WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania wote wamuenzi marehemu 
Askofu Mstaafu Gaberiel Mmole (80) wa Jimbo Katoliki Mtwara kwa wema, 
upole  na utumishi mwema aliouonesha wakati wote wa maisha yake.
Ametoa
 wito huo leo (Jumanne, Mei 21, 2019) wakati wa mazishi ya Askofu Mmole 
yaliyofanyika katika Kanisa Katoliki Mtwara na kuhudhuriwa na viongozi, 
waumini wa Kanisa Katoliki pamoja na wakazi wa mkoa wa Mtwara 
Askofu
 Mmole alizaliwa Januari Mosi, 1939 katika Parokia ya Nangoo, ambapo 
alibatizwa na kupata kipaimara Oktoba 5, 1952. Mwaka 1971 alipata daraja
 ya upadre na kuwa Askofu kuanzia mwaka 1988, alifariki Mei 15, 2019 
Mkoani Mtwara baada ya kuugua kwa muda mrefu. 
Maeneo
 aliyoyatumikia tangu apate daraja la padri ni Paroko msaidizi wa Mnero 
(1972), Pastoral Institute GABA-Uganda (1973), Gombera Namupa seminari 
(1974 hadi Mei 1988), alitangazwa kuwa askofu wa Jimbo la Mtwara Machi 
12, 1988 na alisimikwa kuwa askofu wa Jimbo la Mtwara Mei 25, 1988.
Mwaka
 1951 hadi 1954 alipata elimu ya singi katika shule ya msingi Ndanda, 
1955 alisoma Nyangao Middle School, 1956 akahamia Lukuledi ambako 
alihitimu 1958. Alienda chuo cha ualimu Peramiho 1959 hadi 1960, ambapo 
1962 alijiunga na seminari ndogo ya Namupa na alihitimu 1964. 
1965
 hadi 1966 alichukua masomo ya falsafa kwenye seminari kuu ya Peramiho 
na mwaka 1967 hadi 1971 alichukua masomo ya theolojia katika seminari 
hiyo hiyo ya Peramiho. 1971 alifanya mitihani ya Baccalaureate inayotoka
 chuo kikuu cha Kipapa Urbaniana Roma na kupata shahada ya theolojia.
Ibada
 ya mazishi imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Songea, Mhashamu 
Askofu Damian Dallu ambaye alitumia muda huo kuwaasa Watanzania kuishi 
katika maadili mema na kuheshimiana.
Waziri
 Mkuu amesema enzi za uhai wake Askofu Mmole alitoa kipaumbele katika 
masuala muhimu ya maendeleo ya jamii ikiwemo elimu ambapo alisaidia sana
 watawa waliomaliza darasa la saba na kuwasaidia wajiunge na shule za 
sekondari.
“Hata
 uanzishwaji wa chuo kikuu cha STEMMUCO ambacho ni tawi la SAUT hapa 
Mtwara ni moja ya jitihada zake alizozifanya katika kuhakikisha anawapa 
elimu bora vijana na jamii. 
Kifo
 chake ni pigo kubwa kwa Taifa kwa sababu tumepoteza kiongozi wa kiroho 
aliyesimamia kwa uadilifu ustawi wa jamii ya Kitanzania.”
Kwa upande wake,
 Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Mhashamu Askofu Gervas Nyaisonga 
wa Jimbo Kuu la Mbeya amesema wamepata simanzi kubwa kufuatia kifo cha 
Askofu Mmole kwani walitegemea hekima zake katika Baraza la Maaskofu.
Ameongeza
 kuwa Askofu Mmole alikuwa kielelezo cha dhamira njema na alilitumikia 
kanisa katika hali yoyote, hivyo yatupasa kumuombea apumzike kwa amani.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwaaliwashukuru
 viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini mkoani Mtwara kutokana kwa 
ushirikiano mzuri anaopata unaomwezesha kutekeleza majukumu yake 
ipasavyo.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.