Monday, October 15, 2018

SUKOS YAKABIDHI VIFAA VYA ZIMAMOTO IDARA YA URATIBU WA MAAFA NCHINI



Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akizungumza jambo wakati wa kukabidhi vifaa vya zima moto pamoja na hati ya shukrani kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Utafiti) Idara hiyo  Bw.Bashiru Taratibu walipotembelea Oktoba 15, 2018.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji - SUKOS, Suleiman Kova akimkabidhi vifaa vya zima moto Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto katika maeneo ya kazi.

Mkurugenzi Msaidizi Mipango na Utafiti Idara ya Uratibu wa Maafa Bw.Bashiru Taratibu akiangalia vifaa vya zima moto vilivyokabidhiwa na Taasisi ya Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji –SUKOS Oktoba 15, 2018 kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) akipokea maelezo kutoka kwa Meneja wa Oparesheni Bi.Rahma Kova wakati wa kukabidhi cheti cha Shukrani ya ushirikiano uliopo kati ya SUKOS  na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akikabidhi Hati ya Shukrani kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe walipomtembelea kukabidhi vifaa vya zima moto Ofisini kwake Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa SUKOS Foundation walipotembelea Idara hiyo ili kukabidhi Vifaa vya Zima Moto pamoja na hati ya shukrani kwa namna Taasisi yake inavyoshirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, kulia kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Suleiman Kova.





EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.