Thursday, October 14, 2021

Idara ya Menejimenti ya Maafa yatoa Elimu ya kuzuia na kupunguza hatari na madhara ya maafa


 


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Patrobas Katambi alipotembelea banda la Idara ya Menejimenti ya Maafa katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa Chato, Mkoani Geita.


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tixon Nzunda akipokea maelezo kutoka kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji alipotembelea banda la Idara ya Menejimenti ya Maafa katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa Chato, Mkoani Geita.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Prof. Jamal Katundu akipokea maelezo kutoka Wataalam alipotembelea banda la Idara ya Menejimenti ya Maafa katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa Chato, Mkoani Geita.




Na: Mwandishi Wetu: CHATO

Idara ya Menejimenti ya Maafa imeshiriki maonesho ya wiki ya Vijana Kitaifa wilayani Chato, Mkoa wa Geita na kutoa elimu kwa wananchi ya kuzuia na kupunguza hatari na madhara ya maafa nchini.

Katika maonesho hayo Idara hiyo ilitembelewa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, Viongozi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.

Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa imekuwa ikiadhimisha siku ya kimataifa ya kupunguza madhara ya maafa kila tarehe 13 Oktoba ya kila mwaka kwa lengo la kukuza utamaduni wa usimamizi wa maafa kimataifa na kitaifa, ili kuzuia na kupunguza madhara ya majanga pamoja na kujiandaa kukabiliana na kurejesha hali katika ubora zaidi pale maafa yanapotokea.

Aidha, Idara ya Menejimenti ya Maafa imetumia fursa ya maaonesho hayo kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya maafa na mikakati ya kuepusha na kupunguza maafa nchini.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.