wananchi alisema Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu”

Naibu Katibu Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu ametoa ushauri huo  Katika ziara yake ya kikazi Mkoani Pwani Halmashauri ya Kibaha Mji, alipoenda kujionea utekelezaji wa Operesheni Anwani za makazi.

Afisa Mtendaji mtaa wa mkoani A Kibaha Bwn. Jakson Mwakalima amesema tayari wameshapata mtengenezaji wa vibao vya nyumba, ambavyo mwananchi anaenda kununua kwa shilingi elfu Mbili na kubandika kwenye nyumba yake.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.