Thursday, November 30, 2023

MAANDALIZI KUELEKEA SIKU YA UKIMWI DUNIANI YAKAMILIKA

 


Viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu wamekagua maandalizi ya kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani Desemba 1, 2023 katika Viwanja vya Morogoro Sekondari ambapo maandalizi hayo yamekamili. Katika ukaguzi huo waliongozwa na Mhe. Jenista Mhagama ambaye ndiye Waziri mwenye dhamana ya uratibu.

Ikumbukwe maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani hufanyika kila mwaka ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI”.

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.