Tuesday, June 23, 2020

WIKI YA UTUMISHI WA UMMA -OWM

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi:Dorothy Mwaluko awakumbusha watumishi wa Ofisi yake wajibu wa majukumu yao wawapo kazini na kuwataka kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa kila moja kwenye eneo lake.

Katibu Mkuu amesema hayo kwenye mkutano na watumishi wa  Ofisi yake katika kukamilisha wiki ya Utumishi wa uuma kwa mwaka 2020, iliyobeba kauli mbiu isemayo  “jukumu la mtumishi wa umma katika kujenga na kudumisha amani iliyopo miongoni mwa jamii”

Katika kikao hicho aliwakumbusha kuwa na nidhamu ya kutosha katika uwajibikaji wa kazi na kila mtumishi kuzingatia sheria na taratibu za kazi awapo kazini.

Aidha aliwakumbusha pia watumishi kukamilisha ujazaji fomu za upimaji utendaji kazi yani (OPRAS) ambacho ndicho kipimo sahihi cha uwajibikaji wa mtumishi wa umma.

Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw:Greyson Mwaigombe  alimshukuru Katibu Mkuu kwa niaba ya watumishi wote na kuahidi kutekeleza yale yote aliyo elekeza.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa hazina jijini Dodoma uli hudhuriwa na watumishi wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu na mada mbalimbali zilitolewa za kuwakumbusha watumishi wajibu wao na kuzingatia maadili ya kazi na Usalama mahala pakazi.
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Bi Dorothy Mwaluko katika Mkutano wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Bi Dorothy Mwaluko katika Mkutano wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Bi Dorothy Mwaluko katika Mkutano wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.


MWISHO





EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.