Friday, October 26, 2018

MAJALIWA AKUTANA NA WAKUU WA MIKOA YA LINDI, MTWARA, PWANI NA RUVUMA NA VIONGOZI WA BODI YA KOROSHO KUJADILI BEI YA KOROSHO

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza  na  Wakuu wa Mikoa  ya Mtwara, Lindi, Pwani na Ruvuma  ambayo inalima  korosho na  imeanza kuuza zao hilo, wakuu  wa wilaya za mikoa hiyo, Wenyeviti  wa Vyama Vikuu vya Ushirika katika mikoa hiyo na Viongozi wa Juu wa Bodi ya Korosho Tanzania  kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Oktoba 26, 2018. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi na kushoto ni  aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania, Profesa Wakuru Magigi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na  Wakuu wa Mikoa  ya Lindi, Mtwara, Pwani na Ruvuma  ambao mikoa yao imeanza kuuza korosho, Wenyeviti wa Vyama Vikuu vya Ushirika na Watendaji Wakuu wa Bodi ya Korosho kwenye ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Oktoba 26, 2018. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba.
 Washirki wa Mkutano ulioitishwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  uliowajumuisha Wakuu wa Mikoa  ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Pwani ambao mikoa yao imeanza kuuza korosho, Wenyeviti wa Vyama Vikuu vya Ushirika na Watendaji Wakuu wa Bodi ya Korosho wakimsikiliza Waziri Mkuu wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Oktoba 26, 2018.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.